Tunahitaji 'Kichwa cha Yohana'

Tunahitaji 'Kichwa cha Yohana'

NI BAHATI MBAYA SANA HADHIRA YAKO IMESHINDWA KUELEWA MAUDHUI YA ANDIKO LAKO. UMETUMIA KISA CHA HERODE NA BINTIYE HERODIA KUMSHAURI MH. RAIS ACHUKUE MAAMUZI MAGUMU YA KUFANYA KILE MOYO WAKE HAUPENDI KUFANYA, KUTENDA KILE DHAMIRI YAKE HAIFURAHII KUKITENDA...KUSIKILIZA MAWAZO YA ASIO WAPENDA, KUSIKILIZA USHAURI WA WAPINZANI, KUKAA NAO MEZA MMOJA WAJADILIANE MUSTAKABARI WA NCHI YETU...!!
Swadakta! Kiongozi wetu siku akiwa tayari kutenda hayo, watanzania ni wasamehevu na husahau yote. Wala suluhu si kuwateua kina fulani kutoka upinzani ili tujue kweli mkuu anafanya maamuzi magumu.
 
Tunaiangalia Tanzania na si mtu fulani. Kama huyo mtu ataweza kuivusha nchi na kuipeleka kule tunakotaka basi ni heri. Lakini hao wananchi wanataka nini? Kiongozi wa nchi anapoamini kuwa hawezi kufanya kazi kwenye kelele za upinzani ni udhaifu mkubwa. Ndani ya kelele hizo kuna majibu kwa watz. Waache watu waseme na watazame ili siku ikifika uwathibitishie kuwa hawakuwa sahihi. Hakuna sababu ya kuzima wengine ili tuone kuwa wewe ni mtendaji bora.

Yako mambo anafanya na kuongea, rais unajiuliza kuwa kuna nia kweli ya hayo anayoamini kutaka kuyatimiza? Afanye afanyavyo lakini tujue kuwa lazima na yeye ajiguse na ajitwike jukumu kubwa na lenye lawama la kuwapatia watanzania katiba mpya ambayo ndani yake itapunguza nguvu zake pia. Suala la kusema anawakubali vijana zaidi liwe ni jukumu la taaisi husika kuamua nani awe wapi na kwa nini ili mradi tu tunaingizwa na sheria mama ambayo hatajitwalia sifa kusema alitenda kwa utashi wake, kumbe alipaswa tu kusimama vyema na kuilinda na kutenda kadiri ya sheria mama
Mkuu sheria Mama inaweza kuwepo, lakini hakuna nchi inayoweza kuikwepa kauli kuu ya kiongozi mkuu wa nchi.

Kiongozi mkuu anaweza kuwa na udhaifu wake mwingi lakini bado hatujafikia huko ambako mamlaka ya rais yanaweza kupunguzwa kwa ghafla tu. Ni mchakato wenye kuhitaji muda. Na wakati tunaelekea kwenye ukamilifu wa mchakato huo, basi na tuwe tayati kuuishi uhalisia wa mambo.
 
Tuache unafiki wa kitoto,kwanini tulitaka uhuru kutoka kwa Mwingereza?Ili tujitawale tuweze kuondokana na dhuluma,ukandamizaji,unyonyaji.
Kudai katiba ni haki yetu,asietaka katiba ya Warioba ahamie Korea ya Kaskazini atuachie
Tanzania yetu.
 
Mkuu sheria Mama inaweza kuwepo, lakini hakuna nchi inayoweza kuikwepa kauli kuu ya kiongozi mkuu wa nchi.

Kiongozi mkuu anaweza kuwa na udhaifu wake mwingi lakini bado hatujafikia huko ambako mamlaka ya rais yanaweza kupunguzwa kwa ghafla tu. Ni mchakato wenye kuhitaji muda. Na wakati tunaelekea kwenye ukamilifu wa mchakato huo, basi na tuwe tayati kuuishi uhalisia wa mambo.
Kauli kuu ya rais katika taifa lenye uhuru wa kikatiba itatolewa kwa adabu na kwa maslahi mapana ya taifa tu na si kwa maslahi ya chama chake kama ilivyo sasa. Pale ambapo wananchi wataona rais analeta za kuleta basi kupitia bunge lao wanaweza kumwadabisha. S. Afrika ni mfano mzuri wa nchi yenye siasa ambazo rais pamoja na mamlaka yake anaweza kuitwa na bunge na kuonywa au kufukuzwa kazi. Hapa kwa mazingira haya tutangoja sana
 
Kauli kuu ya rais katika taifa lenye uhuru wa kikatiba itatolewa kwa adabu na kwa maslahi mapana ya taifa tu na si kwa maslahi ya chama chake kama ilivyo sasa. Pale ambapo wananchi wataona rais analeta za kuleta basi kupitia bunge lao wanaweza kumwadabisha. S. Afrika ni mfano mzuri wa nchi yenye siasa ambazo rais pamoja na mamlaka yake anaweza kuitwa na bunge na kuonywa au kufukuzwa kazi. Hapa kwa mazingira haya tutangoja sana
Ni kweli tutangoja sana. Siasa maandazi za kumuita mtu fisadi kwa miaka minane halafu jamii inaaminishwa kwa miezi mitatu kwamba ameshakuwa malaika, sitatufanya tungoje kwa miaka mingi ijayo.

Maslahi ya chama tawala ndio yale yale ya mwananchi wa kawaida, udhaifu fulani fulani katika utekelezaji wa lengo kuu la kuinua maisha ya kila mtanzania, sio kigezo cha kuona kila kinachofanyika hakina maana.
 
Mkuu sheria Mama inaweza kuwepo, lakini hakuna nchi inayoweza kuikwepa kauli kuu ya kiongozi mkuu wa nchi.

Kiongozi mkuu anaweza kuwa na udhaifu wake mwingi lakini bado hatujafikia huko ambako mamlaka ya rais yanaweza kupunguzwa kwa ghafla tu. Ni mchakato wenye kuhitaji muda. Na wakati tunaelekea kwenye ukamilifu wa mchakato huo, basi na tuwe tayati kuuishi uhalisia wa mambo.
Kukwepa kauli ya mkuu wa nchi yawezekana kama "dira" ya nchi ipo imara na sahihi.Trump aweza kuwa kiongozi mpuuzi kuliko wote wa kizazi hiki lakini dira ya Marekani inamdhibiti. Hicho ndo tunataka na kukihitaji sana.
HOJA ni je,kwa aina ya wanasiasa na viongozi tulionao tunaweza?
 
Ni kweli tutangoja sana. Siasa maandazi za kumuita mtu fisadi kwa miaka minane halafu jamii inaaminishwa kwa miezi mitatu kwamba ameshakuwa malaika, sitatufanya tungoje kwa miaka mingi ijayo.

Maslahi ya chama tawala ndio yale yale ya mwananchi wa kawaida, udhaifu fulani fulani katika utekelezaji wa lengo kuu la kuinua maisha ya kila mtanzania, sio kigezo cha kuona kila kinachofanyika hakina maana.
Mahakama ya mafisadi ipo. Waambie wawapeleke hao mafisadi. Na maslahi ya chama hayawezi kuwa maslahi ya wananchi, labda ya wanachama. Ingekuwa hivyo basi leo huu uzi wala usingekuwepo
 
Kichwa cha Yohana kwanza kinatakiwa kwenye huo upinzani ambao unatakiwa ndio uwe rejea mbadala ya Taifa.

Huwezi kutaka mambo makubwa wakati huna maono ya kuyafanikisha mambo hayo.

Wewe huwezi kuona umuhimu wa standard gauge leo hii, lakini itakapokamilika treni ya umeme kutoka Dar mpaka Burundi, hao wanaoishi kando kando yake watawasimulia wajukuu au watoto zako juu ya umuhimu wa usafiri huo.

Flyover zinao umuhimu ambao wakati huu wa ujenzi huwezi kuuona. Hayo mataifa makubwa ambayo waafrika tunaona fahari kwenda kuishi, hayakujengwa ndani ya miaka 56 ya uhuru wao.

Ujerumani ilianza kujengwa upya baada ya vita kuu ya pili. Japan ilipigwa bomu zito pale Hiroshima. Marekani mwaka jana imefikisha miaka 240 ya uhuru.

Hatuhitaji kichwa cha Yohana, kwa sababu hakuna short cut ya kutufikisha kwenye nchi ya ahadi.

Kuifikia nchi hiyo ni mchakato wa miaka mingi, pengine sisi wa kizazi cha sasa turidhike tu na ule ukweli kwamba watakaokuja kuiona Tanzania yenye neema ni wale watakaoishi miaka mingi kutoka leo hii.
Kwahiyo kwako wewe Maendeleo kwenye Taifa ni vitu
 
Mkuu sheria Mama inaweza kuwepo, lakini hakuna nchi inayoweza kuikwepa kauli kuu ya kiongozi mkuu wa nchi.

Kiongozi mkuu anaweza kuwa na udhaifu wake mwingi lakini bado hatujafikia huko ambako mamlaka ya rais yanaweza kupunguzwa kwa ghafla tu. Ni mchakato wenye kuhitaji muda. Na wakati tunaelekea kwenye ukamilifu wa mchakato huo, basi na tuwe tayati kuuishi uhalisia wa mambo.
Hapa ndipo mnapoharibu
Mnasema muda bado LINI??
 
Back
Top Bottom