TUCTA kwa nini hamjamuunga mkono Ester Bulaya kwenye suala la Kikokotoo?

Mzee Ngonyani

JF-Expert Member
Dec 16, 2022
826
1,881
1685697505825.png

Picha: Ester Bulaya

Ninashangaa pamoja na baadhi ya wabunge kuwapigania wafanyakazi kuhusu kubadilisha kikokotoo kinachowanyonya wafanyakazi, Wakiongozwa na mbunge Ester Bulaya lakini viongozi wa TUCTA wamekaa kimya. Hiyo ndo dalili ya usaliti sio bure mtakuwa na maslahi fulani mnapata. Katibu na Mwenyekiti mjitokeze kukanusha kuwa ninyi sio sehemu ya wale waliokubaliana kupitisha kikokotoo cha kinyonyaji.

Halafu mnapangia mstaafu umri wa kuishi duniani eti aishi miaka kumi na mbili na nusu baada ya kustaafu halafu mwisho wake ataishije. Wastaafu wengi sasa hivi wanaishi zaidi ya miaka sabini.

Bahati mbaya hao mawaziri mnaojadiliana nao wenyewe wakimaliza muda wao hupewa hela zao zote, hawasubili miaka 55 au 60. Hata kama mnataka uteuzi yawapasa kutimiza majukumu yenu ya kumsaidia mfanyakazi ambae amekufanya uwe hapo na huyo waziri au serikali ikuone.

Solidarity forever.
 
Huo ujasiri wa kumuunga mkono wanautoa wapi? Viongozi wote wa hiyo TUCTA ni mamluki tu wa ccm. Labda waitapike kwanza ile asali waliyo lambishwa tangu enzi za mwendazake.

Hao viongozi wa hiyo TUCTA, siku zote wapo kwa ajili ya kusimamia ajenda na maslahi ya ccm, na siyo maslahi ya wafanyakazi.
 
Nilitarajia Mei mosi wangepaza sauti lakini wapi. Inavyoonekana hata kwenye hizo sherehe za wafanyakazi huwa serikali inawapangia cha kusema. Swala la kikokotoo ni mwiba mchungu kwa wafanyakazi
 
Nilitarajia Mei mosi wangepaza sauti lakini wapi. Inavyoonekana hata kwenye hizo sherehe za wafanyakazi huwa serikali inawapangia cha kusema. Swala la kikokotoo ni mwiba mchungu kwa wafanyakazi
Dawa kwa wale wafanyakazi majasiri ni kukopa tu limkopo likubwa, na kwenda kujiajiri. Ika siyo kusubiria mafao kupitia hicho kikotoo cha kipumbavu.

Yaani mbunge kila baada ya miaka 5, analipwa milioni 250! Halafu mfanyakazi wa kawaida baada ya miaka zaidi ya 30 kazini, unampa mafao ya 33%!

Ni wafanyakazi mbumbumbu pekee ndiyo watavumilia huu ujinga. Wale wenye akili timamu wote, naamini watajiongeza.
 
Back
Top Bottom