Tumbo ni adui mkubwa wa urembo wako

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,597
215,272
1579411082143.jpeg

Mdada huna mimba lakini umebeba ki fridge, hii ni hatari sana. Hakuna nguo itakayo kupendeza zaidi ya dera.

Sasa umekutana na mkaka amekupenda kwakua mambo yako ya usafi wa nyumba, kupika na maongezi yako pia ameyapenda. Ameamua kukupeleka kwao, mama yake hana tumbo kabisa mama ana maintain figure.

Mama mkwe mtarajiwa baada ya kuona tumbo la mtarajiwa anajawana simanzi. Bibi utamaliza waganga mchawi ni hilo tumbo. Do something about it.

Hata vitabu vitakatifu vilihimiza kujitoa sadaka. Kujinyima kula hata mara mbili kwa wiki inasaidia sana. Pamoja na hayo wataalamu wanahimiza mlo kamili katika kipimo kidogo mara tatu kwa siku.

Bila kusahau mazoezi, imekuwa bibi wewe umenunua IST basi hata kwenda kusuka yeboyebo unapack IST kwa msusi.

Have a nice Sunday.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom