Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

Mkuu Mzito Kabwela, ni kweli bado nipo, ila kiukweli hapa nilipofika, sio kuwa najidai, bali niliishaivuka hiyo stage!, yaani niko over and above hiyo posti unayoitaja!, niliacha kutumwa tangu mwaka 2002!, mimi sasa ni kuku wa kienyeji, with 10+ years ya kuchakura, I don't see my self kama naweza kufugika na kusubiri kuletewa chakula kwa kutumwa tena na yeyote no matter who s/he is!.
Pascal.

Mkuu Pasco nakupata vilivyo. Kipindi fulani niliwahi kuuza mafuta kwenye kituo cha njia panda ya kwenda Tanga na Morogoro Chalinze ulikuwa unapita na LIPIKIPIKI lako kuuubwa. Nimekuuzia sana wese ukawa unasema unakwenda na pikipiki South Africa ukawa unabeba totoz za chalinze kwa kasi ya kutisha. Ulikuwa best yangu sana
 
Last edited by a moderator:
Pascal Mayalla ni jina tuu, lakini wako Pascal Mayalla wengi.
Mimi ni yule Pascal Mayalla aliyekuwa RTD, pia namfahamu Pascal Mayalla fulani alikuwa JWTZ, yupo mwingine alisoma Urusi, kuna mwingine alisoma India, kuna mmoja aliishi US pale Maryland na mpaka leo mke wake yuko kule, kuna Pascal Mayalla aliyekuwa mtangazaji wa Kitimoto, yuko yule aliyekuwa TBC akifanya program za CCM, yuko Pascal Mayalla fulani ni mshauri wa siasa wa ubalozi wa Uingereza nchini, kuna Pascal Mayalla fulani ni mwandishi wa habari wa kujitegemea, kuna Pascal Mayalla fulani alisoma sheria kwa miaka 4 pale UDSM, hadi kuna Pasco wa jf, naye nasikia pia sometimes akichanganywa na Pascal Mayalla, hivyo inategemea huyo unayemfahamu wewe ni yupi!, unaweza ukawa unamfahamu yule Pasco wa jf, ukifikiri ndiye Pascal Mayalla Mtangazaji, kumbe ni watu wawili tofauti!.
Pasco.

Hahahahaaaaa....ntakula ban kwa name calling
 
Wanabodi,

Baada ya Kifo cha Mtangazaji Nguli nchini, Uncle J. Nyaisanga, naomba kuchukua fursa hii, kufanya reflection ndogo ya Watangazaji wa RTD waliotangulia mbele ya haki. Jee unawakumbuka?, unakumbuka vipindi vyao?!, unawakumbuka kwa lipi?!.

Naomba nisizungumzie kulitowatoa duniani, wala hatima ya familia zao walizoziacha huku nyuma maana sio tuu nitazidi kuogopa, bali pia tutazidi kuumia!. Just imagine, kijitaasisi kidogo kama RTD chenye ofisi yake pale BH-Pugu Road kupoteza idadi kubwa hivi ya watumishi wake (tena hawa ninaowataja ni Watangazaji tuu!, achilia watumishi wengine!. Sii bure!, ila lazima tukubali ni kazi ya Mungu, na kazi ya Mungu haina makosa!.

Hii list sio walikufa lini ni random, nikiwakumbuka wengine nitawaongeza!
Tukianzia na

  1. David Wakati
  2. Abdul Masudi (Jawewa)
  3. Eli Mbotto
  4. Stephen Mlatie
  5. Siwatu Luanda
  6. Salama Mfamao
  7. Salim Seif Nkamba (Mjomba)
  8. Michael Katembo
  9. Nelly Kidella
  10. Halima Mchuka,
  11. Omar Jongo
  12. Tumboi Tamimu Risasi
  13. Mohamed Ng'ombo
  14. Abisai Stephen (Uronu)
  15. Stephen Lymo.
  16. Nadhir Mayoka
  17. Juma Ngodae
  18. Rukia Machumu
  19. Karim Besta
  20. Henrick Michael Libuda
  21. Idrissa Sadalah
  22. Bati Kombwa
  23. Iddi Rashid Mchatta
  24. Dominic Chilambo
  25. Hassan Mkumba

Pascal.

Pascal, hebu ongezea na hawa:

26. Tido Muhando (Mzee wa Mwananchi) - Pia nafuatilia sana simulizi zake za kila Jpili - Mwananchi Newspaper.
27. Deborah Mwenda
28. Sarah Dumba
29. Charles Hiral ( Mzee wa BBC)
30. Ishe Muhidin
31. Frolian Kaiza
32. Halima Kiemba
33. Betty Mkwasa ( Mwanasiasa kwa sasa)
34. January Constatine
35. Lando Mabula
36. Abubakar Lyongo
37. Sued Mwinyi
38. Nswima Elnest
39. Malima Ndelema
40. Richard Leo
41. Mohamed Kisengo
42. Christina Chokunogela
43. Shaban Kisu
44. Salim Bonde
45. Sekion Kitojo
46. Ahmed Kipozi
47. Fatma Kipozi
48. Ezekiel Malongo
49. Abdul Ngalawa
50. Hendrick Maiko Libuda
 
Safi sana, hata nyuso zao tu zinaonyesha Waandishi wazalendo - wale makanjanja walikuwa bado hawajazaliwa zama hizo- ha ha ha

Kumbu-kumbu-01.jpg
 
Pascal Mayalla ni jina tuu, lakini wako Pascal Mayalla wengi.
Mimi ni yule Pascal Mayalla aliyekuwa RTD, pia namfahamu Pascal Mayalla fulani alikuwa JWTZ, yupo mwingine alisoma Urusi, kuna mwingine alisoma India, kuna mmoja aliishi US pale Maryland na mpaka leo mke wake yuko kule, kuna Pascal Mayalla aliyekuwa mtangazaji wa Kitimoto, yuko yule aliyekuwa TBC akifanya program za CCM, yuko Pascal Mayalla fulani ni mshauri wa siasa wa ubalozi wa Uingereza nchini, kuna Pascal Mayalla fulani ni mwandishi wa habari wa kujitegemea, kuna Pascal Mayalla fulani alisoma sheria kwa miaka 4 pale UDSM, hadi kuna Pasco wa jf, naye nasikia pia sometimes akichanganywa na Pascal Mayalla, hivyo inategemea huyo unayemfahamu wewe ni yupi!, unaweza ukawa unamfahamu yule Pasco wa jf, ukifikiri ndiye Pascal Mayalla Mtangazaji, kumbe ni watu wawili tofauti!.
Pasco.

nafikiri ninayemtafuta ni yule wa itv enzi hizo na kipindi cha kitimoto yuko wapi yule bwana?
 
Michael Katembo kipindi chake cha mkoa kwa mkoa kikianza anaanza na kukuimbia kwanza mwenyewee then anapiga mh mmmh mmmh mmh maana yake hayajui maneno but anafata mdundo athen anakuba BARRR AAABARAAAAA ni Wamakonde wa Mtwara haooo...then kukawa na mmoja nimemsahau anapiga ijumaa kipindi cha KIjaruba sijui alikuwa ni nani...then Mama na mwana na Ma debora mwenda ..au chei chei shangazi jjioni na Aunt Aloiycia Maneno...Then Club ya Leo Shooooooooooooooooo na Julius Nyaisangah....Then Sikiliza Bwna Umemeeeeeeeee na Satarehe na BPPPP...loh natamani na taarifa ya habari msomaji ni Sango Kipozi lloh au mpira sauti ya kike ya Halima Mchuka

Nilipenda kipindi hiki,ilikuwa saa 7 mchana i think !
 
Pascal, hebu ongezea na hawa:

26. Tido Muhando (Mzee wa Mwananchi) - Pia nafuatilia sana simulizi zake za kila Jpili - Mwananchi Newspaper.
27. Deborah Mwenda
28. Sarah Dumba
29. Charles Hiral ( Mzee wa BBC)
30. Ishe Muhidin
31. Frolian Kaiza
32. Halima Kiemba
33. Betty Mkwasa ( Mwanasiasa kwa sasa)
34. January Constatine
35. Lando Mabula
36. Abubakar Lyongo
37. Sued Mwinyi
38. Nswima Elnest
39. Malima Ndelema
40. Richard Leo
41. Mohamed Kisengo
42. Christina Chokunogela
43. Shaban Kisu
44. Salim Bonde
45. Sekion Kitojo
46. Ahmed Kipozi
47. Fatma Kipozi
48. Ezekiel Malongo
49. Abdul Ngalawa
50. Hendrick Maiko Libuda


Hata hamuelewani, nadhani Pascal amaweka waloptangulia mbele za haki? wewe unaweka na walio hai
 
Mkuu Pasco nakupata vilivyo. Kipindi fulani niliwahi kuuza mafuta kwenye kituo cha njia panda ya kwenda Tanga na Morogoro Chalinze ulikuwa unapita na LIPIKIPIKI lako kuuubwa. Nimekuuzia sana wese ukawa unasema unakwenda na pikipiki South Africa ukawa unabeba totoz za chalinze kwa kasi ya kutisha. Ulikuwa best yangu sana
Mkuu Mzito K, japo mabandiko yako humu, hayaonyeshi muuza wese, unless ni kusaidia tuu kama kazi ya home!, Pikipiki ni kweli, ila hilo la kubeba totoz za Chalinze kwenye pikipiki sio kweli, kwa sababu bike yangu ile, haikuwa na kiti cha abiria!.

Halafu hizo totoz za hapo Linze, mtu ubebe upeleke wapi?, wakati ni za kujiokotea tuu, hata nyuma tuu ya malori, mtu unamaliza shida zako!.
 
Nimemkumbuka Malima Ndelema, huyu alikuwa bingwa wa kipindi cha ngoma za asili za makabila mbalimbali, sijui yu hai bado au sijui yu wapi sasa huyu mtu.

Ni watu waliokuwa wanakupa sababu na kukulazimisha kusikiliza radio tofauti kabisa na sasa!

Haswaa mkuu,sasa hivi tunasikilizishwa taarab,vijembe vya watangazaji bila kupenda,vipindi vya kuelimisha hasa watoto kama kile cha mkoa kwa mkoa kilikuwa kizuri sana mtoto anakuwa anajua nchi yake ina makabila gani na utamaduni wao ni upi,kupitia redio tu.
 
Wanabodi,

Baada ya Kifo cha Mtangazaji Nguli nchini, Uncle J. Nyaisanga, naomba kuchukua fursa hii, kufanya reflection ndogo ya Watangazaji wa RTD waliotangulia mbele ya haki. Jee unawakumbuka?, unakumbuka vipindi vyao?!, unawakumbuka kwa lipi?!.


Hii list sio walikufa lini ni random, nikiwakumbuka wengine nitawaongeza!
Tukianzia na

  1. David Wakati
  2. Abdul Masudi (Jawewa)
  3. Eli Mbotto
  4. Stephen Mlatie
  5. Siwatu Luanda
  6. Salama Mfamao
  7. Salim Seif Nkamba (Mjomba)
  8. Michael Katembo
  9. Nelly Kidella
  10. Halima Mchuka,
  11. Omar Jongo
  12. Tumboi Tamimu Risasi
  13. Mohamed Ng'ombo
  14. Abisai Stephen (Uronu)
  15. Stephen Lymo.
  16. Nadhir Mayoka
  17. Juma Ngodae
  18. Rukia Machumu
  19. Karim Besta
  20. Henrick Michael Libuda
  21. Idrissa Sadalah
  22. Bati Kombwa
  23. Iddi Rashid Mchatta
  24. Dominic Chilambo
  25. Hassan Mkumba

Jee unawakumbuka?, unakumbuka vipindi vyao?!, unawakumbuka kwa lipi?!.
Pia sio vibaya kuwaulizia wale watangazaji wa siku nyingi ambao hatujui walipo, ili kama nao wametangulia tuyaingize majina yao.

RIP All the Fallen Heroes wa Tasnia ya Utangazaji Tanzania!,

Pascal.
naongeza:
26. ALLY SALEHE - MBILI KASOROBO NA MIDUNDO SAUTI YAKE ILIKUWA KAMA YA MASOUD MASOUD NGULI WA MUZIKI
27. KWEGIER MUNTHALI
hawa walikufa kwa ajali ya gari la Kwegier Munthali likigongwa na treni hapo gerezani /shaurimoyo?? waliopona ni pamoja na HILDA MWAIPOPO - sijui yu wa wapi - nilisikia aliolewa Kenya??
28. KHADIJA SAID - MWANAMKE WA KWANZA MTANGAZAJI - SIJUI KAMA YU HAI - KIPINDI CHAKE CHA WATOTO - MAMA WA KIGOMA HUYU.

umenigusa sana juu ya Salama Mfamao - kuna siku alipiga wimbo do you remember wa phil collins na kamvua kalikuwa kananyunya mahala fulani hadi wa leo ukipigwa wimbo huo huikumbuka sauti yake iliyokuwa nzuri.

29. DEBORAH CHIHOTA badae MWENDA.
30. RAY CHIHOTA
hawa walikuwa mtu na dada yake na mzee wao Chihota alikuwa maarufu Temeke na Serikalini. Ray alikufa kwa ajali ya gari Zimbabwe alikoamua kufuata roots. Ray alikuwa kwenye idhaa ya Kiingereza akiendesha kikundi cha vijana wakiimba Pop. Vijana kama kina Hussein Shebe nk. Pia alikuwa anasoma Taarifa za habari kwa Kiingereza
 
PASCO,

Ili tuelezane ukweli; tangu enzi hizo nimekuwa nikisikia from many different sources kuwa RTD ndio sehemu iliyokua inaongoza kwa fitina, uchawi na kurogana kazini...na hata ufuska...!
Could it not be that this high death rate ya wafanyakazi hapo RTD ilichagizwa na hizo factors??

mkuu ilikuwa inasikika sana kuwa watu wa Tanga wanamaliza wenzao!!! mambo ya uvumi dar ikiwa ndogo!!
 
Paschal....

Habari yako mkuu wangu....

Mkuu naomba pia kujua walipo watangazaji mahiri wa RTD na STZ enzi hizo....

Rosemary Mkangara...

Nathan Rwehabura-Mara ya mwisho alikuwa Sahara comm....

Othman Matata....

Kassim Mikongoro...

Daniel Msangya....

Wilson Malosha....

Geoffrey Erneo....

Abdallah Mlawa.....

Yusuph Omar Chunda (mzee wa methali na nahau huyu)....STZ

Makame Abdallah...STZ

Nkwabi Ng'wanakilala - Alikuwa Director wa RTD huyu....Nadhani hata wewe ulikuwa chini yake....

Nikutakie siku njema mkuu....

Bala.
Mkuu Bala,

Rosemary Mkangara... kwa sasa ni mjasiliamali, yupo kwao Gongo la Mboto-

Nathan Rwehabura-Mara ya mwisho alikuwa Sahara comm....bado yuko Sahara ndiye Mhariri Mkuu

Othman Matata....ni nduguye Chama Omar Matata-Ni mhadhiri wa mihadhara ya kidini.

Kassim Mikongoro...bado yuko TBC ni mwakilishi wa Mtwara, alichomewa nyumba yake kwenye zile vurugu.

Daniel Msangya....

Wilson Malosha....Ni PRO Viwanda na Biashara

Geoffrey Erneo....ni PRO-Bodi ya Utalii

Abdallah Mlawa.....ni retired anaishi Ilala Bungoni.

Yusuph Omar Chunda (mzee wa methali na nahau huyu)....STZ -retired yuko Zanzibar

Makame Abdallah...STZ

Nkwabi Ng'wanakilala - Alikuwa Director wa RTD huyu....Nadhani hata wewe ulikuwa chini yake....ni kweli, kwa sasa ni mhadhiri mkuu wa media chuo kikuu cha Tumaini.

Pascal.
 
Sala dumba nae sijui yupo wapi?

Mkuu wa wilaya mojawapo ya wilaya za mkoa wa Njombe. Hawa walitanguliwa na mama mmoja mtangazaji ambae alikuwa wa kwanza kuukwaa ukuu wa wilaya (dodoma??) kwa jina la Thecla-clara Gumbo - inasemekana kutokana na umahili wake wa kutangaza matukio ya siku ya uhuru wa Msumbiji wakati mate wake akiwa chakari na pombe za kireno!!!

Huyu Gumbo aliwahi pata ajali siku hizo pale Salenda (Surrender) bridge alfajiri moja - dar bwana ilikuwa ndogo sana enzi hizo!!

sijui yu wapi mama huyu mcheshi na mtangazaji mahili
 
Back
Top Bottom