Tunamkumbuka Mzee Rashid M. Kawawa - Simba wa Vita

..binafsi siamini kama viongozi hawa waliishi maisha kama yetu walalahoi. lakini hata kama waliishi maisha kama yetu sidhani kama tunapaswa kuwasifia. mimi nilitegemea viongozi hao wangetuwezesha na sisi tuishi maisha mazuri kama wao kwa kutumia juhudi zetu.

Kweli JokaKuu...kuna exaggerations fulani hivi kwa watu kusema hao viongozi waliishi maisha kama ya kwetu sisi walalahoi.

Hao viongozi sidhani kama walikuwa wanapanda vipanya na chai maharage tulizokuwa tunazigombania kwa kupigana vikumbo kila siku. Hao watoto wao walikuwa wakipelekwa shule na kwenda kuchukuliwa na magari yenye vibao vya magari vya SU au ST wakati sisi wengine tukiwahi stendi za mabasi kupigania usafiri wa daladala na UDA.

Huu ni mmoja tu ya mifano mingi ya kuonesha kuwa hawakuishi maisha kama yetu sisi walalahoi.
 
Kama katika wanafunzi wake wote aliyefaulu ni Kawawa peke yake...basi mwalimu alikuwa hajui kufundisha.
 
Omega Psi Phi,

..binafsi sioni sababu ya kumsifia kiongozi wa kuishi maisha ya kimasikini. nasema hivyo kwasababu huu umasikini unakera na si kitu cha kujivunia hata kidogo.

..kuna mwandishi wa habari ameandika eulogy ya Kawawa na kumsifia kwa kwenda kuisha Madale mahali ambapo hakuna barabara nzuri. kwa maono yake huyu mwandishi ni kwamba Kawawa anaishi kama walalahoi wengine. mwandishi anasahau kwamba Kawawa tangu 60s amekuwa akitembelea magari ya kifahari kama landrovers,mercedes,toyota land cruisers etc.

..kama kuna kiongozi anapanda daladala, na kusafiri kwa treni ya reli ya kati, basi huyo ndiyo wa kusifiwa kuwa anaishi kama walalahoi wengine. kinyume cha hapo naomba tuache kuwatukana walalahoi.

NB:

..miaka ambayo watoto wa Kawawa na Nyerere wanasoma shule za serikali zilikuwa zinafaulisha kuliko shule za private. labda kwa hilo naweza kuwasifia. lakini nafasi hizo zilikuwa chache sana sanaaaa.

..shule za private zilipoanza kufaulisha kila kiongozi alipeleka watoto wake huko. wako wananchi wa kawaida walioamua kujinyima nao wanapeleka watoto wao huko.
 
jokaKuu,
Unfortunately Mr. Rugarabamu does not mention where the simba incidents took place. Was it in Rufiji? Was it in Mwibara?
 
Katika miaka ya mwanzoni ya Themanini, Marehemu alikuwa na nyumba pale Bombambili Songea. Nyumba ile ilikuwa ikilindwa sana na FFU muda wote. Ninachonistajabisha ni kiongozi gani ambae alikuwa akiishi humo ndani? Kwani Marehemu hakupata kwenda nyumba huyo kipindi chote ilipokuwa chini ya ulinzi mkali.

Je nyumba hiyo ilikuwa ikitumika kwa kuwekwa viongozi vizuizini miaka hiyo?
 
Jasusi,

..but i dont think it would make much difference whether ppl were mauled by lions in Rufiji or Mwibara. the main point here is that the government put its own ppl in harms way. hata kama huko walikoishi b4, lion attacks were a common thing bado nalazimika kuamini kwamba the government should have relocated them to areas which were safe.

..halafu jibu alilotoa Mzee Rashidi Kawawa alipopewa taarifa za wananchi kutafunwa na simba halikuwa zuri hata kidogo. sioni kama lina tofauti na yale ya kusema "bora tule nyasi", " they can go to hell ," au " kila mtu abebe msalaba wake "
 
Jasusi,

..but i dont think it would make much difference whether ppl were mauled by lions in Rufiji or Mwibara. the main point here is that the government put its own ppl in harms way. hata kama huko walikoishi b4, lion attacks were a common thing bado nalazimika kuamini kwamba the government should have relocated them to areas which were safe.

..halafu jibu alilotoa Mzee Rashidi Kawawa alipopewa taarifa za wananchi kutafunwa na simba halikuwa zuri hata kidogo. sioni kama lina tofauti na yale ya kusema "bora tule nyasi", " they can go to hell ," au " kila mtu abebe msalaba wake "
jokaKuu,
It would make a world of difference. Kwa sababu kama alikuwa Kagera nijuavyo ni kwamba hakuna simba kule. Inakuwa ni problem ya veracity of his allegations. Ndio maana kwenye journalism 101 kuna who, where, what, when and why.
 
Jasusi,

..sasa hayo majibu ya "Simba wa Vita" kwamba wananchi kutafunwa na "Simba wala Watu" unayachukulia vipi?

..hivi majibu hayo ni careless and insensitive sawa na yale mengine kama "wananchi tule nyasi" au "they can go to hell " au " kila mtu abebe msalaba wake"?

NB:

..tatizo ninaloliona hapa ni waandishi wa habari kumpa sifa nyingine ambazo siyo zake.
 
Jasusi,

..sasa hayo majibu ya "Simba wa Vita" kwamba wananchi kutafunwa na "Simba wala Watu" unayachukulia vipi?

..hivi majibu hayo ni careless and insensitive sawa na yale mengine kama "wananchi tule nyasi" au "they can go to hell " au " kila mtu abebe msalaba wake"?

NB:

..tatizo ninaloliona hapa ni waandishi wa habari kumpa sifa nyingine ambazo siyo zake.
jokaKuu,
Kama kweli alisema hivyo it is unfortunate. Lakini kwanza tuthibitishe hoja za Rugarabamu isije ikawa alitunga tu the whole episode.
 
I go with Edward Sokoine. He was our own Stalin if not Putin. We lost him we lost the opportunity to use our heads in resolving life challenges. Tusingelikubali kuendelea kutembea uchi...Urafiki/Mwatex etc wangejua kutengeneza nguo ili tujisitiri. Tungejua what it takes to make good soaps and tooth paste....maana shida mgunduzi.
Tulipogundua mitumba, tukagundua pia na kuviua viwanda.Leo tunapiga miyayo kama watoto wasio na baba.Mali zote ni za wawekezaji!
 
Re: Picha Mbalimbali Za Mzee Rashid Mfaume Kawawa






Nadhani huyo wa kwanza Front Row alievaa mgolole sio Tewa Said Tewa bali ni Michael Kamaliza.
i1347_zamanitanzania.jpg
 
Kifo cha Mzee Kawawa kitawaumbua mafundamentalists kama GT juu ya uongo wao kuwa Kambarage aliwaonea waislamu katika kuwapa vyeo!! Picha za JF zilizobandikwa kwa mfano ile cabinet ya muungano ya kwanza inaonyesha mchanganyiko wa mawaziri wakristo na waislamu wengi tu. GT iangalie hiyo picha na watambue waislamu wenzio waliokuwa mawaziri!!
 
- Hiki kifo mkuu kinabadilisha kabisa marathon ya 2010, inaogopesha sana maana everything lately seems to be working for Lowassa, yes I said it hii ni big plus kwake!

Respect.

FMEs!

Tatizo lako wewe field marshal kamwe huachi kuwaza na kuwazua juu ya lowasa, na tatizo kubwa sio kwamba kweli unaamini ana makosa bali ni chuki zako ulizopata toka alipomwasi baba yako na kujiunga na JK.............uzushi wenu hautosaidia lowasa ana akili timamu hawezi kuingia kwenye uchaguzi ambao ni wazi kuwa lazima ataanguka.....................ujasiri huo anao mzee wako ambae aliingia huku akijua kuwa hatuko tayari kuongozwa na embe bivu lililokwishazeeka.tena ata ubunge hataki kuachia mpaka leo na umri wote
 
FMES,
Umetaja kitu kimoja muhimu kuhusu Kawawa. Uaminifu katika siasa tangu enzi za kina Ceasar ni kitu adimu sana. Nyerere alimwamini Kawawa alipomwachia uwaziri mkuu kwa mwaka mzima mpaka Tanganyika ilipokuwa tayari kuwa jamhuri. For this quality only Kawawa stands heads above the rest. Na siyo hiyo tu. His simplicity was unequaled.

Ingawa hakuwa na elimu kubwa Kawawa alikuwa na busara ya kuzaliwa. He was a born leader.


Pia intelligence na political wit ya Mwalimu vilimuwezesha kujua kwamba Kawawa was the right person kuachiwa ule uwaziri mkuu! Kambona was Mwalimu's 'friend' lakini hakuthubutu kumuachia!
 
..that is possible buddy..EDWARD LOWASSA....anaweza kuwa Jacob ZUMA wa Tanzania....mnajuwa kuwa zuma alikuwa msaidizi mwaminifu wa mbeki ambapo power brokers walipomuona kuwa ni tishio walimchonganisha na mbeki ..na kwa kumtumia mkuu wa COBRA squad....AKISHIRIKIANA na mkuu wa usalama..wakamchomekea zuma rushwa ya silaha kupitia kwa msaidizi wake wa kiuchumi ....na baadaye kashfa mbaya ya mapenzi....kwa kweli ZUMA aliondoka ,madarakani akiwa mchafu na ananuka kuliko lowassa ambaye BUNGE na serikali yenyewe wanashindwa kumtia hatiani....wewe fikiria zuma alikuwa convicted kwenye baadhi ya makosa!!

kifo cha kawawa kwa kweli kinamuacha jk MKIWA .....lakini ni lazima mjuwe kuwa JK has CC[central commetee]..and lowassa may have NEC and GENERAL assembly!!....nadhani mnajuwa kuwa CC ni kila kitu and it can keep JK surving for a while though ni lazima ajihadhari fate ya Mbeki naye isimkute ....kwani hitoria ipo wazi kuwa lowassa was poweful kuliko jk ...tangu walipoanza mbio hizi 1995...na ni lowassa ambaye bid yake iliposhindwa aliamua kubank kwa kikwete na kumfanya awashangaze wachunguzi wa mambo pale Mkutano mkuu mwaka 1995....ambao walidhani baada ya kumtoa lowassa wanambakisha mgombea dhaifu KIKWETE..Akawashangaza hadi ikabidi wa strike deal ambalo baadaye lilimpa urais.......thuogh hata kawawa alikuwa anajuwa kuwa lengo lao na nyerere lillikuwa kumfix kikwete badaye aukose urais 2005 ikifika ...jambo ambalo KAWAWA alikuja kufanya kinyume chake!!!

There is nothing to worry about! Sisi wana CCM tutampa JK support ya kutosha ili amalizie ingwe yake ya miaka 10 maana ndio utamaduni wetu. After all Sheikh Yahya kasema atakayethubutu atakufa!!

Wale wanaowania kuupata urais 2015 hatutakubali tena kutoa kura zetu kwa mtu ambaye ana dhamira ya kuutaka urais for fun na si kwa nia ya kuwatumikia wananchi.
 
Zitto,

..unadai Kawawa alilaumiwa. je,kwanini alilaumiwa? je kuna mahali aliharibu au yalikuwa majungu tu?

..unajua hili suala la watoto wakubwa kusoma shule za serikali wakati ule mnali-exaggerate sana. shule zile zilikuwa za kiwango cha juu na huwezi kuzilingalisha hata na hizi academy za siku hizi.

..pia nafasi za kusoma sekondari zilikuwa chache mno. hapo aliyebahatika atakuwa ni mlalahoi aliyepata nafasi hiyo. hali hiyo isichukuliwe kabisa kama kiongozi amejishusha na kuishi maisha ya walalahoi.

..binafsi siamini kama viongozi hawa waliishi maisha kama yetu walalahoi. lakini hata kama waliishi maisha kama yetu sidhani kama tunapaswa kuwasifia. mimi nilitegemea viongozi hao wangetuwezesha na sisi tuishi maisha mazuri kama wao kwa kutumia juhudi zetu.


NB:

..Kawawa alikuwa na makazi Kibamba, Madale, Bomba-mbili Songea, na Liwale. je huyu unaweza kumuweka ktk kundi la walalahoi?

..wakati wote alikuwa akitibiwa na madaktari bingwa pale Muhimbili tukianza na Prof.Philip miaka ya 80, na mwisho hapa Prof.Mwafongo. je, mama,baba,shangazi, na wajomba zetu, wanapata fursa za kupata matibabu ya kiwango alichokuwa akipata Rashidi Kawawa?

Ukishaitwa kiongozi basi kuna fringe benefits zinazoendana na cheo hicho. Sijawahi kusikia nchi yoyote duniani ambayo viongozi wake wanatazamiwa kutembea kwa mguu kwenda kazini!! Hiyo itakuwa nchi ya 'Kusadikika.!
 
Back
Top Bottom