Tunaitoaje CCM madarakani?

Tunaitoaje CCM madarakani?

Nakufananisha na wale wamisri ambao walikataa kwenda nchi ya ahadi wakayakumbuka yale masufuria na nyama walizokula kule utumwani Misri kwa Pharaoh.
Bora hata waturudishie Benjamin William Mkapa AMANI ya uhakika UCHUMI kwa wote serikali na kwa wananchi wote wanyonge kwa matajiri, serikali yenye hadhi, japo wanamlaumu kuhusu mashirika ya umma hii ilikuwa sera ya ulimwengu wote hata ulaya mashariki walikumbwa na hizo hasara za mashirika yao.
Tusione vibaya kumrudia mkapa kuliko tena kubahatisha bahatisha hata hao wapinzani akipata usijeshangaa kukumbana na matatizo makubwa zaidi watu hugeuka sio akisemacho ndicho.
Mzee Mkapa bado ana nguvu kwa kipindi hiki tz ilichokutana nacho kwangu mm BORA ZIMU LIKUJUALO. Mzee MKAPA the best solution.
 
Kama hatuwezi kufanya lolote kwa viongozi wetu tumewaachia tu watutawale basi hata kikibadilika chama sidhani kama hicho chama kitakachokuja kitakuwa na malaika,watu hawa hawa tu wanaonunuliwa ambao wengine mlikuwa mkiwategemea wangekuwa viongozi wa serikali endapo tungeiondoa ccm.
Katiba mpya ndio kila kitu .Trump mwenyewe na uzwazwa wake wote katiba inamnyoosha.
 
Ikitoka sisiemu kwa hiyo mnaweka chama gani?
Sababu ni wazi sio chadema, hawa ni majizi na wapiga dili na hawajui uongozi. Angalia wanavyoendesha chama chao kama saccos.
Zile billion 2 na ushehe nyinyi ndio mnajua sana kuzitumia ?
 
Waweke CHADEMA madarakani uendelee kulima nyanya.Tatizo nn?
Kwanini wewe shida yako hasa nini embu kuwa analitiko na sio mpiga majungu. Hoja yako DHAIFU sana, haina changamoto wala Vision. Weka mfano. So far JPM anafaa kwa mazingira yetu ya penda dezo. Embu tuambie chama gani sasa utakipa madaraka na sera zake katika mazingira yetu ya Tz. Tatizo tungeanza kudeal na Mentalität mbovu kama zako na watz wengi kuhisi chama au mtu ndo ataibadili Tz. Play your part, fanya kazi, lea watoto wako katika msingi wa utu na kujua umuhimu wa kufanya kazi hata kma kulima nyanya. Hakuna duniani nchi iliyofika juu kwa KUWA NA viongozi wa kucheka cheka na wananchi wapenda maneno mengi na mipasho. Soma historia njoo hapa tuambie. SIASA ZETU BADO NI ZA NITAPATA LINI NAFASI NILE. AND WALA ITS NOT ABOUT CCM ITS ABOUT ME AND YOU. HATA CCM NDANI WANAJIBADILISHA NA NYIE MNABAKI NA JINA BADALA YA KUANGALIA MATOKEO NA MAELEKEO. PAMBANISHA SERA ACHA MASIMULIZI YA VIBANDA VYA KAHAWA. TUONYESHE VISION YAKO.
 
CCM ni Tanzania na Tanzania ni CCM.
CCM ni masta wa siasa za Afrika na dunia yaani ni zaidi ya chama cha siasa.

Unataka kuiondoa halafu waongoze nani? Hawa ambao ruzuku za vyama vyao tu ni vita, wanaofukuzana kila leo, au hawa wanaosema wakipewa urais wataruhusu ushoga Tanzania????? Acha ulofa CCM for life
 
Wadau kwema?
Hivi wadau sisi kama binadamu wa karne ya 21 tumekubali kabisa CCM watutawale miaka 30+?Ujanja woteee tulio nao tumefeli miaka yote hiii? Kwanza naamini humu JF wapinzani ni wengi kuliko CCM, tunashindwa nini?
OK, kuna jibu moja ambalo liko popular miaka yote eti vijijini watu wengi hawajasoma wanajua bado nyerere anatawala na CCM yake,nakwambia si kweli.Nimezunguka vijiji vingi tena interior haswa wanajua Mbowe ni nani na Magufuli ni nani.
The main problem iko hapa:UCHAGUZI tunaibiwa.Tusipo kuwa makini tutakuwa ruled na CCM for another 30 years!tutakuwa ni watu wa kulalamika kimya kimya miaka yote hiii? Tazama leo tumepigwa nakos za uso huko Arumeru tumetulia tu as if we are in the 20th century. Damn!
Ajitokeze mtu hapa atuambie tunashindaje 2020 maana tunatofautiana kimawazo.Tuchukue hata awamu moja tukifeli basi warudi CCM.Ninachoamini mimi nchi ya kidemokrasia inayotawaliwa kwa miaka zaidi ya 30 na chama kimoja maana yake watu wa nchi hiyo bado ni wafungwa hawajawahi kuwa "nje ya box".
Unafikiri ni kwa nini wananchi wa marekani wanajiamini nchini kwao? Sababu wanajua mtawala atakapoleta ujinga atatoka for sure regardless of his /her political party.
Angalia sisi tulivyo waoga ni kwa sababu hatujawahi kuwajibisha utawala kwa kuweka madarakani chama kingine.Ikitokea hii utaona namna watanzania watakavyo kuwa confident.Tumekata tamaa, tumekata tamaa.Majuzi nilikuwa naongea na group la jamaa zangu fulani wanasema hata ufanyaje sa hv huwezi kubadili siasa ya CCM.
Ikishindikana kwa njia ya kura tunaweza kufanyaje? Wasomi tuambieni.Fikiria chama cha upinzani kimechukua nchi mizizi yote ya CCM toka 1970s hadi leo itakavyo wakost CCM kuing'oa kumsafishia ofisi mpinzani, CCM wakifikiria hilo wanachanganyikiwa ndio maana wanatumia nguvu kubwa.
Hivi sisi tuliopo JF,twitter, Facebook, Instagram, whatsapp etc hatuwezi kuwa chachu kwa wengine?
Ni aibu kwa kweli 30yrs+ bado tuko na chama kimoja?China wanaweza kuwa na justification ingawa ni chama kimoja leo ni second world economy.Tanzania ni economy ya ngapi? Mtu aliyekufa mwaka 80 akifufuka leo anamkuta CCM bado yupo.Tuna tabaka la vijana wengi waliosoma kuliko miaka mingine yote, tunafeli wapi? Tutafute muarobaini. Nipe mawazo yako alafu niambie hapa wewe ni MPINZANI au CCM niweke kura yako.
Tumechoka na CCM.
Tatizo la Tanzania ni Watanzania wenyewe msilaumu CCM wala Chadema.
 
CCM ni Tanzania na Tanzania ni CCM.
CCM ni masta wa siasa za Afrika na dunia yaani ni zaidi ya chama cha siasa.

Unataka kuiondoa halafu waongoze nani? Hawa ambao ruzuku za vyama vyao tu ni vita, wanaofukuzana kila leo, au hawa wanaosema wakipewa urais wataruhusu ushoga Tanzania????? Acha ulofa CCM for life
Eti ni masta wa siasa za Africa na dunia.Wachanicheke tu,hawa hawa wenye bunge dhaifu na wanaorudisha korosho ?
 
Narudia tena, sisemi kwamba ccm huwa haipati kura halali, bali wingi wa kura zake hutokana na mazingira yasiyo sawa katika ushindani. Iwapo mazingira yangekuwa kama tunavyoona Simba v/s Yanga, ccm ingekuwa nyepesi tu. Lakini kwa hivi sasa ccm ni taasisi ya kidola na sio chama cha siasa.
Hakuna anayekataa kwamba wakati mwengine ccm huwa wanacheza michezo michafu,hoja hapa ukiondoa hiyo michezo michafu bado ccm ana mtaji mkubwa tu wa kura hivyo tusihishie kusema tu kuwa ccm wanashinda kwa wizi bali pia lazima tukubali kwamba pamoja na yote hayo ccm bado ina watu wengi tu wenye kuipigia kura hadi leo.
Kwa maana hiyo huwezi kusema ccm inashindika tu kirahisi isipotumia nguvu,wakati mwengine watu wameshakariri tu kuwa ccm wanaiba kura hata pale wanaposhinda kiuhalali.
 
Siipendi CHADEMA kama ambavyo siipendi CCM ingawa napata matumaini kwa baadhi ya wanaccm kufanya vizuri ingawa wamezungukwa na wachafu wasio litakia mema Taifa hili labda tupate chama kipya chenye watu wapya wenye fikra pevu kulingana na matakwa ya kidunia.
 
Ivi mm niulize kipi ni bora kutoenda kabisa kupiga kura au kwenda kupiga nimeuliza ivi ili tuwekane sawa mwaka uliopita Wa uchaguzi watu wakijitokeza kwa wingi Sana lkn mwisho wake ni matokeo kuchakachuliwa na ccm ikashinda mm naona bora kutokwenda kwani hata tukienda bado uwezo wa kulinda kula haupo
 
tatizo sisi watanzania ni waoga sana,tukisikia hata sauti ya risasi moja tu kila mmoja anasambaratika,kingine pia upinzani bado hawana mikakati inayoeleweka mfano UKAWA
Tusipende kujiita sisi watanzania kwamba ni waoga. Huo ni uongo mkubwa sana. Hata hzi nchi za kiarabu tunazozitolea mfano kwamba wanafanya mabadiliko ya uongozi kwa njia za maandano ni kwa kupitia njia mojawapo ya hizi hapa:

1. Hao viongozi wao wanakuwa wamechokwa na western powers. Hivyo western powers wanawatumia (wanawaplant) watu
wao wa kusimaimia mazoezi hayo ya kuwaondoa watu madarakani kwa njia ya maandamano.
2. Au jeshi la nchi husika linakuwa limeshachoka kuisapoti serikali iliyoko madrakani hivyo linawaandaa watu wa kuongoza hayo
maandamano bila jeshi lenyewe kuhusika moja kwa moja lakini linajitokeza mwishoni kukamilisha zoez kwa kuchukua
madaraka japo kwa kipindi kifupi cha mpito
3. Au kuna viongozi shupavu wa upinzani wasio waoga ambao wako tayari hata kufa ambao hushawishi wananchi waliochoshwa na utawala ulioko madarakani ili kuandamana kushinikiza uongozi uliopo madarakani kuachia ngazi.

* HIVYO KWA POINT NO. 3 NI KWAMBA BADO HATUNA VIONGOZI JASIRI WA KUWEZA KUSHAWISHI NA KUONGOZA
MAANDAMNO KUDAI MABADILIKO YA UONGOZI WENGI WA VIONGOZI WA UPINZANI TZ NI WACHUMIA TUMBO,

WAOGA NA WANAFIKI WAKUBWA.
 
Hakuna anayekataa kwamba wakati mwengine ccm huwa wanacheza michezo michafu,hoja hapa ukiondoa hiyo michezo michafu bado ccm ana mtaji mkubwa tu wa kura hivyo tusihishie kusema tu kuwa ccm wanashinda kwa wizi bali pia lazima tukubali kwamba pamoja na yote hayo ccm bado ina watu wengi tu wenye kuipigia kura hadi leo.
Kwa maana hiyo huwezi kusema ccm inashindika tu kirahisi isipotumia nguvu,wakati mwengine watu wameshakariri tu kuwa ccm wanaiba kura hata pale wanaposhinda kiuhalali.

Mkuu ni hivi sio wakati mwingine, mahali popote ccm ilipo na ushindani wa kweli ni lazima ifanye hujuma na sasa ni za wazi. Na iwapo ingekuwa inategemea kushinda kihalali tu, leo hii isingekuwepo kwani vizazi vimebadilika, hilo moja. Na sasa hivi chini ya Magu ndio kabisa ccm inafanya hujuma za wazi kwenye box la kura.

Haya ninayokumbia sijahadithiwa bali nayaona kwa macho. Hiki kinachofanyika kwa sasa sio rafu kama tulizozoea huko nyuma bali ni ushenzi na ukatili. Sasa hivi watu wanafanyiwa ukatili wa wazi, na ni lazima kumtangaza mgombea wa ccm hata kama ameshindwa kwa uwiano mkubwa wa kura. Hapo achia mbali ukiukwaji mkubwa wa sheria toka kwa wasimamizi wa uchaguzi. Yaani sasa hivi kwenda kupiga kura ni kupoteza muda kwa yale yanayofanyika kwenye box la kura.

Nguvu pekee ya ccm ni madaraka ya mwenyekiti wa ccm anayoyapata kupitia katiba yenye mapungufu ambaye mara nyingi ni rais. Rais wetu kupitia katiba hii anapata nguvu kubwa ambayo imemlimbikizia madaraka ikiwemo kuwa juu ya vyombo vya dola na sheria. Hapa anaweza kuagiza chochote hata kilicho nje ya katiba na kikafanyika. Amri hizo za nje ya sheria na katiba huitwa amri toka juu, amri hii toka juu ina nguvu kuliko sheria na katiba, na yote haya yanachangiwa na mapungufu ya katiba iliyopo. Hapa tu ndipo ilipo nguvu ya ccm na sio Zaidi. Nasisitiza iwapo ccm italogwa ikakubali kushiriki uchaguzi huru na haki huku ikitegemea kushinda kihalali, ndani ya 10yrs rais hatatoka ccm. Na hata wao hilo wanalijua.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom