AridityIndex
Senior Member
- Mar 22, 2011
- 149
- 38
Heshima Mbele Wanajamvi
Hii ni hoja yangu namba moja, katika mfululizo wa hoja nitakazokuwa nazitoa hapa jamvini. pamoja na U-junior wangu kama member lakini nakuhakikishieni kuwa kwa muda wa miaka 3 sasa nimekuwa nikitembelea Jamvi hili na kujionea mijadala mingi inayolihusu taifa letu.
Nitaeleza kwa kifupi katika hoja yangu sababu za kuchelewa kujiunga. Sababu ni nyingi lakini kubwa zaidi ni hii hali ya kutengwa kwa eneo langu na siasa za Tanzania zinazoendelea. Naomba nieleze bayana kuwa hoja kubwa katika jukwaa hili ni pamoja na hizi hapa.
1. Umeme-dowans, kiwira, richmond, mgao wa umeme maji kukauka nk
2. Ufisadi - meremeta, kiwira nk
3. Udini na malumbano kati ya christian and Muslims
4.Mbiyo za urais
kwa bahati mbaya sana huku kwetu nilikozaliwa na ninakoishi haya mambo ni kama vile hayatugusi sana naomba nielezee kila moja.
Kuhusu Umeme - sisi huku kwetu tuna umeme wa gesi ambao inakadiliwa kuwa tutatumia kwa miaka 300 na wala hakuna mgao wala hakuna kukauka maji kwa hiyo sikuwa na hoja kwa kweli kwenye mijadala ya umeme.
Kuhusu Ufisadi- hapa tumetofautiana kwa kiasi kikubwa sana kimtazamo mwanzoni tuliamini sana suala
hili lakini mijadala ilipoamua kumtumbukiza na BWM ambaye sisi tunaamini hataweza kutokea Rais bora zaidi katika nchi hii na tukiamini kuwa yeye ni zaidi ya maraisi wa awamu zote wengine wanamtusi hapo tukabaki kinywa wazi.
Udini na malumbano ya dini- yaani hapa ndo hatumo kabisa kwetu sisi watu wote tuna ndugu wa dini nyingine kwenye koo zao. Labla niwaeleze kilichotokea ni kwamba katika makabila yetu wale wote waliobaki upande mwingine yaani nchi yetu ya asili ni christian na waliovuka kuja Tz ni muslim lakini koo zetu lugha yetu utamaduni wetu undugu wetu umebaki kama ulivyo na ndiyo maana ukija kwetu utakutana akina anthony omari, Juma Joseph, Rose Abdalah nk. kwa hiyo hapa Watanzania wenzetu mmetuacha mbali kweli.
Mbiyo za Urais - kwetu sisi tunayemuona kuwa anafaa na tunayeamini kuwa atatenda haki ni Membe Tu sasa akitajwa kwenye mijadala anatukanwa. wakati ukweli ni kwamba ni yeye tu ndiye mwenye uwezo wa kuwaponyesha makovu yenu ya hapo juu amekulia kwenye eneo lisilo na makundi ya kikabila na kidini, siyo fisadi na hana tatizo la umeme.
Wakati tukiwa na hamu ya kushirikiana na waTZ wengine katika mabadiliko hoja zetu kama soko la uhakika la korosho, Maji, Uvuvi na shule havipewi umuhimu na viongozi wa mageuzi ya kitaifa je tufanyeje?. Tuendelee kujitenga?
Hii ni hoja yangu namba moja, katika mfululizo wa hoja nitakazokuwa nazitoa hapa jamvini. pamoja na U-junior wangu kama member lakini nakuhakikishieni kuwa kwa muda wa miaka 3 sasa nimekuwa nikitembelea Jamvi hili na kujionea mijadala mingi inayolihusu taifa letu.
Nitaeleza kwa kifupi katika hoja yangu sababu za kuchelewa kujiunga. Sababu ni nyingi lakini kubwa zaidi ni hii hali ya kutengwa kwa eneo langu na siasa za Tanzania zinazoendelea. Naomba nieleze bayana kuwa hoja kubwa katika jukwaa hili ni pamoja na hizi hapa.
1. Umeme-dowans, kiwira, richmond, mgao wa umeme maji kukauka nk
2. Ufisadi - meremeta, kiwira nk
3. Udini na malumbano kati ya christian and Muslims
4.Mbiyo za urais
kwa bahati mbaya sana huku kwetu nilikozaliwa na ninakoishi haya mambo ni kama vile hayatugusi sana naomba nielezee kila moja.
Kuhusu Umeme - sisi huku kwetu tuna umeme wa gesi ambao inakadiliwa kuwa tutatumia kwa miaka 300 na wala hakuna mgao wala hakuna kukauka maji kwa hiyo sikuwa na hoja kwa kweli kwenye mijadala ya umeme.
Kuhusu Ufisadi- hapa tumetofautiana kwa kiasi kikubwa sana kimtazamo mwanzoni tuliamini sana suala
hili lakini mijadala ilipoamua kumtumbukiza na BWM ambaye sisi tunaamini hataweza kutokea Rais bora zaidi katika nchi hii na tukiamini kuwa yeye ni zaidi ya maraisi wa awamu zote wengine wanamtusi hapo tukabaki kinywa wazi.
Udini na malumbano ya dini- yaani hapa ndo hatumo kabisa kwetu sisi watu wote tuna ndugu wa dini nyingine kwenye koo zao. Labla niwaeleze kilichotokea ni kwamba katika makabila yetu wale wote waliobaki upande mwingine yaani nchi yetu ya asili ni christian na waliovuka kuja Tz ni muslim lakini koo zetu lugha yetu utamaduni wetu undugu wetu umebaki kama ulivyo na ndiyo maana ukija kwetu utakutana akina anthony omari, Juma Joseph, Rose Abdalah nk. kwa hiyo hapa Watanzania wenzetu mmetuacha mbali kweli.
Mbiyo za Urais - kwetu sisi tunayemuona kuwa anafaa na tunayeamini kuwa atatenda haki ni Membe Tu sasa akitajwa kwenye mijadala anatukanwa. wakati ukweli ni kwamba ni yeye tu ndiye mwenye uwezo wa kuwaponyesha makovu yenu ya hapo juu amekulia kwenye eneo lisilo na makundi ya kikabila na kidini, siyo fisadi na hana tatizo la umeme.
Wakati tukiwa na hamu ya kushirikiana na waTZ wengine katika mabadiliko hoja zetu kama soko la uhakika la korosho, Maji, Uvuvi na shule havipewi umuhimu na viongozi wa mageuzi ya kitaifa je tufanyeje?. Tuendelee kujitenga?