Tukio la kusikitisha Arusha leo

Tukio la kusikitisha Arusha leo

Kabla ya kuondoka walipaswa kuangalia je oksijeni ilikuwa ya kutosha? vinginevyo uzembe umechangia.
 
hasa nesi na dereva wana kosa gani mpaka wapigwe?
Hapo wafiwa wamekosea si wanahela,kwnn hawajampeleka india?
...halafu wanapoharibu hivyo vifaa,ina maana wengine watatibiwa wapi?
..halafu hiv oxygen inaishaje njiani jamani,ina maana hakuna kiwango kinachoeleweka kwamba kikiwekwa kinatumika/kinakaa muda gani?
 
No comments,
mtu akifiwa anaweza fanya lolote

ukifiwa ukajeruhi watu, nauharibu mali huwezi ukatumia kufiwa kwako kama utetezi mahakamani, utahukumiwa kwa mujibu wa sheria zilizopo!!bila kujali ulifiwa au la!
 
No comments,
mtu akifiwa anaweza fanya lolote

ukifiwa ukajeruhi watu, nauharibu mali huwezi ukatumia kufiwa kwako kama utetezi mahakamani, utahukumiwa kwa mujibu wa sheria zilizopo!!bila kujali ulifiwa au la!
 
kwa NEGLIGENCE hiyo ya Madaktari, Wauguzi pamoja na Management nzima ya Hospitali mpaka kupelekea uhai wa mtu kupotea ninawiwa kuwafungulia mashitaka aisee.
 
Uzembe wa ndugu, wangempleka hospitali ya serikali mapema.
Mkuu labda haujauguliwa, kama ungeuguliwa na ndugu yako wa karibu ungejua jinsi watu wanavyochanganyikiwa. Au labda haujui hospital protocols and Nurse code of ethics
 
Mawazo mbweteko haya....CCM hadi kwenye kifo cha mtu? you have to be critic by logical aguement you CDM....mnataka kutupeleka wapi?
Did I blame CCM for this death? please read and comprehend the contents before you start argue. Otherwise we might think either you're stupid or Idiot
 
Nesi ndiye amesababisha ambulance isiwe na mtungi wa akiba, au kaupiga nyoka mtungi...hebu nieleweshe mkuu!
Mkuu wewe ukiwa kama askari ni wajibu wako kujua bunduki, unayochukua kwa kazi maalum, ina risasi ngapi. Kama mwanafunzi lazima ujue unayo pen yenye wino wa kutosha kabla ya kuingia chumba cha mtihani
 
si vizuri kabisa hosptal kama hi na muonekano wake na mandhari ya nje kwa kukosa huduma muhimu kama mitungi ya gesi yenye gesi ya kutosha madactar wa hosptali hii ni waembe kwani juzi kati tulimpeleka mfanyakazi mwenzetu aliepata ajali akiwahi stuf bas na bahati mbaya akateleza na tairi ya gari kumkanyaga na kumvunja mguu ambapo alivuja damu sana tulipofika hapo eti hatibiwi mpaka zitolewe ela sh.5000000 kwa jili ya doctar kumuona sas nauliza hi hosptal ni biashara au ni msaada kwa wanchi .
?
 
sioni kitu ya ajabu hapo!!! ndio maana daktari anayetoka nje ya chumba cha mgonjwa kwenda kuwapa taarifa ya kifo ndugu wa aliyekuwa mgonjwa inapaswa asiwe amefunga tai shingoni vinginevyo tai inaweza kugeuka kuwa kamba ya kitanzi!
 
Leo arusha kumetokea tukio la kusikitisha sana:Gari la wagonjwa (ambulance) la hospitali ya Selian inayomilikiwa na kanisa la KKKT lilikuwa linampeleka mgonjwa moja aitwaye Hamad Salim Bawazir (familia maarufu arusha) kwenda hospitali ya KCMC ya mjini Moshi baada ya mgonjwa huyo kuzidiwa sana.Mgonjwza huyo alikuwa anatumia hewa ya oksijen kutokana na matatizo ya kupumua na ndani ya gari hilo kulikuwa na mashine iliyokuwa na hewa hiyo.

Katika hali ya kushangaza gari lilipofika eneo la Kikatiti wakati wanaelekea KCMC nesi aliyeambatana na ndugu wa mgonjwa aliwatangazia kuwa oksijen imeisha hivyo inabidi warudi arusha, na mgonjwa alifariki ndani ya dakika 10.
Hapo ikazuka sokomoko la kufa mtu kati ya ndugu wa mgonjwa na mwuguzi huyo pamoja na dereva ambapo paqmoja na kuchezea kichapo ndugu waliharibu gari hilo kwa kuvunja vioo vyote.

Pia jamaa na marafiki wa familia kutoka mitaa ya katikati ya mji wa Arusha kama Bondeni na pangani waliokuwa na hasira kutokana na kitendo hicho walivamia hospitali ya Selian wakitaka kuichoma moto hadi uongozi ulipolazimika kuwaita askari wa kutuliza ghasia.

Taarifa zinadai kuwa huyo ni mgonjwa pili kuishiwa oksijen njiani na tukio kama hilo lilitokea hivi karibuni ambapo mgonjwa moja alifia eneo la Philips ndani ya gari hilo hilo.

Hospitali ya Selian pamoja na kujengwa kwa gharama kuwa sana zaidi ya shilingi bilioni 10 imeshindwa kutoa huduma yenye viwango kwa wagonjwa na imekuwa kama machinjio ya wagonjwa kutokana na uzembe wa madaktari na wauguzi na pia kukosekana kwa menejimenti ya maana.

Hio mitungi ya Oxygen inapimwa pressure au hakuna hata mpimaji hapo ni kunyanyuka nao tu unamfungia mgonjwa na kuwasha Gari. Maana Kwa uzoefu wangu wa kutumia Resuscitator na Breathing aparatus, hivi vitu ni lazima kupima pressure ili kujua kama mtungi una hewa ya kutosha.

anyway haya ndio yanayotutofautisha na nchi zingine duniani na africa kwa ujumla.Only in Tanzania. mamlaka zinazohusika kusimamia haya zimelala.
 
mitungi ya oxygen inakuwa gauge ya kuonesha imebaki kiasi gani?
Ndio maana kila siku unatakiwa kuchukuwa jipya na wa akiba kwa safari. Kama umetumia hiyo mitungi, ukiunyanyua uliojaa na unaokaribia kuisha utajua tofauti kutokana na uzito wake.
 
Did I blame CCM for this death? please read and comprehend the contents before you start argue. Otherwise we might think either you're stupid or Idiot
Hata hivyo magamba wanahusika tu maana serikali wanayo wao na vyombo vyote vya usimamizi wa kama ni hospitali, shule, kila kitu. System ilio feli ni ya magamba. To me magamba mnahusika tu.
 
Back
Top Bottom