Tunaposema mema na ubaya pia vyote vinatoka kwa Mungu hatumaanishi Mungu hatuwazii mema laa hasha.Hapo ndiyo mnapokosea.
Kusema eti ubaya unatoka kwa Mungu.
Ndugu yangu Mungu siku zote anatuwazia Mema lakini kwa sababu shetani na majini ambao wote kwa ujumla walimuasi Mungu ndiyo vyanzo vya matatizo kwa watu lakini kwa sababu Mungu yupo ndiyo anatusaidia.
Kama ni kweli hujawahi enda kwa mganga endelea na imani hiyo itakusaidia sana maana 100% waganga ni wachawi sema ni idara tofauti tu........Alafu kuhusu uumbaji ni kweli kila kitu kimeumbwa na Mungu lakn kadri kilichoumbwa kinavyozidi kuendelea kinaweza kumuasi Mungu na kuwa kinyume nae ndy hayo majini sasa maana mara ya kwanza yalikuwa maraika.
Tunamaanisha halimpati mtu jambo isipokuwa kwa ruhusa yake.Likiwa jema basi neema na likiwa baya basi ni majaribu ya Muumba ili tumrejee na kumkumbuka.
Hata huyo mchawi akuloge vipi kama Mungu hajaruhusu haurogeki ila akitaka unaweza kurogeka ili iwe ni jaribu la kumkumbuka na kurudi kwake.
Maana kuna vitu viwili binadam tunavikumbuka matatizo yakitupata kwanza eidha tuseme Mungu wanguuu ama tuseme mama yanguuu.