Kurunzi
Platinum Member
- Jul 31, 2009
- 10,196
- 11,625
Habari wanajamvi heri ya mwaka 2020
Kwa wale ealiona wenzi wenu tuambie ulipataje najua wangine walisota sana wengine kama walisuka mlevi shimoni na nk.
Mimi binafsi ilikuwa hivi, nilikuwa kwenye harakati za kutafuta nyumba maeneo ya Tabata baada ya kuchoka maisha ya sinza nilipata nyumba yenye sebule, kajiko kadogo , chumba na washing room kwa ilikuwa nyumba mpya haijawahi kukaliwa na mtu, mwenye nyumba alikuwa anataka 120,000 kwa mwezi nikasema poa ingawa bajeti yangu ilikuwa laki, mwenye nyumba alikuwa ni mama wa kichaga alikuwa anaishi Moshi tukakubaliana nimtumie hela kwenye simu yake tulikubaliana nilipe kodi ya miezi sita 720,000.
Kwenye harakati za kutuma hela nikakosea namba ya kutuma ikaenda kwa mtu mwingine nilipagawa hiyo siku ilikuwa mbaya sana kwangu nikawa nawapigia voda huku natetemeka hawapoke kipindi basi ikabidi nipige hiyo namba niliyokosea akapokea sauti ya Dada mmoja nikajieleza huku natia huruma nikimsihi sana anirudidishe, nilimueleza ilikuwa ni kodi ya nyumba tena niliikopa, dada alinijibu usijali nitakurudishia.
Mungu mkubwa alinirudishia hela yangu yote bila kujali makato ya ada ya kutuma kwakweli sikuamini nilimshukuru sana, baada ya hapo tukaanza kuwasiliana kwa ukaribu ilichukuwa miezi mnne tunawailiana tu kwa simu kila tukipanga kuonana nilikuwa na sita kwakuwa nilikuwa na mtu mwingine mkoani ingawa hatukuwa serious sana.
Siku moja walipata msiba wa baba wa mmoja wa staff mwenzao suku ya kuaga ndiyo ilikuwa siku pia tulipanga kuonana basi tukakubaliana tukutane mahali then nimsindikize kwenye msiba nikasema sawa, niseme tu siku hiyo nilikuwa na mchanganyiko wa feelings kama hofu, raha kimuhemuhe nk halahaula nilipo muona tu moyoni nilisema huyu ndiyo atakuwa mke wangu tulikumbatiana kwa hisia kali sana mpaka watu walitushangaa..basi tukaa kwa dakika chache then tukaenda msibani kuaga baada ya hapo tulienda kukaa mahali tukaongea sana kila mtu alikuwa yupo tayari kufunguka nilimtamkia siku hiyo kuwa wewe utakuwa mke wangu na akawa hivyo.
Sasa ni familia ya watoto wawili me na ke miaka 14 ya ndoa.
Kwa wale ealiona wenzi wenu tuambie ulipataje najua wangine walisota sana wengine kama walisuka mlevi shimoni na nk.
Mimi binafsi ilikuwa hivi, nilikuwa kwenye harakati za kutafuta nyumba maeneo ya Tabata baada ya kuchoka maisha ya sinza nilipata nyumba yenye sebule, kajiko kadogo , chumba na washing room kwa ilikuwa nyumba mpya haijawahi kukaliwa na mtu, mwenye nyumba alikuwa anataka 120,000 kwa mwezi nikasema poa ingawa bajeti yangu ilikuwa laki, mwenye nyumba alikuwa ni mama wa kichaga alikuwa anaishi Moshi tukakubaliana nimtumie hela kwenye simu yake tulikubaliana nilipe kodi ya miezi sita 720,000.
Kwenye harakati za kutuma hela nikakosea namba ya kutuma ikaenda kwa mtu mwingine nilipagawa hiyo siku ilikuwa mbaya sana kwangu nikawa nawapigia voda huku natetemeka hawapoke kipindi basi ikabidi nipige hiyo namba niliyokosea akapokea sauti ya Dada mmoja nikajieleza huku natia huruma nikimsihi sana anirudidishe, nilimueleza ilikuwa ni kodi ya nyumba tena niliikopa, dada alinijibu usijali nitakurudishia.
Mungu mkubwa alinirudishia hela yangu yote bila kujali makato ya ada ya kutuma kwakweli sikuamini nilimshukuru sana, baada ya hapo tukaanza kuwasiliana kwa ukaribu ilichukuwa miezi mnne tunawailiana tu kwa simu kila tukipanga kuonana nilikuwa na sita kwakuwa nilikuwa na mtu mwingine mkoani ingawa hatukuwa serious sana.
Siku moja walipata msiba wa baba wa mmoja wa staff mwenzao suku ya kuaga ndiyo ilikuwa siku pia tulipanga kuonana basi tukakubaliana tukutane mahali then nimsindikize kwenye msiba nikasema sawa, niseme tu siku hiyo nilikuwa na mchanganyiko wa feelings kama hofu, raha kimuhemuhe nk halahaula nilipo muona tu moyoni nilisema huyu ndiyo atakuwa mke wangu tulikumbatiana kwa hisia kali sana mpaka watu walitushangaa..basi tukaa kwa dakika chache then tukaenda msibani kuaga baada ya hapo tulienda kukaa mahali tukaongea sana kila mtu alikuwa yupo tayari kufunguka nilimtamkia siku hiyo kuwa wewe utakuwa mke wangu na akawa hivyo.
Sasa ni familia ya watoto wawili me na ke miaka 14 ya ndoa.