Tumia silaha kuu nne

Tumia silaha kuu nne

a sinner saved by Christ

JF-Expert Member
Joined
Feb 19, 2017
Posts
2,457
Reaction score
2,658
TUMIA SILAHA KUU 4

TUMIA SILAHA KUU 4


Silaha ya kwanza
1)usitende dhambi jitahidi usitende dhambi na tubu dhambi zako mara kwa mara,samehe watu waliokukosea,usilale na hasira usikasirike,usiogope woga usiwe na hofu wala woga,uwe na imani kuu amini Yesu anaweza yote,na wewe unayaweza yote kupitia Yesu..((TUBU DHAMBI MARA KWA MARA,JIEPUSHE KUTENDA DHAMBI)

2)SADAKA YA ZAKA katika kila pesa unayopata peleka zaka kanisani moja ya kumi..na jitahidi kusaidia masikini na yatima ,wagonjwa wasiojiweza.Kutoa misaada

3)DAMU YA YESU NA (4) NENO LA MUNGU
Ufunuo 12:11
Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao

Damu ya Yesu ndio iliyotukomboa na kutunya washindi na kufanya watoto wa Mungu,hii damu ya Yesu ndiyo iliyolipa deni zetu zote na kufuta mashitaka yetu yote ..inatushindia VITA VYOTE(KUPITIA DAMU YA YESU)

4)Jaza neno la Mungu kwa wingi moyoni mwako..soma sana biblia hifadhi maneno ya biblia kichwani mwako na moyoni mwako.

NENO la Mungu lenyewe lina uwezo wa kuyafukuza mapepo yote yakatoka yakakimbia na yasirudi tena
SOMA NENO LA MUNGU biblia kila siku

Ebr 4:12
Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo
.
 
hongera sana kwa kumpokea YESU umefanya uamuzi sahihi sana ,umefanya vizuri sana kuamua kumuamini Yesu,umeshampata Yesu umepata yote.,umefanywa kuwa MTOTO WA MUNGU..hongera sana.

Yn 1:12
Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake

HATUA YA KWANZA YA KUFANYA.
1)TUBU dhambi zako zote tena ukiweza kuzitaja kabisa ,dhambi za kuendea miungu mingine,dhambi za mababu na mabibi ,na mwambie Yesu naomba unisamehe dhambi yeyote niliyoifanya ambayo kwako kwa mawazo,maneno ,matendo naomba Yesu unisamehe leo.

2 Nya 7:14
ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao.



Mt 11:28-30
Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

Isa 1:18
Haya, njoni, tusemezane, asema BWANA. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu.

2)KIRI KWAMBA YESU KRISTO NI BWANA NA MWOKOZI WAKO NA HAKUNA MUNGU MWINGINE ILA YEYE TU,
KIRI YESU KRISTO NI MWANA WA MUNGU na Kiri kumtegemea Yesu tu ,na Kumuamini Yesu ,tu SEMA Yesu wewe ni mwamba wangu,nguvu zangu,msaada wangu ,tumaini langu,chanzo cha uhai wangu..nakutumaini wewe peke yako.
Karibu Yesu ukae ndani yangu na mimi niwe ndani yako.

1 Yoh 4:15
Kila akiriye ya kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu, Mungu hukaa ndani yake, naye ndani ya Mungu.

2 Kor 5:17
Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya.(wewe sasa hivi ni mtoto wa Mungu Yesu umezaliwa upya ndani ya Kristo.)

yesu aliyeko ndani yako ana nguvu kubwa sana kuliko hayo mapepo.

1 Yoh 4:4-6 SUV
Ninyi, watoto wadogo, mwatokana na Mungu nanyi mmewashinda, kwa sababu yeye aliye ndani yenu ni mkuu kuliko yeye aliye katika dunia

2)HATUA YA PILI NI kufunga milango iliyobomoka katika ukoo wako ikaruhusu hayo mapepo yawatese familia yako.

hayo mapepo yaliwaingia kwa sababu yalifunguliwa mlango na mababu zenu na mabibi zenu ukoo ,waliwakabidhi kizazi chenu na watoto wenu na wajuu kizazi hadi kizazi kwa majini,mizimu,mapepo kwa shetani.

kwa sababu mlango iliyobomoka bado haijafungwa bado utaendelea kuteseka...natala nikusaidie jinsi ya kufunga hiyo milango.

tumia NENO kutoka kitabu cha EZEKIELI 22:30.

Ezekieli 22:30
Nami nikatafuta mtu miongoni mwao, atakayelitengeneza boma, na kusimama mbele zangu mahali palipobomoka, kwa ajili ya nchi, nisije nikaiharibu, lakini sikuona mtu

Sema hivi Mungu baba mimi mtoto wako nasimama mbele zako kama kwa ajili ya kuziba kujenga mahali palipobomolewa na mababu na mabibi ambao walitukabidhi sisi na vizazi vyetu kwa mapepo mizimu ,laana za ukoo ,uganga wa kienyeji...nasimama hapa kujenga na kuziba palipobomolewa,..uharibifu na mabaya na roho za mauti na kizimu zositupate tena katika ukoo wangu,kwa jina la Yesu.

sema hivi kila siku asubuhi unapoamka kabla hujafanya jambo lolote na usiku kabla ya kulala kwa siku 21 mpaka 30.

(hapa mapepo yote yatakimbia)

pia ongezea na neno linalosema.

Yak 4:7-10
Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia*


3)HATUA YA TATU.

FUFUA NA KURUDISHA UHAI KATIKA VITU VYAKO VILIVYOKUFA kwa sababu ya kutawaliwa na mapepo ya shetani mizimu ya uganga wa kienyeji..maana adui yetu ni mwizi,ni mchinjaji na muharibifu..
unapokaliwa na mapepo lazima ataleta mauti kuua na kuharibu kuchinja na kuiba viti vyako vya ndani yako,kama UCHUMI wako,afya yako,kibali chako,baraka zako.na anakuacha mifupa mikavu iliyokufa


tumia neno la EZEKIELI 37:1-15
Toa unabii iambie mifupa mikavu iliyokufa katika maisha yako ifufuke.

sema hivi ewe afya yangu uliyokufa na kuwa mifupa mikavu,natoa unabii,sikia neno la Mungu pumzi ya Mungu ikuingie ukapate kuishi kuanzia sasa kwa jina la Yesu.

semea maeneo yote ya maisha yako yaliyokufa kama ni ndoa yako,kama ni uchumi wako..chochote semesha kiambie sikia neno la Mungu ,pumzi ya Mungu ikuingie upate kuishi sasa ,kwa jina la Yes na kwa damu ya Yesu.

fanya hivi kila siku asubuhi unapo amka na usiku unapolala kwa muda wa siku 30(utafanikiwa).
 
Isa 54:17 SUV
Kila silaha itakayofanyika juu yako haitafanikiwa na kila ulimi utakaoinuka juu yako katika hukumu utauhukumu kuwa mkosa. Huu ndio urithi wa watumishi wa BWANA, na haki yao inayotoka kwangu mimi, asema BWANA.

Zab 91:10
Mabaya hayatakupata wewe, Wala ugonjwa wowote / tauni haitaikaribia hema/nyumba yako.
Maana Mungu atawaamuru malaika zake, wakulinde popote uendapo Watakuchukua mikononi mwao, usije ukajikwaa kwenye jiwe.
Utakanyaga simba na nyoka, utawaponda wana simba na majoka. Mungu asema: “Nitamwokoa yule anipendaye; nitamlinda anayenitambua! Akiniita, mimi nitamwitikia; akiwa taabuni nitakuwa naye; nitamwokoa na kumpa heshima. Nitamridhisha kwa maisha marefu, nitamjalia wokovu wangu.”

Zaburi 118:17
Sitakufa, bali nitaishi, nami nitayasimulia matendo makuu ya, Mungu.

Zaburi 35
1 Ee Bwana, utete nao wanaoteta nami, Upigane nao wanaopigana nami.

2 Uishike ngao na kigao, Usimame unisaidie.

3 Uutoe na mkuki uwapinge wanaonifuatia, Uiambie nafsi yangu, Mimi ni wokovu wako.

4 Waaibishwe, wafedheheshwe, Wanaoitafuta nafsi yangu. Warudishwe nyuma, wafadhaishwe, Wanaonizulia mabaya.

5 Wawe kama makapi mbele ya upepo, Malaika wa Bwana akiwaangusha chini.

6 Njia yao na iwe giza na utelezi, Malaika wa Bwana akiwafuatia.

7 Maana bila sababu wamenifichia wavu, Bila sababu wameichimbia shimo nafsi yangu.

8 Uharibifu na umpate kwa ghafula, Na wavu aliouficha umnase yeye mwenyewe; Kwa uharibifu aanguke ndani yake.

9 Na nafsi yangu itamfurahia Bwana, Na kuushangilia wokovu wake.

10 Mifupa yangu yote itasema, Bwana, ni nani aliye kama Wewe? Umponyaye maskini na mtu aliye hodari kumshinda yeye, Naam, maskini na mhitaji na mtu amtekaye
 
KILA MTOTO WA MUNGU ANAYEMCHA MUNGU (ana ulinzi wa UKINGO/UKUTA kutoka kwa Mungu unaomzingira pande zote yeye pamoja na mali zake kama mtumishi wa Ayubu)

Ayubu 1:10
Wewe hukumzingira kwa ukigo pande zote, pamoja na nyumba yake, na vitu vyote alivyo navyo? Kazi za mikono yake umezibarikia, nayo mali yake imeongezeka katika nchi.

Lakini adui yetu,mshitaki wetu shetani huzunguka kama simba aungurumaye akitafuta mtu ammeze (1 Petro 5:8) na huyu adui yetu kazi yake ni kuiba,kuchinja na kuharibu(yohana 10:10)

Wakati mwingine huyu adui yetu anaua na kuiba vitu vyako vya ndani kama NDOA yako,UCHUMI wako,IMANI yako au hata afya yako hata kama kwa nje unaonekana upo sawa ,ila kwa ndani ameshakumaliza unabaki kama kasha tupu,kopo tu kwa nje zuri ndani halina kitu.

SIFA YA VITU VYAKO VYA NDANI VILIVYOKUFA
NDOA iliyokufa ndani...wanandoa hawazungumzi pamoja ,tena wanaweza wakaishi kila mmoja na chumba chake,upendo wao unapoa unafutika kabisa,wanachukiana ,wanalaumiana kila mmoja ana mshutumu mwenzake mbaya,kupigizana makelele.

UCHUMI uliokufa...umasikini..kufikisika,pesa kupotea,kufunga kwa milango ya fursa za biashara na uchumi zilizokuwa wazi mwanzo,kupata pesa kwa shida kazi kubwa kama tembo mapato kiduchu kama panya,na hata ukipata matumizi mengi yanaibuka kuimaliza,madeni makubwa kuliko uwezo wako,wale watu waliokuwa wanakusapoti kwa fursa za kiuchumi kujitenga mbali,kila jitihada za kujikwamua kiuchumi zinafeli

AFYA..magonjwa yasiyo isha maradhi kuugua mara kwa mara..maradhi sugu

FANI YAKO NA UJUZI
Kudumaa hata kama una ujuzi hupigi hatua wala hupati fursa,haunufaiki kwa kiwango stahili na fani yako na hupigi hatua unadumaa.

TABIA ZINAZOPELEKEA KUPASUKA/KUVUNJIKA NYUFA KATIKA KUTA/UKINGO WA ULINZI WA MUNGU..unaokuzingira mtoto wa Mungu.
Ukuta/ukingo ulinzi wako kutoka kwa Mungu hupasuka na kuweka uwazi pale mtoto wa Mungu anapofanya mambo yafuatayo.

1)DHAMBI ZISIZOTUBIWA/kutokutubu dhambi zetu haraka kwa wakati mapema sana .
Dhambi zisizotubiwa zinabomoa ukuta..(dhambi zenu ndio zina achilia mauti ,ndio zinawatenga na Mungu hata asiweze kusikia,hata sadaka za mtu mwovu ni chukizo.
Ni lazima kuishi maisha ya TOBA kila wakati TUBU DHAMBI kila mara ,mtakatifu na azido kutakaswa..

2)LAANA ZA UKOO
wazazi wetu mababu na mabibi walitenda dhambi kabla yetu hata kabla hatupo ila maovu yao tunapatilizwa yametupata sisi hata kizazi cha tatu na cha nne,unakuta walitambikia MIZIMU,waganga wa kienyeji,wakaweka maagano kwa mizimu ,na majini ya ukoo yakatumiliki sisi na vizazi vyetu vijavyo..

3)KUTOKUSAMEHE watu,vinyongo kuweka vinyongo visasi moyoni

4)HASIRA CHUKI

5)MANENO YAKO mwenyewe ukijilaani mwewe bila kujua ,mfano unakuta mtu anajilaani mwenyewe bila kujua mfano anasema ,MIMI huu naona lazima nitakufa tu sitapona,au mimi ni wa kupata hasara tu,mimi siwezi,mimi sina uwezo,sina akili,kwetu wote huwa tuna ugonjwa wetu,kwetu hatuoi,..mimi ni masikini..n.k..UMENASWA kwa maneno ya kinywa chako mwwnyewe usijinenee mabaya

5)Uzinzi,ulevi n.k yani dhambi zote zinaingia kwenye point namba moja ya dhambi,lakini hapa nakuongezea point moja ambayo ulikuwa huijui...KUZURURA USIKU WA MANANE MBALI NA NYUMBANI KWAKO...mfano kuanzia saa sita usiku ukiwapo nyumbani kwako kuna ukingo wa ukuta wa ulinzi wa Mungu unaokulinda.

hapa nitoe mfano kabisa

kuna mtumishi wa Mungu tulikuwa tunamfuatilia kwa muda wa miaka miwili kupitia roho fuatilizi hapa tulitumia KIOO vitu vyote vya kioo kama vioo vya makabati ya nguo hasa vioo vinavyowekwa vyumba vya kulala vikitazama kitanda chako.(ni kama cctv kamera )

alikuwa mtumishi wa Mungu mtakatifu sana kwa muda wa miaka miwili ya kumfuatilia hatukuweza kumuangusha,alitumika kanisani kuhubiri,kufundisha vijana habari za ndoa akiwa na ndoa nzuri yenye upendo furaha na amani na familia yake.
Mtu wa maombi sana...yani mlokole kweli kweli..toa sadaka hakosi ibada ..na watu wote walimuona kama mfano wa kuigwa na mshauri wa watu..katika masuala ya kiroho na ndoa

tatizo lake lilikuwa moja tu ...*HASIRA KALI INAYOLIPUKA KAMA MOTO WA PETROLI"

ukuta wake ukingo wa Mungu ukaweka mwanya ukapasuka kwa hasira zake za mara kwa mara..

tukaanza kumshambulia kiroho..kidogo kidogo .hasira yake tukaiongeza mara dufu..tukaachilia roho ya umasikini..akaanza kupata changamoto za kiuchumi..tukaanza kumshambulia na mke wake..kumuwekea roho ya malalamiko/lawama

siku moja ametoka kazini amechoka na huko kazini bosi wake kamfokea sana kutokana na sisi kumuharibia hata kazini kwake kila anachofanya kinaonekana kibaya hata kazini..alipofika nyumbani kakuta mkewe anamsubiri na malalamiko kuwa hana msaada nyumbani hata hela ya saluni hajaacha,ada ya mtoto hajalipa,bili kadhaa za nyumbani mkewe kamjaza hasira kuwa hata nyumbani kwao ameanza kudharaulika kwa kumfananisha na wanaume wengine walio waoa dada zake shemeji zake wengine kuwa yeye ametia aibu na maneno mengine ...ya KUMJAZA HASIRA.

mwanzoni alijitahidi kubadilisha maongezi alihitaji kusali na kupumzika tu alijitahidi kunyamaza na kubadilisha stori..mkewe aliendelea kumoigia kelele kuanzia saa 4 usiku mpaka saa sita usiku na robo...jamaa alihitaji kula na kupumzika tu kulala kwa amani na kusali..lakini uvumilivu ukamshinda ...AKALIPUKA HASIRA akafungua mlango na kuanza kutoka nje ....mkewe na watoto wakawa wanamvuta asiondoke usiku abaki nyimbani huku wanalia ...akawasukumu akaondoka usiku huo...na hajui anakoenda anenda popote atakapokuwa ili mradi apate sehemu ya kutuliza mawazo yake mbali na makelele.

Bila kujua kuwa sisi ndio tunaosababisha hayo yote ni kazi yetu ya nguvu za giza.

HAPA ALIFANYA MAKOSA WAWILI kwa pomoja yanayozidi kubomoa ukingo wa ukuta wa ulinzi wa Mungu kwake.
1)KUONDOKA eneo la nyimbani kwake USIKU kuanzia saa6
2)AKIWA AMEJAA HASIRA.

kufupisha tulimsukumia roho ya ulevi...tulianza kidogo kidogo .kumuwekea burudani kidogo kwenye pombe na kuona kwamba pombe ndio inayomuondolea matatizo
baadae tukamuwekea URAIBU na utegemezi wa pombe...akawa mlevi sugu ..

NDOA ikavunjika baadae wakapeana talaka mke akarudi kwao na watoto.

baadae maisha ya IMANI yakashuka akaacha kusali.
mwanzo alikunywa pombe kwa siri kwa kujificha baadae kakawa mlevi sugu...

akageuka aibu mfano mbaya ..kwa jamii.

Mwisho wa siku ..so sad RIP.

IAMBIE MIFUPA MIKAVU ILIYOKUFA KATIKA MAISHA YAKO IFUFUKE(Ezekieli 37 1-15)
Toa unabii juu ya mifupa hii. Iambie hivi: Enyi mifupa mikavu, sikilizeni neno la Mwenyezi-Mungu. Bwana Mwenyezi-Mungu awaambia hivi: Nitaifanya pumzi iwaingie, nanyi mtaishi.

CHUKUA HATUA HII
Tambua eneo lolote katika maisha yako ambalo limekufa ambalo ndio kiunabii linaitwa mifupa mikavu lisemeshe maneno ya ezekieli 37 ;1-15

sema hivi wewe NDOA YANGU-mifupa mikavu taja eneo husika katika ndoa kama ni (mawasiliano hamzungumzi/mawasiliano hakuna,upendo umepote,n.k) sema nakutolea unabii,sikia neno la Mungu nitafanya pumzi ya Mungu ikuingie nawe utaishi, fanya hivyo kila siku asubuhi unapoamka na jioni unapolala kwa muda wa siku 21 mpaka 30...utanishukuru baadae.

maeneo yote yenye mifupa mikavu yaliyokufa kwenye maisha yako,iwe ni uchumi wako eneo lako la kazi ,AFYA YAKO n.k

JENGA UPYA UKINGO WA UKUTA WA ULINZI WA MUNGU ULIOBOMOKA(Ezekieli 22:30*
Ezekieli 22:30

Nami nikatafuta mtu miongoni mwao, atakayelitengeneza boma, *na kusimama mbele zangu mahali palipobomoka", kwa ajili ya nchi, nisije nikaiharibu, lakini sikuona mtu.

tambua mambo yaliyobomoa ukingo wa ukuta wa ulinzi wa Mungu kwako.

kama ni laana za ukoo

tamka maneno haya

BWANA MUNGU nasimama mbele yako kama kwa ajili ya familia yangu ukoo wangu kuziba pale walipobomoa kwa maagano ya ukoo ya damu za ukoo,naziba pale mababu zangu walipopabomoa ,uharibifu hautatupata familia yengu.

tamka maneno hayo kila siku mfululizo.
NB NI MUHIMU kutamka kila siku mfululizo bila kuruka hata siku moja kwa muda wa siku kuanzia 21-30..kadiri unavyotamka kila siku kwa uaminifu na imani,kwa ujasiri utapata matokeo.

siku nyingine nitongelea kuhusu roho fuatilizi zinazofuatilia maisha yako bila wewe kujijua nyumbani kwako ni kama kamera inayomulika
maisha yako kirioho ,kiuchumi adui anajua kuwa siku tatu zijazo au wiki moja mbele utapata mafanikio kwenye eneo fulani au utapata pesa hivyo nazuia hizo baraka zisikufikie ndio maana hata ukikaribia kupata hela mkono unawasha..ina maana yake..

vioo glass vitu vyote vya vioo hata hii simu,madirisha ya kioo,na vioo vya kabati za chumbani na dressing table pembeni ya kitanda chako,wanyama na ndege kama mijusi,paka,n.k

cha kufanya takasa kwa mafuta vioo vyako visitumike kuchunguza maisha yako kupeleka taarifa ulimwengu wa giza .

kama huwa unajisikia kama kuna mtu anakuangali rohoni unajihisi kama kuna mtu mahali anakuona kwenye television yake...(wengi watapuuza haya ni chakula cha kiroho cha watu wazima waliokomaa kiroho .sio watoto wanaonyonya maziwa ..watakuja kupinga..ila roho mtakatifu atusaidie kutambua MBINU ZOTE ZA ADUI ANAZOTUMIA tupate maarifa..

Hosea 4:6
Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa
 
NAFUDIA TENA KUSEMA ILE CHANJO ITAKAYOKUJA IPO KARIBU CHANJO YA LAZIMA KWA WATU WOTE IPO KARIBU SANA KUJA...

Hiyo chanjo ni chapa CHAPA ...

MWANA WA MUNGU USICHANJE HIYO CHANJO.
Kama huamini unabii huu ,kaa vizuri na Roho mtakatifu...muulize Mungu wako..akufunulie akusemeshe hata katika ndoto...

USICHANJE HIYO CHANJO ITAKAYOKUJA UTAKUWA UMEPOKEA CHAPA...

zipo njia nyingi za kupokea chapa hiyo chanjo ni mojawapo.
japo zipo njia nyingine pia
 
Gal 5:19-21
Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya,
1)uasherati
2)uchafu,
3)ufisadi,
4)ibada ya sanamu,
5)uchawi,
6)uadui,
7)ugomvi,
8)wivu,
9) hasira,
10)fitina,
11)faraka,
12)uzushi,
13)husuda,
14)ulevi,
15)ulafi,

na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.

Kor 6:9-11
Au hamjui ya kuwa
1)wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu?

Msidanganyike;
2) waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu,
3) wala waabudu sanamu,
4) wala wazinzi,
5)wala wafiraji,
6)wala walawiti,
7)wala wevi,
8)wala watamanio,
9)wala walevi,
10) wala watukanaji,
11) wala wanyang’anyi.

Na baadhi yenu mlikuwa watu
wa namna hii; lakini mlioshwa, lakini mlitakaswa, lakini mlihesabiwa haki katika jina la Bwana Yesu Kristo, na katika Roho wa Mungu wetu.

Kol 3:5
Basi, vifisheni viungo vyenu vilivyo katika nchi,
1)uasherati,
2)uchafu,
3)tamaa mbaya,
4)mawazo mabaya,
5)na kutamani, ndiyo ibada ya sanamu

Ufu 21:8
1)Bali waoga,
2)na wasioamini,
3)na wachukizao,
4)na wauaji,
5)na wazinzi,
6)na wachawi,
7) na hao waabuduo sanamu,
8)na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo
moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili.**
 
SWALI
Kaka naumia na hizo njozi za mapolice ni njozi inayojirudiarudia,
Police maana yake nini katika ulimwengu wa roho.

JIBU
Jeshi la mapolisi katika ndoto maana yake ni wachawi(washirikina,walozi,wanga)

bundiki na silaha zao ..ni makombora yao ya kichawi..

ukiota wamebeba bunduki bunduki au mabomu au mikuki ....ndio makombora yao kichawi...wanakurushia....mana yake wanakushambulia katika ulimwengu wa roho..
Zab 27:3
Jeshi lijapojipanga kupigana nami, Moyo wangu hautaogopa. Vita vijaponitokea, Hata hapo nitatumaini.
CHA KUFANYA SASA..

Sali omba Mungu ,tumia damu ya Yesu..silaha yetu na nguvu zetu ni jina la Yesu na damu ya Yesu,na jeshi la malaika

ufunuo 12:11
Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-kondoo

isaya 54:17
zaburi 91:10-15
zaburi 35.
zaburi 18 na zaburi 19

jeshi la malaika walioko upande wetu ni wengi kuliko hao
wao watataja farasi ,wao watataja farasi lakini sisi tunakuja kwa kulitaja jina la Yesu.

Isa 41:10-13
usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu.

USIOGOPE KABISA.
2 Kor 10:4
maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;

Usiogope kabisa ukiogopa tu unakosea unawafungulia mlango,vaa silaha za imani,tumia upanga wa neno...neno la Mungu ni silaha ,upanga mkali sana...fuatilia masomo na mafundisho yote niliyokutumia...

wachawi wanatakiwa wakuogope wewe na sio wewe uwaogope wachawi... kwa sababu wewe unamtumainia YESU BWANA WA MAJESHI...mfalme wa utukufu mwenye nguvu na utukufu..wewe ni mshundi tayari kupitia Yesu,wewe ni mwana wa Mungu mfalme ,sasa unaogopaje mapepo na wachawi,badala wao ndio waungue na kukukimbia si utumie silaha unazo ..OMBA tumia damu ya Yesu,jina la Yesu,kemea,tumia NENO ambaye huyo neno ndio Yesu

Ebr 4:12
Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.


OMBA wewe mwenyewe kwa mdomo wako na kwa moyo wako..muombe Yesu kwa imani kwa kumaanisha kwa ujasiri.

hauhutaji kuombewa wala kutumia mafuta ya upako,wala kwenda popote hapo hapo ulipo Yesu yupo upo naye yupo karibu yako anakuona anakujua na anakusikia,ila ni lazima UOMBE.
 
Back
Top Bottom