Tume ya Uchaguzi iondolewe mamlaka ya kuengeua wagombea bila kupitia Mahakamani

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,627
46,272
Mojawapo ya vigezo, tunu na utamaduni muhimu wa demokrasia ni ushindani wa haki wa wagombea kupitia sanduku la kura. Kunapokosekana huo ushindani demokrasia inakuwa imekanyagwa na kusiginwa. Kwa msingi huo Tume ya taifa kuwa na mamlaka ya kuengeua wagombea ni kosa kubwa sana katika mchakato wa kidemokrasia.

Ni wakati sasa tume ya taifa kuondolewa hayo mamlaka ya kuengeua wagombea na yapewe kwa mahakama. Kama kuna dosari yoyote kwa mgombea basi wagombea wenzake, wanachi au serikali ikafungue kesi mahakamani na mgombea husika apewe nafasi ya kujitetea kupitia wakili. Wakati haya yanafanyika mahakamani uchaguzi wa nchi, jimbo, kata au mtaa husika usimame mpaka maamuzi ya kesi yafikiwe na mahakama.

Taasisi na mifumo yetu ina matobo mengi sana yanayoikwamisha nchi kuwa demokrasia halisi, inahatijika kazi ya ziada kuondokana na demokrasia ya kiini macho "sham democracy", suluhu ya kudumu ya haya yote ni Katiba Mpya.
 
Kupeleka kesi ya mtu ambaye hakukidhi sifa mahakamani ni kuchelewesha mchakato mzima wa uchaguzi. Atakayeenguliwa anaruhusiwa kwenda kulalamika mahakamani lakini siyo kuizuia tume kufanya kazi zake za kuhakikisha kuwa kila mgombea ana sifa zinazotakiwa.

Ushauri mzuri ni kuondoa masharti ya mtu kugombea ili kila mtu aruhusiwe kugombea mradi awe na checti cha kuzaliwa au passport ya Tanzania, na hivyo hakutakuwa na haja ya tume kuhakiki sifa za wagombea.
 
Naunga mkono hoja, na vigezo vya kugombea visiwe vya kukomoana kama CCM walivyopitisha kigezo cha degree dakika ya mwisho ili kumzuia Mbowe asigombee, vigezo visiamuliwe na tume au serikali viwemo kwenye katiba na kueleweka bila matundu
 
Tunahitaji Katiba Mpya ili iweke utaratibu wa kupata Tume Huru ya Uchaguzi. Kama hili haliwezeksni wazalendo anzeni mgomo baridi, anza kususia kununua pombe na soda.
 
Mtu akienguliwa na tume halafu mahakama ikasema anavyo vigezo baada ya miezi mitatu kupita wakati ambapo uchaguzi umeisha bila yeye kushiriki, wananchi waliotaka kumpigia kura na yeye wanaipataje haki yao?
Au unamaanisha kesi yake ikiwa mahakamani uchaguzi usifanyike mpaka kesi iishe?
Kupeleka kesi ya mtu ambaye hakukidhi sifa mahakamani ni kuchelewesha mchakato mzima wa uchaguzi. Atakayeenguliwa anaruhusiwa kwenda kulalamika mahakamani lakini siyo kuizuia tume kufanya kazi zake za kuhakikisha kuwa kila mgombea ana sifa zinazotakiwa.

Ushauri mzuri ni kuondoa masharti ya mtu kugombea ili kila mtu aruhusiwe kugombea mradi awe na checti cha kuzaliwa au passport ya Tanzania, na hivyo hakutakuwa na haja ya tume kuhakiki sifa za wagombea.
 
Mojawapo ya vigezo, tunu na utamaduni muhimu wa demokrasia ni ushindani wa haki wa wagombea kupitia sanduku la kura. Kunapokosekana huo ushindani demokrasia inakuwa imekanyagwa na kusiginwa. Kwa msingi huo Tume ya taifa kuwa na mamlaka ya kuengeua wagombea ni kosa kubwa sana katika mchakato wa kidemokrasia.
Sawa kabisa, nahisi hayo mambo hayatokea tena. Tunaanza kuwa wamoja kama zamani, MUNGU MKUBWA.
 
Mtu akienguliwa na tume halafu mahakama ikasema anavyo vigezo baada ya miezi mitatu kupita wakati ambapo uchaguzi umeisha bila yeye kushiriki, wananchi waliotaka kumpigia kura na yeye wanaipataje haki yao?
Au unamaanisha kesi yake ikiwa mahakamani uchaguzi usifanyike mpaka kesi iishe?
Inategemea huyo anayepeleka kesi anahitaji mahakama iamue nini.

Kama mahakama inaweza kuchelewesha kutoa uamauzi, hali hiyo haitabidilishwa kwa kuiongezea jukumu la kuhakiki wagombea.
 
Mojawapo ya vigezo, tunu na utamaduni muhimu wa demokrasia ni ushindani wa haki wa wagombea kupitia sanduku la kura. Kunapokosekana huo ushindani demokrasia inakuwa imekanyagwa na kusiginwa. Kwa msingi huo Tume ya taifa kuwa na mamlaka ya kuengeua wagombea ni kosa kubwa sana katika mchakato wa kidemokrasia.

Ni wakati sasa tume ya taifa kuondolewa hayo mamlaka ya kuengeua wagombea na yapewe kwa mahakama. Kama kuna dosari yoyote kwa mgombea basi wagombea wenzake, wanachi au serikali ikafungue kesi mahakamani na mgombea husika apewe nafasi ya kujitetea kupitia wakili. Wakati haya yanafanyika mahakamani uchaguzi wa nchi, jimbo, kata au mtaa husika usimame mpaka maamuzi ya kesi yafikiwe na mahakama.

Taasisi na mifumo yetu ina matobo mengi sana yanayoikwamisha nchi kuwa demokrasia halisi, inahatijika kazi ya ziada kuondokana na demokrasia ya kiini macho "sham democracy", suluhu ya kudumu ya haya yote ni Katiba Mpya.
Kwanza tume yote ivunjwe pale pamejaa uozo tupu
 
Inategemea huyo anayepeleka kesi anahitaji mahakama iamue nini.

Kama mahakama inaweza kuchelewesha kutoa uamauzi, hali hiyo haitabidilishwa kwa kuiongezea jukumu la kuhakiki wagombea.
Mahakama haikiki wagombea bali inaamua kesi zinazofikishwa mbele yake.
 
Unahisi tu ila sio ajabu yakiendelea kutokea na yatatokea tu bila Katiba nzuri na tume huru
Sawa kabisa, nahisi hayo mambo hayatokea tena. Tunaanza kuwa wamoja kama zamani, MUNGU MKUBWA.
 
Mtu akienguliwa na tume halafu mahakama ikasema anavyo vigezo baada ya miezi mitatu kupita wakati ambapo uchaguzi umeisha bila yeye kushiriki, wananchi waliotaka kumpigia kura na yeye wanaipataje haki yao?
Au unamaanisha kesi yake ikiwa mahakamani uchaguzi usifanyike mpaka kesi iishe?
Kujibu hoja za hawa ni kupoteza muda tu. Wao na magufuli aliamini kwamba demokrasia ni kutumia maguvu pasi na akili . Achana nae
 
Back
Top Bottom