Tuambie jinsi ulivyompata mwenzi wako

Tuambie jinsi ulivyompata mwenzi wako

Kurunzi

Platinum Member
Joined
Jul 31, 2009
Posts
10,196
Reaction score
11,625
Habari wanajamvi heri ya mwaka 2020

Kwa wale ealiona wenzi wenu tuambie ulipataje najua wangine walisota sana wengine kama walisuka mlevi shimoni na nk.

Mimi binafsi ilikuwa hivi, nilikuwa kwenye harakati za kutafuta nyumba maeneo ya Tabata baada ya kuchoka maisha ya sinza nilipata nyumba yenye sebule, kajiko kadogo , chumba na washing room kwa ilikuwa nyumba mpya haijawahi kukaliwa na mtu, mwenye nyumba alikuwa anataka 120,000 kwa mwezi nikasema poa ingawa bajeti yangu ilikuwa laki, mwenye nyumba alikuwa ni mama wa kichaga alikuwa anaishi Moshi tukakubaliana nimtumie hela kwenye simu yake tulikubaliana nilipe kodi ya miezi sita 720,000.

Kwenye harakati za kutuma hela nikakosea namba ya kutuma ikaenda kwa mtu mwingine nilipagawa hiyo siku ilikuwa mbaya sana kwangu nikawa nawapigia voda huku natetemeka hawapoke kipindi basi ikabidi nipige hiyo namba niliyokosea akapokea sauti ya Dada mmoja nikajieleza huku natia huruma nikimsihi sana anirudidishe, nilimueleza ilikuwa ni kodi ya nyumba tena niliikopa, dada alinijibu usijali nitakurudishia.

Mungu mkubwa alinirudishia hela yangu yote bila kujali makato ya ada ya kutuma kwakweli sikuamini nilimshukuru sana, baada ya hapo tukaanza kuwasiliana kwa ukaribu ilichukuwa miezi mnne tunawailiana tu kwa simu kila tukipanga kuonana nilikuwa na sita kwakuwa nilikuwa na mtu mwingine mkoani ingawa hatukuwa serious sana.

Siku moja walipata msiba wa baba wa mmoja wa staff mwenzao suku ya kuaga ndiyo ilikuwa siku pia tulipanga kuonana basi tukakubaliana tukutane mahali then nimsindikize kwenye msiba nikasema sawa, niseme tu siku hiyo nilikuwa na mchanganyiko wa feelings kama hofu, raha kimuhemuhe nk halahaula nilipo muona tu moyoni nilisema huyu ndiyo atakuwa mke wangu tulikumbatiana kwa hisia kali sana mpaka watu walitushangaa..basi tukaa kwa dakika chache then tukaenda msibani kuaga baada ya hapo tulienda kukaa mahali tukaongea sana kila mtu alikuwa yupo tayari kufunguka nilimtamkia siku hiyo kuwa wewe utakuwa mke wangu na akawa hivyo.

Sasa ni familia ya watoto wawili me na ke miaka 14 ya ndoa.
 
Naskiaga malaika, malaika kumbe wapo!! Hongera mkuu kwa kupata malaika.. angekuwa mwengine hapo ni ama sahivi angekuwa anasimulia kwenye ule uzi wa kushuhudia nguvu za giza kwa jinsi ambavyo ungemfanya nafikiri angejutia uhai wake wote... Lkn bado najiuliza huyo Ni binadamu toleo la ngapi..? Maana kwa jinsia ke ni ngumu Sana kumtenganisha na fedha!,bila shaka atakuwa na uhusiano na wanawake wa karne ya 2, wanasayansi wanahangaika kutafuta viumbe toka nje ya dunia yetu wkt kumbe tunaishi nao!
 
Naskiaga malaika, malaika kumbe wapo!! Hongera mkuu kwa kupata malaika.. angekuwa mwengine hapo ni ama sahivi angekuwa anasimulia kwenye ule uzi wa kushuhudia nguvu za giza kwa jinsi ambavyo ungemfanya nafikiri angejutia uhai wake wote... Lkn bado najiuliza huyo Ni binadamu toleo la ngapi..? Maana kwa jinsia ke ni ngumu Sana kumtenganisha na fedha!,bila shaka atakuwa na uhusiano na wanawake wa karne ya 2, wanasayansi wanahangaika kutafuta viumbe toka nje ya dunia yetu wkt kumbe tunaishi nao!
Bado wapo mkuu ni juzi tu hapa nami nilikua namtumia mama angu chochotr kitu nikakosea namba ilikua toka bank kwemda M Pesa ilibidi nipige hiyo namba alipokea mdada nikamueleza huwezi amini alinirudishia pesa yangu yote nilishangaa sana yani.

Mungu ambariki sana dada G toka Mwanza
 
Hongera mkuu....

Mimi bado narukaruka kutafuta mwenza PM na sijibiwi miaka sasa imepita.

Niliota ubavu wangu upo hapa JF.

Sijui nachokifanya ni sahihi?

[emoji23][emoji23][emoji23]endelea tu kurukaruka
 
hizi ni story za kufikirika ambazo huwa zinaandikwa bila kuzingatia time frame so mwandishi anaweza akahisi amewakamata mapembe watu wengi kumbe kuna watu vichwani mwao wanadata ambazo hazifutiki....next time atajitahidi kutuletea story yenye kaukweli kidogo
Assuming jamaa alioa kesho yake baada ya kukutana msibani basi ni almost miaka 15 coz kuna ile miezi minne ya kuwasiliana..
Miaka 15 from now ni almost 2004
Kwahyo unataka kusema 2004 kulikuwa na Mpesa??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Assuming jamaa alioa kesho yake baada ya kukutana msibani basi ni almost miaka 15 coz kuna ile miezi minne ya kuwasiliana..
Miaka 15 from now ni almost 2004
Kwahyo unataka kusema 2004 kulikuwa na Mpesa??
Alivyosema wana miaka 14 moja kwa moja nikaweka ?? Kwa sababu Mpesa na tigo pesa kama sikosei zimeanza 2008-2009

Ila zilipamba moto kuanzia 2010
 
Back
Top Bottom