Tuliosoma nje ya nchi tunanyanyapaliwa sana

Malyenge

JF-Expert Member
Jan 16, 2012
6,658
3,646
Habari za asubuhi.

Somo tajwa hapo juu lahusika.

Sisi tuliosoma nje ya nchi tukirudi Tanzania kwenye taasisi za serikali tunanyanyapaliwa sana. Suluba inaanzia hapa:

Kwanza tunaambiwa tukavithibitishe vyeti vyetu TCU. Tukifika TCU usumbufu tunaopata pale ni mkubwa sana!

Unaambiwa upeleke ushahidi kwamba ni kweli ulikwenda nje ya nchi.

Wanataka visa yako ioneshe ni student visa wakati unaondoka. Pia uoneshe sehemu ya passport ulivoondoka na ulovyofika kule yaani uoneshe sehemu iliyogongwa muhuri.

Hayo si issue sana maana mwisho unatakiwa ulipie.

Kubwa ni lile unapofanya kazi wakubwa hawakupi kipaumbele wala kuthamini elimu yako. Wanakuona ni adui na unajifanya mjuaji.

Linapokuja suala la promotion utasugua benchi mpaka utajuta kwa nini ulikwenda kusoma nje ya nchi.

Waliosoma hapa nchini utawaona wanapeta tu na maisha yao yanaenda vizuri. Vyeo wanapewa mpaka unashangaa mtu kapataje maana uwezo wa kiuongozi au kiufundi unamzidi kwa kila kitu.

Kwa kweli hali hii inatuumiza sana.
Je, ni kosa kusoma nje ya nchi?
 
Nje gani unayoizungumzia wewe? Uganda au? Kama uganda lazima tukuthibitishe mzee maguashi mengi mno, pia mnatabia ya kwenda ulaya halafu mnasoma amazon koleji za huko ulaya sàa kwanini tusikuhakiki? Ila kama umesoma vyuo vya ukweli halafu unarudi tz na kulilia ajira za gvt lazima tukupime mkojo mzee maana kwa eksipozzya uliyoipata huko bado unataka kulilia hizi ajira za kusubiri mei mosi mkuu wa nchi atasemaje kuhusu mshahara utakuwa na matatizo sio bure
 
Habari za asubuhi.
Somo tajwa hapo juu lahusika.
Sisi tuliosoma nje ya nchi tukirudi Tanzania kwenye taasisi za serikali tunanyanyapaliwa sana. Suluba inaanzia hapa:
Kwanza tunaambiwa tukavithibitishe vyeti vyetu TCU. Tukifika TCU usumbufu tunaopata pale ni mkubwa sana!
Unaambiwa upeleke ushahidi kwamba ni kweli ulikwenda nje ya nchi. Wanataka visa yako ioneshe ni student visa wakati unaondoka. Pia uoneshe sehemu ya passport ulivoondoka na ulovyofika kule yaani uoneshe sehemu iliyogongwa muhuri.
Hayo si issue sana maana mwisho unatakiwa ulipie.

Kubwa ni lile unapofanya kazi wakubwa hawakupi kipaumbele wala kuthamini elimu yako. Wanakuona ni adui na unajifanya mjuaji.
Linapokuja suala la promotion utasugua benchi mpaka utajuta kwa nini ulikwenda kusoma nje ya nchi.
Waliosoma hapa nchini utawaona wanapeta tu na maisha yao yanaenda vizuri. Vyeo wanapewa mpaka unashangaa mtu kapataje maana uwezo wa kiuongozi au kiufundi unamzidi kwa kila kitu.
Kwa kweli hali hii inatuumiza sana.
Je ni kosa kusoma nje ya nchi?
Tatizo linaqnzia wengi mnaenda nje sababu ya kukosa sifa ndani,mtu qualification za kusoma degree ndani zimedunda anaambiwa njuweni college ya indonesia itampatia degree na div 4 yake....lazima uhakiki uwepo
 
Habari za asubuhi.
Somo tajwa hapo juu lahusika.
Sisi tuliosoma nje ya nchi tukirudi Tanzania kwenye taasisi za serikali tunanyanyapaliwa sana. Suluba inaanzia hapa:
Kwanza tunaambiwa tukavithibitishe vyeti vyetu TCU. Tukifika TCU usumbufu tunaopata pale ni mkubwa sana!
Unaambiwa upeleke ushahidi kwamba ni kweli ulikwenda nje ya nchi. Wanataka visa yako ioneshe ni student visa wakati unaondoka. Pia uoneshe sehemu ya passport ulivoondoka na ulovyofika kule yaani uoneshe sehemu iliyogongwa muhuri.
Hayo si issue sana maana mwisho unatakiwa ulipie.

Kubwa ni lile unapofanya kazi wakubwa hawakupi kipaumbele wala kuthamini elimu yako. Wanakuona ni adui na unajifanya mjuaji.
Linapokuja suala la promotion utasugua benchi mpaka utajuta kwa nini ulikwenda kusoma nje ya nchi.
Waliosoma hapa nchini utawaona wanapeta tu na maisha yao yanaenda vizuri. Vyeo wanapewa mpaka unashangaa mtu kapataje maana uwezo wa kiuongozi au kiufundi unamzidi kwa kila kitu.
Kwa kweli hali hii inatuumiza sana.
Je ni kosa kusoma nje ya nchi?
Duuuh, poleni sana.

Nina imani umekosa koneksheni tu.

Wale wanaoenda kusoma kuanzia degree ya 2 nao wanakumbana na hayo yote?
 
Ukafanye interview ya watu 10000 kwa nafasi 2. Uje ulipwe laki 7 wakati ada yako ilikuwa milioni 50 kwa mwaka.
Inafikirisha kidogo
Kuna rafiki yangu alitaka kumpeleka mwanae Uturuki sababu hakupata sifa za kujiunga na udaktari nchini. Alitaka akope benk ampeleke. Ninamuambia acha ujinga wewe. Mpeleke vyuo vya kawaida asome. Utaishia kutumia milioni zaidi ya 100, ulipe mkopo mpaka unastaafu. Halafu anapata kazi ya 700k. Huu uwekezaji mbovu kabisa
 
Hivi utasoma nje halafu uje ufanye kazi ya serikali kweli? Au umeenda kusoma masters? Ila kama undergrad umeenda kusoma nje na unataka kazi za serikali kimsingi hauna future na huko nje hakuja kusaidia kitu...
 
Kuna rafiki yangu alitaka kumpeleka mwanae Uturuki sababu hakupata sifa za kujiunga na udaktari nchini. Alitaka akope benk ampeleke. Ninamuambia acha ujinga wewe. Mpeleke vyuo vya kawaida asome. Utaishia kutumia milioni zaidi ya 100, ulipe mkopo mpaka unastaafu. Halafu anapata kazi ya 700k. Huu uwekezaji mbovu kabisa
Tena mwambie aache ujinga labda kama ana hospital yake mwenyewe anataka mtoto aje aiendeshe sawa. Madaktari wako mtaani huku wamejaa wengine wanaamua kwenda JKT ili waajiriwe JWTZ. Miaka 6 ijayo akigraduate hataamini macho yake
 
Back
Top Bottom