Achilia mbali kuwa na plan B tu, sasa hivi inabdi uwe mpaka na plan Z. Mimi nina mpaka plan Z...
Nakumbuka sana mafundisho ya dini nikiwa secondary kuhusu Urafiki, Uchumba na Ndoa; tuliambiwa (na kweli ina make sense) kuwa ni vizuri kuwa na marafiki wengi, lakini mchumba ni mmoja na kipindi cha uchumba maana yake unakuwa umefungwa (huwezi kuruhusu mchumba mwingine in case umemkubali wa kwanza); hiki ni kipindi cha kuchunguzana tabia kabla ya kujifunga moja kwa moja kwenye ndoa.
Lakini kwa sasa idadi kubwa ya watu (hasa wadada) walioko kwenye uchumba wana kuwa na bima au plan B au mpango wa kando. Hali hii ikija kugundulika mara nyingi hupelekea muhusika kukosa yote hata kama alikuwa anapenda kuolewa.
Sasa wana jamvi naomba tujadili kuhusu:-
- ulazima au umuhimu wa plan B
- Kiini cha tatizo hasa ni nini?
- Nini kifanyike ili hii hali isiendelee?
cc lara 1, amu, Paloma, Nicas Mtei, Eiyer, Evelyn Salt na walioko kwenye ndoa watuambie waliolewa/oa na plan A au B gfsonwin, @fp, snowhite, Dark City, Mtambuzi, Wiyelele Kaizer hata wale walio kwenye complicated situation kama The Boss, KIKUNGU SnowBall Kongosho et el karibuni.
Ha ha ha, unaweza jikuta una plan hadi infinity
We mbaya, umemfanyia nini mwenzio. Ila kweli inaboa sana kuwekwa plan B
Katika mapenzi ya kileo wadada walio wengi hupenda kuwa na "Plan B", nadhani hufanya hivyo kutokana na kupenda ubwerere wa mambo. Unamkuta mdada anakuwa na wapennzi wengi kiasi kwamba kawapangia kila mmoja position yake bila wenyewe kujijua, unakuta kuna mpenzi wakumlipia kodi ya nyumba, kuna wakumvisha, kuna wakumlisha na kuna wa kumpatia burudani. Hii yote inatokana na wadada kutotaka kuzitumia pesa zao.
Ukija upande wa pili, wakaka nao pia huwa hawatabiriki bhana unamkuta leo sosoliso yuko na Paloma ila ukimkuta kesho unamkuta yuko na Blue G ,hii pia inapelekea wadada wetu kuwa na "Plan B" ili pakiharibika huku wanako pakuegeshea mgongo huku wakitafuta wapi penye mapenzi ya kweli.
BTW hii tabia ya kuwa na "Plan B" haina umuhimu wowote chamsingi ni kila mmoja kuwa mwaminifu katika mapenzi yake na kujua ni nini alichofata katika mahusiano hayo. Wadada acheni kutegemea sana wakaka katika kuyaendesha maisha yenu kwani hata nyinyi mnaweza bila kuwezeshwa. Pia wakaka acheni tabia za kuwabadilisha dada zetu kama nguo.
Kila mtu amcague ampendae kwa dhati na amchunguze kwa kadri awezavyo ndipo afanye maamuzi stahiki.
Juzi tu!Achilia mbali kuwa na plan B tu, sasa hivi inabdi uwe mpaka na plan Z. Mimi nina mpaka plan Z...
yap sikuwa na mdate, but kwangu mm nilifikiri plan b ni mtu ambaye yupo as ukikosa bara basi pwani upatehny, asante kwa kushare your story ingawa sidhani kwamba mumeo alikuwa plan B kwani hukuwa unamdate kipindi uko na mchumbao.
Juzi tu!
umeshapona mpaka umekuwa na hadi plan Z?
kuna mkaka rafiki yangu alikuwa anataka kuoa. tumeshaanza vikao vya harusi na kwa binti tayari vikao vya sendoff mdada akakaa na wazazi akawaambia hawezi tena kuolewa na yule kaka, wamrudishie mahari.....
kwa vile nilikuwa karibu naye akatufwata kutupa mkasa kuwa binti ndo keshammwaga.....
sasa tunamwambia tuahirishe vikao? maana hubby alikuwa mwenyekiti wa kamati, akasema no tuendelee.... naomba tu this weekend unisindikize kutoa mahari kwa plan b.......
basi weekend tukaenda kutoa mahari, vikao vikaendelea, harusi ikafungwa..... chezeya plan b!
sasa asingekuwa na plan b kungekuwa na mlolongo mkuuubwaaa tena wa kuahirisha vikao na harusi
yap sikuwa na mdate, but kwangu mm nilifikiri plan b ni mtu ambaye yupo as ukikosa bara basi pwani upate
All the best,hahaha dunia ya leo kama maigizo sometimes matukio inakuwa vigumu kuamini lakini ndipo human race ilipofikia. Ila na huyo jamaa noma lakini namuonea huruma aliyemuoa maana atakuwa kamuoa si kwa kupenda bali kuficha aibu ambayo ingempata. Haa sasa we wadhani nitabaki naugulia mpaka lini.
kuna msemo unasema when life F*** you keep on moving otherwise it will keep on F*** you until you find yourself enjoying it and you will never move on.
Na mimi sitaki endelea kuwa mtu wa majozi I am moving on with plan B, C, D
All the best,
that's all I can wish you for now
wengi wanachofanya sio kuwa na plan b bali muoaji mostly ndo anakuwa yuko no 2 mdada yupo na mtu wake anaempenda,lakini huyo mtu hana mpango wa kuoa so muoaji anapojitokeza,dada anakubali ndoa huku anakuwa mgumu kumuacha wa kwake so waoaji wengine wanachunguza ndo wanagundua hilo na kusitisha ndoa, ndoa kwenye jamii yetu ni deal sana bado,kuolewa ni bahati wanasema,so kukataa muoaji hata kama hapendwi ni ngumu..
Nashukuru kwa mchango.Dada Kaunga siku hizi mambo ni kidijitali yaani kuwa na channel nyingi zaidi:
- Ukiomba kazi lazima uandike barua za maombi kwenda ofisi zaidi ya moja incase moja inabuma nyingine inaweza kujibu.
- Ukiwa na Profession moja usiridhike, fashion ni kusoma fani zaidi ya moja. Dunia ya leo unaweza kufukuzwa au kupunguzwa kazini ukaendelea kufanya kazi ya fani iliyopo sokoni huku ukisubiria majibu ya fani yako uipendayo.
- Kwa kuwa siku hizi uchumba mpaka ndoa ni ishu, na waoaji walio wengi siku hizi ni mpaka waonje "Kalimati" kwanza waone kama ina sukari au la, na kwa kuwa wadada walio wengi wanajijua wameshatumika vya kutosha (kama ni gari linasoweza kusoma mileage 200,000km), sasa wanahofu jamaa akigundua injini imekongoroka na kushushwa mara kadhaa wakati yeye amekwisha watangazia wenzake ndoa ni aibu. Hivyo anamua kuwa na 'Multiple relashionship' ili mmoja akichoropoka akamate kwingine mambo yaendelee.
- Suala kuu hapa ni kutojiamini.
what i believe is smtms watu huwa wna date wrong choice na baadae Mungu huwa analeta the correct choice kwao.duuuh kwa hiyo alikuwa second option. Mimi sipendi kuwa second option ya mtu maana kuna probability kubwa siku first optiion akirudi wakayamaliza nikabaki ninalia na moyo.