Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 25,946
- 38,657
- Thread starter
- #21
Kumbe kila mtu anapaswa kuota kwa mipaka ya familia yake?mkuu kwani we ni nani kwenye nchi hii hadi uwaotee wakubwa badala ya familia yako?
au we ni Tumia akili yule wa kitengo nyeti anakuja na habari ni ndoto.
Mwaka 2001 mwezi March nilikuwa Shinyanga kijijini Likonongo nikiwa na maafisa wa UNICEF na Wizara ya Afya kwenye mradi wa PHAST.
Katika mojawapo ya recap ya ahsubuhi niliwasimulia ndoto niliyoiota kuwa niliona marekani kuna moto na majengo yameporomoka. Niliandika kwenye diary maana nilistuka usingizini nikasoma Bible na Kusali maana niliona wafu wengi sana....
Miezi 6 mbele ndo ikatokea balaa la Sept 11. Nilichokiona kuhusu kuungua na kuporomoka kilikuwa sawia kabisa mkuu.
Nasema nimeota ndoto inayojirudia rudia lakini sikufanikiwa kuona sura.
Nikewaza sana kabla sijawashirikisha hapa. Inawezekana kuna mtu anaweza kutusaidia kwenye tafsiri.
Mimi siyo mtafsiri wa ndoto ujue


