Tujikumbushie matukio na mambo ya miaka 2000

Tujikumbushie matukio na mambo ya miaka 2000

ELI COHEN

JF-Expert Member
Joined
Jun 19, 2023
Posts
9,376
Reaction score
28,486
Hii ndio miaka millenials wapo primary and secondary huku bado wadogo zao gen z wapo kwenye mifuko na mayai🤣

Miaka hio tunaulizana mbna isidingo Haiishi maana tangu late 90s watu wanaangalia😬

Miaka 2000 ndio ilikuwa golden age ya burudani na media katika nchi hii

Between 2000 hadi 2009 taifa lilikuwa limeshatengeneza watu ambao leo ni legends katika taifa hili.

Maigizo/mchezo ya kaole ndani ya ITV, pale ndipo tulipomtambua kanumba na ray, hadi wao kuanza safari ya filamu. Ile filamu ya girlfriend ya wakina TID ilishika kasi sana😁

Nakumbuka kanda za albamu za wasanii zilimiminika katika nyumba za watu, mimi binafsi nakumbuka albamu ya wachuja nafaka, ile nyambizi ya dully sykes, maisha na muziki ya mr 2, etc zilikuwa pale home.

Miaka 2000 star wa mpila alikuwa juma kaseja, huku mastaa wengine wakiwa wakina sunta, huyu dada ambae alitaka kula hela za mengi zote😁,

Miaka 2000 ilikuw na original comedians, wakina kibakuli🤣, bambo, pembe, joti na mpoki pamoja wakifanya vituko😂

Miaka ya 2000 yalitokea matangazo ya TV maarufu, kama chai jaba, lile tangazo la wasanii kuimba usione soo sema nae nafikiri kampeni ya ugonjwa wa ukimwi, alafu matangazl ya condom yalikuwa mengi sanaa maana ukimwi ulikuwa mkali 🤣

Miaka ya 2000 ujambazi hatarii, kuna tukio moja la kuvamia benk hata itv walionesha tena kwa kuiba kuiba marisasi yanapiga (taarifa ya habari)
Screenshot_20260130_204705_Google.jpg

Screenshot_20260130_204954_Google.jpg

Screenshot_20260130_205438_Google.jpg

Screenshot_20260131_103223_Google.jpg
 
Usinikumbushe enzi ze ambapo ukimwi ulikuwa kwenye kilele chake. Nakumbuka nilifungua duka kubwa la kondom kwa kuamini kuwa wateje watakuwa wengi lakini niliambula hasara.

Enzi hizo bado sinaanza kumgonga bibie Mnachihanguuu .
Aiseeee! Joto la dsm ni kali sana kiasi kwamba ukiweka buku mfukoni ukitoa unakuta Nyerere kavua shati.
 
Oya silent nipe hii stori vizuri mtu wangu🤣🤣
Mkuu jisomee mwenyewe aisee 👇.

 
Nakumbuka kipindi hicho 2001 ndio mama ananizaa, ilikuwa usiku tena alikuwa peke yake nyumbani,ndani ya nyumba ya makuti ikiwa imemulikwa na mwanga hafifu wa kibatari,akashikwa na uchungu,akajiegamiza kwenye nguzo akanizaa na akakata kondo peke yake,mzee alikuta tu mwamba Jaga Kaya Ogihonge analia. Nilifurahi sana siku hiyo ya kuzaliwa
 
Nakumbuka kipindi hicho 2001 ndio mama ananizaa, ilikuwa usiku tena alikuwa peke yake nyumbani,ndani ya nyumba ya makuti ikiwa imemulikwa na mwanga hafifu wa kibatari,akashikwa na uchungu,akajiegamiza kwenye nguzo akanizaa na akakata kondo peke yake,mzee alikuta tu mwamba Jaga Kaya Ogihonge analia. Nilifurahi sana siku hiyo ya kuzaliwa
Omelaa
 
Kipindi Bora kabisa dunia imewahi kupitia ni 2000s hadi 2010

Filamu
Jumba la dhahabu ya Tuesday Kihangala
Shumileta na Nsyuka ya Musa Banzi na Sultan Tamba
Johari njia panda ya ray na kanumba
Misukosuko ya J bras na Seba

Muziki
1. Juma nature na hakuna kulala, ugali, mugambo wanaruka na kukanyagana
3. Temba na chege na Tmk wanaume family na Dar mpaka Moto
4. Mb Dogg na sagabrasha, latifa
5. Z anto na bint kiziwi na mpenzi jini
6. Ferooz na profess J state he
7. Mandojo na domokaya bila kusahai sog dogg

TV NA RADIO
1. Chemsha bongo ya redio one stereo
2. Mizengwe ya ITV
3. Nani zaidi ya redio one
4. Kwetu fleva ya DJ majizo ya magic FM
5. Mchezo ya Mzee jangala radio Tanzania
6. Matangazo ya chai Jaba na fataki na funda moja la ziada litakuumbua
7. Channeli ya C2C mtu kwao ilikuwa inapiga muziki balaa
8. Redio free afrika na kipindi cha sitasahau na je huu ni uungwa cha fredwaa

Kulikuwa ni kipindi cha dhahabu kwa kweli haitakaa itokee, sasa hv ni kama vile kila kitu kimepoteza mvuto
 
Back
Top Bottom