Mpita Njia
JF-Expert Member
- Mar 3, 2008
- 6,999
- 1,187
Aaaaa Ndallo unaniangusha sasa... na wewe si ni muzee wa mujinbi? sasa unafanyaje biashara kwa kumuachia mtu mzigo kabla ya kupokea mkwanja!!!!!!Kutokana na kichwa cha habari hapo juu ni kua hapa katika maeneo ya mijini kuna hawa mafundi saa wamekuja kugeukia ufundi wa simu na papo hapo nimeona tangazo kwenye banda la fundi saa likisema - TUNANUNUA SIMU MBOVU! chakunishangaza ni kua mimi ninasimu kama 3 hivi za siku nyingi na ni mbovu, basi nikampelekea huyu bwana fundi saa nikamwambia nimeleta simu mbovu si mnanunua kama mlivyojieleza hapa? basi jamaa akazipokea akaniambia ndio wananunua simu mbovu na nimuachie halafu nimrudie baadae, mimi nikajua nakuja kuchukua michuzi japokua kitu chenyewe ni kibovu potelea mbali anipe hela yoyote, niliporudi huyu fundi akaniambia hawezi kununua nikamuuliza kwanini? akanijibu eti simu zenyewe hazifai kwakua ni mbovu mno!!! Jamani naomba kuwasilisha hii hoja kitu kibovu ni kipi?
Last edited by a moderator: