Tunahitaji nini, maarifa ya mtu, cheti au jina?

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,852
141,786
Mr X ana maarifa lakini hana cheti, Mr Y ana cheti lakini hana maarifa na Mr Z ana maarifa na cheti lakini jina ni la mwanakijiji mmoja std seven anayechunga huko kijijini.Ili taifa liendelee na kusonga mbele tunamuhitaji nani na yupi haitajiki kati ya X,Y na Z?Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni.Jioni njema!
 
Ni vizuri tukawa wakweli, kama mtu Jina sio lako basi sema Jina sio langu na nililipata kwa njia hii. Mbona yule Jidulamabambase alikuwa akisema wazi kuwa alirudia shule na Jina lililoko kwenye vyeti ni lile alilotumia kurudia.

Tunahitaji watu wenye maadili kabla ya kuangalia vyeti au ujuzi.
 
Mr X ana maarifa lakini hana cheti, Mr Y ana cheti lakini hana maarifa na Mr Z ana maarifa na cheti lakini jina ni la mwanakijiji mmoja std seven anayechunga huko kijijini.Ili taifa liendelee na kusonga mbele tunamuhitaji nani na yupi haitajiki kati ya X,Y na Z?Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni.Jioni njema!
Ukiijua kweli itakuweka huru. Kweli ni X, Y au Z?
 
Cheti kina certify kwamba anayekimiliki,ndio mmiliki wa maarifa yaliyomo ndani ya cheti,

Ili uhalali upatikane lazima umfahamu kwa jina anayeyamiliki taarifa hayo,sio jina la cheti ni juma maharage,halafu cheti hicho kinachukuliwa na haruna mapumba,halafu haruna mapumba akiwasilishe mbele ya mamlaka na kukiombea kazi.

Ni kosa la jinai,na anatakiwa ashtakiwe na kurudisha mishahara yote aliyopokea
 
Labda ungeanza kutuambia kiwango chako cha elimu kisha utuambie maana ya "academic qualification" katika soko la ajira.Hivi kwa nini wanapoguswa miungu wenu huwa mnatafuta kila fursa za kuhalalisha upuuzi wao?

Kila position ya ajira/utumishi ina academic qualification zake,hata huyo aliyefoji cheti cha Elimu anafahamu umuhimu wa Elimu,isipokuwa amekosa uwezo wa kiakili wa kumuwezesha kuifikia ngazi ya kielimu anayoitamani na ndiyo maana alikwapua cheti cha watu ili walau aonekane ana sifa.

Imeandikwa kuwa "utakula kwa jasho lako", kwa nini tunapohoji mtu anayetumia vyeti vya mtu mwingine kujipatia ridhiki/uongozi kwa njia haramu iwe nongwa?Sheria ichukue mkondo wake,kila mtu awe pale alipo kwa njia sahihi na si kwa mbeleko ya kufoji vyeti,kufunga watu viatu na kujipendekeza.

Acha kujitoa ufahamu,unawakumbuka maelfu ya vijana wa UDOM waliofukuzwa chuoni kwa kile tulichoambiwa hawakuwa na sifa stahiki?Kwa nini leo tuwaruhusu vihiyo kushika nyadhifa kwa vyeti vya kughushi.
 
Kama wewe ni kiongozi unaongoza na wapinzani wanakufurahia, basi rudi nyuma na uangalie ulipokosea. Kama unaongoza na wapinzani wanapiga kelele, basi ujue unapatia kwenye uongozi wako.- by John Pombe Magufuli (president of Tanzania)
 
Labda ungeanza kutuambia kiwango chako cha elimu kisha utuambie maana ya "academic qualification" katika soko la ajira.Hivi kwa nini wanapoguswa miungu wenu huwa mnatafuta kila fursa za kuhalalisha upuuzi wenu?

Kila position ya ajira/utumishi ina academic qualification zake,hata aliyefoji cheti cha Elimu anafahamu umuhimu wa Elimu,isipokuwa amekosa uwezo wa kiakili wa kumuwezesha kuifikia ngazi ya kielimu anayoitamani na ndiyo maana alikwapua cheti cha watu ili walau aonekane ana sifa.

Imeandikwa kuwa "utakula kwa jasho lako", kwa nini tunapohoji mtu anayetumia vyeti vya mtu mwingine kujipatia ridhiki/uongozi kwa njia haramu iwe nongwa?Sheria ichukue mkondo wake,kila mtu awe pale alipo kwa njia sahihi na si kwa mbeleko ya kufoji vyeti,kufunga watu viatu na kujipendekeza.

Acha kujitoa ufahamu,unawakumbuka maelfu ya vijana wa UDOM waliofukuzwa chuoni kwa kile tulichoambiwa hawakuwa na sifa stahiki?Kwa nini leo tuwaruhusu vihiyo kushika nyadhifa kwa vyeti vya kughushi.

Kuwapiga wanaomzidi umri n.k

Tafsiri ya Chama Cha Majambazi inaelekea kuwa kweli
 
Mr X ana maarifa lakini hana cheti, Mr Y ana cheti lakini hana maarifa na Mr Z ana maarifa na cheti lakini jina ni la mwanakijiji mmoja std seven anayechunga huko kijijini.Ili taifa liendelee na kusonga mbele tunamuhitaji nani na yupi haitajiki kati ya X,Y na Z?Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni.Jioni njema!
the end justifies the means, huh?

yeah right.

embu angalia hizi mifano hai....

1. wanaoishi kwa ujambazi / uhalifu utakuta wana maisha mazuri kuliko waishio kwa lawful means. kwa hiyo uhalifu ni halali, siyo?

2. siku hizi nyumba nyingi nzuri za ibada zinajengwa kwa fedha chafu. ukiona nyumba ya ibada ipoipo tu, angalia vyanzo vya kipato cha waumini wake. kwa hiyo hela chafu ni halali kwa sababu zimejenga nyumba nzuri za ibada, siyo?

nk, nk.

let me rest my case....
 
Mr X ana maarifa lakini hana cheti, Mr Y ana cheti lakini hana maarifa na Mr Z ana maarifa na cheti lakini jina ni la mwanakijiji mmoja std seven anayechunga huko kijijini.Ili taifa liendelee na kusonga mbele tunamuhitaji nani na yupi haitajiki kati ya X,Y na Z?Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni.Jioni njema!
hii inaletwa sasa? hapo nyuma uliongelea?
 
Mr X ana maarifa lakini hana cheti, Mr Y ana cheti lakini hana maarifa na Mr Z ana maarifa na cheti lakini jina ni la mwanakijiji mmoja std seven anayechunga huko kijijini.Ili taifa liendelee na kusonga mbele tunamuhitaji nani na yupi haitajiki kati ya X,Y na Z?Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni.Jioni njema!
kama ungekua unaelewa maana ya elimu usingesema Mr. Y hana maarifa na pengine pia hujui maana ya maarifa nini? mtu azaliwi na maarifa. Utashi unapo ongezewa elimu maana yake mtu huyo anakua na uwezo mkubwa zaidi kupata maarifa kuliko X na huyo mpuuzi Z anaedanganya. mfano ukimuajiri mr z kitakachotokea utamwamini anauwezo wa kupata maarifa kutimiza majukumu yake hivyo hutawaza kumfua kila mara kama ambavyo ungefanya kama ungemwajiri mtu amabae hana elimu kabisa... shida sana kufanyakazi na mtu mwenye cheti feki na aliye bweteka na kuona elimu isingemsaidia sana ktk kazi zake kwani anaziweza tu, ni tabu sana!
 
Back
Top Bottom