Charles Damson wa Mbeya. Huyu ilibidi atolewe nje ya uwanja kwa gari ya polisi akiwa amevalishwa yunifomu za askari polisi. Wakati washabiki wenye hasira wakiwa bado wanamsubiri mlangoni ili wampe kichapo huku wakidhani atatoka kwa mavazi ya kawaida au ya kirefarii, ujanja ulitumika kwa 'kumuazima' nguo hizo za kipolisi na hakuna hata mshabiki aliyegundua, hadi baadaye baada ya giza kuingia na wakaambiwa alishatolewa zamani!