LEGE
JF-Expert Member
- Oct 14, 2011
- 5,123
- 9,168
Wakuu naishi Dar nataka kununua gesi kwaajili ya matumizi ya nyumbani kwaajili ya kupikia.
Je? Ni gesi aina gani ni nzuri hapa na maana ni kampuni gani hutoa Huduma ya uhakika.
Kati ya ORXY lake oil milayo n.k
Na bei zao zikoje??
Je? Ni gesi aina gani ni nzuri hapa na maana ni kampuni gani hutoa Huduma ya uhakika.
Kati ya ORXY lake oil milayo n.k
Na bei zao zikoje??
Habari za wakati wakuu?
Natumai wengi wetu huku tunatumia gesi kama nishati majumbani mwetu.
Takribani mwezi sasa nimekuwa nikiumiza kichwa kwa uamuzi niliouchukua wa kubadili aina ya gesi ninayotumia nyumbani.
Hapo mwanzo nilikuwa natumia gesi kutoka kampuni ya Lake,kwa mtungi mdogo (15 kg) niliweza kudumu nayo takribani miezi mitatu.
Mtungi huo nilianza kuutumia mnamo mwezi wa 4 hadi ilipoisha July katikati.
Nilipata ushawishi wa kuhama kampuni ya Lake na kuhamia Mihan kutoka kwa ndugu yangu wa karibu aliyenishawishi kuwa Mihan inadumu zaidi.
Baada ya kubadili najuta kwani mambo siyo kabisa,gesi hii inakwisha haraka sana.
Niliujaza mtungi huu mwezi jana tarehe 5 lakini kwa uzoefu wangu hapa ulipofikia haitopita wiki haijaisha!
Mwanzo kabisa nilikuwa natumia CAM Gas mtungi wa kg 30 (kwa jiko la plate 3).Kiukweli hii nilikuwa nadumu nayo miezi mitano na zaidi.
Lakini kwa hali ya kiuchumi ilivyobadilika nikaamua kutumia hii mitungi midogo lakini naona hali siyo.
Naomba tushauriane kwa uzoefu ipi gesi nzuri kiuchumi? Maana gesi hii kuisha ndani ya mwezi mmoja kumenishangaza.
Note
Sina lengo la kuiharibia biashara kampuni yoyote,zaidi nataka tupeane mawazo ya gesi ipi itakayoendana na hali halisi ya sasa,asanteni.
Wasalaam,
Nifah