1000 digits
JF-Expert Member
- Oct 16, 2012
- 7,802
- 10,290
Heshima kwako!!Kuna sababu nyingi ambazo zinakifanya CCM iendelee kutawala hata miaka 40 ijayo. Nazo ni kama ifuatavyo.
1. Uoga wa watz. Yaan hawajazoea mambo ya vita na mshike mshike. Tofauti na nchi zingn kam za kiarabu
2. Ubinafsi na njaa. Kila mmoja anajijali na hutamani apate peke yake. Akishapata husahau wengne. Ndo maana utawaona watu kama Kitila Mkumbo, polepole, Mwita, etc
3. Ujinga na umaskini. Hivi vyote vinarandana. Mtu mjinga mara nyingi niaskini. Hatambui haki zake, na mustakabali mzima wa maisha yake. Na hajui chanzo cha matatizo yake. Akiambiwa kua tz bila ccm itakua na vita huamini hivo. Na umaskin hupelekea watu kujipendekeza na kua wasaliti.
4. Unafiki na kujipendekeza. Hii ndo kansa inayotutafuna. Apataye cheo husahau. Na hata wananchi waitwao wanyonge wanaonyesha unafiki wa wazi kwa kuimba ngojera za kusifu nana pia wakiwa ni watu wa kujikomba kwa wakubwa angalau aweze kupata mli na cheo.
5. Matabaka, utengano na udini. Hivi vinashbiana kwa ukaribu. Ukiskia huyu alieko madarakani kama ni dini flan basi atapigiwa makofi wakijinadi kua na sisi tumepata raisi. Huwez pata suppprt na kam ni kura atapta.
6. Ukabila na ukanda. Hii inaelekeana na no 5 ingawa utofauti wake ni pale unaposkia huyu katokea kanda flani na ni kabila flan. So utakuta anapifiwa kura na watu wengi wa kabila lake, regardless yy ni chama chake.
7. Upinzani dhaifu wenye unafiki ndan ake. Juzi CHADEMA wakaitiaha press kwenda kujitetea sakata la gari la CAG badili ya kujadili ubadhilifu uliobainishwa na CAG. Mtazame aliekua mgombea wa ACT 2015 alivokubali matokeo haraka ili apate cheo.
Mambo ni meng mda ni mchache
Hivyo vitu hapo juu vitayafanya madiliko ya kweli yachelewe kwa miongo kadhaa mbele mpaka pale kila mmoja atachoka na kunena kwa lugha moja, na hata pale ambapo mawe nayo yatachoka na kujiunga kwenye unenaji. Hapo mbuyu utaangushwa. Ila sio leo.
Ukombozi hakika unakaribia.
Uliyoyasema ndiyo hasa yanayofanyika nimekua nikijiuliza sana hivi haya watu wanayajua?.
Nimeona sasa watu wameanza kujua ukweli.
Hapo kwenye udini na Ukabila hua ni Janga kubwa sana.
Zito alifukuzwa Chadema kwa sababu ya udini na ukabila Lowasa alipigwa vita kwa sababu ya udini na ukabila.
Lipumba alipingwa kwa sababu ya udini.
Yani Tanzania hatuchagui au kuandaa kwa Sera hasa ndani ya Vyama?
Lakini pia tujiulize tunaitoa CCM na kuweka Chama kipi?
Mana vyote vinaongozwa kidikteta kuliko hata CCM.
Huwezi kuitoa CCM yenye pesa zote za Hazina na dola yote na nafasi zote za kugawa vyeo vyenye maslahi makubwa wakati huo huo tumeshindwa kumtoa kwenye uenyekiti mtu mmoja aliyefeli na kupata sifuri darasa la kumi na NNE anayeitwa Mbowe.
Tungewabadili kwanza Watu kama akina Mbowe kidemokrasia ndipo ingetokea nji sahihi ya kumpata Nabii wa kutuvusha.
Bado tunang'ang'ania kupanda kwa kutumia ngazi fupi isiyofika kwenye tawi la mti wa matunda.
Dawa ni kubadili ngazi na kuweka ngazi nyingine ndefu zaidi.
Bila Demokrasia ndani ya vyama hatutaweza kamwe kufikia Demokrasia ya kweli.
Ndio maana namchukia sana Mbowe mana amejenga mazingira Yale Yale ya CCM ndani ya Chadema na upinzani.
Kwa Sasa Juma Mwalimu anafaa kabisa kukabidhiwa Chama lakini ukabila utamnyima ,Heche anafaa sana lakini ukabila bado upo Chadema ya Mbowe.
Kuna ugumu gani kwa chadema kuweka katiba inayomshughulikia Mwenyekiti yeyote atakayechukua nafasi ya Mbowe kama ataonekana kupwaya?
Woga wa kumtoa Mbowe ndio uliojijenga kwa wananchi na kushinda kuitoa CCM.Wanaogopa vyama vingine.
Ukiangalia kwenye udini lazima ujiulize ,Je,Waislam waliokua wanaisema sana serikali ya CCM kuwa imejaa uonevu na inawaonea Waislam na kutowasikiliza malalamiko yao leo wako wapi?
Au wanasubiri ninic?
Kwa nini wasiendelee na harakati zao kama zilikua na nia njema?
Bila shaka walikua wanatumiwa na watu ndani ya au nje ya CCM ili kutafuta nafasi za kiutawala. Suala halikua ni dini bali madaraka.
Wakati Waislam walipokua wanalalamika Mara kwa Mara Kwa wakristo walisahau kuwa Kuna Tatizo kwenye katiba inayosababisha watu wanalalamika kutokana na watu wote kutegemea kutendewa hisani na Mtu mmoja as if he/ she is a living God anayegawa riziki.
Watu wakafikia mahali wanahesabu idadi ya wateuliwa kwa kuangalia dini badala ya uwezo wa mtu.
Yote hayo ni mifumo mibovu ya Katiba iliyoasisiwa na CCM na kuendelezwa kama Imani.
Kuna madhehebu wanaichukulia CCM kama Chama kilichoanzishwa na manabii na watakatifu toka mbinguni na hakistahili kunyima kura hata kama.
Hawa ni tatizo pia kwenye kuleta mabadiliko na kujenga Taifa la kidemokrasia linaloshindana kwa hoja za kimaendeleo badala ya kutafuta vyeo na maslahi.