Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 20,925
- 30,273
Hili tope walilojipaka CCM katika uchaguzi huu watalisafishaje?
Hii mipango ya wizi wa kura nadhani ilifanywa kwa haraka katikati ya kampeni baada ya kupima kina cha maji na kuona kina ni kirefu.
Matokeo yake ndiyo haya kura zinakamatwa mitaani, na nje na ndani ya vituo vya kupigia kura.
Tanzania tumegeuka tumekuwa kichekesho cha dunia.
Tumejivua nguo wenyewe huku tukijiangalia kwenye kioo.
Ile "intellect," iliyokuwapo ndani ya enzi za "chama," haikurithishwa chini kwa vijana?
Nimejifunza kutia kicheko mahali pa kunipa majonzi.
Vinginevyo ningekuwa na huzuni ya kudumu.
Hivi kweli ndani ya CCM katika viongozi wakuu waliopita kweli hawaoni kama tunalo tatizo linalohitaji kurekebishwa?
Nina rafiki zangu CCM toka matokeo ya uchaguzi tukikutana wanashindwa kunitazama machoni.
Nahisi kama vile wamefedheheka wanaona aibu.
Kura zinastaajabisha.
Hii mipango ya wizi wa kura nadhani ilifanywa kwa haraka katikati ya kampeni baada ya kupima kina cha maji na kuona kina ni kirefu.
Matokeo yake ndiyo haya kura zinakamatwa mitaani, na nje na ndani ya vituo vya kupigia kura.
Tanzania tumegeuka tumekuwa kichekesho cha dunia.
Tumejivua nguo wenyewe huku tukijiangalia kwenye kioo.
Ile "intellect," iliyokuwapo ndani ya enzi za "chama," haikurithishwa chini kwa vijana?
Nimejifunza kutia kicheko mahali pa kunipa majonzi.
Vinginevyo ningekuwa na huzuni ya kudumu.
Hivi kweli ndani ya CCM katika viongozi wakuu waliopita kweli hawaoni kama tunalo tatizo linalohitaji kurekebishwa?
Nina rafiki zangu CCM toka matokeo ya uchaguzi tukikutana wanashindwa kunitazama machoni.
Nahisi kama vile wamefedheheka wanaona aibu.
Kura zinastaajabisha.