Tujuzane na kushauriana ipi gesi bora kwa matumizi ya nyumbani

LEGE

JF-Expert Member
Oct 14, 2011
5,123
9,168
Wakuu naishi Dar nataka kununua gesi kwaajili ya matumizi ya nyumbani kwaajili ya kupikia.

Je? Ni gesi aina gani ni nzuri hapa na maana ni kampuni gani hutoa Huduma ya uhakika.

Kati ya ORXY lake oil milayo n.k

Na bei zao zikoje??

Habari za wakati wakuu?
Natumai wengi wetu huku tunatumia gesi kama nishati majumbani mwetu.
Takribani mwezi sasa nimekuwa nikiumiza kichwa kwa uamuzi niliouchukua wa kubadili aina ya gesi ninayotumia nyumbani.

Hapo mwanzo nilikuwa natumia gesi kutoka kampuni ya Lake,kwa mtungi mdogo (15 kg) niliweza kudumu nayo takribani miezi mitatu.
Mtungi huo nilianza kuutumia mnamo mwezi wa 4 hadi ilipoisha July katikati.

Nilipata ushawishi wa kuhama kampuni ya Lake na kuhamia Mihan kutoka kwa ndugu yangu wa karibu aliyenishawishi kuwa Mihan inadumu zaidi.
Baada ya kubadili najuta kwani mambo siyo kabisa,gesi hii inakwisha haraka sana.
Niliujaza mtungi huu mwezi jana tarehe 5 lakini kwa uzoefu wangu hapa ulipofikia haitopita wiki haijaisha!

Mwanzo kabisa nilikuwa natumia CAM Gas mtungi wa kg 30 (kwa jiko la plate 3).Kiukweli hii nilikuwa nadumu nayo miezi mitano na zaidi.

Lakini kwa hali ya kiuchumi ilivyobadilika nikaamua kutumia hii mitungi midogo lakini naona hali siyo.

Naomba tushauriane kwa uzoefu ipi gesi nzuri kiuchumi? Maana gesi hii kuisha ndani ya mwezi mmoja kumenishangaza.

Note
Sina lengo la kuiharibia biashara kampuni yoyote,zaidi nataka tupeane mawazo ya gesi ipi itakayoendana na hali halisi ya sasa,asanteni.
Wasalaam,
Nifah
 
wakuu naishi dar nataka kununua gesi kwaajili ya matumizi ya nyumbani kwaajili ya kupikia.
je ? ni gesi aina gani ni nzuri hapa na maana ni kampuni gani hutoa Huduma ya uhakika.
kati ya oryx lake oil milayo n.k

na bei zao zikoje??

Nakushauri oryx maana mawakala wake ni wengi kwa hiyo upatikanaji wake ni rahisi bei kwa sasa ni 54,000 lakini hiyo ni pale unapoenda kubadili mtungi mtupu upewe wenye gas ikiwa na maana tayari unao mtungi.

Wote hao oryx, na wengine mitungi wanaijazia sehemu moja hivyo ni gas ile ile.
 
nakushauri oryx maana mawakala wake ni wengi kwa hiyo upatikanaji wake ni rahisi bei kwa sasa ni 54000 lakini hiyo ni pale unapoenda kubadili mtungi mtupu upewe wenye gas ikiwa na maana tayari unao mtungi.
Wote hao oryx, na wengine mitungi wanaijazia sehemu moja hivyo ni gas ile ile.

Tatizo oryx kila siku wanapandisha bei hadi wanakera. Bora Mihan.
 
wakuu naishi dar nataka kununua gesi kwaajili ya matumizi ya nyumbani kwaajili ya kupikia.
je ? ni gesi aina gani ni nzuri hapa na maana ni kampuni gani hutoa Huduma ya uhakika.
kati ya oryx lake oil milayo n.k

na bei zao zikoje??

Nunua ya Songosongo.
 
Kwangu mm mihan n nzur....nimenunua mtung wa kg30 tang mweZ wa 1 mpaka Sasa nadunda na sion dalili ya kuisha mweZ huu wala ujao.....
Inategemea na matumizi ya mtu, mimi naishi peke yangu nilinunua kg 30 ya oryx tarehe 15 October mwaka jana, natumia gas kwa kila kitu imeisha tarehe 23 mwezi wa nne.

Kwa hiyo matumizi ya gas yana matter sana kama unapika sana itaisha mapema pia regulator na aina ya jiko mfano langu linakula 30g/hr wakati majiko meng ni 120g/hr
 
nakushauri oryx maana mawakala wake ni wengi kwa hiyo upatikanaji wake ni rahisi bei kwa sasa ni 54000 lakini hiyo ni pale unapoenda kubadili mtungi mtupu upewe wenye gas ikiwa na maana tayari unao mtungi.
Wote hao oryx, na wengine mitungi wanaijazia sehemu moja hivyo ni gas ile ile.
Mbona nasikia hizo za oryx kuna ambazo ni fake!! Hizo fake huwa zinajaziwa wapi? Kama unayo taarifa
 
Mbona nackia hizo za oryx kuna ambazo ni fake!! Hizo fake huwa zinajaziwa wapi? Kama unayo taarifa

Fake kwa vipi mkuu maana gas inayotumika majumbani ni butane. Ila kuna madai kuwa oryx hawana usimamizi mzuri wakati wa kujaza gas jambo linalopelekea mitungi mingine kuwa na kg pungufu, lakini mimi nikienda nunua gas naomba wapime uzito wa mtungi nihakiki
 
fake kwa vipi mkuu maana gas inayotumika majumbani ni butane. ila kuna madai kuwa oryx hawana usimamizi mzuri wakati wa kujaza gas jambo linalopelekea mitungi mingine kuwa na kg pungufu, lakini mimi nikienda nunua gas naomba wapime uzito wa mtungi nihakiki
Nimekuona kama mtaalam vile kutokana na maelezo yako, ndio maaana nikauliza. MAANA Huku kwetu mtaani kuna hayo maneno. Ni katika kupata elimu zaidi
 
wakuu naishi dar nataka kununua gesi kwaajili ya matumizi ya nyumbani kwaajili ya kupikia.
je ? ni gesi aina gani ni nzuri hapa na maana ni kampuni gani hutoa Huduma ya uhakika.
kati ya oryx lake oil milayo n.k

na bei zao zikoje??

Gesi ya Mtwara ndio nzuri
 
Kwangu mm mihan n nzur....nimenunua mtung wa kg30 tang mweZ wa 1 mpaka Sasa nadunda na sion dalili ya kuisha mweZ huu wala ujao.....

jisanja;
Mbona unaandika vitu vya ajab ajab hiviHivi unajua kuwa gas zoote hujazwa mahali pamoja? Hivi wajua kuwa mitungi ni kipimo sawa cha kilo sawa zilizoandikwa? Iweje hiyo yako iwake miezi yoote hiyo isiishe?
Waambie watu hawa kuwa weye kwa mama ntilie huishiii, home labda kikombe kimoja cha chai tu. Hakiwezi maliza mtungi, ila usiwadanganye watu na mihan yako. Au wamekuahidi kitu?
Mleta hoja, gesi ni gesi tu hakuna nzuri zaidi ila oryx ni bora kwani yapatikana kila mahali. Usitishwe na bei kubadilika kwani hawa watu ni wafanyi biashara. Hawatoi bure, bei ni moja tuuu ikibadilika ni kwa wote.
 
jisanja;
Mbona unaandika vitu vya ajab ajab hiviHivi unajua kuwa gas zoote hujazwa mahali pamoja? Hivi wajua kuwa mitungi ni kipimo sawa cha kilo sawa zilizoandikwa? Iweje hiyo yako iwake miezi yoote hiyo isiishe?
Waambie watu hawa kuwa weye kwa mama ntilie huishiii, home labda kikombe kimoja cha chai tu. Hakiwezi maliza mtungi, ila usiwadanganye watu na mihan yako. Au wamekuahidi kitu?
Mleta hoja, gesi ni gesi tu hakuna nzuri zaidi ila oryx ni bora kwani yapatikana kila mahali. Usitishwe na bei kubadilika kwani hawa watu ni wafanyi biashara. Hawatoi bure, bei ni moja tuuu ikibadilika ni kwa wote.

Ha ha ha Mbona povu linakutoka sana mkuu?? Mimi napika sinaga Kawaida ya Kula magengen.....Nafikir hua kuna utofaut katika ujazo au consumption energy ya aina ya jiko unalotumia......Hebu ngoja wataalam waje hapa waseme m na ww n watumiaji tu mkui
 
Back
Top Bottom