Tunahitaji mjadala wa Mabadiliko ya Elimu. Maprofesa watatupiga na kitu kizito tusipokuwa makini

ego

JF-Expert Member
Apr 10, 2013
1,620
1,407
Watanzania wamepiga kelele we mara wakateuliwa maprofesa kushika Wizara ya Elimu na wakatueleza tutulie mabadiliko yako yanafanyiwa kazi.

Niseme kitu kimoja " Sijawahi kuwaamini maprofesa wetu", nahisi watastup[iga na kitu kizito.

Nimefuatilia michango ya maprofesa wetu mpaka juzijuzi hapa wametufanyia utafiti wa chanzo cha uchafuzi mto mara na kuzua taharuki.

Natabiri watajifungia na wakiibuka wataibuka na kuingiza elimu ya kushona, ujenzi, ufundi umeme, ufundi magari, kilimo kwenye mitaala ya elimu ya msingi.

To be honest only a layman asiyestahili hata kuongoza familia yake ndiye anayeweza kuibuka na mapendekezo ya kuingiza elimu ya ufundi au skills kwenye mitaala kama utatuzi wa changamoto zetu.

Msomi yoyote aliyeelimika ataanzia kujiuliza hivi changamoto za wastanzania ni nini?

1. Je, Jamii inakosa vijana wenye skills ----- Hapana vijana wapo wengi tu wanaofundishwa mitaani, wanaotoka vyuo vya veta, SIDO = hivyo skills siyo tatizo

2. Nini Changamoto ya vijana wenye skills ----- wengi wanalamikia ajira, kijana mmoja anajifunza kuchomelea anakosa ajira, anajifunza kushona anakosa ajira, anajifunza ujenzi na bado unakuta anaishi kwa kubaingaiza akiwa na taaluma zaidi ya mbili = Tatizo ni maarifa ya kuwawezesha kujiajiri

3. Je, Jamii inakosa wasomi wenye elimu ya juu ---- hapana vyuo vikuu na vya kati vinavyotoa vyeti, shahada na astashahada vimekuwa vingi

4. Je, nini changamoto kwa hawa wasomi wa elimu ya juu ---- Wengi changamoto kwao ni ukosefu wa ajira na umakini katika kutekeleza majukumu ya taaluma zao

Kwa kifupi chgangamoto kubwa kwa jamii nzima

1. ukosefu wa ajira baada ya kuhitimu taaluma zao

2. Ukosefu wa umakini

3. Ukosefu wa maadili hasa kwenye eneo la uaminifu

4. ..............

Mabadiliko katika mitaala yalenge kutatua changamoto zetu. Kama shida ya watanzania wengi ni kukosa ajira na kushindwa kujiajiri basi elimu muhimu kwa ajili ya ujasiliasmali iingizwe.

Watu wafundishwe kubaini fursa zilizowazunguka, watu wafundishwe nidhamu za ujasiliamali kama kujizuia vitu vya anasa kudunduliza mtaji, kumtumikia mtu ili upate ujuzi na mtaji, jinsi ya kufanya kazi na taasisi za mikopo, namna ya kutafuta masoko na bidhaa au huduma, uaminifu katika kutoa huduma, jinsi ya kubuni wazo la biashara kama ni kuzalisha kwa kubuni, kukopi au kuuza bidhaa za wengine.

Jamii ifundishwe namna ya kuingia Joint venture, miiko ya venture, majukumu ya pande zote. hapa nitoe ufafanuzi kwamba unakuta mtu yuko ofisini na anatamani kufanya kilimo hana mda lakini anaweza kupata mtaji.

Kuna kijana amekosa ajira ana mda wa kulima lakini hawa hawaji pamoja na kukubaliana kuingia ubia ili walime kwa pamoja.

Mwenye mtaji anatamani ampate kijana wa kumtumikia bure na kijana hayuko tayari kubeba maono ya wengine.

wanabaki kuogopana na wote kushindwa kuingia ubia wenye tija kwa wote.

Tunataka jamii ya kesho kila mwana jamii aone ubia kama fursa, ajue akihitaji mbia siyo kwa ajili ya kumnyonya au kumwibia.

Hawa wote wajue namna ya kufuatilia shughuli zao na wajue kuna changamoto na wawekwe tayari kuzitatua.

Wote wajue namna gani wanaweza kutumnia taasisi za mikopo kuendeleza shughuli zao.

Ila wasije kutwambia kutatua changamoto zetu ni kwamba kila mtanzania akimaliza darasa la saba ajue taaluma ya ushonaji, this will be nonsense, kujua kushona kutamsaidiaje mhitimu aliyemaliza chuo kikuu akakosa ajira?

Nani kawaambia ufundi cherehani ni taaluma ambayo kila mwenye ujuzi atapata ajira na apate ujira. ni vijana wangapi wako mtaani leo wamesoma cherehani na hawana ajira.

Mabadiliko ya elimu yanatakiwa ku add value kwenye elimu yetu ili kila mmoja kile alichojifunza kifanye kazi na siyo kuongeza ujuzi wa kipuuzi ambao hauna guarantee ya ajira.

Tunahitaji watu wetu wawe creative, wawe na focus ya kuona fursa kwenye jamii, wawe na nidhamu za kikazi na kijasiliamali n.k

Waache kujifungia na kufanya mambo mpaka yaishe alafu ndiyop waibuke na mambo ambayo hata kama wamebuni ugoro watakaa kuyatetea ili waonekane wamefanya bora.

Walete mjadala jamii ijadili ni kitu wanakitaka katika mabadiliko ya elimu, wao wapendekeze baadhi na mjadala wa jamii utasaidia kuongeza na kupunguza.
 
Watu wafundishwe kubaini fursa zilizowazunguka, watu wafundishwe nidhamu za ujasiliamali kama kujizuia vitu vya anasa kudunduliza mtaji, kumtumikia mtu ili upate ujuzi na mtaji, jinsi ya kufanya kazi na taasisi za mikopo, namna ya kutafuta masoko na bidhaa au huduma, uaminifu katika kutoa huduma, jinsi ya kubuni wazo la biashara kama ni kuzalisha kwa kubuni, kukopi au kuuza bidhaa za wengine.
We jamaa ni chuo gani hakifundishi hayo uliotaja?
Vyuo vipi TZ havifundishi elimu ya ujasiliamali ?
Wewe na maprofesa nani anajua zaidi?
Yani Jopo la maprofesa na wabobezi waliosoma nchi mbalimbali na kufanya kazi sehemu mbali mbali hawajui kitu kuliko wewe ambae hata hatujui wasifu wako ?
Ungekuwa unapotential serikali ingekuita uwasaidie ila hujulikani wala huna cha kuthibitisha ila porojo.
Umewahi fanya tafiti yoyote, au umeandika kitabu nikarejee maandiko yako ?
Yani sisi tukubaliane na common sense zako tuache kuwasikiliza watafiti wetu waliondaliwa kwa muda mrefu na waliofanya tafiti nyingi!
Huu ujinga uliouandika ufute !
Tumeshuhidia mabadiriko makubwa sana ktk awamu ya 5 kwa sababu ya kuwaamini wasomi, Magu jambo moja alilofanya ni kuwaamini wasomi na vijana na kuwandoa vihio.
Waache wasomi watengeneze dira, watakopokosea utawakosoa warekebishe sio kuwapa maksi 0 ni ujinga!
Haya mambo unayoandika ulijifunza mwemyewe tangu uzaliwe !
Huna adabu we mtoto, nakukemea kama baba, wewe unaonesha hata wazazi wako unawadharau.
Maprofesa ni kama wazazi wetu, wanajua kila kitu kuhusu Tanzania, koma we!
Usichanganye maprofesa na wanasiasa, nchi inakwamishwa na wanasiasa sio maprofesa.
Wewe hujui hata tatizo letu lilipo.
Nakwambia hata wewe mtanzania ni sehemu ya tatizo usitafute kisingizio.
Profesa kakupa elimu, wewe unashindwa kuitimia halafu unamlaumu ?
 
We jamaa ni chuo gani hakifundishi hayo uliotaja?
Vyuo vipi TZ havifundishi elimu ya ujasiliamali ?
Wewe na maprofesa nani anajua zaidi?
Yani Jopo la maprofesa na wabobezi waliosoma nchi mbalimbali na kufanya kazi sehemu mbali mbali hawajui kitu kuliko wewe ambae hata hatujui wasifu wako ?
Ungekuwa unapotential serikali ingekuita uwasaidie ila hujulikani wala huna cha kuthibitisha ila porojo.
Umewahi fanya tafiti yoyote, au umeandika kitabu nikarejee maandiko yako ?
Yani sisi tukubaliane na common sense zako tuache kuwasikiliza watafiti wetu waliondaliwa kwa muda mrefu na waliofanya tafiti nyingi!
Huu ujinga uliouandika ufute !
Tumeshuhidia mabadiriko makubwa sana ktk awamu ya 5 kwa sababu ya kuwaamini wasomi, Magu jambo moja alilofanya ni kuwaamini wasomi na vijana na kuwandoa vihio.
Waache wasomi watengeneze dira, watakopokosea utawakosoa warekebishe sio kuwapa maksi 0 ni ujinga!
Haya mambo unayoandika ulijifunza mwemyewe tangu uzaliwe !
Huna adabu we mtoto, nakukemea kama baba, wewe unaonesha hata wazazi wako unawadharau.
Maprofesa ni kama wazazi wetu, wanajua kila kitu kuhusu Tanzania, koma we!
Usichanganye maprofesa na wanasiasa, nchi inakwamishwa na wanasiasa sio maprofesa.
Wewe hujui hata tatizo letu lilipo.
Nakwambia hata wewe mtanzania ni sehemu ya tatizo usitafute kisingizio.
Profesa kakupa elimu, wewe


kuitimia halafu unamlaumu ?

We jamaa ni chuo gani hakifundishi hayo uliotaja?
Vyuo vipi TZ havifundishi elimu ya ujasiliamali ?
Wewe na maprofesa nani anajua zaidi?
Yani Jopo la maprofesa na wabobezi waliosoma nchi mbalimbali na kufanya kazi sehemu mbali mbali hawajui kitu kuliko wewe ambae hata hatujui wasifu wako ?
Ungekuwa unapotential serikali ingekuita uwasaidie ila hujulikani wala huna cha kuthibitisha ila porojo.
Umewahi fanya tafiti yoyote, au umeandika kitabu nikarejee maandiko yako ?
Yani sisi tukubaliane na common sense zako tuache kuwasikiliza watafiti wetu waliondaliwa kwa muda mrefu na waliofanya tafiti nyingi!
Huu ujinga uliouandika ufute !
Tumeshuhidia mabadiriko makubwa sana ktk awamu ya 5 kwa sababu ya kuwaamini wasomi, Magu jambo moja alilofanya ni kuwaamini wasomi na vijana na kuwandoa vihio.
Waache wasomi watengeneze dira, watakopokosea utawakosoa warekebishe sio kuwapa maksi 0 ni ujinga!
Haya mambo unayoandika ulijifunza mwemyewe tangu uzaliwe !
Huna adabu we mtoto, nakukemea kama baba, wewe unaonesha hata wazazi wako unawadharau.
Maprofesa ni kama wazazi wetu, wanajua kila kitu kuhusu Tanzania, koma we!
Usichanganye maprofesa na wanasiasa, nchi inakwamishwa na wanasiasa sio maprofesa.
Wewe hujui hata tatizo letu lilipo.
Nakwambia hata wewe mtanzania ni sehemu ya tatizo usitafute kisingizio.
Profesa kakupa elimu, wewe unashindwa kuitimia halafu unamlaumu ?
Ningependa kufafanua hoja yangu ya kutokuwa na imani na maprofesa wetu kwa kutolea mifano mbalimbali kama mchango walioutoa maprofesa Lipumba, Na Muhongo juu ya kuendeleza miradi iliyoanzishwa awamu ya 5.

Ningependa kuendelea zaidi kwa kutolea mfano wa ripoti ya profesa mayele.

Sitaki tuingie huko na ningekuona wa maana kama ungeelewa hoja yangu ya msingi ni nini na ukajidili hilo. Kitendo cha kujadili background inaonyesha ni tatizo.

Ninachokisema, mustakabli wa nchi yetu ni elimu tunayowapa vijana. Kama tunataka kuwapa future watoto wetu na tujiepushe na kuwakabidhi kina profesa mayele wakae huko peke yao watumie rasilimali zilizotengwa kufanya maboresho ya elimu na mwisho waibuke na mapendekezo ambayo kila mtanzania ataona haya siyo tunayoyatatua.

Shida inayoweza kutukabili ni kuletewa maboresho ambayo haleti majibu ya changamoto zetu na kwa sababu rasilimali zimeshatumika basi tuganganie kuleta mabadiriko yasiyo na tija.

Ninachokipendekeza ndicho wataalamu ambao hawatumii madesa hufanya katika tafiti na wala haihitaji elimu kubwa kujua hilo isipokuwa kwa mbumbumbu wachache.

Ukimuuliza mtanzania leo wa kawaida ambaye mtoto wake amemaliza chuo kikuu na hana kazi kama elimu yetu ina matatizo atakwambia ni kweli, anaweza asijue mbinu ya kuboresha lakini ukimweleza ili kuboresha watoto hawa wafundishe ushonaji wakiwa elimu ya msingi atakuona mpuuzi maana unachokipendekeza haoni kingemsaidiaje mtoto wake.

Mabadiriko ya elimu tunayoyategemea ni yale tu yayomkomboa mtanzania aliyekosa ajira ajiajiri,

Mabadiriko ya elimu tunayoyategemea ni yale yatayomfanya msomi awe mbunifu

mabadiriko ya elimu tuanyoiyategemea ni kuona maadili ya watanzania yanaimarika

mabadiriko ya elimu tunayoyategemea ni kuona mtanzania anajua elimu ya siasa, kila mtu ajue tofauti kati ya viongozi wa kuajiriwa na kuchaguliwa, ajue majukumu ya kila kiongozi anayempa kura, ajue wajibu wa raia wakati wa uchaguzi na baada ya uchaguzi

mabadiriko tunayoyataka ni kuona watanzania wakishirikiana katika kuzalisha mali na kufanya biashara na siyo kama tulivyo sasa tunaogopana

mabadiriko tunayoyataka ni kuona kila mtanzania anatamani rasilimali za tanzania zinainuisha tanzania.


Wasio jua mapungufu ya elimu yetu ndiyo wanaona haya yote yanafundishwa vyuoni

ingia mtaani muulize mtu alihetimu kidato cha 4 akuandalia andiko la kuanzisha biashara, (business plan) waulize waliomaliza chuo kikuu wakuandalie business plan.

Hawajui
 
Ningependa kufafanua hoja yangu ya kutokuwa na imani na maprofesa wetu kwa kutolea mifano mbalimbali kama mchango walioutoa maprofesa Lipumba, Na Muhongo juu ya kuendeleza miradi iliyoanzishwa awamu ya 5.

Ningependa kuendelea zaidi kwa kutolea mfano wa ripoti ya profesa mayele.

Sitaki tuingie huko na ningekuona wa maana kama ungeelewa hoja yangu ya msingi ni nini na ukajidili hilo. Kitendo cha kujadili background inaonyesha ni tatizo.

Ninachokisema, mustakabli wa nchi yetu ni elimu tunayowapa vijana. Kama tunataka kuwapa future watoto wetu na tujiepushe na kuwakabidhi kina profesa mayele wakae huko peke yao watumie rasilimali zilizotengwa kufanya maboresho ya elimu na mwisho waibuke na mapendekezo ambayo kila mtanzania ataona haya siyo tunayoyatatua.

Shida inayoweza kutukabili ni kuletewa maboresho ambayo haleti majibu ya changamoto zetu na kwa sababu rasilimali zimeshatumika basi tuganganie kuleta mabadiriko yasiyo na tija.

Ninachokipendekeza ndicho wataalamu ambao hawatumii madesa hufanya katika tafiti na wala haihitaji elimu kubwa kujua hilo isipokuwa kwa mbumbumbu wachache.

Ukimuuliza mtanzania leo wa kawaida ambaye mtoto wake amemaliza chuo kikuu na hana kazi kama elimu yetu ina matatizo atakwambia ni kweli, anaweza asijue mbinu ya kuboresha lakini ukimweleza ili kuboresha watoto hawa wafundishe ushonaji wakiwa elimu ya msingi atakuona mpuuzi maana unachokipendekeza haoni kingemsaidiaje mtoto wake.

Mabadiriko ya elimu tunayoyategemea ni yale tu yayomkomboa mtanzania aliyekosa ajira ajiajiri,

Mabadiriko ya elimu tunayoyategemea ni yale yatayomfanya msomi awe mbunifu

mabadiriko ya elimu tuanyoiyategemea ni kuona maadili ya watanzania yanaimarika

mabadiriko ya elimu tunayoyategemea ni kuona mtanzania anajua elimu ya siasa, kila mtu ajue tofauti kati ya viongozi wa kuajiriwa na kuchaguliwa, ajue majukumu ya kila kiongozi anayempa kura, ajue wajibu wa raia wakati wa uchaguzi na baada ya uchaguzi

mabadiriko tunayoyataka ni kuona watanzania wakishirikiana katika kuzalisha mali na kufanya biashara na siyo kama tulivyo sasa tunaogopana

mabadiriko tunayoyataka ni kuona kila mtanzania anatamani rasilimali za tanzania zinainuisha tanzania.


Wasio jua mapungufu ya elimu yetu ndiyo wanaona haya yote yanafundishwa vyuoni

ingia mtaani muulize mtu alihetimu kidato cha 4 akuandalia andiko la kuanzisha biashara, (business plan) waulize waliomaliza chuo kikuu wakuandalie business plan.

Hawajui
Kina lipumba ndio watunga sera za elmu ? Unaujua mchakato wa mtu kufikia kuwa mtunga sera ya elimu.
Maprofesa wachache ndio generalization ya uozo wa wote?.
Toa hoja thabiti ili tuamini kuwa maprf wa TZ hamna kitu!
Swali wewe umefanya nini kutoa soluhisho la tatizo la elimu duni?
Kama unaamini tatizo la elimu yetu ni maprofesa basi wewe una shida kubwa na ombwe la ufahamu wa mfumo wa elimu.
Kwa ufupi kwenye curricilim development profesa ni mdau mmoja tu, kuns wadau wengi zaidi ya hao.
Hujanijibu kuwa hayo mambo uliotaja ni chuo gani hakifundishi?
Ni ujinga mkubwa kwa mtanza kuendelea kuamini na kusingizia ombwe lake la kielimu limesababishwa na mtu fulani.
Mtu wa kwanza wa kulaumu ni wewe mwenyewe mtafuta elimu.
Mtume Muhamad S.A.W amewahi sema miaka 1400+ iliopita
"Kaitafuteni elimu hata China".
Unajua maana yake ?
Suala la kuitafuta elimu ni la kwako serikali ni mdau wa pili.
Unamfahamu Elon Musk,Mark Zuckerberg, Bill gate nk, unafikiri hao watu serikali zao ndio ziliwapa elimu bora iliotukuka au ni jitihada zao wenyewe ?
Mkuu kushindwa kuandika business plan huo ni uzembe wako, kwani wapo waliojifunza kupitia hivyo vyuo na wanajua haswa.
Kushindwa kujiajiri mpaka uwezeshwe na serikali ni uzembe wa hali ya juu.
Use all fucult of your mind to conqure all odds !
Kumbuka kuna akili uliozaliwa nayo kama binadamu ambayo nayo ina nafasi yake, hio elimu ni ziada tu na kuna watu hawajawahi fika hata veta au la saba .
Kama serikali imeshindwa kutimiza matakwa yako/ya watanzania kwa nini muendelee kuitegemea?
Watanzania tuache lawama zisizo na faida tuchikue hatua(This is the era of globalization), mungu katupa akili kwa nini utegemee akili za wengine kututatilia shida zilizokubuhu!
Nfugu nisikulaimu sana zamani ninilikuwa na akili tako kskini vaada ya kuwa enlighted nikaacha hizo habar.
My hand is respondible for everything ,the second hand is just an extra and is not necessary.
Nimalizie kwa ku dedicate wimbo huuu "teach me teacher" burning spear , listen it carefully and try to meditate it.
Siku njema.
 
Kina lipumba ndio watunga sera za elmu ? Unaujua mchakato wa mtu kufikia kuwa mtunga sera ya elimu.
Maprofesa wachache ndio generalization ya uozo wa wote?.
Toa hoja thabiti ili tuamini kuwa maprf wa TZ hamna kitu!
Swali wewe umefanya nini kutoa soluhisho la tatizo la elimu duni?
Kama unaamini tatizo la elimu yetu ni maprofesa basi wewe una shida kubwa na ombwe la ufahamu wa mfumo wa elimu.
Kwa ufupi kwenye curricilim development profesa ni mdau mmoja tu, kuns wadau wengi zaidi ya hao.
Hujanijibu kuwa hayo mambo uliotaja ni chuo gani hakifundishi?
Ni ujinga mkubwa kwa mtanza kuendelea kuamini na kusingizia ombwe lake la kielimu limesababishwa na mtu fulani.
Mtu wa kwanza wa kulaumu ni wewe mwenyewe mtafuta elimu.
Mtume Muhamad S.A.W amewahi sema miaka 1400+ iliopita
"Kaitafuteni elimu hata China".
Unajua maana yake ?
Suala la kuitafuta elimu ni la kwako serikali ni mdau wa pili.
Unamfahamu Elon Musk,Mark Zuckerberg, Bill gate nk, unafikiri hao watu serikali zao ndio ziliwapa elimu bora iliotukuka au ni jitihada zao wenyewe ?
Mkuu kushindwa kuandika business plan huo ni uzembe wako, kwani wapo waliojifunza kupitia hivyo vyuo na wanajua haswa.
Kushindwa kujiajiri mpaka uwezeshwe na serikali ni uzembe wa hali ya juu.
Use all fucult of your mind to conqure all odds !
Kumbuka kuna akili uliozaliwa nayo kama binadamu ambayo nayo ina nafasi yake, hio elimu ni ziada tu na kuna watu hawajawahi fika hata veta au la saba .
Kama serikali imeshindwa kutimiza matakwa yako/ya watanzania kwa nini muendelee kuitegemea?
Watanzania tuache lawama zisizo na faida tuchikue hatua(This is the era of globalization), mungu katupa akili kwa nini utegemee akili za wengine kututatilia shida zilizokubuhu!
Nfugu nisikulaimu sana zamani ninilikuwa na akili tako kskini vaada ya kuwa enlighted nikaacha hizo habar.
My hand is respondible for everything ,the second hand is just an extra and is not necessary.
Nimalizie kwa ku dedicate wimbo huuu "teach me teacher" burning spear , listen it carefully and try to meditate it.
Siku njema.


Tunafeli kwa sababu ya kuwategemea watu kama wewe na kuwapa nafasi ya kufanya maamuzi

mimi nadhani wewe hutambui maana ya elimu ila unajaribu kuisemea.

najizuia nisitumie maneno makali maana ukisema "suala la kutafuta elimu ni la kwako serikali ni mdau wa pili" haya ni maneno ya mtu aliyekalili maneno asiyejua maana yake

Wataalamu wanasema asilimia 90 ya matendo na fikra za wanadamu hutoka kwenye kujifunza. Mtoto anajifunza kutoka katika mazingira yaliyomzunguka na kutoka katika elimu rasmi.

Kazi ya mifumo ya elimu rasmi ni kubadirisha fikra na hulka za vijana ili ziendane na dira ya taifa. Maana yake ni kwamba kama mtoto anakulia mazingira ambayo amezungukwa na watu wasiojua kanuni za afya, watu wanaokula bila kunawa, watu wasijua mbinu za kubalina na magonjwa mbalimbali ya kiafya, mtoto huyu atakuwa anajifunza tabia na utendaji kutoka katika mazingira anayoishi.

Lakini sasa jamii inakuwa dira ya kutaka kuhakikisha kila mwanajamii anatoka katika tabia zao za asili walizokuwa wakifanya bila kujua madhara yake na kufanya hivyo ni kuhakikisha vijana wote wanaelimishwa njia sahihi. Hapa wanabuni mitaala inayoendana na changamoto hiyo ya jamii. kwamba ni mabadiriko gani ya kijamii unayoyataka katika jamii.

Lakini katika hii jamii itafika wakati watu wote watakuwa wameelimika na kujua umuhimu wa kufuata kanuni za afya bora lakini sasa unakuta jamii hii ilikuwa inaishi kwa kuwinda wanyama. jamii hii wamekuwa wengi kiasi kwamba uwindaji pekee hauwezi kutosheleza na wanaharibu mazingira, Uchumi wa dunia umebadirika. Hapa sasa kunaibuka ajenda nyingine ya kuwafundisha watoto mbinu mpya za kiuchumi na kuwaelimisha madhara ya mbinu za kizamani. hapa napo mitaala inabadirika.

Lakini sasa ukikaa ukaona kwa jirani yako wanalima na kuvuna na wewe kila siku unalima na kushindwa kuvuna basi unaenda kwa jirani yako na kumuuliza unatumia mbinu gani jirani yangu. Yeye atakueleza labda napandia kinyesi cha ngombe na kumwagilia maji na wewe unaanza kufanya hivyo. Hii ndiyo mitaala tunayosema kuwa ukikaa umefundisha watoto wako na umekaa hakuna aliyevumbua hata kibatari basi unaenda kwa yule ambaye watoto wake wanavumbua majibu mapya kila siku na unachukua nayowafundisha watoto wake na kuwafundisha wako.

Haya kwenye elimu anayeamua watoto wajifunze nini ni wenye dhamana ya kutunga sera na miongozo na mitaala ya elimu. Hawa ndiyo wanaweza kutazama mabadiriko yanayotokea katika jamii yetu na kurekebisha mitaala ili iwe na tija. Ni mpumbavu (samahani mpumbavu siyo tusi bali ni mtu asiyejua ambaye bado ukimueleza haelewi, mjinga anakuwa hajui lakini ukimueleza anaelewa) pekee anayeweza kudai elimu ni jukumu la mtu mwenyewe na serikali ni mdau wa pili. Mtu aliyeko kwenye mazingira yenye changamoto atajitambuaje yeye ajitafutie majibu? ni sawa na kumwambia mgonjwa ajitibu.

Wanaotunga mitaala ndiyo wenye dhamana ya kutazama changamoto za jamii na kuleta mitaala yenye majibu na siyo kumvisha jukumu kila mwajamii kuwa atafute majibu yake.

kama tumeona huko nje wametokea kina Bilgate, kina Elon kwa wenye akili wanatafiti hivi huko mtoto wa miaka 3 mpaka 5 anafundishwa nini? Mtoto wa miaka 6 mpaka 12 anafundishwa nini? mtoto wa miaka 13 - 18 anafundishwa nini?. Yawezekana tukawana mazingira tofauti lakini hao waliofanikiwa je walivyokuwa hatu kama ya kwetu walifanya nini kilichobadiri fikra zao.

lakini narudia tena tusiwaamini kina manyele wa kuibuka na taarifa za mkoa una ngombe laki tatu na ndiyo chanzo cha kuchafuka mto mara. Tunachohitaji ni kuweka dira sahihi kwa watoto wetu na taifa letu na tusilee upumbavu wa aina yoyote katika hili.
 
Tunafeli kwa sababu ya kuwategemea watu kama wewe na kuwapa nafasi ya kufanya maamuzi

mimi nadhani wewe hutambui maana ya elimu ila unajaribu kuisemea.

najizuia nisitumie maneno makali maana ukisema "suala la kutafuta elimu ni la kwako serikali ni mdau wa pili" haya ni maneno ya mtu aliyekalili maneno asiyejua maana yake

Wataalamu wanasema asilimia 90 ya matendo na fikra za wanadamu hutoka kwenye kujifunza. Mtoto anajifunza kutoka katika mazingira yaliyomzunguka na kutoka katika elimu rasmi.

Kazi ya mifumo ya elimu rasmi ni kubadirisha fikra na hulka za vijana ili ziendane na dira ya taifa. Maana yake ni kwamba kama mtoto anakulia mazingira ambayo amezungukwa na watu wasiojua kanuni za afya, watu wanaokula bila kunawa, watu wasijua mbinu za kubalina na magonjwa mbalimbali ya kiafya, mtoto huyu atakuwa anajifunza tabia na utendaji kutoka katika mazingira anayoishi.

Lakini sasa jamii inakuwa dira ya kutaka kuhakikisha kila mwanajamii anatoka katika tabia zao za asili walizokuwa wakifanya bila kujua madhara yake na kufanya hivyo ni kuhakikisha vijana wote wanaelimishwa njia sahihi. Hapa wanabuni mitaala inayoendana na changamoto hiyo ya jamii. kwamba ni mabadiriko gani ya kijamii unayoyataka katika jamii.

Lakini katika hii jamii itafika wakati watu wote watakuwa wameelimika na kujua umuhimu wa kufuata kanuni za afya bora lakini sasa unakuta jamii hii ilikuwa inaishi kwa kuwinda wanyama. jamii hii wamekuwa wengi kiasi kwamba uwindaji pekee hauwezi kutosheleza na wanaharibu mazingira, Uchumi wa dunia umebadirika. Hapa sasa kunaibuka ajenda nyingine ya kuwafundisha watoto mbinu mpya za kiuchumi na kuwaelimisha madhara ya mbinu za kizamani. hapa napo mitaala inabadirika.

Lakini sasa ukikaa ukaona kwa jirani yako wanalima na kuvuna na wewe kila siku unalima na kushindwa kuvuna basi unaenda kwa jirani yako na kumuuliza unatumia mbinu gani jirani yangu. Yeye atakueleza labda napandia kinyesi cha ngombe na kumwagilia maji na wewe unaanza kufanya hivyo. Hii ndiyo mitaala tunayosema kuwa ukikaa umefundisha watoto wako na umekaa hakuna aliyevumbua hata kibatari basi unaenda kwa yule ambaye watoto wake wanavumbua majibu mapya kila siku na unachukua nayowafundisha watoto wake na kuwafundisha wako.

Haya kwenye elimu anayeamua watoto wajifunze nini ni wenye dhamana ya kutunga sera na miongozo na mitaala ya elimu. Hawa ndiyo wanaweza kutazama mabadiriko yanayotokea katika jamii yetu na kurekebisha mitaala ili iwe na tija. Ni mpumbavu (samahani mpumbavu siyo tusi bali ni mtu asiyejua ambaye bado ukimueleza haelewi, mjinga anakuwa hajui lakini ukimueleza anaelewa) pekee anayeweza kudai elimu ni jukumu la mtu mwenyewe na serikali ni mdau wa pili. Mtu aliyeko kwenye mazingira yenye changamoto atajitambuaje yeye ajitafutie majibu? ni sawa na kumwambia mgonjwa ajitibu.

Wanaotunga mitaala ndiyo wenye dhamana ya kutazama changamoto za jamii na kuleta mitaala yenye majibu na siyo kumvisha jukumu kila mwajamii kuwa atafute majibu yake.

kama tumeona huko nje wametokea kina Bilgate, kina Elon kwa wenye akili wanatafiti hivi huko mtoto wa miaka 3 mpaka 5 anafundishwa nini? Mtoto wa miaka 6 mpaka 12 anafundishwa nini? mtoto wa miaka 13 - 18 anafundishwa nini?. Yawezekana tukawana mazingira tofauti lakini hao waliofanikiwa je walivyokuwa hatu kama ya kwetu walifanya nini kilichobadiri fikra zao.

lakini narudia tena tusiwaamini kina manyele wa kuibuka na taarifa za mkoa una ngombe laki tatu na ndiyo chanzo cha kuchafuka mto mara. Tunachohitaji ni kuweka dira sahihi kwa watoto wetu na taifa letu na tusilee upumbavu wa aina yoyote katika hili.
Nilikuuliza wewe unajua zaidi ya watunga sera,maprofesa na wizara ya elimu ?
Mpaka sasa hujanijibu.
Unaandiko maneno mengi yasio na tija.
Nimekuuliza wewe umefanya nini tangible kutoa suluhu, hujaeleza wala huna.
Wenzio wamefanya research na kuandika maandiko mengi yanayotoa suluhu wewe unaongea common sense(porojo).
Nchi zinaendeshwa kwa tafiti na watafiti ndio wanapewa nafasi watekeleze waliyo tafiti.
Maprofesa wataendelea kuaminiwa na serikali zote kuanzia iliopo na zijazo, they have credentials! And they deserve.
 
Nilikuuliza wewe unajua zaidi ya watunga sera,maprofesa na wizara ya elimu ?
Mpaka sasa hujanijibu.
Unaandiko maneno mengi yasio na tija.
Nimekuuliza wewe umefanya nini tangible kutoa suluhu, hujaeleza wala huna.
Wenzio wamefanya research na kuandika maandiko mengi yanayotoa suluhu wewe unaongea common sense(porojo).
Nchi zinaendeshwa kwa tafiti na watafiti ndio wanapewa nafasi watekeleze waliyo tafiti.
Maprofesa wataendelea kuaminiwa na serikali zote kuanzia iliopo na zijazo, they have credentials! And they deserve.
Huhitaji kuniuliza ninajua kuliko watunga sera bali mtu makini huchukua hoja ninazozisema na kusubiri hao ninaojaribu kubashiri kuwa mabadiriko wanayooenda kutuletea siyo, wakileta hoja zao pima.

Hapo ndipo utajua nani anajua zaidi

Lakini kwangu mimi nimekueleza kama jamii tusisubiri walete kazi iliyoisha na pengine ndipo tuanze mjadala.

Hoja yangu ni watueleze sasa mwanzoni kabisa kuwa tunapanga kuweka kwenye elimu ya msingi na sekondari elimu ya ushonaji, elimu ya kilimo na tuanze kujadili hayo.

Nimewahi kumsikia mweshimiwa raisi wetu akigusia hilo kuwa tunataka kuwapa watoto wetu skills za kuwasaidia na hivyo nahisi wanatuletea hayo. Naomba niseme kama kuna mtaalamu amependekeza haya ninasema huyo ningekuwa na uwezo nikufuta vyeti vyake.

Kabla ya kuanzisha mafunzo ya ufundi veta 1994 kwa mtaalamu kama angependekeza tuweke elimu ya ufundi kwenye mitaala ya msingi na sekondari angekuwa sahihi. Kabla ya kuwa na Vyuo vya elimu ya kati na juu vya kutosha vinavyotoa certificates, diploma, degree kwa mtu kusema tuweke elimu ya ufundi kwenye mitaala ya msingi na sekondari alikuwa sahihi.

Lakini sasa tumejenga vyuo vya veta vya kutosha, tumejenga vyuo vya kati na juu vya kutosha na wanaotoka huko wanakosa ajira, yet mtu aje anasema tuingize elimu ya ufundi msingi na primary tumuone wa maana kisa ana initial profesa, That is stupidity.

Ni lazima elimu ya msingi itoe msingi.

uwe mwanasheria, uwe mwalimu, uwe mhandisi, uwe dkitari kuna mambo ambayo sote tunatakiwa kuyaelewa na haya ndiyo yafundishwe huku chini tunakosoma pamoja.

kama ni kufundishwa maadili basi uwekwe mkazo kwenye maadili

kama ni kufundishwa vyakula ili tujue tuleje basi mkazo uwekwe huku.

takwimu zinaonyesha katika nchi kama Tanzania wasomi ndiyo wanaoongoza kwa kuugua magonjwa ya tabia kama sukari, pressure, vitambi.

kwa nini tusiseme elimu tuliyonayo imeshindwa kutukomboa katika kutambua chakula bora ni kipi na tuleje ni kuwa na afya.

hakuna common understanding ya je mtu anatakiwa kula ugali kiasi gani, na kwa mboga zipi. kila mmoja kipimo ni tumbo lake na mfuko wake. mfuko ukikuruhusu unapita baa unakula kilo moja ya kitimoto na bia sita, vyote ni sukari, wanga na mafuta.

Tumbo likituna tunaona ni dalili za kuwa na feza.

Jamii yetu inahitaji ukombozi wa kifikra na ukombozi huo utaanzia kwenye mabadiriko ya mitaala.
 
Kwa tamaa za viongozi wetu mabadiliko magumu sana kutokea
Tusiwaruhusu hawa watu watuharibie kizazi kijacho kwa ufinyu wa fikra.

tunahitaji elimu bora huo ndiyo ukombozi pekee wa watoto wetu.
 
Hoja yangu ni watueleze sasa mwanzoni kabisa kuwa tunapanga kuweka kwenye elimu ya msingi na sekondari elimu ya ushonaji, elimu ya kilimo na tuanze kujadili hayo.
Kwani hizo elimu hazipo ?
Ningekuunga mkono iwapo ungesema wafanye tathmini iwapo elimu inayotolewa kama inatolewa kwa usahihi.
Sekondari hakuna elimu ya ushoni ila msingi ipo.
Unachokitaka tayari kipo ktk mtaala ila hakuna mwenye muda nacho hata wazazi.
Tanzania hakuna shida kwenye curricilum design bali kwenye curruculum implementation.
Mkuu una ufahamu mdogo sana kuhusu mtaala uliopo na mapungufu yake.
Kausome kwanza mtaala, soma sera za elimu, ndio uje kujadili maana naona unaandika vitu ambavyo sio sahihi.
Wataalamu walileta competence base curriculum watekelezaji hawafuati na kutenda inavyotakiwa, je kuna sababu ya kulaumu curriculum developer?
Mfano somo/mtaala wa engilsh linaagiza(Main objectives/competence)
.To read text.
.To read and interpret text
.To listen text.
.To interpret text from a reader
.To speak fluently.
Nenda mashuleni asses kama shule zinazingatia hizo objectives.
Most of schools wanafundusha
.Grammer
.Comprehension
.Tenses.
Nk
Wakati vyote hivyo vimechopekwa katika objectives hizo juu, sio mada bali ni part and parcel of obove ojectives.
Taasisi ya ukuzaji mitaaka ipo vizuri na update. ila taasisi ya kusimamia mitaala ndio hovyo hovyo hovyo! hapa nazungumzia wizara ya elmu na tamisemi na tutawi twao.
Hazisimamii sawasawa mitaala inayotungwa.Walimu wanajifunfishia fundishia tu na kukalilisha mitihani basi.

Necta hawatungi mitihani kama curriculum inavyotaka, mfano hapo juu ktk kingereza wanapima
.Listerning skill tuswali tutano.
.Reading skill maswali 5.
Na grammer 50%+
Necta Hawapimi
.Speaking skill.
.Interpretation/translation skill nk

Upande wangu sioni tatizo kwa maprofesa watunzi wa mtaala bali wasimamizi wa mtaala hasa maafisa elimu, Wathibiti ubora, walimu wakuu, walimu na wazazi.
 
Kuna watu nimekutana nao wanamaliza chuo hawajui vyakula common vya Mtanzania viko makundi gani ya chakula!
Huhitaji kuniuliza ninajua kuliko watunga sera bali mtu makini huchukua hoja ninazozisema na kusubiri hao ninaojaribu kubashiri kuwa mabadiriko wanayooenda kutuletea siyo, wakileta hoja zao pima.

Hapo ndipo utajua nani anajua zaidi

Lakini kwangu mimi nimekueleza kama jamii tusisubiri walete kazi iliyoisha na pengine ndipo tuanze mjadala.

Hoja yangu ni watueleze sasa mwanzoni kabisa kuwa tunapanga kuweka kwenye elimu ya msingi na sekondari elimu ya ushonaji, elimu ya kilimo na tuanze kujadili hayo.

Nimewahi kumsikia mweshimiwa raisi wetu akigusia hilo kuwa tunataka kuwapa watoto wetu skills za kuwasaidia na hivyo nahisi wanatuletea hayo. Naomba niseme kama kuna mtaalamu amependekeza haya ninasema huyo ningekuwa na uwezo nikufuta vyeti vyake.

Kabla ya kuanzisha mafunzo ya ufundi veta 1994 kwa mtaalamu kama angependekeza tuweke elimu ya ufundi kwenye mitaala ya msingi na sekondari angekuwa sahihi. Kabla ya kuwa na Vyuo vya elimu ya kati na juu vya kutosha vinavyotoa certificates, diploma, degree kwa mtu kusema tuweke elimu ya ufundi kwenye mitaala ya msingi na sekondari alikuwa sahihi.

Lakini sasa tumejenga vyuo vya veta vya kutosha, tumejenga vyuo vya kati na juu vya kutosha na wanaotoka huko wanakosa ajira, yet mtu aje anasema tuingize elimu ya ufundi msingi na primary tumuone wa maana kisa ana initial profesa, That is stupidity.

Ni lazima elimu ya msingi itoe msingi.

uwe mwanasheria, uwe mwalimu, uwe mhandisi, uwe dkitari kuna mambo ambayo sote tunatakiwa kuyaelewa na haya ndiyo yafundishwe huku chini tunakosoma pamoja.

kama ni kufundishwa maadili basi uwekwe mkazo kwenye maadili

kama ni kufundishwa vyakula ili tujue tuleje basi mkazo uwekwe huku.

takwimu zinaonyesha katika nchi kama Tanzania wasomi ndiyo wanaoongoza kwa kuugua magonjwa ya tabia kama sukari, pressure, vitambi.

kwa nini tusiseme elimu tuliyonayo imeshindwa kutukomboa katika kutambua chakula bora ni kipi na tuleje ni kuwa na afya.

hakuna common understanding ya je mtu anatakiwa kula ugali kiasi gani, na kwa mboga zipi. kila mmoja kipimo ni tumbo lake na mfuko wake. mfuko ukikuruhusu unapita baa unakula kilo moja ya kitimoto na bia sita, vyote ni sukari, wanga na mafuta.

Tumbo likituna tunaona ni dalili za kuwa na feza.

Jamii yetu inahitaji ukombozi wa kifikra na ukombozi huo utaanzia kwenye mabadiriko ya mitaala.
 
Kwani hizo elimu hazipo ?
Ningekuunga mkono iwapo ungesema wafanye tathmini iwapo elimu inayotolewa kama inatolewa kwa usahihi.
Sekondari hakuna elimu ya ushoni ila msingi ipo.
Unachokitaka tayari kipo ktk mtaala ila hakuna mwenye muda nacho hata wazazi.
Tanzania hakuna shida kwenye curricilum design bali kwenye curruculum implementation.
Mkuu una ufahamu mdogo sana kuhusu mtaala uliopo na mapungufu yake.
Kausome kwanza mtaala, soma sera za elimu, ndio uje kujadili maana naona unaandika vitu ambavyo sio sahihi.
Wataalamu walileta competence base curriculum watekelezaji hawafuati na kutenda inavyotakiwa, je kuna sababu ya kulaumu curriculum developer?
Mfano somo/mtaala wa engilsh linaagiza(Main objectives/competence)
.To read text.
.To read and interpret text
.To listen text.
.To interpret text from a reader
.To speak fluently.
Nenda mashuleni asses kama shule zinazingatia hizo objectives.
Most of schools wanafundusha
.Grammer
.Comprehension
.Tenses.
Nk
Wakati vyote hivyo vimechopekwa katika objectives hizo juu, sio mada bali ni part and parcel of obove ojectives.
Taasisi ya ukuzaji mitaaka ipo vizuri na update. ila taasisi ya kusimamia mitaala ndio hovyo hovyo hovyo! hapa nazungumzia wizara ya elmu na tamisemi na tutawi twao.
Hazisimamii sawasawa mitaala inayotungwa.Walimu wanajifunfishia fundishia tu na kukalilisha mitihani basi.

Necta hawatungi mitihani kama curriculum inavyotaka, mfano hapo juu ktk kingereza wanapima
.Listerning skill tuswali tutano.
.Reading skill maswali 5.
Na grammer 50%+
Necta Hawapimi
.Speaking skill.
.Interpretation/translation skill nk

Upande wangu sioni tatizo kwa maprofesa watunzi wa mtaala bali wasimamizi wa mtaala hasa maafisa elimu, Wathibiti ubora, walimu wakuu, walimu na wazazi.

Haya mambo yanahitaji mjadala tena mjadala mpana sana.

kwako wewe naona umejaribu kulinganisha utendaji wa taasisi tofauti

mimi ninatazama output product ya kutoka kwenye mifumo yetu ya elimu.

ukisoma global definition ya maana ya mtaala inasema ni mwongozo wa nini kifundishwe, mbinu za kufundisha, upimaji mafunzo na matokeo tarajiwa.

hivyo sisi layman tukiona kinachotoka ni tofauti na matarajio tunasema mwongozo mzima ni ovyo

Nitakupa mfano mmoja kukuonyesha tatizo

wakati nafanya kazi na wachina, wao wachina wana spirit ya kufanya kazi, wanataka mda wote mtu yuko bize anafanya kazi. Sasa sisi tunapokuwa na jamii za watu wetu wametoka kwenye jamii zinazokaa na kupiga soga na sisi tunataka watu wetu wabadilike na njia pekee ni kutumia elimu yetu kujenga tabia hii.

Ukipita mtaani unakuta watoto wamejaa vituo vya daladala wamesimama tu wanapiga kelele, ukipita mashuleni unakuta wanafunzi wamejaa kwenye madarasa wanapiga kelele.

Hivi unategemea mtoto ambaye ametokea miaka 3 anasoma chekechea mpaka miaka 18 anamaliza kidato cha nne amezoea kukaa na kupiga soga tu na wenzake anawezaje kuwa serious katika kazi?

Umri huu ndiyo umri wa kujenga tabia za mtu, mazoea unayomjengea ndiyo tabia anayoibeba maishani mwake.

kwa hiyo sasa tukiwa na tatizo hili kwenye jamii ndipo tunatakiwa kuita wataalamu kwamba jamani pitieni hicho kitu kinachoitwa mtaala, twambieni tufanye nini ili watoto hawa tujenge kizazi kipya chenye hulka mpya.

wao watatueleza changamoto zilizotupeleka kwenye tatizo hili na kutushauri ili tutoke huku tufanye moja mbili tatu. na hapa kutueleza siyo huu upuuzi unaoita mtaala eti ni kuandika

kila mtoto awahi shule
kila mtoto afanye kazi zake kwa mda
kila mtoto asipige kelele
n.k

eti tuite mtaala na matokeo yasipokuwepo twende kulaumu wafundishaji.

Ni lazima mtunzi wa mtaala aeleze changamoto zilizopo katika jamii zinazopelekea watu kujenga tabia za kupiga soga na siyo kufanya kazi kwa userious mpaka iishe.

Mtunga mtaala aeleze nini kifundishwe ili kukabiliana na changamoto hiyo

mtunga mtaala aeleze hicho kinachofundishwa kifundishwe kwa mbinu gani.

Mtunga mtaala aeleze mbinu za kupima mafanikio katika kile anachojaribu kutatua

siyo mambo ya mtu kuandika

"Mfano somo/mtaala wa engilsh linaagiza(Main objectives/competence)
.To read text.
.To read and interpret text
.To listen text.
.To interpret text from a reader
.To speak fluently."

Sisi tunachokitaka ni kujua malengo ya kufundisha somo la kingereza elimu ya msingi ni nini? Je mtoto anayemaliza elimu ya msingi tunataka awe na maarifa gani katika somo hilo la kingereza. Mtoto amejifunza kingereza miaka 7 tunataka baada ya hapo awe amepata nini?

labda tunataka kila anayemaliza darasa la saba aweze kusalimia kwa ufasaha katika lugha ya kingereza
labda tunataka mtoto anayemaliza darasa la saba aweze kujua kutambulisha familia yake kwa ufasaha
labda tunataka mtoto anayemaliza darasa la saba aweze kupokea mgeni na kumuelekeza anakokwenda
yaani tufanye utafiti na kujua kwa ngazi ya darasa la saba hii lugha iwe na manufaa gani kwa muhitimu

siyo to haya malengo mfu ya kila mtoto ajue " to read text" anajua kuread text lakini hajui kingereza hata cha kusalimiana


Ukifanya kazi na wazungu unagundua wazungu wako tofauti na wachina, wazungu wako smarti kwenye time table, wazungu wako smart kwenye anaanza kitu anahakikisha amekimaliza kwa kupata sound conclusion, wazungu wako systematic hawataki kuruka ruka mara hiki hakijaisha umekimbilia kingine mara umechukua kile. akikuta kitu kipo anakiheshimu sana na anapokuja kuweka kingine anahakikisha ametazama kinaingilianaje na vitu vilivyopo au vitakavyokuja.

Sisi tuko shagala bagala, hatujui kuweka time table kwamba kesho asubuhi nitafanya a, baadae b, c n.k. Tunakurukupa tunachukua kitu kimoja hakijaisha tunakiacha na kukurupukia kitu kingine. unaweza kuwa na kitu cha thamani kipo na tunapokuja kufanya kipya hatujali tunaweza kuharibu tu, au hatujali vinavyofuata tunaweza kuweka ilimradi.

Mambo haka haya ndiyo tofauti ya wataalamu wetu na wataalamu wa kutoka nje.

haya ndiyo tunataka watu wa mitaala watizame kwamba hizi tabia tulikosea wapi na je tufanye nini ili tuweke tabia mpya kwa watu wetu.

yawezekana tumerundika mambo mengi katika masomo na mda hautoshi, matokeo ni kufundisha kwa kumbizana. mnachukua topic mnaianza mtoto hajaielewa mshachukua nyingine yaani ni kumbizana tu. Mwisho wa siku ni kuharibu tabia za watoto kwa kuwajengea tabia ya kukimbilia kufanya mambo mengi, ameshika hili, mara hajamaliza kashika lile, mara kaliacha.

yawezekana tunahitaji kuwafundisha watoto wetu kwamba ukishika jambo likamilishe hilo kwanza ulifanye kwa ufasaha na siyo kukimbia. Tangu wakiwa wadogo watoto waelewe kwamba hawataenda kufanya jambo jipya kabla hawajakamilisha walilolianza. watoto waelewe kuwa kila jambo lina umuhimu wake hivyo wasijaribu kuchukua nafasi ya jambo moja na kuharibu jingine.

sasa mtu wa mitaala atuongoze kuwa ili tufanye hili tunahitaji kutumia mbinu gani

maisha yamebadirika tunahitaji watu wetu wawe na value na siyo kikimbilia kuwakalilisha.

mtu anajigamba kuwa masomo ya ushonaji yapo msingi lakini ukimuuliza kuna mtoto hata mmoja anamaliza msingi anajua kushona?

kwa nini usiwe bize kumjengea tabia za kazi shule ya msingi, wajinga wanafikiri kumfundisha mtoto tabia za kazi ni kumfanyisha kazi, hapana, mtoto ajue nikianza kufanya jambo sitakiwi kucheza mpaka nilimalize, tuwajengee watoto tabia ya kutafiti zaidi badala ya kutegemea kukalilishwa tu mfano mtoto apewe homework anazoweza kutafiti mwenyewe kama kuulizwa wafanya wanaofugwa majumbani wakatafiti wanakula nini, wadudu wana miguu ngapi, yaani mambo ambayo mtoto mwenyewe anakuwa bize kutafuta majibu na siyo kutegemea kuuliza tu.

kwa nini usimuelimishe kwenye mambo ya fedha katika elimu ya msingi ili hata akiamaliza akajifunza ushonaji kwa mjomba wake anakuwa anajua kuweka akiba, anajua kutengeneza bajeti yake ya maisha kulingana na kipato chake, anajua ni vitu gani avipe kipaumbele katika maisha badala ya kuishi kwa tamaa simu kubwa, nguo nzuri n.k visivyomba mafanikio yoyote, kwa nini usimfundishe mbinu za kuwekeza, kwamba anajua nikianza kulipwa nikitunza asilimia fulani baada ya mda nanunua cherehani ya kwangu.

Sasa watunga mitaala ndiyo watueleze kwamba tukitaka kufanya haya je tutumie mbinu gani?
 
Kuna watu nimekutana nao wanamaliza chuo hawajui vyakula common vya Mtanzania viko makundi gani ya chakula!
Elimu yetu ni ujinga mtupu

hakuna msomi wa kitanzania anayejua
mtoto kwa siku anatakiwa kula protini kiasi gani, vitamin kiasi gani, wanga kiasi gani

na atleast tutafsiri kuwa mtoto anatakiwa kunya angalau maziwa kiasi gani, ale nini kwa kiasi gani

hebu ulliza kwenye jamii yetu
kijana anatakiwa kula ugali kiasi gani? na je ale na nini maharage kiasi gani? mboga za majani kiasi gani?

hatujui kabisa tunakula kutokana na mfukoni una shilingi ngapi

unakuta wasomi ndiyo wanaongoza kuwa na vitambi na presha na sukari kwa kuwa wanazidisha ulaji wa vyakula fulani.

Tunataka waandaji wa mitaala wajue kuwa haina maana kwa kila mtanzania kujua maana ya protini, vitamins na kdhalika bali kila mtanzania tunataka ajue aleje au aishije ili awe na afya nzuri na mitaala ilenge huko
 
Watupige mara ngapi na hicho 'Kitu Kizito' ?

Tanzania: Siasa na Elimu zimechanganywa katika mfuko mmoja. Zinahitaji kutenganishwa.
 
Maamuzi yoyote kuhusu Elimu na Mfumo wake yasitolewe na Wanasiasa kama Wabunge bali yatolewe na wahusika kama Walimu na hao mnaowaita "Maprofesa" lakini wasiwe wanasiasa.
 
Back
Top Bottom