real life skills
JF-Expert Member
- Jul 16, 2021
- 233
- 236
Huyo Chakubamga ni mnafiki kama shetani. Anatafuta attention kwa kuhujumu serikali ya chama chake mwenyewe. Ingekuwa raisi Samia ni dikteta kama alivyokuwa hayati Magufuli,chakubanga angekuwa ameshafanywa kitu mbaya!Waungwana Asalam aleykum!
Nimemfuatilia ndugu yangu Humphrey Polepole kwenye darasa lake la uongozi kwenye utube, nami nimebaini yakuwa anafanya Jambo jema Sana kwa Taifa.
Naamini mutakubaliana na Mimi kuwa elimu ni Jambo la msingi Kati ya Mambo muhimu tunayohitaji Kama Taifa.
Ndugu Humphrey Polepole anatoa mada mzuri za elimu na anapata uungwaji mkono na watu wengi
Inachofurahisha ni kwamba mada zake hazitetei chama chochote, dini yoyote Wala kabila lolote, kitu ambacho ni Nadra kukiona, kwa watoa mada wengi, wengi wao huegemea kutetea maslahi yao, chama Chao au hata dini yao
Kwakweli Taifa litafakari hili na liunge mkono
Kila chama kitengeneze kipindi Cha kuelimisha watu juu ya masuala ya Taifa na chama Chao, kwa wiki au kwa mwezi watu wasikilize na waulize maswali na wapewe ufafanuzi
Wizara mbalimbali, ama ofisi za mikoa, bunge, ama mahakama pia jeshi la polisi, warushe vipindi Kama hivi kuelimisha watu juu ya masuala yote yanayoendelea katika idara zao, watu wasikilize na kuhoji pia
Nimeshangaa watu wanapiga simu kwa Humphrey Polepole wanahoji Mambo ambayo walipaswa kuulizwa watu wengine serikalini, Kama vile ishu za tozo, na chanjo
Cha kushangaza baadhi ya watu wanabeza juhuji hii ya Polepole, eti kwa Nini asifanye enzi za mwendazake.
Hivi mnasahau Mama Samia alinyamaza kimya enzi za jiwe na Sasa anachukuwa hatua kadhaa zilizo kinyume?
JPM pia alinyamaza kimya enzi za JK na akachukuwa hatua alipopata urais?
Ukimfuatia JK, Mkapa, pia Mwinyi utagundua yapo Mambo walikaa kimya, na waliyachukulia hatua walipopata urais
Tatizo la chama changu CCM, wanajua kuunga juhudi kwa anachofanya mwenyekiti tu. Haya ya Polepole yangekuwa ni ubunifu wa Raisi ungeona mapambio, na hekaheka za kila mteule wa Raisi kuunga juhudi!
Jamani, Polepole anaupiga mwingi, Tumuunge mkono!
Chakubanga ni wa kupuuzwa tu. Hana lolote uchu wa madaraka unamsumbua na kwa kuwa nchi hii kuna wajinga wengi,kuna watu wanamsikiliza,but the guy is useless and hopeless kabisa!