Tujikumbushe sakata la Rada

Rev. Kishoka,

Nafikiri ilipofikia kwa nchi yetu ni kutokumwamini mtu mpaka imeonekana wazi hana madhambi.

Kwa muda mrefu nimekuwa mtetezi wa prof. Mwandosya kwa kutumia knowledge ndogo niliyo nayo juu yake. Lakini baada ya kushuhudia yale yanayojitokeza juu ya madhambi ya serikali ya awamu ya tatu, naanza kuwa na wasiwasi na watu wote waliokuwa na nafasi muhimu kwenye hiyo serikali.

Njia pekee ya kurudisha imani kwa sisi wananchi ni kwa wahusika wote kuchunguzwa ipasavyo ili wale wazuri wawe cleared.

Mwanahabari anasema deal la radar lilifanyika wakati prof hayuko madarakani, hiyo ni kweli, lakini pesa zililipwa wakati yeye yuko madarakani. Pia yule Mhindi alilipwa commission yake mwaka 2001 wakati prof. Mwandosya ni waziri. Je wakati anatoa mgawo, yeye prof. hakuambulia kitu?

Kwenye suala la TTCL, mimi niliwahi kufuatilia karatasi kwa karatasi. Kule timeline inakataa na nina uhakika kwamba uhusika wake ulikuwa wa kubambikiziwa zaidi ya ukweli.

Ununuzi wa ndege ya rais ulikuwa chini yake, je huyo Mhindi hakumkatia kitu?

Mtanzania, people here think this prof is clean, Mmmmm, better ask Mo Ibrahim, how much he spent on the prof. You remember the Mwanza speed boat boats saga, how he went fists with Magufuli!! Open your minds, with CCM no clean fish, all rotten!
 
Mtanzania, people here think this prof is clean, Mmmmm, better ask Mo Ibrahim, how much he spent on the prof. You remember the Mwanza speed boat boats saga, how he went fists with Magufuli!! Open your minds, with CCM no clean fish, all rotten!

IO,

Tupage basi ng'ombe japo mzima si mkia pekee...!
 
Mtanzania, people here think this prof is clean, Mmmmm, better ask Mo Ibrahim, how much he spent on the prof. You remember the Mwanza speed boat boats saga, how he went fists with Magufuli!! Open your minds, with CCM no clean fish, all rotten!

Lete data, amasivyo ni majungu tu...Ni ngapi Mo Ibrahim alimpa, na ni ufisadi gani wa boti...enlighten us...Magufuli alizuia zisipite hapa baada ya wahandisi kusema hazitaharibu barabara...Boti zikakubaliwa na serikali ya Kenya zipite kwao.

As I always say...No research, no right to speak...
 
angalau kidogo wazungu watusaidie kwa hili, manake juhudi za wananchi wa kitanzania peke yake huwa zinachukuwa muda mrefu hata ile kuwafichua tu mafisadi.

wakifanikisha hili wazungu utakuwa ni msaada wao BORA ZAIDI kwa tanzania kuliko mengine yoyote waliyowahi kuitoa
 
Mtanzania, people here think this prof is clean, Mmmmm, better ask Mo Ibrahim, how much he spent on the prof. You remember the Mwanza speed boat boats saga, how he went fists with Magufuli!! Open your minds, with CCM no clean fish, all rotten!

IO,

Lete mambo mkuu, mimi juu ya hili niko wazi kusikiliza pande zote. Siku hizi nimeacha kuwaamini hawa viongozi wa CCM, hata wale niliokuwa nawajua kwa karibu kama wasafi, sasa naanza kujiuliza mara mbili mbili.

Ilifika mahala deals zilikuwa kama ndio sera za viongozi wote wa CCM.

Mwaga kila kitu hapa, ili ambao tuko mbumbumbu tufunguliwe macho.

Najua prof. ana maadui wengi kwa muda mrefu, tena maadui wenye nguvu kama akina Lowassa, Rostam nk. Kwenye hili simweki JK kwasababu pamoja na kushindwa kazi jamaa ana uungwana wa aina fulani. Pamoja na ugomvi wake na Prof. lakini ingelikuwa kwa mapenzi yake naamini wangeshikana mikono na kuamua yaishe. Ila watu kama akina Lowassa na Rostam hakuna cha mambo yaishe. Sasa kama hawa watu wameshindwa kuja na kashfa za Prof. Mwandosya, huenda jamaa sio mchafu ukiachia maamuzi ya pamoja ya baraza la mawaziri.

Nakumbuka suala la boats ambazo Magufuli alikataa zisisafirishwe, je Prof. alikula chake hapo? Najua alikuwa na mikakati ya kutatua tatizo la usafiri kanda ya ziwa na kisha kutumia hayo mafanikio kwenye kampeni zake za urais, je kufanya hivyo ni kosa? Kama kuna la zaidi basi lilete mkuu.

Hilo la Mo Ibrahim najua litakuwa linahusiana na TTCL. Lete habari zaidi.
 
Wakuu,

Mimi naomba hii thread tuitenganishe. Huko nyuma nilikuwa na wazo la kuwajadili mawaziri wote waandamizi kwenye serikali ya awamu ya tatu. Labda huu ni wakati mzuri wa kuanza kuwajadili baadhi yao. Ningependekeza tufungue thread mpya ya kumjadili prof. Mwandosya kama ni msafi au fisadi.

Isichanganywe na mambo mengine na badala yake nguvu zote zielekezwe kwake. Tukimaliza tutaendelea na mawaziri wengine. Huu ni mwaka wa kumkoma nyani bila kumwangalia usoni.

Mnaonaje wakuu?
 
Salaleee! KADA MPINZANI huko aliko sijui kajinyonga? maana alikuwa hapa jamvini akitetea hawa mafisadi kwa nguvu zake zote lakini amegundua wanamfedhehesha kila kukicha.
HAWA MAFISADI HAWABEBEKI HATA KWA KITAMBAA CHA GUNIA.Kada rudi mkuu uombe radhi kwa uliyonena kwani hayakutoka moyoni mwako ila ulitumwa.
 
JK na Mwandosya walipokuwa wizara ya madini. Nimeitoa kwa Mjengwa.
 

Attachments

  • JKnaMwandosya.jpg
    JKnaMwandosya.jpg
    52.1 KB · Views: 43
Posted Date::4/24/2008
Uingereza sasa yafuatilia vigogo wengine 11 katika kashfa ya rada
* Wamo mawaziri na makatibu wakuu
* SFO yachunguza akaunti zao za benki

Na Ramadhan Semtawa
Mwananchi

BAADA ya akaunti ya Andrew Chenge, kuchunguzwa kwa tuhuma za kujipatia mabilioni ya shilingi kutokana na ununuzi wa rada ya kijeshi kutoka kampuni ya BAE System ya Uingereza, imebainika kuwa mchakato wa ununuzi wa rada hiyo unagusa vigogo wengine kumi wa serikali iliyopita na iliyopo madarakani

Kwa mujibu wa uchunguzi wa gazeti hili, uchunguzi wa vigogo hao kuhusika kwenye kashfa hiyo unafanywa na Taasisi ya Kuchunguza Makosa makubwa ya Jinia (SFO) ya Uingereza, ili kubaini kama nao walipata chochote.

Vyanzo huru vya habari vya Mwananchi kutoka serikalini, katika orodha hiyo ya vigogo ambao akaunti zao zinachunguzwa wamo mawaziri waandamizi katika serikali iliyopita na ya sasa.

Mawaziri hao wanatajwa kuhusika na kashfa hiyo kutokana na nyadhifa zao na uwajibikaji wao wa moja kwa moja au kutokana na nafasi zao kuhusika moja kwa moja na uidhinishaji mkataba na malipo.

Katika orodha hiyo pia wamo naibu waziri mmoja, makatibu wakuu wa wizara, wataalamu na maafisa waandamizi katika wizara iliyokuwa ya Mawasiliano na Uchukuzi na Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA) kutokana na mamlaka kuhusika moja kwa moja katika suala zima la usimamizi wa usafiri wa anga.

Taarifa hizo zimedokeza kwamba, kabla ya Chenge kuhojiwa, makachero wa SFO walifika nchini na kupata ruhusa ya kumchunguza.

Ununuzi wa rada hiyo kwa kiasi cha Sh70bilioni uliwahi kupigiwa kelele, kwamba utaitia hasara nchi kwa kuwa hizo ni fedha nyingi na kwamba mahitaji halisi ya nchi ingeweza kununua rada ya Sh5bilioni.

Hata hivyo, serikali ya awamu ya tatu ilipuuza malalamiko ya wananchi na kununua rada hiyo kwa madai kuwa ni kwa ajili ya usalama wa anga la nchi.

Sakata la ununuzi wa rada hiyo kwa Tanzania, ni sawa na linalotikisa nchini Saud Arabia ambayo imeuziwa vifaa vya kijeshi, huku Pauni1 bilioni zikidaiwa kuingizwa katika akaunti ya Mwana wa Mfalme Bandari, ambaye hata hivyo amekana kuwa na kiasi hicho cha fedha.

Kwa Tanzania, hadi sasa Chenge anachunguzwa ndiye anayechunguzwa na Taasisi ya Uingereza ya Makosa Makubwa ya Jinai, (Serious Fraud Office) kwa madai ya kujilimbikizia sh 1.2 bilioni katika akaunti yake moja katika kisiwa cha Jersey.

Wakati Chenge mwenyewe akiwa ameweka bayana msimamo wake wa kushirikiana na SFO na kutaka watu wasubiri matokeo ya taarifa ya uchunguzi huo.

Hata hivyo, uchunguzi wa SFO haumanishi kwamba wanaochunguzwa wamekula rushwa ya rada, bali kuangalia fedha zao zilipatikana kwa njia ipi na kama zina uhusiano na ununuzi wa rada hiyo.

SFO inachunguza ili kubaini kama dalali wa ununuzi wa rada hiyo kati ya serikali ya Tanzania na BAE System, Shailesh Vithlani aligawa fedha za kamisheni Sh12 bilioni kwa baadhi ya wanasiasa na maafisa wa Serikali ya Tanzania.
Wanamuogopa MKAPA kumuhoji?
 
Mnakumbuka muda mrefu waTZ tulilalamika sana kuhusu RADA sasa imekuwa mzigo kwa sisi waDanganyika kwani inahitaji zaidi ya Bilioni 10 za walipa kodi ili kununua kifaa cha 'UPS'.Vigogo kadhaa wameripotiwa kupigana vikumbo kugombea zabuni hiyo ya 'UPS' ambayo imetangazwa na serikali.
Je hii RADA inafaida yoyote kwa sisi taifa dogo la Tanzania?maana tunazidi kuumia na faida yako kwa mwananchi wa kawaida kuiona ni vigumu sana.
 
"Kwa miezi miwili sasa rada haifanyi kazi baada ya kuharibika na kifaa kilichoharibika kinaweza kuwa na thamani ya zaidi ya sh bilioni 10 na hivi tunavyosema, tayari makampuni kadhaa ya ndani na nje, yamechangamkia zabuni hiyo," amethibitisha Ofisa Habari wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Abel Ngapemba.

Lakini kumbukeni huyu Basili Mramba alisha sema kuwa waTanzania tupo tayari hata kula nyasi lazima RADA inunuliwe sijui naye alikuwa na % yake kama Chenge mlio karibu na hawa watu tusaidieni.
 
a 10 billion UPS? how big it must be!

iliyokuwepo imeharibika na haitengenezeki? au ndiyo madeal ya ulaji tena ......

Just wondering aloud ...
 
Hata mimi nashangaa is 10 bn or 10 mn? Maana hii price haingii kichwani kwangu kabisa! Mkuu fidel80 hebu tunaomba confirmation ya hii namba!
 
radar 40 billion, UPS 10! yaani robo ya thamani ya radar ni ups?! hii figa ya kweli jamani?
 
Ninavyo fahamu, ups ni chombo cha kuhifadhi umeme ili kama umeme wa tanesco ukizimika, hifadhi ya umeme iendelee kufanya kazi kwa muda badala ya chombo kinachotumika kisizimike ghafla. Vifaa vingi vinawekewa chmbo hiki, ups - computer, majokofu nk. Kwa kawaida, ups si chombo ghali ukilinganisha na chombo inacho kilinda. Kinachoshangaza hapa ni hivi kweli hiyo ups ya rada ya bae bei yake ni shilingi bilion 10!!! Jamani mwogopeni muumba.

Macinkus
 
But the Minister for Foreign Affairs and International Relations, Jakaya Kikwete, rejects such arguments.
"People say we do not need this system, what are they waiting for? When two jumbo jets crash over Tanzania, will people accept the need for us to have a radar system? This problem is real not fiction," he says.

The foreign minister emphasised not just the government's delight at the new system but also the need for new revenue.
The new system will enable Tanzania to track foreign craft flying over its airspace and consequently collect tax from them, he says.
"We are looking at an increased revenue of $2-5m a year. People are only talking of the $40m that we will spend purchasing the system but what about the revenue it generate?" says Mr Kikwete
.

JE MPAKA SASA WAMEKUSANYA REVENUE YA KIASI GANI, KUNA MWENYE DATA HAPA....jamani hizi sanaa zilianza zamani...hata muungwana alikuwa mmoja wao....$ 2-5m a year my foot where is the money...
http://news.bbc.co.uk/2/hi/africa/1723673.stm
 
What are the specs for the battery?

What are the specs for the Radar itself?

Is there a standby generator to automatically switch the power on?

Since Tanesco is unpredictable, has anyone thought of investing money in solar energy to ensure that the summer draught do not hinder Tanesco ability to supply electricity to our defense and aviation systems?

What does JWTZ use as back up for its Radars?

What was the term guarantee from BAE for service and replacement of parts?

Who came up with the price of $1,000,000.00 for radar UPS battery? Is the price for the Battery only or its is going to include shipping and instalation?

What caused the Battery to fail at first place?

If the battery was bad, what have they been using to supply back up power for the radar in the past 2 months?

If the Radar has been switched off for the past 2 months, what have they been using to monitor civil and millitary aviation activity flying on our skies?

Why no action has been taken in the last 2 months if it is known that this radar is critical to the security of our country and it has not been operating?
 
Ninavyo fahamu, ups ni chombo cha kuhifadhi umeme ili kama umeme wa tanesco ukizimika, hifadhi ya umeme iendelee kufanya kazi kwa muda badala ya chombo kinachotumika kisizimike ghafla. Vifaa vingi vinawekewa chmbo hiki, ups - computer, majokofu nk. Kwa kawaida, ups si chombo ghali ukilinganisha na chombo inacho kilinda. Kinachoshangaza hapa ni hivi kweli hiyo ups ya rada ya bae bei yake ni shilingi bilion 10!!! Jamani mwogopeni muumba.

Macinkus



Mkuu hapa wameweka hata posho za hao watakao enda kukichunguza vile vile wameweka cha juu chao n.k ndo serikali yetu ilivyo usanii kila mahala.
 
Aa,bwana wee, hatujui kama kweli imeharibika au vipi.Kuna methali moja ya kiswahili isemayo wajinga ndio waliwao.Ina wezekana hata haijaharibika,ila wanaendelea kutula tu,si unajua tenaa.
 
Back
Top Bottom