Tunaenda ICU!

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,956
22,144
[h=3]Tunaenda ICU![/h]

Baadhi ya Wanaume baada ya tendo la ndoa hujikuta hoi bin taabani.
Na wanawake wengi hulalamika sana na hii tabia ambapo mwanaume akishamaliza tu hujikoka usingizi na kuanza kukoroma within seconds.
Na hali huwa mbaya zaidi kwani kabla ya sex mwanamke hakuandaliwa kwa muda wa kutosha na mwanaume anamaliza haraka hata kabla mwanamke hajafikishwa popote na kitu cha ajabu zaidi mwanaume akimaliza analala fofofo.

Pia Wanaume wenyewe hawawezi kuondokana na hili kwani ni suala la kisaikolojia na lipo nje ya uwezo.
Hata hivyo akijifunza anaweza kuwa tofauti.

Mwanaume huweza kutengeneza mbegu (semen) kila baada ya masaa 42 hadi 72 na hiki kitendo husababisha mgandamizo wa kimwili wa kutaka kuzitoa kwa njia ya sex.
Pia wanasayansi wanasema kwamba kila drop moja la majimaji ya mbegu za kiume (seminal fluid) huwa kunakuwa na zaidi ya mbegu za kiume milioni 300 na mwanaume ana uwezo wa kutoa hizo mbegu kupitia sex (ejaculation) mara 2 au 3 kwa siku.

Kitendo cha kutoa hizo mbegu huhusisha nguvu za kimwili na kihisia na huwa na pressure kubwa sana wakati zinatoka na kumfanya mwanaume kuwa hoi kabisa.
Huo utoaji wa nguvu ni kama mlipuko wa nje wa bomu (outward explosion) tofauti na mwanamke ambaye kwake huwa internal/ inward/inside explosion.

MENGINEYO
Pia wanaume wanaoishi vijijini Utafiti unaonesha kwamba wao hushiriki tendo la ndoa mara nyingi zaidi kuliko wanaume wa mijini, hii ni kutokana na wanaume wa mijini kukumbana na misukosuko ya maisha na kuathirika kisaikolojia hivyo kuathiri mwili kutaka sex.

Wanaume huwa frustrated sana na wanawake kwa sababu wanawake mara nyingi hawapendi sex.
Wanawake nao huwa frustrated sana na wanaume kwa sababu wanaume kila wakati wao wanataka sex.
Wanawake wanawalaumu wanaume kwa sababu hawajui kupenda.
Wanaume nao wanawalaumu sana wanawake kwa sababu wanaongelea sana upendo lakini hawataki kuweka katika vitendo (sex)
Binadamu hufanya mapenzi kwa sababu ya homoni ya testosterone ambayo kwa kiasi kikubwa ni kwa wanaume.
Mwanaume wa kawaida huzalisha hii homoni mara 20 kuliko mwanamke, ndiyo maana mwanaume anakuwa na drive kubwa ya sex.

Hii ina maana kwamba jinsi mwanaume anavyojisikia kukosa sex kwa siku moja ni sawa na mwanamke anavyojisikia kukosa sex kwa siku 20.

Mwanaume anaweza kuzalisha mtoto kila anapofanya mapenzi wakati mwanamke anaweza kuzaa watoto kwa kila baada ya miaka miwili, hii ina maana kwamba mwanamke anatakiwa kuchagua nani anatakiwa kuwa baba wa mtoto.Wanaume siku zote wanatafuta quantity wakati wanawake siku zote wao ni kutafuta quality.

Ndiyo maana wanaume hutafuta sex kwenye mahusiano na wanawake hutafuta upendo.
Kwa mwanamke upendo ni proof kwamba mwanaume atabaki kwake na kuwa naye wakati wanaume wao baada ya sex ndiyo hujisikia mwanamke anampenda.

Men fall in love through sex; women fall in sex through love.
 
Busu hiloooooooo pokea! Busu husaidia kuwezesha moto wa mahaba kuendelea kuwaka kati ya wapenzi.
Kumbuka mpenzi wako huhitaji kujisikia yupo appreciated na zaidi anapata mapenzi (love and affection) kutoka kwako na njia nzuri ni kumpa busu.

Bahati mbaya ni kwamba wanandoa wengi wameshikwa na kunaswa na mtego wa u-busy hadi imefika wanasahau kuwabusu wapenzi wao.
Niambie wewe unayesoma sasa hivi hapa umembusu mke wako au mume wako lini?
Nahisi umesahau!

Plainly; mahusiano yanahitaji kazi, hasa kwa huyo special someone wako in your life kama ulifanya kazi kumpata kwa nini sasa ulegeze kamba, kaza uzi hakikisha uzi uleule uliotumia kumpata ndo huohuo unatumia kudumisha penzi na si kudumu tu bali linakuwa sustainable.

Kubusu hujenga intimacy kati ya mke au mume pia hufanya bonding iwe strong na kuhufanya wewe mwenyewe ujisikia vizuri na afya njema.

Nini faida za kubusu kiafya?
Busu ni afya kwa meno yako, wataalamu wamefanya tafiti na kugundua kwamba busu kuzuia plague kujijenga kwenye meno na hii ina maana utapunguza safari kwa daktari wa meno.

Busu ni afya kwa moyo wako (heart) kwani wakati wa kubusiana mnazalisha adrenaline ambazo husababisha moyo kuongeza speed na damu kwenda sehemu zote za mwili.

Kila mwanaume au mwanamke ambaye humuaga mwenzake asubuhi kwa busu utafiti unaonesha anaongeza miak 5 zaidi kuishi duniani.
Kama huwa hubusu wakati unaagana na mwenzi wako asubuhi unajipiga panga miaka 5 kuishi.

Kubusu hukuongezea self esteem na kujisikia upo appreciated kwani busu ni tamu na raha.

Mabusu hupunguza kuzeeka (aging) kwani mnapobusiana huhusisha misuli zaidi ya 29 kwenye eneo la mashavu na shingo.

Kubusu huchoma calories kati ya 6 – 12 na mkiongeza na love making huweza kufikia 300 na utajisikia raha.

Kubusu huondoa stress, huweza kutoa ocytocin, homoni ambayo hufanya mtu kujisikia vizuri.

Hakikisha unapobusu ni zaidi ya sekunde 10 ili kupata matokeo.

Hivyo basi wewe na mpenzi wako go ahead, kwa afya na furaha sherehekea kila siku kwa kupigana mabusu.

Je, kuna aina ngapi za mabusu?

Tutaendelea.............................................................​
 
Eti unaweza kumjua mwanamke bikira kwa kumwangalia jinsi anavyotembea! Kutokana na maandiko ya agano la Kale (Biblia) (Kumbukumbu la torati 22:13 17)
Wanaume wa kiisraeli walikuwa wanatahiriwa (circumcision) na hiki kitendo cha kutahiriwa au kukata govi (foreskin) kilikuwa ni agano (covenant) na Mungu wao, agano la damu kwa maana kwamba ubikira wa mwanaume ulitolewa kwa Mungu.
Hii ilikuwa na maana kwamba mwanaume sasa alikuwa ni mali ya Mungu (belong to God).
Kwa kutahiriwa damu ilitoka na damu kutoka ni kuonesha kutoa bikira na yeye kuwa na mahusiano na Mungu.

Mwanaume aliunganishwa na Mungu ambaye sasa anakuwa chanzo cha uwezo wake.
Agano la mwanaume na Mungu lilihitaji damu kutoka katika govi la uume na si katika sehemu nyingine ya mwili wa mwanamke kwa sababu uume ndiyo ulitumika pia kwa kuvunja kizinda (hymen) mwanamke kutoka damu kwa ajili ya agano kati ya mwanaume na mwanamke mbele za Mungu kuwa kitu kimoja.

Hii ina maana kwamba kwa mwanamke bikira kutoa damu ni muhuri wa agano kati ya mwanaume na mwamke mbele za Mungu.

Je, katika agano jipya bado tunahitaji damu ya binadamu kwa ajili ya agano?
Baada ya Yesu Kristo kuja yeye alitoa damu ya thamani msalabani ambao hutuunganisha wanadamu wote na Mungu.
Mwanaume na mwanamke wote wanaunganishwa na damu ya Kristo na wao kwa pamoja wanakuwa bikira (bibi harusi mtarajiwa) hadi siku Yesu akija kulichukua kanisa na kila mmoja ambaye atakutwa hana bikira maana ataachwa.
(Kama umeokoka utanielewa nazungumzia kitu gani)
Hivyo basi suala la msingi hapa si mwanamke kuwa bikira na kutoa damu ya agano kwa mume au mume kutahiriwa kutoa damu ya agano kwa Mungu bali kuikubali damu ya agano jipya ambayo ni Yesu Kristo.
Kumpokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi ndiyo ubikira wa kweli

Je, inawezekana mwanamke bikira kuwa na mimba?
Ndiyo inawezekana, ikitokea sperms zinkawa deposited nje ya uke hata kama hakukuwa na penetrative sex kwani sperm ni genius au smart sana zikipata mwanya hasa kutokana na kufunguka kwa vitundu kwenye kizinda (hymen)

Je, ukiwa Bikira muda mrefu unaweza usizae watoto?
Uwongo mtu hasa kama mwanaume bado ana uwezo wa kuzalisha sperms na kama mwanamke bado anapata siku zake.

Je, unaweza kujua bikira kutokana na anavyotembea?
Thubuti! Hakuna external signal ambayo huweza kukufahamisha kama kweli mwanamke ni bikira au mwanaume ni bikira ukweli anajua yeye.

Je, Ukisubiri sex hadi uolewe au uoe ni mshamba kama si xxxxx?
Ukweli ni kwamba wewe ni smart sana kuliko wajinga wote wanaojiingiza kwenye masula ya sex kabla ya ndoa, Wazinzi na waasherati hawana nafasi katika ufalme wa Mungu.
Pia kusubiri kunakufanya uishi kwa amani na kutimiza malengo ya maisha bila hofu ya UKIMWI.

Je, Ukiwa in love na mtu lazima mfanye mapenzi?
Kuwa na mpenzi haina maana sex lazima, Pia inatokana na mipaka mliyowekeana.

Je, kwa mwanamke kudumisha urafiki na mwanaume sex ni muhimu?
Ukweli unajidanganya, kama urafiki wako ok shaky kiasi hicho kumbuka sex si tiketi ya kukufanya akupende zaidi bali tiketi ya kukupiga chini muda wowote na yeye kubeba kitu kipya kabisa.
Kama huamini nitumie email nitakupa mifano zaidi ya 100.​
 
Uchumba ni mtamu acha kabisa, ila kumbuka ndoa ni kitu halisi!
(Picha kwa hisani ya YM - Arusha Tanzania)
Kumekuwa na maswali mengi sana naulizwa na vijana wengi wa kike na wakiume ambao wanataka kujua ni yupi anaweza kuwa mchumba halisi ambaye atakuwa mke au mume wake.

Ukizingatia kwamba kuoa au kuolewa ni uamuzi ambao unaweza kupelekea kuwa mtu wa furaha katika maisha yako au mtu huzuni na kujuta siku zote katika maisha yako.
Mambo ya msingi kuangalia ni haya:

MAHUSIANO HUWA RAHISI TANGU SIKU YA KWANZA:
Tangu siku ya kwanza nilipojikuta naonana uso kwa uso upendo uliokuwa kati yangu na yeye ulikuwa natural, nilijihisi nimemuona mwanamke ambaye namfurahia kila kitu, namkubali kama alivyo, nilihisi kama tulizaliwa tuishi pamoja na sasa nimempata mtu ambaye nimekuwa namtafuta, nilijiona atanitosheleza kimwili na kiroho, ninapoongea nayenaridhika kwa mvuto alionao.
Kila kitu katika mahusiano na urafiki wetu kilikuwa natural na kutupa hisia mpya kabisa hapa duniani.

Wapo ambao katika safari ya uchumba hadi ndoa hufikia kuzipiga na kugombana mara nyingi sana, leo wanazipiga au kununiana au hugombana na kesho wanapatana tena na kurudiana.
Wanaendelea na kasheshe hizo hizo mara kwa mara hadi wanaoana.

Inawezekana unarudiana naye labda kwa kuogopa ukiachana naye hutapata mtu mwingine wa kuoana naye, au umri unaona umeenda sana, au unataka kuondoa nuksi ili na wewe ujulikane uliolewa, au rafiki zako watakucheka au una hamu sana na sex, Kumbuka ni busara kuachana wakati wa uchumba kuliko kuachana ikiwa ndoa.
Ukiingia kwenye ndoa utakumbana na storm ambayo itakuja kupima kama sababu zako za kuoana zilikuwa strong kuliko storm yenyewe na kama zilikuwa weak storm itakuchukua bila huruma.

UHUSIANO MZURI NA FAMILIA, NDUGU NA MARAFIKI:
Inaweza kuwa tofauti kidogo hasa linapokuja suala la dini, kabila, nk kwani mara nyingi wazazi na familia nyingi huwa na lao kuhusu kabila au dini.
Ikitokea kwamba mchumba wako ni kabila moja, dini moja na bado ndugu zako, familia yako au marafiki zako hawaelewani naye ni vizuri kufikiria upya.
Wewe umelelewa na familia na kutokana na hayo malezi ndivyo ulivyo na umempata huyo mchumba kutokana na tabia yake aliyokulia au kulelewa na hiyo familia na kama bado hakubadilika maana yake hapo kuna bendera nyekundu inawaka na inaashiria kuna kitu hakipo sawasawa.

Kawaida ukishaingia kwenye mapenzi (fall in love) huweza kupunguza uwezo wako wa kuamua na kuona kasoro ndiyo maana wanasema love is blind.
Hii haina maana kwamba unatakiwa kuvunja mahusiano eti kwa sababu ya ndugu, familia au marafiki hawakubaliani na huyo mchumba wako ila ni kawaida kwamba inawezekana kuna kitu ndugu zako na familia yako wanakiona na wewe hukioni ambacho mbele ya safari mkiwa kwenye ndoa unaweza kukumbana nacho na bahati mbaya umewakana wazazi ndugu na marafiki.
Utaenda kwa nani kuomba ushauri maana umekuwa kichwa ngumu.

Jaribu kuchunguza kile ambacho ndugu zako au familia au marafiki wanasema vibaya kuhusu huyo mtu wako inawezekana ni kweli.
Ni kawaida kama umepata mtu wa kufanana na wewe basi huweza kujichanganya kirahisi sana na ndugu zako, familia yako na marafiki zako.

HUTAONA KITU KIKUBWA CHA KUMBADILISHA:
Kawaida, hata kama mnapendana kuliko binadamu yeyote chini ya jua, bado tofauti ndogondogo zitakuwepo; hata migogoro itajitokeza pia.
Ila kama kuna jambo kubwa sana unaona ni muhimu sana yeye abadilike basi hiyo ni ishara kwamba fikiria kwa makini.

Tatizo ukishashambuliwa na chemicals za love unaweza kujikuta unadhania kwamba haina shida kwa tatizo au kasoro alizonazo na utavumilia.
Ukiingia kwenye ndoa chemistry ya mapenzi hushuka na kupanda kutokana na jinsi mnavyojitahidi kuimarisha ndoa yenu; hapo ndipo sasa utagundua kwamba ulichemka and too late.
Usiingie kwenye ndoa ukidhania utambadilisha mtu sana sana wewe ndo utabadilishwa.
Kama umegundua kuna kitu ambacho ni tatizo kubwa sana mbele ya safari na hutaweza kuishi nacho ni vizuri ku move out kuliko kupoteza muda wako na kujifariji na baada ya miaka 3 ya ndoa ujikute upo kwenye jehanamu yako mwenyewe na upweke uliokithiri.
Watu hupata upweke lakini upweke wa kwenye ndoa ni mbaya kuliko upweke mwinghine wowote duniani.

NI RAFIKI
Mvuto wake ni kitu muhimu sana katika mahusiano.
Ndani ya mahusiano lazima kuwa na mzizi mkuu wa urafiki ambao hata mkiwa wawili sehemu yoyote duniani bado mnajiona hamjapungukiwa na pia bado mnajiona ndiyo marafiki bora duaniani.
Je, unajiona unahitaji kutumia muda na yeye tu?
Je, unajisikia raha kuwa na yeye wawili tu?
Je, unahisi yeye ndiye anastahili wewe kumwambia siri zako na kwamba ni yeye tu anakufahamu kuliko mtu yeyote duniani, kama ni NDIYO, basi mshike vizuri.
Kuwa best friends hata baada ya kuoana ni raha sana, na ndoa hudumu, maana hakuna anaye bore mwenzako.

UNAPOFIKIRIA KUOANA NAYE HAIKUPI SHIDA:
Kama unajikuta unapofikira kuoana naye huna wazo lingine la kuhisi ndoa inaweza kuwa na matatizo na unajisikia amani ya kweli moyoni na kwamba future yako na yeye itakuwa sawa basi umepatia.

Mwisho Kumbuka Kumuomba Mungu akupe amani ya kweli na huyo mtu wako maana yeye ndiye anajua liubavu lako lipo wapi.

“Marriage is not about finding a person you can live with, it’s about finding the person you can’t live without.”

 
[h=3]Wapo wengi![/h]

Kuna maboksi mengine kabla ya kuyabeba fikiria kwanza! Wakati mwingine huwa tunajikuta tumebeba maboksi ambayo tunadhani ni yetu na kwa furaha kubwa huwa tunawaringishia wengine hasa kutokana uzuri wa boksi kwa nje tukitegemea na ndani litakuwa na kitu kizuri.
Hata hivyo tukifika majumbani tunashangaa kuku vitu vilivyomo ndani ya boksi ni kinyume chake.


Maisha ya mahusiano nayo wakati mwingine ni kama kubebeshana maboksi tena kwa hiari kabisa.
Tatizo huanza pale box lenyewe likijua kwamba wewe ni mbebaji mzuri basi utachakaa kwa kubeba hili boksi.
Na linaweza kuwa ni boksi lililokuja na viboksi vingi ndani yake kama vile hasira, ukari, au manyanyaso ya kila aina, maneno magumu na mazito ambayo hukuumiza zaidi ya kupigwa ngumi na mateke, yaani unajikuta umeruka majivu na kukanyaga moto.

Kuna kitu kinaitwa “Narcissism” hili ni neno la kigiriki lenye maana ya mtu kuipenda zaidi nafsi yake kuliko kawaida (extreme self-loving).
Hili Neno linaendana na story ya kijana wa Kigiriki ambaye alivutiwa na taswira yake mwenyewe kwenye bwawa kiasi cha kushindwa kuondoka hadi alifia hapo.

Hili tatizo huanzia wakati mtu bado mtoto mdogo hasa baada ya kukosa upendo na anapokuwa mtu mzima anakuwa hajui maana ya kupenda na kupendwa.

Utafiti unaonesha ni asilimia 75 wana kaasili ka narcissists.
Na Adolph Hitler alikuwa kinara wa hizi tabia ingawa huyu alikuwa hatari hata hivyo tunao akina Hitler wengi sana kwenye mahusiano yetu ya kila siku.

Hawa akina Hitler wanachofanya ni kukubebesha kiboksi cha wewe Kujiona una hatia, wanakupa hofu, woga, mashaka, wanakufanya usijiamini ili wakupelekesha wanavyotaka wao.
Hawa wanaweza kukudhalilisha kimwili, kimapenzi, kihisia na pia wanaweza kuzira kuongea (silence) na wanachofanya ni kuku-control wewe idara zote za maisha yako unakuwa kama mfungwa fulani kwa kuwa umeingia kwenye anga zao.

Hata unapoishi nao unakuwa unaishi maisha ya mateso, mtindo wa jela na kunyimwa uhuru.
Hii aina ya mahusiano ni hatari tupu na huhitaji msaada wa ushauri kwa wataalamu wa masuala ya ndoa na mahusiano.

Wengine ni watu wenye status kubwa katika jamii zetu anaweza kuwa mameneja, wahadhiri wa vyuo vikuu, matajiri, wabunge au mawaziri na hawa watu huonekana watu wa heshima kubwa sana mbele ya jamii kwani ni wapole, wema, watii, ni marafiki, wastaarabu, wamevaa ngozi ya kondoo huku ndani ni mbwa mwitu wakali na wenye njaa.
Hawa watu ni lethal.

Ukifanya kosa moja tu kwao unastahili kupewa adhabu ambayo utajuta kuwa naye katika maisha.
Hawa wanaume au wanawake hufurahia sana kutesa wake zao au waume zao, hawana huruma na hawafai kabisa katika jamii.

Tupendane katika ndoa zetu
 
Kwakweli ni rehema ya Mungu itumike tu kutuokoa watoto wake na makwazo ya hii dunia!
 
mara nyini wanawake bikira huwa wana aibu sana halafu ni wagumu sana kuingilika, wagumu kuomba mzigo na mara nyingi hawajui kuwa marafiki na oposite side....ana aibu sana usoni, hajui kujieleza wala kujitetea kwenye masuala hayo, zaidi ya yote atakutoa baru tu uondoke....iyo ni kabla hajaonjeshwa, akija onja tu, analegea hadi mwisho na kila kitu anakuwa fundi ...kuanzia maneno hadi vitendo.
 
hahaha, mimi huwa nakuwa hoi, kwasasa nimeacha kabisa kupiga mzigo asubui kabla ya kwenda kazini, kwasababu siku nzima nitalala kazini kwenye meza...
 
Loo. Hiyo ni kweli. Lakini picha yako mimi binafsi nime..... saaana nawe. sijui twaweza wasiliana?
 
Loo. Hiyo ni kweli. Lakini picha yako mimi binafsi nime..... saaana nawe. sijui twaweza wasiliana?

soma kwanza ukue kiakiliusije beba box lenye uzito zaidi yako ukamlaumu Mungu
 
Back
Top Bottom