TUGHE: Zitto Kabwe ashtakiwe

TUGHE: Zitto Kabwe ashtakiwe

Status
Not open for further replies.
masikini nimesikitika, yani tuna safari ndefu kufika tunapopataka halafu tunataka maendeleo na mabadiliko kwa fikra za namna hii tutafika kweli. nimeumia jamani.

unajua maisha ya kujipendekeza mabaya sana msamehe bure. bora wazungu warudi kututawala kuliko hawa waswahili wenzetu wenye fikra mgando!!
 
kwani wananchi wote ndo wamemwajiri Rais? Ni wale tu waliopiga kura na kumchagua JK ndo wanapaswa kujua mshahara wake na si wananchi wote. yaani hata machadema nanyi mnajiita ni mwajiri wa JK?
4275608271_4e731bb018.jpg
 
masikini nimesikitika, yani tuna safari ndefu kufika tunapopataka halafu tunataka maendeleo na mabadiliko kwa fikra za namna hii tutafika kweli. nimeumia jamani.
Umeona eh, japo umechelewa kusikitika lakini mradi umeng'amua hilo ni hatua kadhaa tu mbele huku wengine wakipiga hatua nyingi nyuma kama huyu Chabruma, hebu angalia avatar yake kwanza!

 
Siamini kama kweli TUGHE wametoa kauli ya ajabu ka hii, kama ni kweli basi hakuna sababu ya kuwa chini ya TUGHE na ndo mana mimi nilikataa kusaini fomu ya kuchangia 2% ya mshahara wangu TUGHE.
 
Zito kavunja sheria za nchi. Kama kuna sheria inamlinda basi aiseme kilichomtuma kufanya hivyo.
 
yaani mburula kama wewe umwajiri Rais? kichekesho sana. binafsi namlaumu sana ZITTO kwa move aliyoianzisha tena kwa maslahi yake binafsi ndani ya chama.
Mkuu, Rais ameajiriwa au hajaajiriwa?, kama ameajiriwa, ameajiriwa na nani?
 
Rais aliomba kazi ya kutuongoza, nasi tulimpa kwa njia ya kura. Rais naye amewateua Mawaziri na Vigogo wengine ili wamsaidie kutuongoza vizuri. Sasa inakuwaje dhambi/siri kwa Mwajiri kutaka kujua mishahara wanayojipangia bila sisi wenye nchi kuhusishwa? Haiingii akilini hata siku moja kwa Mwajiri kutojua mshahara wa mtumishi wake aliyemwajiri, vinginevyo utakuwa Mwajiri fake!
Wezi wote hawataki mabosi wao wajue wanaiba wanakujaga kazini hata na mashati yenye viraka na ndala zilizochanika lakini mwisho wa wiki ni ndani ya tinted na viwalo vya bei mbaya; Hilo ni tangazo tosha kwamba nchi imeporwa na wezi wanatunga sheria za kulinda wizi wa mali ya bosi - ni kama ameshakufa vile
 
yaani mburula kama wewe umwajiri Rais? kichekesho sana. binafsi namlaumu sana ZITTO kwa move aliyoianzisha tena kwa maslahi yake binafsi ndani ya chama.

huyo unaemwita mburula jk alimpigia magoti na kumfuata kijijini ili ampe kazi...unafikiri mchezo jk kuzunguka na helkopta tatu
 
Hivi kwa mfano kama Kikwete hizo pesa anapeleka wapi?, halipi kodi ya nyumba, hanunui nguo, halipi umeme wala maji, hanunui chakula, hizo pesa zote analipwa za kupeleka wapi?
Nilisoma hapa juzi, mishahara ya maraisi kama Obama wa USA, Kenyata, Msumbiji, Uingereza, China na nyingine nyingi hata nchi inayoitwa ya kidikteta Zimbabwe yote imewekwa wazi.
Swali ninalojiuliza ni kama hao walioiweka hiyo mishahara wazi nao walisitahili kushikiwa kama TUGHE wanavyotaka iwe kwa Mh. Zitto.
Ndio maana nchi hii haitakaa iendelee na aina ya watu wanaoitawala kwa sasa, kwa nini mshahara uwe siri wakati umeutolea jasho. ....nikijijibu hapa ni kuwa usiri huu ni kwa sababu (mfano) waziri mkuu kwa hakika hasitahili 24m ukilinganisha na anachoifanyia nchi hii kama ilivyo kwa mwalimu anaye shape mustakabali wa taifa hili asivyostahili 250,000/-!

 
masikini nimesikitika, yani tuna safari ndefu kufika tunapopataka halafu tunataka maendeleo na mabadiliko kwa fikra za namna hii tutafika kweli. nimeumia jamani.

mkuu unaenda wapi unataka kufika nchi hii ilishakombolewa kitambo kilichopo ni watu kama wewe kuwasaidia kujikomboa kutoka katika dhana ya kufanya mambo yasiyo ya maana kwa taifa hili.
 
Mkuu, Rais ameajiriwa au hajaajiriwa?, kama ameajiriwa, ameajiriwa na nani?
Mkuu utauliza maswali mengi na hutajibiwa, kukurahisishia hebu tafuta report ya Prof. Wangwe inayoeleza ni nani wanamuunga mkono mkulu!

 
Mkuu utauliza maswali mengi na hutajibiwa, kukurahisishia hebu tafuta report ya Prof. Wangwe inayoeleza ni nani wanamuunga mkono mkulu!

Nitaitafuta mkuu, lakini unaweza kunipa hints kidogo kama hautajali.
 
kwani wananchi wote ndo wamemwajiri Rais? Ni wale tu waliopiga kura na kumchagua JK ndo wanapaswa kujua mshahara wake na si wananchi wote. yaani hata machadema nanyi mnajiita ni mwajiri wa JK?

Unaupeo mdogo sana... Sasa wale ambao kura zao hazikutosha raisi wao nani??? Raisi ni mfanya kazi wetu wote hata kama hukumpigia kura ila alichaguliwa na wengi huyo ni wa wote na kujua mshahara wa raisi its not an ishue hao tughe wanashindwa kupigana watumushi wao wapate maslahi bira wanang'ang'ana na ishu zisizo na manufaa tayari tumesha ujua kama aliropoka au alipanga kusema haileti madhara yoyote sisi kuujua mshahara wa raisi.
 
CHAMA cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya Nchini (TUGHE) kimetaka Zitto ashtakiwe kwa kutamka mshahara wa Rais na Waziri Mkuu hadharani.
Wapuuzi wa maisha hao.... Ndio jamaa huwa wanawadharau
 
we umemwajiri kivipi?

Naona mpango wa makamba unafanya kazi. Mmenunuliwa simu mje kutoa hoja au kutetea ujinga? Toa hoja itakayowafanya watu wakubaliane na wewe sio kuleta masikhara.
 
Naona mpango wa makamba unafanya kazi. Mmenunuliwa simu mje kutoa hoja au kutetea ujinga? Toa hoja itakayowafanya watu wakubaliane na wewe sio kuleta masikhara.

mkuu naona leo umeingia asubuhi ukitoka mchana ataingia nani?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom