Tunaitoaje CCM madarakani?

Tunaitoaje CCM madarakani?

Walisheni na nyie huo ujuaji wenu wawachague,mtu wa miaka 18 siyo mtt anajua zuri na baya ati,ni maamuzi yao kuwanyima kura zao hakuna anayewashawishi bali wanajua nyie njaa ndiyo inawasumbua
Huu Ujinga ndiyo Mnawalisha watu wa Vijijini Ili Waogope Wawachague Upuuzi tu!
 
Kabla hujafikiria unaitoaje CCM madarakani ,jiulize CCM ikiisha toka madarakani atakayeingia madarakani ni nani na wa namna gani ?.
Tumeshuhudia wapinzani hao hao waliotegemewa na wananchi kwa misimamo yao thabiti wakiamia CCM na kuwaacha wananchi waliowapigia kura wakiduwaha haaaa!.
Baadhi ya walio wengi upinzani ni wale walio kuwa CCM wakakosa nafasi za uongozi au uteuzi ndani ya CCM au serikalini na hivyo kuelekea upinzani .
Kutambua huyu ndiye au huyu siye wa kuibadili CCM ni kitendawili kwani ni Watanzania wachache wenye uzalendo wa kweli wa tayari kufia nchi yao.
Tanzania ilikuwa nchi ya chama kimoja na usingeweza kupata elimu ya juu bila kupitia CCM, sasa ni nani unayeweza kumpata ambaye hakupitia CCM?
 
Kuna chama hakipati kura kwenye uchaguzi au huwa hazitoshi tu?
Point yangu ni kwamba hata ccm asipocheza michezo michafu kwenye uchaguzi bado kura anazopata kwa hao waigizaji ni nyingi huwezi kushindanisha na chama kama cha Hashim Rungwe huko,hivyo pamoja na yote yanayosemwa kuhusu ccm ila bado wana mtaji wa kutosha wa wapiga kura hadi leo.
 
So far hakuna kiongozi wa upinzani anayeonesha dalili ya kutumia njia hizo tunasubiri kupiga kura tutumbukie tena kwenye bwawa kama kawaida.
Nani anaweza kufanya hayo ikiwa mnaficha sura zenu hata humu jf sembuse hadharani?msidanganye watu
 
Bora hata waturudishie Benjamin William Mkapa AMANI ya uhakika UCHUMI kwa wote serikali na kwa wananchi wote wanyonge kwa matajiri, serikali yenye hadhi, japo wanamlaumu kuhusu mashirika ya umma hii ilikuwa sera ya ulimwengu wote hata ulaya mashariki walikumbwa na hizo hasara za mashirika yao.
Tusione vibaya kumrudia mkapa kuliko tena kubahatisha bahatisha hata hao wapinzani akipata usijeshangaa kukumbana na matatizo makubwa zaidi watu hugeuka sio akisemacho ndicho.
Mzee Mkapa bado ana nguvu kwa kipindi hiki tz ilichokutana nacho kwangu mm BORA ZIMU LIKUJUALO. Mzee MKAPA the best solution.
 
Kama hatuwezi kufanya lolote kwa viongozi wetu tumewaachia tu watutawale basi hata kikibadilika chama sidhani kama hicho chama kitakachokuja kitakuwa na malaika,watu hawa hawa tu wanaonunuliwa ambao wengine mlikuwa mkiwategemea wangekuwa viongozi wa serikali endapo tungeiondoa ccm.
 
Ikitoka sisiemu kwa hiyo mnaweka chama gani?
Sababu ni wazi sio chadema, hawa ni majizi na wapiga dili na hawajui uongozi. Angalia wanavyoendesha chama chao kama saccos.
 
Kwanini wewe shida yako hasa nini embu kuwa analitiko na sio mpiga majungu. Hoja yako DHAIFU sana, haina changamoto wala Vision. Weka mfano. So far JPM anafaa kwa mazingira yetu ya penda dezo. Embu tuambie chama gani sasa utakipa madaraka na sera zake katika mazingira yetu ya Tz. Tatizo tungeanza kudeal na Mentalität mbovu kama zako na watz wengi kuhisi chama au mtu ndo ataibadili Tz. Play your part, fanya kazi, lea watoto wako katika msingi wa utu na kujua umuhimu wa kufanya kazi hata kma kulima nyanya. Hakuna duniani nchi iliyofika juu kwa KUWA NA viongozi wa kucheka cheka na wananchi wapenda maneno mengi na mipasho. Soma historia njoo hapa tuambie. SIASA ZETU BADO NI ZA NITAPATA LINI NAFASI NILE. AND WALA ITS NOT ABOUT CCM ITS ABOUT ME AND YOU. HATA CCM NDANI WANAJIBADILISHA NA NYIE MNABAKI NA JINA BADALA YA KUANGALIA MATOKEO NA MAELEKEO. PAMBANISHA SERA ACHA MASIMULIZI YA VIBANDA VYA KAHAWA. TUONYESHE VISION YAKO.
So far hakuna kiongozi wa upinzani anayeonesha dalili ya kutumia njia hizo tunasubiri kupiga kura tutumbukie tena kwenye bwawa kama kawaida.
 
Kwanini wewe shida yako hasa nini embu kuwa analitiko na sio mpiga majungu. Hoja yako DHAIFU sana, haina changamoto wala Vision. Weka mfano. So far JPM anafaa kwa mazingira yetu ya penda dezo. Embu tuambie chama gani sasa utakipa madaraka na sera zake katika mazingira yetu ya Tz. Tatizo tungeanza kudeal na Mentalität mbovu kama zako na watz wengi kuhisi chama au mtu ndo ataibadili Tz. Play your part, fanya kazi, lea watoto wako katika msingi wa utu na kujua umuhimu wa kufanya kazi hata kma kulima nyanya. Hakuna duniani nchi iliyofika juu kwa KUWA NA viongozi wa kucheka cheka na wananchi wapenda maneno mengi na mipasho. Soma historia njoo hapa tuambie. SIASA ZETU BADO NI ZA NITAPATA LINI NAFASI NILE. AND WALA ITS NOT ABOUT CCM ITS ABOUT ME AND YOU. HATA CCM NDANI WANAJIBADILISHA NA NYIE MNABAKI NA JINA BADALA YA KUANGALIA MATOKEO NA MAELEKEO. PAMBANISHA SERA ACHA MASIMULIZI YA VIBANDA VYA KAHAWA. TUONYESHE VISION YAKO.
Kasome historia ya Singapore na Malaysia ndiyo utajua kwa nini kwa hizi siasa za CCM, hatuwezi kufika popote.

Failure of the organization is failure of the management.

Tanzania tumeshindwa kupiga hatua kuelekea kwenye maendeleo ya kweli kutokana na kuukosa uongozi unaofaa. CCM wanajua, Rais anajua, na kila mwenye akili anajua.

Kama tungekuwa na viongozi wenye upeo, dhamira, utashi, hekima na uzalendo, wangeruhusu mifumo ya demokrasia na utawala bora vifanye kazi ili siku moja tuwapate viongozi wenye uwezo wa kuwaongoza Watanzania katika njia iliyo sahihi ya kuyafikia maendeleo yanayohitajika.

Hakuna nchi iliyowahi kuendelea kwa kuwa nq utawala wa kimabavu au kidikteta. Watu wanaitaja China, nchi ambayo kwa miaka mingi watu wameishi kwenye umaskini mkubwa, walisaidiwa tu na uwingi wa watu na ukubwa wa nchi kuweza kutekeleza miradi mikubwa lakini maisha ya mwananchi mmoja mmoja yakiwa duni kabisa.

Kuanzia miaka ya 2000 mpaka sasa, China imepiga hatua kubwa, nayo ni baada ya kubadilisha sera zake nyingi, na hivyo kuvutia uwekezaji mkubwa wa mataifa ya nje. Bila huo uwekezaji, China bado ni duni. Na China haiwezi kukubali kuondoa uwekezaji wa nje, ndiyo maana hata Rais wao mara nyingi yupo Ulaya na America kutafuta uwekezaji.

China, kila mwaka inapata uwekezaji wa nje unaofikia dola bilioni 70. Leo, sisi kwa kukosa uongozi wenye uelewa na maono tunaamini kuwa China ndiyo itakayofanya uwekezaji mkubwa nchini mwetu.

Katika Dunia nzima, mitaji mikubwa ya uwekezaji ipo America, Europe na Australia. Ni uwekezaji mkubwa kutoka mabara hayo, ndio ulioibadilisha South Korea, Brazil na China. Huo ndiyo ukweli, upende au uchukie.
 
Point yangu ni kwamba hata ccm asipocheza michezo michafu kwenye uchaguzi bado kura anazopata kwa hao waigizaji ni nyingi huwezi kushindanisha na chama kama cha Hashim Rungwe huko,hivyo pamoja na yote yanayosemwa kuhusu ccm ila bado wana mtaji wa kutosha wa wapiga kura hadi leo.

Naomba nikusisitizie, iwapo ccm itashiriki uchaguzi katika uwanja ulio sawa, haina uwezo wa kupata zaidi ya 55% ya kura za urais, wabunge au madiwani. Iwapo itakuwa na idadi hii haiwezi kupitisha wala kutunga sheria zenye maslahi kwa chama chao. Na huo ni msimu mmoja kwa idadi hiyo na msimu unaofuata haitapata juu ya 50% kwenye kiti chochote. Huu wizi wa kura, ukatili na unyama wakati wa uchaguzi kwa kushirikiana na tume ya uchaguzi na vyombo vya dola ni juu ya hofu hii ya kutokukubalika. Kama una amini wanauwezo huo au wanakubalika sana, washawishi wafuate huu ushauri wako uone kama ccm haijaifuata KANU ya Kenya kaburini.
 
Ikitoka sisiemu kwa hiyo mnaweka chama gani?
Sababu ni wazi sio chadema, hawa ni majizi na wapiga dili na hawajui uongozi. Angalia wanavyoendesha chama chao kama saccos.

Chama chochote kinaweza kuendesha nchi hii maana hakuna standard iliyowekwa ya kufikia, bali kila mtu anaamua akitakacho. Angalia enzi za Nyerere aliongoza kwa mitazamo yake tukaishia kuvaa viraka. Akaja Mwinyi akaruhusu alivyoruhusu muda wake ukaisha. Akaja Mkapa akaboresha alichoweza, yeye akauza viwanda vyote kwa bei ya chuma chakavu, akabinafsisha mpaka benki huku Nyerere akibaki analialia. Akaingia mtoto wa mjini naye akafanya yake, aliyepiga akapiga, aliyeliwa naye akaliwa.

Sasa hivi yupo Nabii Magufuli, huyu kaingia na gia kubwa mpaka kila mtu kageuka mwendawazimu akitegemea muujiza wa nchi kupaa. Saa hii amekata pumzi, anapika data za uchumi kama hana akili nzuri, hamadi amekamatika na wanaojua uchumi IMF, saa huu kaishia kuficha data kwa kichaka cha vita vya kiuchumi. Kichekesho mkaguzi wa mahesabu ya umma anawekewa mizengwe waziwazi, huku ofisi yake ikiwa ni sehemu ya matumizi yenye utata ya fedha za umma! Sasa nchi ya hivyo ni chama gani kitashindwa kuendesha? Mtu yoyote mwenye akili timamu anaweza kuongoza nchi huu kwa kutumia neno moja tu Amani basi.

Cc:Misuli, jingalao, jmc06, paskali mayalla, sophist, Phillipo Bukililo
 
Naomba nikusisitizie, iwapo ccm itashiriki uchaguzi katika uwanja ulio sawa, haina uwezo wa kupata zaidi ya 55% ya kura za urais, wabunge au madiwani. Iwapo itakuwa na idadi hii haiwezi kupitisha wala kutunga sheria zenye maslahi kwa chama chao. Na huo ni msimu mmoja kwa idadi hiyo na msimu unaofuata haitapata juu ya 50% kwenye kiti chochote. Huu wizi wa kura, ukatili na unyama wakati wa uchaguzi kwa kushirikiana na tume ya uchaguzi na vyombo vya dola ni juu ya hofu hii ya kutokukubalika. Kama una amini wanauwezo huo au wanakubalika sana, washawishi wafuate huu ushauri wako uone kama ccm haijaifuata KANU ya Kenya kaburini.
Mkianza kuizungumzia hiyo ccm utasema hata kampeni haifanyi wala hazina athari kwao wao wanategemea wizi wa kura tu,akishinda mbunge wa upinzani haki imetendeka ila akishinda wa ccm basi wameiba kura.
 
Mkianza kuizungumzia hiyo ccm utasema hata kampeni haifanyi wala hazina athari kwao wao wanategemea wizi wa kura tu,akishinda mbunge wa upinzani haki imetendeka ila akishinda wa ccm basi wameiba kura.

Narudia tena, sisemi kwamba ccm huwa haipati kura halali, bali wingi wa kura zake hutokana na mazingira yasiyo sawa katika ushindani. Iwapo mazingira yangekuwa kama tunavyoona Simba v/s Yanga, ccm ingekuwa nyepesi tu. Lakini kwa hivi sasa ccm ni taasisi ya kidola na sio chama cha siasa.
 
watanzania hatuna haja ya kuitoa ccm, bali tunataka serikali bora inayopatikana CCM
 
Tatizo hakuna Chama Mbadala!! Sasa niambie tuiondoe CCM tuweke chama gani? Chadema??!! Kama ruzuku tu imewaishinda sembuse nchi!! Si watakopeshana raslimari zetu zote!!?? Halafu nani anaweza kutuongoza huko kwenye chama mmbadala? Mbowe, Lema, Msigwa? Hatufanyi majaribio. Tusubiri kikipatikana chama mmbadala na ninafikiri kitatoka ndani ya CCM na sivinginevyo!
Tutatengeneza katiba mpya hii itatusaidia wakibolonga CHADEMA nao tutawatoa. Kwani uimara wa chama ni nini?ni Fedha. Tutachanga. Chama kimekaa madarakani miaka karibia 40 kitaacha kuwa imara?
 
Wewe unafaidi nini ? Absolutely nothing. You enjoy your poverty of mind.
hahahahaha jomba naona umelewa amani..umechoka na ccm sasa unataka utuletee mafisadi yenu...nendeni zenu.kule..wacha ccm itawale hata. milele..kama inatuletea maendeleo tatizo lako nini...yaani shida yako.unataka zamu tu ya kula baaasi..unaona wenzio wanafaidi。ni wakati wao.wacha wafaidi lakini wanaendelea kipiga kazi sana..mtasubiri sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom