Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 22,606
- 29,755
Waziri wa Elimu mhe. Adolf Nkenda amesimamia maamuzi ya Baraza la Mitihani la Taifa kuhusu uamuzi wa kufuta matokeo ya baadhi ya wanafunzi ambao wamegundulika kufanya wizi wa mitihani yao ya Taifa.
Amewaomba Wabunge waunge mkono msimamo wa Baraza kwenye uamuzi huo. Na bahati mbaya sana kwa wabunhe wetu wamekosa hoja kwa umoja wao kuitaka serikali itoe plan B kwa waliofutiwa mitihani kwa sababu kuwaondoa kwenye mfumo wa elimu ambayo ndiyo msingi wa maendeleo ya Taifa ni sawa na kuwanyima haki ya kuishi kama watanzania wengine.
Leo jamii inahangaika kwa kila familia kubeba mzigo wa watoto wao wanaoahindwa kuendelea na masomo kwa sababu mbalimbali ikiwemo kufeli, utoro, mimba na hili la kuondolewa sifa ya kuelimika.
Serikali isiyojali wananchi wake huwa na kawaida ya kuwatengenezea sababu za kuwakwamisha kufikia malebgo yao. Kwa mfano, shule ambazo wanafunzi hao wanatoka zimekwepa kuadhibiwa kama vituo vya mitihani ilihali inajulikana kuwa kila shule ina serikali ya wanafunzi na ofisi za nidhamu ambazo kwa sehemu kubwa zinahusika na ulinzj na usalama wa shule, kanuni na mwenendo wa wanafunzi wawapo shuleni. Hapa mwenye akili afahamu.
Tukija kwenye hili la kufuta matokeo.
Waziri anasimama kwa kujiamini na ufahari kuutangazia umma namna serikali inavyojisikia vyema na haki kuwafutia matokeo watoto ambao wamebainika kushiriki wizi wa mitihani. Mimi binafsi ninaungana na jamii kukemea wizi na udanganyifu kwenye mitihani. Lakini kama mzazi. Kama kiongozi naangalia anguko la kesho la jamii endapo tutakuwa na wimbi kubwa la raia ambao ni illiterate. Ninapendekeza serikali iweke umuhimu wa kuangalia namna ya kushughulika na wimbi la wizi wa mitihani.
Ukiniukiza nini kifanyike ninashauri kwamba, wanafunzi wote waliofutiwa mitihani kwa sababu za wizi wanapaswa kulipia upya ada za mitihani na watarudia kufanya mtihani wa taifa unaofuata yaani wwtarudi kwenye shule zao na kufuata taratibu za kufanya mitihani lakini muda wote wa kusubiria mitihani watakuwa nyumbani au tuisheni za mitaani. Lengo ni kuwafanya wajutie na kuona aibu ya kurudia kosa walilolifanya.
Serikali pia iangalie namna ya kuwarejesha kwenye mstari wa elimu wanafunzi ambao wamekosa alama za kuendelea ngazi zinazofuata za elimu. Yaani ianzishwe mamlaka itakayosimamia mtaala maalumu wa mafunzokazi kwa wanafunzi hawa ili wakifaulu muhula wa miaka 2 waweze kukubaliwa kujiunga elimu ya diploma na hata digrii huko mbele.
Mfumo huu utassidia sana kuibua wabunifu na wanataaluma wabobezi kww sababu siyo wote waliofeli hawana uwezo darasani bali kuna memgi yanajiri kipindi cha kufanya mitihani.
Ninamshauri Prof Adolf, asiendelee kusimamia mfumo kandamizi wa elimu bali kwa taaluma yake ya uprofesa aje na ubunifu namna ya kulikabili tatizo badala ya kuishi nalo kama inavyofanyika sasa.
Ninapoona mtoto wa jirani yangu amefeli au amefukuzwa shule au amefutiwa mtihani sijisikii vizuri kama mzazi. Nawaza endapo atakosa elimu, halafu baadaye akaja kuwa kiongozi sijui itakuwaje kama taifa na jamii.
Seriaki ibebe mzigo wa hawa vijana badala ya kuwaachia wazazi na jamii kisha baadaye kuja kuwashughulikia kama wahalifu pale wanapoona hawana cha kupoteza.
Wanafunzi hawa ni wenetu. Ni wa Taifa kwa jumla.
Amewaomba Wabunge waunge mkono msimamo wa Baraza kwenye uamuzi huo. Na bahati mbaya sana kwa wabunhe wetu wamekosa hoja kwa umoja wao kuitaka serikali itoe plan B kwa waliofutiwa mitihani kwa sababu kuwaondoa kwenye mfumo wa elimu ambayo ndiyo msingi wa maendeleo ya Taifa ni sawa na kuwanyima haki ya kuishi kama watanzania wengine.
Leo jamii inahangaika kwa kila familia kubeba mzigo wa watoto wao wanaoahindwa kuendelea na masomo kwa sababu mbalimbali ikiwemo kufeli, utoro, mimba na hili la kuondolewa sifa ya kuelimika.
Serikali isiyojali wananchi wake huwa na kawaida ya kuwatengenezea sababu za kuwakwamisha kufikia malebgo yao. Kwa mfano, shule ambazo wanafunzi hao wanatoka zimekwepa kuadhibiwa kama vituo vya mitihani ilihali inajulikana kuwa kila shule ina serikali ya wanafunzi na ofisi za nidhamu ambazo kwa sehemu kubwa zinahusika na ulinzj na usalama wa shule, kanuni na mwenendo wa wanafunzi wawapo shuleni. Hapa mwenye akili afahamu.
Tukija kwenye hili la kufuta matokeo.
Waziri anasimama kwa kujiamini na ufahari kuutangazia umma namna serikali inavyojisikia vyema na haki kuwafutia matokeo watoto ambao wamebainika kushiriki wizi wa mitihani. Mimi binafsi ninaungana na jamii kukemea wizi na udanganyifu kwenye mitihani. Lakini kama mzazi. Kama kiongozi naangalia anguko la kesho la jamii endapo tutakuwa na wimbi kubwa la raia ambao ni illiterate. Ninapendekeza serikali iweke umuhimu wa kuangalia namna ya kushughulika na wimbi la wizi wa mitihani.
Ukiniukiza nini kifanyike ninashauri kwamba, wanafunzi wote waliofutiwa mitihani kwa sababu za wizi wanapaswa kulipia upya ada za mitihani na watarudia kufanya mtihani wa taifa unaofuata yaani wwtarudi kwenye shule zao na kufuata taratibu za kufanya mitihani lakini muda wote wa kusubiria mitihani watakuwa nyumbani au tuisheni za mitaani. Lengo ni kuwafanya wajutie na kuona aibu ya kurudia kosa walilolifanya.
Serikali pia iangalie namna ya kuwarejesha kwenye mstari wa elimu wanafunzi ambao wamekosa alama za kuendelea ngazi zinazofuata za elimu. Yaani ianzishwe mamlaka itakayosimamia mtaala maalumu wa mafunzokazi kwa wanafunzi hawa ili wakifaulu muhula wa miaka 2 waweze kukubaliwa kujiunga elimu ya diploma na hata digrii huko mbele.
Mfumo huu utassidia sana kuibua wabunifu na wanataaluma wabobezi kww sababu siyo wote waliofeli hawana uwezo darasani bali kuna memgi yanajiri kipindi cha kufanya mitihani.
Ninamshauri Prof Adolf, asiendelee kusimamia mfumo kandamizi wa elimu bali kwa taaluma yake ya uprofesa aje na ubunifu namna ya kulikabili tatizo badala ya kuishi nalo kama inavyofanyika sasa.
Ninapoona mtoto wa jirani yangu amefeli au amefukuzwa shule au amefutiwa mtihani sijisikii vizuri kama mzazi. Nawaza endapo atakosa elimu, halafu baadaye akaja kuwa kiongozi sijui itakuwaje kama taifa na jamii.
Seriaki ibebe mzigo wa hawa vijana badala ya kuwaachia wazazi na jamii kisha baadaye kuja kuwashughulikia kama wahalifu pale wanapoona hawana cha kupoteza.
Wanafunzi hawa ni wenetu. Ni wa Taifa kwa jumla.