GUSSIE
JF-Expert Member
- Dec 2, 2014
- 3,866
- 11,100
Uchumi unajengwa na mambo makuu mawili tu uuzaji na ununuaji iwe bidhaa au huduma (Demand and Supply). Mnyororo huu ukiyumba wa uuzaji na ununuaji tegemea maafa makubwa sana kwenye uchumi wa nchi
Hali mbaya ya maisha ilishaonekana hata kabla ya vita na niliandika uzi huu
Madhara ya uchumi huwa yanachukua muda mrefu sana kuonekana kuanzia miezi sita na kuendelea, Ongezeko la bei za mafuta na bidhaa kwa sasa hii ni rasha rasha tu, Vita ikiendelea ya Russia na Ukraine kila kitu kitaongezeka bei kwa asilimia mia moja (100%)
Nchi za ulaya na Marekani ndio watoa misaada mikubwa Africa, Hizi nchi za ulaya na Marekani ndio wanaotusaidia pesa za kigeni kwa utalii na kutupatia mikopo na misaada mbalimbali kama wakati wa korona, Hizi nchi kwa sasa wanapambana na hali zao za maisha kudhibiti mfumuko wa bei.
Tanzania tutapata wapi pesa za kigeni ili kuweza kudhibiti thamani yetu ya shilingi?
Ni watalii gani wana raha ya kuja Afrika wakati gharama zao za kumudu maisha ulaya zinazidi kuongezeka?
Mafuta ya ndege bei zimepanda, Nauli zitaendelea kupanda Katika sekta ya usafirishaji na hii itazifanya bidhaa zetu tutakazo uza nje kuonekana ni ghali sana.
Malengo ya Putin bado hayajulikani na mwisho wa vita hii hakuna anayejua lengo lake kiuchumi, zimebaki Propaganda tu lakini uhalisia na mwisho wa hii vita ni siri kubwa.
Athari za uuzaji na ununuaji bidhaa tayari Tanzania umeshaanza kuonekana kwa kasi ya ajabu sana.
Serikali ijitahidi kutoa ruzuku kwa Makampuni ya uagizaji wa mafuta ili kufidia gharama zao za usafirishaji.
Serikali isipoingilia kati tutegemee maisha màgumu zaidi miezi mitatu ijayo.
Nini cha kufanya kwa Raia binafsi?
Raia tunapaswa kudhibiti sana matumizi yetu na kupunguza sana baadhi ya mambo yasiyo ya msingi
Raia tunapaswa hasa wenye familia kubwa kuanza kupambana kutafuta bidhaa za msingi kwa maisha ya kitanzania kama mchele, unga,Mafuta ya kupika, maharage na Dagaa na kuanza kuyahifadhi.
Hali mbaya ya maisha ilishaonekana hata kabla ya vita na niliandika uzi huu
Je uchumi wa mfukoni umeporomoka zaidi toka uchaguzi wa Oktoba 2020?
Members, Hili ni swali ambalo linaangazia uchumi halisi wa watu binafsi kwenye mitaa yaani uwezo wa Mtu mmoja mmoja kumudu maisha yake ya kila siku (Micro enonomics) kutoka oktoba mwaka 2020 mpaka oktoba mwaka huu 2021 Uchumi wa Mtu binafsi tutaupima kwa vigezo vifuatavyo ndani ya mwaka mmoja...
www.jamiiforums.com
Madhara ya uchumi huwa yanachukua muda mrefu sana kuonekana kuanzia miezi sita na kuendelea, Ongezeko la bei za mafuta na bidhaa kwa sasa hii ni rasha rasha tu, Vita ikiendelea ya Russia na Ukraine kila kitu kitaongezeka bei kwa asilimia mia moja (100%)
Nchi za ulaya na Marekani ndio watoa misaada mikubwa Africa, Hizi nchi za ulaya na Marekani ndio wanaotusaidia pesa za kigeni kwa utalii na kutupatia mikopo na misaada mbalimbali kama wakati wa korona, Hizi nchi kwa sasa wanapambana na hali zao za maisha kudhibiti mfumuko wa bei.
Tanzania tutapata wapi pesa za kigeni ili kuweza kudhibiti thamani yetu ya shilingi?
Ni watalii gani wana raha ya kuja Afrika wakati gharama zao za kumudu maisha ulaya zinazidi kuongezeka?
Mafuta ya ndege bei zimepanda, Nauli zitaendelea kupanda Katika sekta ya usafirishaji na hii itazifanya bidhaa zetu tutakazo uza nje kuonekana ni ghali sana.
Malengo ya Putin bado hayajulikani na mwisho wa vita hii hakuna anayejua lengo lake kiuchumi, zimebaki Propaganda tu lakini uhalisia na mwisho wa hii vita ni siri kubwa.
Athari za uuzaji na ununuaji bidhaa tayari Tanzania umeshaanza kuonekana kwa kasi ya ajabu sana.
Serikali ijitahidi kutoa ruzuku kwa Makampuni ya uagizaji wa mafuta ili kufidia gharama zao za usafirishaji.
Serikali isipoingilia kati tutegemee maisha màgumu zaidi miezi mitatu ijayo.
Nini cha kufanya kwa Raia binafsi?
Raia tunapaswa kudhibiti sana matumizi yetu na kupunguza sana baadhi ya mambo yasiyo ya msingi
Raia tunapaswa hasa wenye familia kubwa kuanza kupambana kutafuta bidhaa za msingi kwa maisha ya kitanzania kama mchele, unga,Mafuta ya kupika, maharage na Dagaa na kuanza kuyahifadhi.