GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,697
- 109,125
Najua kuanzia sasa nguvu Kubwa ya Kupindua Meza (kwa Fitna za nje ya Uwanja) zitaanza Kutumika ili Kuwafunga Kaizer Chiefs FC Wikiendi ijayo huku tukidanganywa sana kuhusu uwezo wa Timu yetu na Kuaminishwa mno na Kauli Mbiu za Kibabe za Kuujaza Uwanja ili Mapato yapatikane wakati wenye Kuujua vyema Mpira tumeshajua kuwa Safari yetu kwa Msimu huu ndiyo imefikia Tamati hapa na kwa wengi huu ni Ukweli Mchungu.
Kwa nilivyozitizama Klabu Kubwa Tatu ambazo nimehisi huenda Simba SC ikakutana nazo kama itabahatika Kupindua Meza kwa Kaizer Chiefs FC huenda huko mbele tukaja Kufungwa hata Goli 13 na mojawapo ya hizo Timu kwani zina uwezo mkubwa sana na Wachezaji wa Daraja la Juu ambao kwa Simba SC yetu ni Maji marefu kweli kweli Kushindana ( Kupambana ) nao.
Jana nimewatizama Wydad Casablanca, Esperance du Tunis na Mamelodi Sundowns (ambao Wote hawa ni African Soccer Giants kwa sasa ) ambao najua kama Simba SC itakutana na Mmoja wapo katika CAF CL Semi Finals kuna Hatari ya Kupokea Kipigo Kitakatifu (cha Kishalubela) zaidi ya tulichokipokea Jana pale Soccer City FNB Stadium Johannesburg Afrika Kusini kutoka kwa Kaizer Chiefs FC.
Ushauri wangu wa bure tu kwa Simba SC (ambao najua utawaudhi Wapuuzi, Wanafiki na Washamba kadhaa) ni kwamba Simba SC tusitumie Nguvu Kubwa Kupindua Matokeo bali tuitumie tu hiyo Mechi kama sehemu ya Kujifunza zaidi na kupata Uzoefu ili basi Msimu ujao tukiingia tuwe tumejidhatiti vya Kutosha kwa Kufika mbali Kimashindano.
Kwa Kikosi cha sasa cha Simba SC Kulazimisha kufika Nusu Fainali ya CAF CL na kukutana na hao Giants Watatu niliowataja hapo juu ( ambao uwezo wao ni maradufu ya Kaizer Chiefs FC waliotuadhibu Kikatili jana ) ni Kujitafutia tu Aibu nyingine na tuzidi Kuchekwa na Watani zetu wakubwa Yanga SC ( japo na Wao Timu yao hivi sasa ni kama tu Mgonjwa anayekaribia Kukata Roho ) katika Kuwania Ubingwa wa VPL ambao kuna uwezekano mkubwa wasiupate kwa miaka kadhaa mpaka wakijirekebisha Kiufundi na Timu yao pamoja na Uongozi wao mzima.
Nimefurahi kumsikia Mwekezaji Mo Dewji akisema kuwa amehairisha Kununua Magari yake Mawili aina ya Ferrari na Rolls Royce ili astarehe nayo na ajikite Kuisaidia zaidi Klabu yake pendwa ya Simba SC.
Nami GENTAMYCINE namshauri Mwekezaji Mo Dewji kwamba kama kweli kapania kuachana na Starehe ya Kuyanunua hayo Magari ili aisaidie Simba SC namuomba hizo Pesa azitumie Kusajilia Wachezaji wakubwa, mahiri na wa Kiwango cha Kimataifa na Kimashindano hasa ili tukicheza tena Champions League Msimu ujao lengo letu lisiwe tena kufika Robo au Nusu bali liwe ni Kufika Fainali na kubeba Kombe kabisa la Afrika kwa mara ya Kwanza.
Binafsi kwa Kikosi cha Simba SC cha sasa ( ambacho si cha Kucheza Nusu Fainali ya CAF CL ) kutokana na kuwa na Mapungufu makubwa hasa ya Kiufundi hata tukiishia hapa Robo Fainali kwa kutolewa jumla na Kaizer Chiefs FC Wikiendi ijayo bado nitajiona nimejitahidi na Kukazia katika Lengo na kamwe sitochukia au kujisikia vibaya kwani nitakuwa nimetolewa katika hatua nzuri ya Kimashindano na Timu Bora pia kwa bara la Afrika.
Timu ikirejea Kesho Watafutwe haraka Wataalam wa Saikolojia ili wawajenge upya Wachezaji wetu na warudi katika hali zao kwani kwa Jicho langu Kali la Kisaikolojia leo katika recovery session yao pale Kambini Afrika Kusini nimeona almost 95% ya Wachezaji wa Simba SC wamekuwa affected psychologically hivyo kama hawatopata thorough counseling huenda Timu ikapoteza kwa margin kubwa zaidi ya Goli zile Nne ( 4 ) za Jana.
Mpira wa sasa ni wa Kisayansi zaidi hivyo nasi tubadilike na tuacheni na huu Upuuzi Upuuzi wetu wa mambo ya Kiswahili ya nje ya Uwanja ( sijui Kuroga sana na Kupulizia mno Dawa 4-4-2 Vyumbani ) hayatatusaidia lolote na sana sana tutazidi Kuharibikiwa tu na kuonena ni Wapumbavu wa Kiwango kisichovumilika tena katika hii dunia ya Kisasa yenye kuhitaji Fikra, Ubunifu na Mipango thabiti yenye Mikakati endelevu.
Kwa nilivyozitizama Klabu Kubwa Tatu ambazo nimehisi huenda Simba SC ikakutana nazo kama itabahatika Kupindua Meza kwa Kaizer Chiefs FC huenda huko mbele tukaja Kufungwa hata Goli 13 na mojawapo ya hizo Timu kwani zina uwezo mkubwa sana na Wachezaji wa Daraja la Juu ambao kwa Simba SC yetu ni Maji marefu kweli kweli Kushindana ( Kupambana ) nao.
Jana nimewatizama Wydad Casablanca, Esperance du Tunis na Mamelodi Sundowns (ambao Wote hawa ni African Soccer Giants kwa sasa ) ambao najua kama Simba SC itakutana na Mmoja wapo katika CAF CL Semi Finals kuna Hatari ya Kupokea Kipigo Kitakatifu (cha Kishalubela) zaidi ya tulichokipokea Jana pale Soccer City FNB Stadium Johannesburg Afrika Kusini kutoka kwa Kaizer Chiefs FC.
Ushauri wangu wa bure tu kwa Simba SC (ambao najua utawaudhi Wapuuzi, Wanafiki na Washamba kadhaa) ni kwamba Simba SC tusitumie Nguvu Kubwa Kupindua Matokeo bali tuitumie tu hiyo Mechi kama sehemu ya Kujifunza zaidi na kupata Uzoefu ili basi Msimu ujao tukiingia tuwe tumejidhatiti vya Kutosha kwa Kufika mbali Kimashindano.
Kwa Kikosi cha sasa cha Simba SC Kulazimisha kufika Nusu Fainali ya CAF CL na kukutana na hao Giants Watatu niliowataja hapo juu ( ambao uwezo wao ni maradufu ya Kaizer Chiefs FC waliotuadhibu Kikatili jana ) ni Kujitafutia tu Aibu nyingine na tuzidi Kuchekwa na Watani zetu wakubwa Yanga SC ( japo na Wao Timu yao hivi sasa ni kama tu Mgonjwa anayekaribia Kukata Roho ) katika Kuwania Ubingwa wa VPL ambao kuna uwezekano mkubwa wasiupate kwa miaka kadhaa mpaka wakijirekebisha Kiufundi na Timu yao pamoja na Uongozi wao mzima.
Nimefurahi kumsikia Mwekezaji Mo Dewji akisema kuwa amehairisha Kununua Magari yake Mawili aina ya Ferrari na Rolls Royce ili astarehe nayo na ajikite Kuisaidia zaidi Klabu yake pendwa ya Simba SC.
Nami GENTAMYCINE namshauri Mwekezaji Mo Dewji kwamba kama kweli kapania kuachana na Starehe ya Kuyanunua hayo Magari ili aisaidie Simba SC namuomba hizo Pesa azitumie Kusajilia Wachezaji wakubwa, mahiri na wa Kiwango cha Kimataifa na Kimashindano hasa ili tukicheza tena Champions League Msimu ujao lengo letu lisiwe tena kufika Robo au Nusu bali liwe ni Kufika Fainali na kubeba Kombe kabisa la Afrika kwa mara ya Kwanza.
Binafsi kwa Kikosi cha Simba SC cha sasa ( ambacho si cha Kucheza Nusu Fainali ya CAF CL ) kutokana na kuwa na Mapungufu makubwa hasa ya Kiufundi hata tukiishia hapa Robo Fainali kwa kutolewa jumla na Kaizer Chiefs FC Wikiendi ijayo bado nitajiona nimejitahidi na Kukazia katika Lengo na kamwe sitochukia au kujisikia vibaya kwani nitakuwa nimetolewa katika hatua nzuri ya Kimashindano na Timu Bora pia kwa bara la Afrika.
Timu ikirejea Kesho Watafutwe haraka Wataalam wa Saikolojia ili wawajenge upya Wachezaji wetu na warudi katika hali zao kwani kwa Jicho langu Kali la Kisaikolojia leo katika recovery session yao pale Kambini Afrika Kusini nimeona almost 95% ya Wachezaji wa Simba SC wamekuwa affected psychologically hivyo kama hawatopata thorough counseling huenda Timu ikapoteza kwa margin kubwa zaidi ya Goli zile Nne ( 4 ) za Jana.
Mpira wa sasa ni wa Kisayansi zaidi hivyo nasi tubadilike na tuacheni na huu Upuuzi Upuuzi wetu wa mambo ya Kiswahili ya nje ya Uwanja ( sijui Kuroga sana na Kupulizia mno Dawa 4-4-2 Vyumbani ) hayatatusaidia lolote na sana sana tutazidi Kuharibikiwa tu na kuonena ni Wapumbavu wa Kiwango kisichovumilika tena katika hii dunia ya Kisasa yenye kuhitaji Fikra, Ubunifu na Mipango thabiti yenye Mikakati endelevu.