Tuambie kwanini huwa unazima simu usiku?

Tuambie kwanini huwa unazima simu usiku?

Nipo kama bundi muda wowote ukipiga napokea...
Thubutuuuuu! Labda ukiwa huna wa kumla kichwa Usiku huo😁😁😁😁 ambapo kuna muda asubuhi nakuona kuwa ulikesha ukiwanga uzi wa Usiku wa manane 😂😂!
 
Habari machalii…

Leo nazungumza na jamaa zangu mnaozima simu ikifika usiku. Kwanini unapenda kuzima simu ikifika usiku?

Ikitokea dharura watu wakitaka kukujulisha usiku huo watakupataje?

Haya tuambie kwanini unapendelea kuzima simu?
Simu yangu kuzima ni pale inapokuwa Haina chaji tu mkuu
 
Thubutuuuuu! Labda ukiwa huna wa kumla kichwa Usiku huo😁😁😁😁 ambapo kuna muda asubuhi nakuona kuwa ulikesha ukiwanga uzi wa Usiku wa manane 😂😂!
Mara chache sana nauendea huo uzi, mara nyingi nakua busy na mambo yangu usiku wa manane ambayo niachiwe mwenyewe...
 
Kuna hizi simu za saa tano saa sita halafu mtu anakuuliza umelala? Ilihali anakusikia kabisa umelala. Hata kama ni wewe kwa nini usizime simu au kuweka DND au konki au flight mode?!

Binafsi simu yangu ikifika jioni ni kwa ajili ya familia. Wengine tupatane kesho.
 
Back
Top Bottom