Tujenge shule yetu, walimu 10 wanahitajika

Tujenge shule yetu, walimu 10 wanahitajika

Nitafute kwa namba 0628944712 mkuu hata mwenyewe nina wazo la namna hiyo pia naweza kupa wazo namna ya kupata hata gali
 
Hili wazo zuri ila 25m kuanzisha madarasa kumi haiwezekani. Mi naona mjipe muda tena wa kwenda kutafuta pesa zingine kama 50m huku mkikopa kama 20m benki ili ziwe 70m angalau muanze hata na madarasa matatu. Mkifosi kuna mmoja wenu mjanja atajitokeza na kuwaliza hizo 25m. Waalimu kajipangeni upya. Kama hamjaanza kuchangishana msianze na kama kuna ambaye kashatoa hela arudishiwe kwanza. Biashara ya shule naifahamu A to Z.
 
Shule za primary kimuundo ni nzuri kwa faida kuliko secondary. Mm ni mwalimu wa secondary, nina experience na biashara ya shule kwa takriban miaka mitano, ukianzisha primary school unapata watoto bado wadogo, ww ndo unaaanza nao, unawamold kitabia, unawapa first sight ya elimu ww, wanapata muda wa kukuzoea na kuanza kukupenda, kisha wanakuelewa. Hapo unakua na guarantee ya ufaulu wao wakimaliza darasa la saba. Ila changamoto ya sekondary ipo kwenye ufaulu tu..uwe na uhakika wa kupata pool nzuri ya watoto kutoka mashule tofauti, yaan pool nzuri kitabia lakini pia msingi wa kingereza na utayar wa watoto, experience yangu inaonesha watoto wengi wanamaliza shule ya msingi hata kiingereza hawajui, sasa na ww ndo unakabidhiwa hao watoto. Ni vgumu kufikia malengo kwakweli kwa njia hio.
Uko sahihi mkuu shule za primary zinalipa kuliko sekondari. Mwaka 2015 nilitafiti kidogo kuhusu mchakato wa kuanzisha shule.
Kwa maeneo ya mjini eneo la shule linapaswa kuwa walau hekari 3 na nusu na vijijini hekari 7.
Pia kuna kigezo cha kuwa na 60m bank wakati unaanza, baada ya kukamilisha ujenzi wa majengo kwa asilimia 75.
Na haya majengo yakaguliwe na kupitishwa na mkandarasi wa Mkoa/Wilaya.
Haya ni masharti ktk muongozo wa kuanzisha shule wa 1982(outdated)
Wakati ule shule zilikuwa zinaanza bila kukidhi vigezo vyote ila awamu hii tuombe Mungu conservative wawe flexible.
Mwaka jana nilikuwepo ktk mchakato wa ku register chuo , jamaa yangu ni Principal pale everything was good ila urasimu ulichelewesha sana usajiri.

Kiujumla ni wazo zuri safi sana mkuu umenirudisha 2015 tukiwa na wazo la kuanzisha pre/primary school mimi na washkaji.

My advice : Don't underestimate construction cost.,na uzoefu kidogo na masuala ya ujenzi.
 
Kwa kuanza haina haja ya madarasa kumi....walau madarasa ma 4 hivi, ofisi, vyoo, maji, umeme, ....by then nilitembelea shule 2 Arusha....kilimani hii ni shule kubwa tayari....ya pili ni kimandoru shule ya kkkt hii ndo ilikuwa kwenye expansion ila ilikuwa simple sana....last year nilitembelea shule mpya inaitwa Tulia Asc haina hayo madarasa 10 ila miundombinu muhimu yote ipo.
Naifahamu shule moja iliyoanza na two classes plus ofisi.
So guys let us be realistic.
 
Ni lazima awe mwalimu professional au hata mtu ambaye ameishia o level ili mradi ajue vyema kufundisha vyema lugha ya kiingereza na kiswahili.
Unaweza kufundisha mkuu ikiwa utakubaliana na wahusika wenye taasisi yao japo kisheria isn't right lazima uwe na professional au licence ya kufundisha....ukipata nafasi ya kufundisha maana yake ni kuwa jina lako na cv havitawasilishwa kwa mamalaka husika kukaguliwa.

NB : Baada ya mchakato wa majengo kukamilika lazima walimu wathibitishwe kuwa na vigezo vya kufundisha.
 
Mkuu vipi kuhusu usajili umeshalifuatilia hilo hasa vigezo?, kumbuka shule siyo majengo, mim naweza shauri kama bado embu fuatilieni vigezo na mambo yote ya usajilikabla msije mkajenga vyumba vya madarasa mkavigeuza mabanda ya kuku wa kienyeji.

Ikiwezekana mkachukue vibali vya mwanzo huku mkiahidi kuanza ujenzi mara moja, hapa ikibidi washirikisheni wadau wa elimu mkoa husika kuanzia mkoani adi tarafa msije lia baadae
 
Mkuu vipi kuhusu usajili umeshalifuatilia hilo hasa vigezo?, kumbuka shule siyo majengo, mim naweza shauri kama bado embu fuatilieni vigezo na mambo yote ya usajilikabla msije mkajenga vyumba vya madarasa mkavigeuza mabanda ya kuku wa kienyeji.

Ikiwezekana mkachukue vibali vya mwanzo huku mkiahidi kuanza ujenzi mara moja, hapa ikibidi washirikisheni wadau wa elimu mkoa husika kuanzia mkoani adi tarafa msije lia baadae
..wakikwama watakodisha majengo, usiwatishe.
 
Vipi kama mtu anazo hizo 2m na fani yake si mwalimu?
 
Back
Top Bottom