Dr Matola PhD
Platinum Member
- Oct 18, 2010
- 61,430
- 108,589
- Kwa mtizamo wangu ni mtu aliyelemewa na wasaidizi wazembe na waongo wanaomdanganya na wasiopendana wao kwa wao na ni wanafiki.
- Moyo wa kuwatumikia watanzania anao ila vikwazo ktk mfumo inaonekana vimemshinda haswa ukizingatia mavuguvugu mengi (mfano kipindi kile wanataka wamuondoe kwenye uenyekiti wa taifa wa CCM) mpaka sasa anaiogopa sana CCM!
- Uongozi wake unatia shaka.
- Machoni pa watanzania walio wanyonge anaonekana ni msaliti.
Hotuba zake tatu za hivi karibuni zimejaa manung'uniko na malalamiko ya mtu ambaye haeleweki, hapendwi, hasifiwi au ambaye hashukuriwi. Hotuba yake kwa wazee wa CCM wa Dar-es-Salaam baada ya mgogoro wa madaktari na hotuba yake ya Mei Mosi mbele ya wafanyakazi kule Tanga zinatuonesha hisia za mtu ambaye wananchi wake inaonekana hawamshukuru vya kutosha.
Katika hotuba zote tatu Rais amejaribu kutuonesha ni jinsi gani amejitahidi kufanya mambo kadha wa kadha ambayo kwa kweli watu wangemshukuru kuwa ameyafanya lakini inaonekana hashukuriwi. Ni hotuba ambazo zimejaa "tenda wema nenda zako" nyingi. Madaktari hawamshukuru, wafanyakazi hawamshukuru, wapinzani hawamshukuru, na hata wana CCM wenzake yawezekana hawamshukuru. Lakini pia kwenye hotuba ile ya mambo ya nishati ambapo alisifia serikali yake kufanya mengi katika kuzalisha umeme nchini kuliko serikali zilizomtangulia nayo pia ilijaa kutokuwa appreciated.
Ndio sababu najiuliza ni kweli yawezekana Rais Kikwete anaona Watanzania hawamshukuru vya kutosha na kuappreciate vitu alivyovifanya? Ni kweli Kikwete amefanya makubwa sana ambayo anapaswa kushukuriwa kwayo? Ni kweli kwamba Watanzania wanambebesha lawama kwa kumuonea tu japo "amejitahidi" sana kufikia malengo mbalimbali kulinganisha na viongozi wengine waliomtangulia?
Kama ni kweli amefanya yote ambayo anadai amefanya ni kitu gani basi kinawafanya Watanzania wasiyaona mambo hayo na kumpatia pongezi zaidi kiasi kwamba badala ya kuongeza kura zake mwaka 2010 alizipunguzwa kwa asilimia 20 hivi? Kwamba pamoja na yote mazuri anajikuta anashinikizwa kuvunja baraza, utawala wake ukilaumiwa sana na wananchi wakiwa na kiu zaidi ya mabadiliko na uongozi. Tumeona juzi hata baadhi ya viongozi wa chama chake wakimuambia waziwazi kuwa "awe mkali kidogo".
Labda tujiulize swali la ugomvi zaidi - ni uongozi gani ambao Kikwete anapatia taifa kiasi kwamba anafanya mambo mengi mazuri lakini analaumiwa zaidi? Yaani, anafanya mambo ambayo anaamini ni makubwa lakini mbele ya wananchi yanaonekana kama 'hakunaga'?
Yawezekana, we are missing to recognize the genius in our midst? are we that blinded by whatever to the extent that we can not appreciate the work of superb and beloved leader? Ni matatizo ya sisi wananchi kutomtambua yeye au ni tatizo la yeye kutotambulika?
Hivi mara ya mwisho inflation kuwa 20% ilikuwa lini? anybody...
sidhani kama kwake yeye mwenyewe ime sink in kwamba kweli yeye ni rais. He is still dumbfounded. Atakumbuka shuka asubuhi tu
Mr President is the failure of himself, until now am failing to understand what was his motive running for the presidency. Sasa naamini mwalimu alivyosema uyu bado mtoto, hakumaanisha mtoto kwa umri but he meant mtoto kwa uwezo wake na uelewa wake wa kupembua mambo ni mdogo. Lakini mwisho wa siku wa kulaumiwa ni sisi wananchi why at first time tulimweka uyu jamaa? Naona yeye mwenyewe labda ashafanya assessment na kagundua approval rate yake is below marginal level sasa kilichobaki ni kulalama lalama tu.
KIJANI: Pengine hatuna shukurani, lakini baadhi ya tunayoyanung'unikia ni:Humjui Kikwete1
Hotuba za Kikwete zote, ni fundisho kwa watu kama wewe wanaolalamika na kunung'unika kila siku lakini mnachonung'unika hakijulikani.
Hotuba aliyoongea na wazee kuhusu madaktari, licha ya kuwaelewesha kilichojiri, alitamba sana na hata kukejeli. Na mpaka leo tumeona madaktari ni kimya na wala hutowasikia tena wakilalamika. Huyo ndio JK.
Hotuba ya juzi umeona alivyowanyamazisha kwa kukurupuka na kudakia hoja kwa mafanikio ya jitihada zake.
Humjui Kikwete1
JasusiTatizo moja la Kikwete ni kwamba mara nyingine anasahau kuwa yeye ndiye rais wa maamuzi na kujiona kama observer tu. Nakumbuka kuna wakati alisema asilimia 30% ya bajeti huishia mifukoni mwa watu. What did he do about it? Nothing. Halafu alipokuwa Davos akasema tatizo moja la uwekezaji ni kwamba mfumo wetu bila ya rais kuingilia kati hufiki popote. He is in a position do to something about it, but instead akawakaribisha wale waliokuwa wanamsikiliza pale Davos waje wamuone yeye ili mambo yao yaende sawa. Sasa which is which? Katika hili suala la mawaziri, kama kweli ni yeye alipendekeza ripoti ya CAG ijadiliwe bungeni, mbona hakuwachukulia hatua za mara moja mawaziri wake aliowateua mwenyewe? Kulikuwa na sababu gani za kuliweka taifa in suspense kama ilivyo sasa kuhusiana na kama mawaziri wanajiuzlu au hapana? Angefuta baraza la mawaziri mara moja Watanzania wangemuelewa, lakini hivi sasa inaonekana kuwa ni mchezo wa maigizo tu.
Humjui Kikwete.
Laiti ungemjuwa usingeleta pumba ulizozileta.
Ni hotuba ipi aliyonung'umika kama utakavyo iwe?
Hotuba za Kikwete zote, ni fundisho kwa watu kama wewe wanaolalamika na kunung'unika kila siku lakini mnachonung'unika hakijulikani.
Hotuba aliyoongea na wazee kuhusu madaktari, licha ya kuwaelewesha kilichojiri, alitamba sana na hata kukejeli. Na mpaka leo tumeona madaktari ni kimya na wala hutowasikia tena wakilalamika. Huyo ndio JK.
Hotuba ya juzi umeona alivyowanyamazisha kwa kukurupuka na kudakia hoja kwa mafanikio ya jitihada zake.
Kikwete, hakupewa "favor" kuupata Urais kama ilivyokuwa kwa wote wa kabla yake. Kikwete alijuwa kabisa kuwa anataka awe Rais na alijipanga hivyo kwa miaka mingi sana na akaupata licha ya kuletewa mizengwe na Nyerere katika uhai wake.
Nakuona una haha kutafuta la kusema kuhusu Kikwete lakini ukweli ni kwamba hamumuwezi kabisa, kila afanyacho hufanya kwa maslahi ya wananchi na si ya kwake binafsi. Leo hii kikwete angekuwa na madudu japo asilimia 1 tu ya madudu ya Mkapa sijui kama angebaki kwenye Urais, maana mlivyomsakama si kidogo, lakini hamna zaidi ya kuzuwa tu na kutafuta kisichopo, mtatafuta sana lakini bure tu.
Humjui Kikwete, unamsikia tu na unamkisia, he is way too far ahead from your way of thinking. Wewe bado una fikra za kizamani sana, za wakati wa dhiki za chai kukorogwa kwa lawalawa badala ya sukari.
Mnajionea nafsi zenu wenyewe na ndio mpaka zinawafanya mnakuja kubwabwaja hapa hapa, ati "tunamuonea Kikwete", una ubavu upi wewe wa kumuonea Kikwete?
Humjui Kikwete1