"Mwaka 2000 wagombea 32 waliongoza katika kura za maoni za CCM, lakini ilibainika kuwa walikuwa wametumia pesa. Tulikuwa na njia kadhaa za kuthibitisha rushwa hiyo… Tulikuwa tukituma timu mbili au zaidi za kufanya uchunguzi, kila mmoja ikitoa ripoti ya siri inayojitegemea.
"Tulipobaini kuwa ripoti za timu zote zilikuwa zinafanana, ndipo tulipoamua kuwaengua wahusika. Wakati fulani tulilazimika kuchukua mtu wa nne katika kura za maoni, tukawaacha watatu. Wakati mwingine tuliamua kufuta matokeo na kura kurudiwa."
Anasema kwamba wakati mmoja mgombea mmoja wa Mkoa wa Dar es Salaam alibainika kuwa alitumia pesa ili kujipatia kura, lakini walipobaini kulikuwa na kasoro, ilibidi watume timu za kuchunguza. Waliridhika na ripoti za timu hizo, na ndipo wakaamua kumwengua.
"Lakini cha ajabu viongozi wakubwa kabisa katika chama, tukiwa kwenye kikao cha chama , wakasimama kidete kumtetea mtu aliyetoa rushwa. Ilikuwa bahati sana, kwamba tulimjulisha mapema mwenyekiti wetu Rais Benjamin Mkapa) kuhusu ripoti hizo. Pamoja na kutetewa kwa nguvu zote, Mwenyekiti akaamua mhusika aenguliwe.
Someni hapa jamani Mangula alijitahidi alipokuwa kiongozi..............
Mhhh kazi kwelikweli.Ninasoma hii habari nashindwa kuamini kuwa Mangula aliyesifia ushindi wa kishindo wa 2005 anagundua leo kuwa kuna rushwa ndani ya THITHIEMU na kuna wanamtandao,KWELI KAZI IPO.
Matendo yao majukwaani yanakuwa kinyume kabisa na pale wanapokuwa kwenye uchaguzi ndani ya chama. Matokeo yake, wanapoingia madarakani kwa njia za rushwa, wanashindwa kuikemea wakipata nyadhifa zao. Hii ni hatari, na sijui tufanye nini, na hasa pale wapiga kura wanapotaka rushwa kwa nguvu. Labda tutahitaji Sokoine (Edward) mwingine ili watu waziogope pesa hizo haramu, alisema Mangula akirejea kukithiri kwa vitendo vya rushwa katika uchaguzi ndani ya CCM unaohitimishwa wiki hii.
Huyu Mangula hivi angalichaguliwa angaliweza kuyasema haya? Maana kidogo napata kigugumizi cha kuelewa, watu tuliimba CCM ni mbovu lakini alikaa kimya na alishiriki katika mkakati wa kuiba kura zetu mwaka 2005.
Nakumbuka kugongana naye katika hotel moja ya kada mmoja wa CCM pale Moshi mwaka 2005. Tulikuwa floor moja na kwa kuwa walikuwa na special OP ilibidi awaulize mimi nilikuwa nani na kwa niko naye floor moja. Nikaitwa na wahudumu nikaombwa kuhama kwa kuwa alikuwa kalalamika na kwamba maofisa wa Serikali walikuwa floor ile. Nikasema nami walikuwa hawanijui na beside all the shit I was paying the same money as they did nikagoma.
Huyu Mzee nikakutana naye kwenye ngazi tena usiku ule akaniuliza nilitoka wapi bila ya hata salaam nikasema nilitokea nyumbani na nikamwacha hapo anajiuliza. Huyu hana lolote ni kisu kimemfika mfupani ndiyo maana anawaka.