Tunakusanya Kero ambazo ungependa zisemewe Bungeni na Nje ya Bunge na Viongozi wa CHADEMA

Status
Not open for further replies.
you must be from ARDHI UNIVERSITY!... WE SHALL REMEMBER YOU MWANAHARAKATI REGIA MTEMA!! rest in peace...!!
 
watanzania tunaelekea wapi viongozi wetu wanaenenda kama wamekatika vichwa mbona huu mgao wa umeme siuelewi ndo umeanza au unaishia? Hebu kawaulizie
 
Mifuko ya hifadhi hasa NSSF wahakikishe kuwa wanachama wao wanafaidika na michango wanayoitoa kwa kuwapatia mikopo, siyo kupeleka mabilioni ya wanachama wake kwa watu ambao wala hawajui pesa hizo zimetoka wapi, mfano kwa nini wafanyabiashara binafsi wanapewa mikopo na nssf lakini mwanachama hapewi?

Kwanini mabilioni ya wanachama yanapelekwa kwenye miradi hasa ya majengo wakati wanachama hawafaidiki? Hatutaki majibu ya longolongo kwani tumekuwa tukiahidiwa kwa zaidi ya miaka mi5 sasa wakati hatuoni utekelezaji.

Tunahitaji kufaidika na michango yetu sasa badala ya kusubiri "pensheni" ambayo unalipwa kiduuuuuchu miaka michache kabla ya kufa.

Upelekwe muswada Bungeni wa kurekebisha utendaji wa hii mifuko ya jamii. Kwanza haina utaratibu unaoeleweka wa kuwalipa mafao wanachama waliochangia mifuko hiyo. Pili tofauti ya malipo kati ya mfuko mmoja ni mwingine ni kubwa hasa ukiangalia kiwango cha mchango kila mwezi. Hiyo SSRA ifanye kazi kubwa kudhibiti mifuko hii maana wanafanya kila mfuko na lwake kwa gharama za watu maskini. Wanawanufaisha matajiri na wale waliochangia kubaki hoi. Huu ni wizi wa mchana kutwa. Lazima wabanwe watoe mafao yanayowawezesha waliochangia mifuko hiyo kunufaika na jasho lao. Mfuko wa PPF ndio unaongoza kwa wizi huu.
 
WC,Kilombero ina Wabunge 4,Vitimaalum 3, Suzan Kiwanga-CHADEMA,Getrude Lwakatare-CCM,Regia Mtema-CHADEMA na huyo mwingine wa Jimbo.
kero yangu ni juu ya kufeli kwa wanafunzi wa kidato cha pili hasa katika sekondari ya kibamba iliyopo katika manispaa ya kinondoni.Kwako Mh: Mnyika.
 
wanafunzi wanapofeli kwa kiasi kikubwa namna hii walimu waliohusika wawajibishwe. Hii ni hatari kwa taifa la kesho, ni afadhali walimu watangaze mgomo ijulikane kuliko kuwatendea watoto namna hii. (kwenu walimu kibamba sekondari)
 
USAFIRI WA UMMA KATIKA MIJI LIWE DARAKA LA SERIKALI KUU KUPITIA MANISPAA NA HALMASHAURI ZA MIJI AU MAJIJI. Serikali iwe tayari kutoa ruzuku kwa baadhi ya miji. Sekta binafsi imeshindwa.
 
Serikari itoe tamko juu ya Idara ya ukaguzi wa shule bado inaihitaji au haiitaji kwa maendeleo ya Elimu nchini.Idara hii iliyoanzishwa kisheria inapuuzwa na aithaminiwi.
 
nina vitu vichache
a) analiyelinda wanyama mfano tembo,chui,nyati nk analipwa ujira mdogo je afanyeje? maana maisha magumu mishahara kwa watu wa juu na wabunge tu je tunataka rasilimali za nchi hii ziishe? au ziendelee kuharibiwa kwa ugumu wa maisha?
b) anayelinda raia je ajitoeje mhanga kama akifa ndo mwanzo wa mateso ya familia yake? maana hakuna mfuko wala tasisi inayohangaika na waliokufa kwa ajili ya wengine na je serikali inampango gani wa kuwa na mfuko huo kwa ajili ya kusaidia watoto/wazazi/ndugu zao ambao jamaa/wazazi wao wamekufa kwa ajili ya wengine kuishi?
c) kuna maana gani kuendelea kuchimba madini kama hayana faida kwetu? asilimia tatu tu japo watasema kuwa kuna faida nyingi za uongo kwa vile wao wanahisa katika migodi hiyo
d) je wananchi wanaoishi karibu na migodi si watanzania maana wanauawa na wawekezaji na ikitokea wananchi wanalalamika hakuna hatua je wasemee wapi?
e) wawekezaji wameleta faida gani kwetu maana sehemu zote walikowekeza ni maumivu kwa wananchi waliokaribu badala ya kunufaika?
f)je serikali ina maana gani kukumbatia wawekezaji madhalimu tena kutumia askari wetu kuua wananchi wanaolalamika uonevu wa mwekezaji huyo?
g)Je kuna utaratibu upi unaotumika kwa wakuu wa wilaya/wakuu wa mikoa kushirikishwa katika kuonea wananchi maana kuna wakuu hao wameonekana wakiwatetea wawekezaji kama ni jamaa zao/au ndugu zao je hawalipwi au hawapewi rushwa na hawa wawekezaji ili kusaidia kuwaumiza wananchi waliokaribu na machimbo ya madini?
h) je wanyonge wakaishi wapi kama miji inapimwa inalipishwa gharama kubwa pasina kuzingatia uwezo wa wananchi eneo husika na je waende kuishi maeneo yapi? maana kila eneo sasa lina mtu, mapori yanazuiwa, kila sehemu mwekezaji
i) je inapodhihirika kuwa mtendaji wa serikali alidanganya je anachukuliwa hatua gani kama aliamua kuficha ukweli kwa kupewa hongo au kuahidiwa cheo na mfanyaji wa makosa?
j) je vyuoni wakuu wote ni miungu watu maana wanafukuza wanafunzi hata kwa kudai haki zao je wanyamaze hata wakinyimwa haki zao? na njia ya majadiliano wakuu hawa hawataki je wafanyeze kwa kupata haki yao?
k) ni lini ewura itaacha kudanganya bei elekezi? na ni lini itazingatia maoni ya wnyonge? maana nchi hii ya wafanyabiashara mlaji/asiye mfanyabiashara hana maana na hawampi chochote wa ewura ili kuwasaidia?
l) baadhi ya mamlaka zivunjwe hazina tija wala faida zaidi ya kuongeza mzigo kwa wananchi mfano EWURA,SUMATRA,TFDA,TBS, maana wanadanganya sana tena hawana aibu na hawana uzalendo kabisa wala huruma kwa wananchi wanyonge.
 
Regia mtema ebu peleka na hii ya kero za pantoni. kwa maelezo zaidi soma kwenye jukwaa la siasa sms yenye heading MAWAZO YAKINIFU KUHUSU KIVUKO (MV MAGOGONI NA MV KIGAMBONI)
Chonde Chonde fanya hivyo tafadhali.
 
Nina hoja;
Ni wazi kuwa miundo mbinu haswa barabara zinajengwa kwa gharama kubwa, itakuwa haina maana kama baada ya muda mfupi tu tutashuhudia zikibomaka na kurudi kule tuliko toka. Kwa akili ya kawaida haina maana kujenga barabara kisha kutokuwa na taratibu ya kuzitunza. Si ajabu ukipita mijini na haswa Dsm ukakuta barabara ya lami lakini imefunikwa na mchanga, mitaro ya maji ya mvua imefunikwa na tope. Ni lini tutakuwa na taratibu (SOP) za kutunza hizi barabara.
 
Mzazi kuna msemo wa kikrosto unaokwenda hivi toa kwanza boriti katika jicho lako kabla yakutoa kibanzi katika jicho la mwenzio CDM yenyewe ni kero hususani Makao makuu inabidi hiyo ofisi ihamwe kuwe na ofisi yenye hadhi sijui kama kuna huo mpango halafu kuwe na watumishi watendaji wasio wanasiasa na wabunge wasipewe portfolio nyingine ndani ya chama, kuna vichwa kibao mzazi hakunahaja ya mtu kuwa nanyadhifa mbili mbili kama mbunge na mkuu wa nidhamu bungeni na wakati huo huo msimamizi wa mambo ya katiba na sheria ; wanasiasa wasiwe watendaji kabisa mzazi
 
Nawakilisha:
Hakuna kitu kinachokera kama serekali kuwapuuzia wanataaluma ambao ndiowanatengeneza maofisa mbali2, mfano wanataaluma wanapandishwa vyeo lakinimshahara unakuwa wa kwenye barua ya promotion tu. Mtu huyo anaweza maliza threeyears, cheo kipya mshahara wa zamani. mbali na hilo, kodi ya kwenye hizi salaryslip ni too much jamani, mana bora ungeona nini kinachofanyika lakini hatahuelewi hii 30 percent inayokatwa kwenye mishahara yetu inakwenda wapi, mana nasitunapata uchungu na mambo ya ufisadi yalivyoenea tunakuwa tunahisi kodi zetundio zinaminywa, this is not health.
Kingine ni hizi fine za parkingmijini, yani kwangu mimi ni kero kubwa sana. kwanza sehemu nyingine hakunaalama ya no parking mijamaa ile inakuvizia tayari wanachain gari lako, halafuyani wanataja tu hela ya fine as if unalipa elfu mbili. This time tanzania kuwana gari is like kila mtu anataka kukukomoa. Jamani kuwe na utaratibu unaoelewekawapi haparuhusiwi kupark, na iwe visible, na pia hivi viwango vya fine hebuvitathminiwe upya mana the price is too high. Lastly, hizo hela watuwanazolipishwa faini zijulikane zinafanyiwa nini, mana manispaa zetuzinakusanya still mitaani kuchafu, makaro yamejaa takataka barabara mbovu,everything is like living in hell!!!Haya ni maoni yangu
 
watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu serikali inampango gani nao? na usiwe mpango wa maneno utekelezwe mara moja kwani wapo wenye vipaji vya hali ya juu kwa nini mbunge usijisikie vibaya kupata milo mitatu kwa siku wakati mtanzania mwenzako hata pa kunywa maji hana kwa kweli ni kero kubwa tutafute sababu za wao kuondoka nyumbani kwao na kukimbilia mtaani sio kuwapa majina ya ajabu na lawama bila kujua sababu ikiwezekana itungwe sheria itakayo wabana wazazi na walezi wanao sababisha watoto hawa kuingia kwenye mazingira haya tuwajengee ustawi wa jamii uwezo wa kushughulikia swala hili kwani ni kama hawapo wakati wanahusika moja kwa moja hili tatizo limegeuzwa biashara ni jukumu la serikali kuhakikisha mazingira bora ya raia wake. tusiifumbie macho kero hii ni hatari kwa taifa hawa tukiwaacha ndio mateja na majambazi wa baadae tuandae walinzi wa nchi wa baadae sio wabomoa nchi wajao naomba ulifikishe hili kwenye campaign mpaka helkopter zinaletwa tunashindwaje hili
 
kwanza mh regia mtema nakupongeza kwa thread hii.

Pili, napatwa na wasiwasi kama umeweza kuchukua maoni yote zaidi ya 100!!!

Kwa matumaini nawasilisha kero au mapendekezo haya hapa chini:-

a- nssf kukopesha wanachama wake. Unakuta nina akiba kwenye nssf kama 5 mil ila siwezi kukopa.

b- ardhi ni uti wa mgongo wa kilimo, na kilimo ni uti wa mgongo wa uchumi wa tanzania.kilimo hutoa ajira, kilimo hulisha nchi.

mimi nashangaa vigogo wanajimilikisha ardhi kama ekari 2000, 1000, 500, 200, 100 wakati wananchi wanatafuta sehemu ya kulima wanakosa. Rejea list ya mh mdee bungeni alivyowataja vigogo.

hapa tanzania kuna hekari nyingi sana zipo wazi, hazilimwi, na mtu akithubutu kulima anaambiwa mvamizi. Hivi kimsingi, je ardhi ya tanzania ni ya rais au ni ya wana wa nchi???

Pia kuna mashamba ya nafco na ranch kibao zipo idle.

Wawekezaji wanakuja wanapewa ardhi bwere ree ila wananchi hasa vijana hawana kimbilio.

Watanzania tupo gizani hatujui ardhi ya kulima itapatikanaje? Wizara ya ardhi, ofisi ya waziri mkuu zote hizo hawako wazi jinsi ya kupata ardhi.

Pia hata viwanja katika manispaa zetu ni ghali mno. Unakuta manispaa wanapima ardhi halafu wanauza zaidi ya million 5, je, wananchi wa hali ya chini na vijana wataweza kununua?

Sasa manispaa hizo hela wanapeleka wapi wakati ardhi ipo bure? Hawajanunua?

nasubiri kusikia hii hoja bungeni , pia ushauri wako ni mzuri, nasuburi mheshimiwa.

ardhi ipimwe kwa ada nafuu na wapewe wananchi kwa makazi bora na kilimo au ufugaji
 
Napata wakati mgumu kama rasilimali tulizo nazo zitatufaisha wananchi hasa wananchi wanaozunguka maeneo yenye machimbo. Kuna sehemu ndani ya tanzania yetu machimbo yanaendelea lakini wananchi hawajuwi wala Mbunge hajawahi kuzungumza na waliomchagua ili wajadiliane namna gani wanaweza kunufaika na uwepo wa mgodi ndani ya eneo lao baadala ya kushuhudia magari mazito yakibeba udongo na kuharibu barabara zao. Mfano halisi upo kata ya Isansa ambako kuna mgodi wa makaa ya mawe though wananchi hata hawajui na godfrey zambi amekaa kimya tokea aingie bungeni amefika isansa mara 2 mara zote kuomba kura. Jamani tusemeeni hl.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom