Wadau kwema?
Hivi wadau sisi kama binadamu wa karne ya 21 tumekubali kabisa CCM watutawale miaka 30+?Ujanja woteee tulio nao tumefeli miaka yote hiii? Kwanza naamini humu JF wapinzani ni wengi kuliko CCM, tunashindwa nini?
OK, kuna jibu moja ambalo liko popular miaka yote eti vijijini watu wengi hawajasoma wanajua bado nyerere anatawala na CCM yake,nakwambia si kweli.Nimezunguka vijiji vingi tena interior haswa wanajua Mbowe ni nani na Magufuli ni nani.
The main problem iko hapa:UCHAGUZI tunaibiwa.Tusipo kuwa makini tutakuwa ruled na CCM for another 30 years!tutakuwa ni watu wa kulalamika kimya kimya miaka yote hiii? Tazama leo tumepigwa nakos za uso huko Arumeru tumetulia tu as if we are in the 20th century. Damn!
Ajitokeze mtu hapa atuambie tunashindaje 2020 maana tunatofautiana kimawazo.Tuchukue hata awamu moja tukifeli basi warudi CCM.Ninachoamini mimi nchi ya kidemokrasia inayotawaliwa kwa miaka zaidi ya 30 na chama kimoja maana yake watu wa nchi hiyo bado ni wafungwa hawajawahi kuwa "nje ya box".
Unafikiri ni kwa nini wananchi wa marekani wanajiamini nchini kwao? Sababu wanajua mtawala atakapoleta ujinga atatoka for sure regardless of his /her political party.
Angalia sisi tulivyo waoga ni kwa sababu hatujawahi kuwajibisha utawala kwa kuweka madarakani chama kingine.Ikitokea hii utaona namna watanzania watakavyo kuwa confident.Tumekata tamaa, tumekata tamaa.Majuzi nilikuwa naongea na group la jamaa zangu fulani wanasema hata ufanyaje sa hv huwezi kubadili siasa ya CCM.
Ikishindikana kwa njia ya kura tunaweza kufanyaje? Wasomi tuambieni.Fikiria chama cha upinzani kimechukua nchi mizizi yote ya CCM toka 1970s hadi leo itakavyo wakost CCM kuing'oa kumsafishia ofisi mpinzani, CCM wakifikiria hilo wanachanganyikiwa ndio maana wanatumia nguvu kubwa.
Hivi sisi tuliopo JF,twitter, Facebook, Instagram, whatsapp etc hatuwezi kuwa chachu kwa wengine?
Ni aibu kwa kweli 30yrs+ bado tuko na chama kimoja?China wanaweza kuwa na justification ingawa ni chama kimoja leo ni second world economy.Tanzania ni economy ya ngapi? Mtu aliyekufa mwaka 80 akifufuka leo anamkuta CCM bado yupo.Tuna tabaka la vijana wengi waliosoma kuliko miaka mingine yote, tunafeli wapi? Tutafute muarobaini. Nipe mawazo yako alafu niambie hapa wewe ni MPINZANI au CCM niweke kura yako.
Tumechoka na CCM.