Tunamuonea Rais Kikwete?

Ukitaka kujua kwamba JK ni Rais wa namna gani, angalia alivyoshiriki msiba wa Kanumba.

Kwamba ameahirisha safari ili ashiriki. Pili katoa ubani milioni 10, tatu kawakumbusha wasanii kwamba ahadi yao anaikumbuka na hajaisahau anasubiri uongozi wa wasanii wafanyie kazi mambo fulani then wampelekee "ripoti".

Misiba mingapi inatokea na hatusikii akiahirisha safari ili ashiriki na badala yake anatuma wawakilishi? Je, kulikuwa na haja ya kusema hayo? Kulikuwa na haja ya kutangaza "ubani" ametoa kiasi gani na kukumbushia ahadi zake? Why asubiri kwenye msiba? Was that a right place ya kukumbushia hilo?

Hilo la kutoshukuriwa, anajitakia mwenyewe na mojawapo ya vitu vinavyomponza ni hilo hapo juu.
 
Jk ni mzee wa mipasho or malkia wa mipasho, sio kosa lake ni kosa la eneo analotoka ama kutokea ama kukulia ama hulka ya watu wa pwani kote ndivyo walivyo, mfano watu wa mombasa zanzibar lindi mtwara malindi pemba bagamoyo somalia nk. Wao siku zote wanajifanya wajuwaji kumbe hawajui chochote washabiki wa zuri sana lakini sio wachezaji wa zuqi,yuko uwanjani anacheza mpira timu yake imefungwa nae pia kashindwa kufunga goli la wazi kabisa, anaanza kulalamika ooo nataka mnishukuru nimekoa magoli mengi sana tulikuwa turudi na kikapu cha magoli! Upntezf point 3 za bure na za wazi kabisa uje utuambie umeokoa magoli mengi sana? Tunachotaka ni ushindi sio uokoaji wa magoli. Pwani pwaa!!!! Hakuna kitu humo.tunahitaji ushindi na sio kutaka shukrani zisizostahiki.
 

Uhuru wa vyombo vya habari ni swala ambalo hata mkapa lilishaanza kumshinda. Angejifanya jeuri kama Mkapa angejiharibia utukufu mwiiiingi aliokua nao kipindi kile. Na ukuzingatia uhuru wa kutoa maoni ni haki yetu, tumshukuru kwa kipi? Kama akiona ni zawadi basi azuie aone atakachokumbana nacho!
 
Tatizo moja la Kikwete ni kwamba mara nyingine anasahau kuwa yeye ndiye rais wa maamuzi na kujiona kama observer tu. Nakumbuka kuna wakati alisema asilimia 30% ya bajeti huishia mifukoni mwa watu. What did he do about it? Nothing. Halafu alipokuwa Davos akasema tatizo moja la uwekezaji ni kwamba mfumo wetu bila ya rais kuingilia kati hufiki popote. He is in a position do to something about it, but instead akawakaribisha wale waliokuwa wanamsikiliza pale Davos waje wamuone yeye ili mambo yao yaende sawa. Sasa which is which? Katika hili suala la mawaziri, kama kweli ni yeye alipendekeza ripoti ya CAG ijadiliwe bungeni, mbona hakuwachukulia hatua za mara moja mawaziri wake aliowateua mwenyewe? Kulikuwa na sababu gani za kuliweka taifa in suspense kama ilivyo sasa kuhusiana na kama mawaziri wanajiuzlu au hapana? Angefuta baraza la mawaziri mara moja Watanzania wangemuelewa, lakini hivi sasa inaonekana kuwa ni mchezo wa maigizo tu.
 
...Alidhani kuwa Rais ni lelemama atakenuakenua tu na kufanya uVDG miaka yake 10 ikatike halafu huyo anaenda kujidai na retirement fund yake nono...sasa Urais unamtokea puani....Baraza jipya la Mawaziri atatangaza lini? bado anamsubiri Migiro au wengi aliowagusa hawataki kuwa Mawaziri!?...Wiki inakatika sasa nchi haina baraza la mawaziri...nasema haina baraza la mawaziri kwa sababu hawa waliopo sidhani kama hata kama wanafanya kazi zozote kwa kuwa wako very anxious kujua bado wamo au wametemwa.
 
Humjui Kikwete.

Laiti ungemjuwa usingeleta pumba ulizozileta.

Ni hotuba ipi aliyonung'unika kama utakavyo iwe?

Hotuba za Kikwete zote, ni fundisho kwa watu kama wewe wanaolalamika na kunung'unika kila siku lakini mnachonung'unika hakijulikani.

Hotuba aliyoongea na wazee kuhusu madaktari, licha ya kuwaelewesha kilichojiri, alitamba sana na hata kukejeli. Na mpaka leo tumeona madaktari ni kimya na wala hutowasikia tena wakilalamika. Huyo ndio JMK.

Hotuba ya juzi umeona alivyowanyamazisha kwa kukurupuka na kudakia hoja kwa mafanikio ya jitihada zake.

Kikwete, hakupewa "favor" kuupata Urais kama ilivyokuwa kwa wote wa kabla yake. Kikwete alijuwa kabisa kuwa anataka awe Rais na alijipanga hivyo kwa miaka mingi sana na akaupata licha ya kuletewa mizengwe na Nyerere katika uhai wake.

Nakuona una haha kutafuta la kusema kuhusu Kikwete lakini ukweli ni kwamba hamumuwezi kabisa, kila afanyacho hufanya kwa maslahi ya wananchi na si ya kwake binafsi. Leo hii Kikwete angekuwa na madudu japo asilimia 1 tu ya madudu ya Mkapa sijui kama angebaki kwenye Urais, maana mlivyomsakama si kidogo, lakini hamna zaidi ya kuzuwa tu na kutafuta kisichopo, mtatafuta sana lakini bure tu.

Humjui Kikwete, unamsikia tu na unamkisia, he is way too far ahead from your way of thinking. Wewe bado una fikra za kizamani sana, za wakati wa dhiki za chai kukorogwa kwa lawalawa badala ya sukari.

Mnajionea nafsi zenu wenyewe na ndio mpaka zinawafanya mnakuja kubwabwaja hapa hapa, ati "tunamuonea Kikwete", una ubavu upi wewe wa kumuonea Kikwete?

Humjui Kikwete!
 
Kumbe mpo wengi msio na shukrani na msiotambua mambo bwelele ambayo Kikwete kawafanyia. Jamani karudisha 'chenji ya rada' hamshukuru?

wanasema huwezi kuuza samaki ukachukia shombo.... wacha tu anuke shombo
 

Hapo kwenye red hapo....
 
Mzee mwanakijiji naomba unisaidie kumfikishie ujumbe huu hapa chini.

Tutamshukuru kwa lipi wakati mfumko wa bei unazidi kupaa na mwanae ndo mdau wa kuhodhi bei za mafuta?
Tutamshukuru kwa lipi wakati wazi wazi watu wanatafuna nchi mchana peupe na yeye anakenua tu bila kuchukua hatua?
Tutamshukuru kwa lipi ili hali tangu ameingia madarakani sijaona anamwajibisha mtu?
Tutamshukuru vipi ili hali maendeleo na kasi tuliyokuwa nayo 2005 tumejikuta tumepiga hatua kurudi nyuma?
Tutamshukuru kwa lipi ili hali amejaza viongozi wabovu katika maeneo nyeti kwa uswahiba?

Mwisho naomba umuulize anataka tuje tumshukurie wapi Brazil,Marekani,Italy,Namibia,Malawi,Ethiopia,Sudan,Uk,France,Uswis,South Africa, atutajie tu kwamba watanzania tumfuate nchi gani tukampe shukrani zetu na machungu yetu ya moyoni.
 

Tungetarajia nini kutoka kwa mpiga tumba kwenye ngoma ya kikwere?!

Napita tu, baadae
 

uteuzi wa wasaidizi wake una mushkeli. anaweka wasaidizi wenye family ties na yeye. jairo anasemwa ni shemeji yake (dada ya mkewe wa kwanza). ndiyo maana inampa shida kuwawajibisha!
 
Wananchi siyo wajinga au wapungufu wa kuona mambo. Kwa bahati nzuri au mbaya Kikwete amechukua uongozi kukiwa na 'reference' hivyo ni rahisi sana kulinganishwa na waliopita.

1. Kikwete amechukua nchi ikiwa na 'template' ya kila jambo. Ameshindwa kujaza nyama katika mifupa 'skeleton'
Hapa ndipo kunakuja swali, hivi JK amefanya kitu gani kipya tofauti na watangulizi wake tukifahamu alilelewa katika mfumo anaouelewa vema.

2. Wananchi wanajiuliza alipochukua nchi 'inflation' ilikuwa 9% sasa ipo 20%! wanaopokea maumivu ni wananchi hao hao kulikoni?

3. Kikwete hajawahi kusimamia jambo lolote kama Rais. Amekuwa anakwenda na upepo ili kutoudhi au kufuhisha watu.
Hapa ndipo wananchi wanajiuliza kigeu geu 'flip flop' inasaidiaje taifa? Mfano, wakati analaani ufisadi, Kikwete hajasimama kwa vitendo kuonyesha anafanyia kazi maneno yake. Amekuwa kichaka cha mafisadi

4. Kikwete anaonekana kama 'msanii' na hajasimamia hoja zake kama mgombea au sera za chama
a: Aliahidi kurudisha nyumba za serikali, tumeona anajenga na hana uthubutu hata wa kuzungumzia hayo
b: Alisema atahakikisha waliohusika na kashfa ya rada wanafika mbele ya sheria. Hakuna lolote linaloendelea
c.Aliahidi kupambana na wauza dawa, majina yapo mezani kwake mwaka wa sita sasa
d. Akaahidi maisha bora, sasa ni bora maisha! umasikini umetamalaki kuliko huko nyuma. Inflation 20%
e: Akaahidi kushughulikia kero za muungano, sasa anazuia usijadiliwe

5: Kitendo chake cha kuruhusu washirika na maswahiba wapore rasilimali za nchi, wakombe kodi kwa wanaoishi kwa dola 1 kwasiku bila kuchukua hatua kinatia maudhi sana

Haya ni kwa uchache na mifano tu. Siyo kwamba wananchi wanamchukia bali hawana matumaini naye na hasira zao si kwa JK kama binadamu ni kwa Rais ambaye wataishi naye miaka 4 ijayo bila matumaini.
 

Tutashukuru vipi wakati inflation ni double digit almost 20%?!
 
Mzee mwanakijiji naomba unisaidie kumfikishie ujumbe huu hapa chini.

Tutamshukuru kwa lipi wakati mfumko wa bei unazidi kupaa na mwanae ndo mdau wa kuhodhi bei za mafuta?

Uzushi huo, weka ushahidi wa kuwa mwanae ndiye mwenye "kuhodhi" bei za mafuta, na ukishindwa kuweka ushahidi basi jijuwe kuwa wewe ni mnafik.

Tutamshukuru kwa lipi wakati wazi wazi watu wanatafuna nchi mchana peupe na yeye anakenua tu bila kuchukua hatua?

Ingekuwa sio jithada zake binafsi ungeyajuwa hayo? unaonesha ni mwepesi wa kusahau kuwa kwa miaka 44 ya mwanzo toka tupate Uhuru hakuna uwazi kwa mahesabu ya Serikali kama ilivyo sasa. Au hulijui hilo? Fikiri!

Tutamshukuru kwa lipi ili hali tangu ameingia madarakani sijaona anamwajibisha mtu?

Una tatizo la kusahau, kama kuna wakati ambapo kuna kesi na mashtaka mengi zaidi ya rushwa na wizi wa mali za serikali basi ni huu wa Kikwete, tumeona vigogo vya mpingo vikifikishwa mahakamani, tumeona mpaka mawaziri wakisambatishwa, tumeona wabunge ambao ndio wawakilishi wako wakikemea na kuwawajibisha mawaziri, au yote hayo uliwahi kuyaona kabla ya awamu ya Kikwete? Fikiri!


Tutamshukuru vipi ili hali maendeleo na kasi tuliyokuwa nayo 2005 tumejikuta tumepiga hatua kurudi nyuma?

Weka ushahidi, maendelo ya Tanzania katika miaka 6 ya Kikwete ni zaidi ya maendeleo ya Rais wowote wa kabla yake, tena kwa ushahidi kabisa. Na hili utaumbuka vibaya sana, tuwekee maendeleo yako ya kabla ya 2005, kwenye chochote ukipendacho tukuoneshe ya leo yakoje halafu u "compare", Nakuhakikishia huna na huwezi kufanya hilo. Utajisuta, kama upo tayari kujisuta weka hapa!

Tutamshukuru kwa lipi ili hali amejaza viongozi wabovu katika maeneo nyeti kwa uswahiba?

Fikra za kijinga hizo, huoni vyama vinavyoweka viongozi kwa mapenzi na uhawara? mkwe, mchumba na mahawara? nakusikitikia sana kama hayo hujayaona!

Mwisho naomba umuulize anataka tuje tumshukurie wapi Brazil,Marekani,Italy,Namibia,Malawi,Ethiopia,Sudan,Uk,France,Uswis,South Africa, atutajie tu kwamba watanzania tumfuate nchi gani tukampe shukrani zetu na machungu yetu ya moyoni.

Alikwambia anataka shukurani yako? hafanyi kazi zake ili umshukuru, huo ni muono finyu kabisa na wala hayupo pale kwa kushukuriwa, umesahau kuwa yeye ni "chaguo la Mungu"?


Huyo uliemuomba akusaidie anashindwa hata kujisaidia mwenyewe, ataweza kukusaidia wewe? Fikiri!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…