Tumeanza kula matunda ya mikutano ya Tundu Lissu Ulaya na Marekani

Eleza alivyo itukana na kuichafua nchi.
Ukijisaidia njiani ukaonwa, aliyekuona akisema umejisaidia njiani anakuwa hajakutukana!
Btw kwa mara ya pili unakosa uvumilivu wa kutoandika juu ya Lissu kama ulivyo haidi.....
 
Mwanzo nikafikiri ukekosea njia, kumbe umegeuza JF mahali pa kutupia takataka na matapishi.... next time tutakushtaki uondolewe humu.
 
Tofautisha Serikali na Taifa wewe, ni vitu viwili tofauti. Serikali inapigiwa kura na kuondolewa madarakani na Serikali nyingine kuingia madarakani lakini Taifa linabaki lile lile whether kuna Serikali A, B au C.

 
Nijuavyo kisafi ndio kinachafuliwa... Kichafu hakiwezi kuchafuliwa tena... Between nashindwa kuelewa TL anaichafuaje nchi

Jr
 
mzee ebu taja moja ambalo lisu kasema na nilauwongo please
 
kwa akili yako huko unakoelekea hushindwi kusema amesababisha tsh kuporomoka
 
Nadhani kwa Afrika Nzima karne hii ya 21 Tundu Lisu amekua Sauti ya kupinga Ukoloni wa Mtu Mweusi kumtawala Mwafrika Mwenzake Kikatili bila kujali maumivu yake. Watawala wa Kiafrika wanatia aibu sana kwa wanavyoshindwa kujenga mifumo bora ya kisiasa na kijamii na kiuchumi.
Yanayofanyika Tanzania kisiasa hayakua na ulazima wowote kama Katiba ingefuatwa na kiheshimu maamuzi ya wapiga kura.

Utawala huu ulikua na nafasi nzuri sana ya kufanya mambo mazuri na kupata heshima kubwa sana kama ungesimamia katiba na sheria nyingine kama zile za Uchaguzi. Kung'ang'ania kuilinda CCM na makada wake wenye tuhuma nyingi matokeo yake yanaligharimu Taifa.
Awamu yetu hii ilikua na uwezo wa kuunda katiba bora na kuleta maendeleo makubwa sana na baada ya muda wao kuisha wanheheshimika sana na kuenziwa kwa pale watakapoishia kuliko kuwaza kuifanya dunia kuwa pepo kwa kuwagawanya watu kwa makundi huku watawala wakiwa daraja la juu sana na wenye mamlaka na maamuzi kama miungu na mwisho wa yote wakaishia kushitakiwa na kumalizia maisha yao duniani kwa vifungo gerezani.

Hata kwenye kutafuta maisha kuna watu wanaotafuta fedha kwa udi na uvumba huku wakiumiza wengine kwa dhulma,rushwa na utapeli alimradi wapate fedha nyingi. Hii sio sawa katika maisha bora ya binadam wenye utu . Wachamungu watakataa na kusema bora kupata fedha kidogo kwa halali bila kuumiza wengine kuliko kupata nyingi kwa kuumiza wengine.

Asili ya binadamu ni binadam na ameumbwa na Mungu.Na haijawahi kutokea mtawala akatenda anavyotaka yeye bila kupingwa na binadamu wenzake na mwishowe akapoteza umaarufu na hata kuporomoka kisiasa.

Serikali ingemtibu Lisu na kuonyesha ushirikiano wa kukerwa na majangili yasiyojulikana yaliyotaka kumuua Lisu kama wanavyokerwa na majangili yanayoua Tembo nadhani Lisu asingelalamika kama anavyolalalamika kwa majirani baada ya kuona wazazi hawamjali na wanahamasisha asipewe hata chakula ( mshahara wake).

Serikali ikitaka kujisafisha ianze kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa.
Na ikiwezekana viongozi wa dini wajitolee kuiunga mkono kwa kuwa waangalizi wa mwenendo mzima wa uchaguzi serikali za mitaa ili wakiwaombea watawala basi wamwambie Mungu ukweli. Mana huwezi kutubu dhambi usiyoijua au kudhani kuwa umekosea.

Lisu ni mwanga mpya wa Tanzania na Afrika. Tunajivunia kuwa Taifa letu kuwa na MTU huyo Tundu Antipasi Lisu. Ameitangaza nchi kwa Muda mfupi.

Mungu ampe Lisu nguvu na uponyaji na ulinzi dhidi ya wenye uchu wa madaraka na Vyeo na husuda.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kila siku unajaza nyuzi za tundu Lissu km kakutafunia mamayako hayo ni mambo yenu binafsi.
Usichoshe kuweka uzi humu kanunue kurasa wa mbele wa Tanzaniite ulalamike.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Serikali hii hii inayojulikana kuunda kikundi cha mauaji kilichojipa jina la "Wasiojulikana"?. Ni lazima uchunguzi ufanyike tuwajue hawa wanaoweka misingi ya mauaji na chuki ambayo itazaa vita katika nchi yetu. Hii serikali siyo ya kubembelezana nayo tena.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…