Tuache Wivu kwa Nehemia Mchechu

Tuache Wivu kwa Nehemia Mchechu

Status
Not open for further replies.
Kujadili mishahara ya watumishi Tanzania ni upotezaji wa muda sababu hakuma mwenye uhakika wote huwa mnaleta story mlizosikia tu na kila mtu anakuja na kiasi anachohisi.
Mimi nna uhakika i have been dealing with Payrolls za watumishi wa umma
 
Hivi naomba niulizie kwa huyo mchechu ,wahindi ndio watu special kwenye shirika lenu kupanga?
Na wanatumia kigezo gani kupata nyumba zote za mijini? Mbona sisi hatupati?
Hili swali nlishawahi kumuuliza huyu jamaa pesonale. Akasema huu ubadhirifu ulishafanyika miaka mingi nyuma. Watu wana mikataba ya ajabu. Yeye alichoweza kufanya ni kupandisha kodi ya upangishaji. Kuwaondoa ni ngumu kwakuwa sheria inawalinda.
 
Hivi naomba niulizie kwa huyo mchechu ,wahindi ndio watu special kwenye shirika lenu kupanga?
Na wanatumia kigezo gani kupata nyumba zote za mijini? Mbona sisi hatupati?
tulitakiwa tuanzia hapa sio kuquestion mshahara kwani akija anae lipwa laki mbili atabadilisha haya,kwani before mchechu hizo nyumba mlikaa waswahili wangapi?kingine kunanyumba za NHC zilikuwa mali ya hao wahindi kabla ya sera za ujamaa
 
Watu wana wivu tu na mchechu. Hata rais ana wivu na mchechu.

Watu kibao wanalipwa zaidi ya mchechu ila hawaongelewi. Mchechu yamemkuta hayo kisa tu alikua team lowassa.

Yule mama wa tanzania investment centre anakula 38+m, na wengine wa dawasco,tpdc,tcra,rea nk ila hawaguswi.

Ni wivu tu kwa mchechu. Sioni sababu ya kumuonea wivu mchechu.
Hivi Rais alimtaja jina? Nadhani issue sio Msechu bali kuna mishahara ya ajabu hata watu hawastahili. Kwa Msechu jamani siwezi kusema sana kwa sababu aliyofanya ni amazing! Ila tu serekali itafute namna ya kujenga bei za nyumba nafuu. Halafu bahati kwa sasa utawala wa haki bais kweli wale wa hali ya chini ndio wapate hizo nyumba na mtu asipate nyumba zaidi ya moja!
 
Kwani yeye tu ndio CEO ambaye shirika lake lina mchango mkubwa? Kwanza sijui NHC inachangia kiasi gani kwenye pato la taifa. Kwa hoja yako basi DG wa TANAPA ndo anatakiwa ale hela ndefu maana tourism ina mchango mkubwa kwenye GDP ya nchi.
Unaujua mshahara wa Kijazi???
 
akitokea tajiri akanifanya kwa kocha Newcastle, akanipa hela za kumsajili Messi,Ronaldo,Ibrahimovic,Aguero,Thiago Silva,Neymar,Pogba.De gea na wengineo,ninachukua EPL.

Inawezekana NHC imepewa meno ambayo wakurugenzi wengine hawakupewa ndio maana mnamuona Mchechu anapaform. Anawezakuja kuondoka yakajakutwa madeni ya hatari pale,period
 
Hivi naomba niulizie kwa huyo mchechu ,wahindi ndio watu special kwenye shirika lenu kupanga?
Na wanatumia kigezo gani kupata nyumba zote za mijini? Mbona sisi hatupati?
Wahindi walianza kuishi kwenye National Housing kabla Msechu hajawa DG huko na wala kabla hajazaliwa...
 
sijawahi kusikia raisi wowote duniani anataka kugusa kila kitu hadi sekta binafsi.
huyu magu uongozi kasomea wapi? uongozi sio kuchafuana,uongozi sio ubabe,uongozi sio kisasi,uongozi sio kujifanya kujua bali kusikiliza zaid na kuongea kidogo.
 
akitokea tajiri akanifanya kwa kocha Newcastle, akanipa hela za kumsajili Messi,Ronaldo,Ibrahimovic,Aguero,Thiago Silva,Neymar,Pogba.De gea na wengineo,ninachukua EPL.

Inawezekana NHC imepewa meno ambayo wakurugenzi wengine hawakupewa ndio maana mnamuona Mchechu anapaform. Anawezakuja kuondoka yakajakutwa madeni ya hatari pale,period
Manchester City inamilikiwa na mtu tajiri sana duniani, je ilishawahi fika hata Quarter Finals za CL??

Real Madrid imekuwa club tajiri duniani kwa miaka zaidi ya kumi mfululizo, lakini ilikaa miaka 10 bila kubeba CL..

BTW, Investment za NHC ni favorable.. Deni sio shida, kuna kitu kinaitwa Payback Period.. Baada ya muda hayo madeni yatajilipa na Shirika litaanza kujiendesha kwa faida. Mfano; ukikopa Million 50 ukajenga nyumba then ukaja kuiuza kwa Million 70 hapo umepata faida ya Million 20..
 
Kila mtu anamchango kwa taifa hili, ingekuwa hivyo basi wengine wakae pembeni wamwachie Shirika afanye mwenyewe
 
Nimekuwa nafuatilia mjadala hasa wa Rais Mtukufu bwana Magufuli kuhusu mishahara ya watumishi kuwa mikubwa.

KIMSINGI Nadhani rais ana nia njema ya kujenga moyo wa uzalendo kwa watu ili watangulize maslahi ya Taifa kwanza na yao binafsi yaje baadae.

Tatizo langu nikwamba watu wengi tumejikita zaidi kumshambulia Nehemia Mchechu CEO wa NHC. Eti tu kwa kiwango tunachokiita kikubwa cha mshahara wa M35. Wengi wetu hatuzungumzii Mchechu alikutoka alikuwa analipwa 26M.

Na alianza project ya kujenga nyumba akiwa kwenye taasisi yake ya zamani. So serikali iliona atafunika NHC zaidi kwasababu ni wazi shirika lilishakuwa kinapumulia mipira.

NHC kifupi ikishakaribia kufa Bwana Mchechu hakuomba kazi NHC serikali ilimfuata. Mchechu amefanya kazi kubwa sana NHC ukilinganisha na ilivyokuwa mwanzo. Mchechu anastahili kulipwa zaid ya hapoo.

NHC ni shirika la 3 now kwa Ubora wa mashirika ya Nyumba africa lakwanza NHS ya SA yapili Ethiopia na Tatu Tanzania. Sasa mnataka huyu kijana wa watu afanye nini? Watu wanaongea hoja ya nyumba za NHC kuwa za bei kali sio za watu wa hali ya Chini.

Thats true but we have to know kwamba Sera ya NHC haijawahi kuwa na sera hiyo ya nyumba za bei nafuu kwa watu wa Hali ya Chini. Hakuna mahala popote NHC iliwekwaa kwaajili ya kujenga makazi ya Wanyonge.

So kama kuna watu tunahitaji NHC iwe ya wanyonge ni kuwakumbusha watunga Sera wetu wakabadili sera ya NHC kuacha kujiendesha kibiashara. Mchechu hata kwa hako ka M30 anatuhurumia tuu.

Wenye vyeo kama chake huko kwenye taasisi aliyotoka sasa hivi wanakula mpaka M75. Ifike mahali tusisukumwe kwa wivu pekee juu ya Mchechu tuache wivu tumuache afanye kazi.


Nimepita Dakawa juzi kuulizia Nyumba ya kununua ya chini kabisa room 2 ni sh M35. Hata hivyo nikaambiwa nyumba za kuuza zimeisha ila za kupangisha zipo hapo. Ina maana wanajengewa matajiri wanaoweza kununua pao kwa papo na kuzipangisha kwa maskini. NHC fo the rich ones. God save.
 
Manchester City inamilikiwa na mtu tajiri sana duniani, je ilishawahi fika hata Quarter Finals za CL??

Deni sio shida, kuna kitu kinaitwa Payback Period.. Baada ya muda hayo madeni yatajilipa na Shirika litaanza kujiendesha kwa faida. Mfano; ukikopa Million 50 ukajenga nyumba then ukaja kuiuza kwa Million 70 hapo umepata faida ya Million 20..

Nyumba ikishakaa miaka nne kuendelea inachakaa na matengenezo inakuwa gharama kubwa, technologia inabadilika, mfumo wa umeme na maji usisema, Liangalie jengo la NIC/ Bima jijini - auziwe nani @ siku kuungua. Ndio maana serikali ikaamua kuziuza za kwake. NHC ukiacha kawe inajenga maporini pasipo soko. Huko Dakawa na Songea wapi na wapi.
 
Mkuu ahsante kwa kuliweka hivyo, kwa kuongezea duniani hapa hakuna kitu kinaitwa wanyonge, hizi huwa ni kauli za wanasiasa kuteka mind za watu wasiojitambua, bidhaa zinazalishwa kwa fedha na zinauzwa kwa fedha, kinachotakiwa ni kufanya kazi kwa bidii kama huna maarifa, na kufanya kazi kwa bidii na maarifa kama ulibahatika kupata maarifa, serikali inaweza kuleta unafuu flani ktk huduma flani kwa kupunguza kodi, lazima mjue kuwa itaongeza gharama sehemu nyingine ambayo kwa vyovyote vile lazima itakuathiri.

Nimekuwa nafuatilia mjadala hasa wa Rais Mtukufu bwana Magufuli kuhusu mishahara ya watumishi kuwa mikubwa.

KIMSINGI Nadhani rais ana nia njema ya kujenga moyo wa uzalendo kwa watu ili watangulize maslahi ya Taifa kwanza na yao binafsi yaje baadae.

Tatizo langu nikwamba watu wengi tumejikita zaidi kumshambulia Nehemia Mchechu CEO wa NHC. Eti tu kwa kiwango tunachokiita kikubwa cha mshahara wa M35. Wengi wetu hatuzungumzii Mchechu alikutoka alikuwa analipwa 26M.

Na alianza project ya kujenga nyumba akiwa kwenye taasisi yake ya zamani. So serikali iliona atafunika NHC zaidi kwasababu ni wazi shirika lilishakuwa kinapumulia mipira.

NHC kifupi ikishakaribia kufa Bwana Mchechu hakuomba kazi NHC serikali ilimfuata. Mchechu amefanya kazi kubwa sana NHC ukilinganisha na ilivyokuwa mwanzo. Mchechu anastahili kulipwa zaid ya hapoo.

NHC ni shirika la 3 now kwa Ubora wa mashirika ya Nyumba africa lakwanza NHS ya SA yapili Ethiopia na Tatu Tanzania. Sasa mnataka huyu kijana wa watu afanye nini? Watu wanaongea hoja ya nyumba za NHC kuwa za bei kali sio za watu wa hali ya Chini.

Thats true but we have to know kwamba Sera ya NHC haijawahi kuwa na sera hiyo ya nyumba za bei nafuu kwa watu wa Hali ya Chini. Hakuna mahala popote NHC iliwekwaa kwaajili ya kujenga makazi ya Wanyonge.

So kama kuna watu tunahitaji NHC iwe ya wanyonge ni kuwakumbusha watunga Sera wetu wakabadili sera ya NHC kuacha kujiendesha kibiashara. Mchechu hata kwa hako ka M30 anatuhurumia tuu.

Wenye vyeo kama chake huko kwenye taasisi aliyotoka sasa hivi wanakula mpaka M75. Ifike mahali tusisukumwe kwa wivu pekee juu ya Mchechu tuache wivu tumuache afanye kazi.
 
Nyumba ikishakaa miaka nne kuendelea inachakaa na matengenezo inakuwa gharama kubwa, technologia inabadilika, mfumo wa umeme na maji usisema, Liangalie jengo la NIC/ Bima jijini - auziwe nani @ siku kuungua. Ndio maana serikali ikaamua kuziuza za kwake. NHC ukiacha kawe inajenga maporini pasipo soko. Huko Dakawa na Songea wapi na wapi.
Kwahiyo ulitaka watu wa Songea na Dakawa wasipate huduma?? Na wewe nyumba yako unayoishi unahama kila baada ya miaka minne?? Au ni nini umeongea hapa?? Project nyingi za NHC kabla hata hazijaisha watu tayari wameshafanya booking... Juzi hapa walionyesha Mtwara na wakasema tayari watu wengi wameshafanya bookings kwenye hiyo mijengo wanayojenga..
 
Mwambie aliekutuma kuwa na yeye ni jipu....not long from now atatumbuliwa...
 
Watz bado tumeathiriwa na fikra za ujamaa,tunachukia sana watu wenye mafanikio,hatutaki kuwatumia kama case study ili na sisi tuwe kama wao.Fikra za namna hii ndio imesababisha Tanzania kuchelewa kupata maendele.Ktk uchumi wa kibepari mwenye bidii na kipaji ndio huzawadiwa (rewarded).
 
Watz bado tumeathiriwa na fikra za ujamaa,tunachukia sana watu wenye mafanikio,hatutaki kuwatumia kama case study ili na sisi tuwe kama wao.Fikra za namna hii ndio imesababisha Tanzania kuchelewa kupata maendele.Ktk uchumi wa kibepari mwenye bidii na kipaji ndio huzawadiwa (rewarded).

Mafanikio ganiiiiii? Kwanza huyo hakufuatwa na Serikali inaonekana ulianzisha mada hii umesahau Mada iliyomhusu Mchechu humu JF pindi Jengo refu la Indira Gandhi lilipo poromoka na kuua watanzania kibao. Huyu Mchechu aliomba kazi kitambo kupitia Shirika moja la Kimataifa katika Usaili na linaloheshimika sana Tanzania na Duniani kote. Alifeli katika michakato ya usaili lakini Figisufigisu zikafanywa akapewa ulaji kwa maslahi ya watu. Hivi wewe ukipewa MAHELA na support yote kutoka Serikali tena na mihela mingine ni mideni kwa Serikali utashindwa kusimamisha mijengo? Hebu niambie Nyumba ya bei nafuu ni Mil. 60 - 80 ya vyumba 3? Halafu Viwanja anajiuzia mwenyewe. Huyu cheki bobu alizani Kijibenki alichokuwa anakiongoza ni sawa na kitu kinaitwa SHIRIKA LA NYUMBA LA TAIFA lidude,kubwa. Matokeo yake kaingia kichwakichwa kimenuka kudadadeki... eti mshahara Mil. 35. Anakula nini? anaishi wapi? labda Dubai kila jioni baada ya masaa ya kazi anachukua ndege ya kukodi anarudi kupumzika hadi kesho yake kazini. Vinginevyo aje hapa ajustify matumizi ya Mil. 35. Jipu hili.
 
Kwenye uchaguz mkuu, wakurugenzi wote wa mashirika ya umma walshajulkana walowaunga mkono, kati ya Lowassa na Magufuli,,,,Muda c mrefu, Mchechu atapgwa chini....Ikitokea hvo, tutakuwa tumepoteza jembe kwa sababu za kisiasa,,,,kwa ufupi, Lowassa alwakamata watu wengi wenye ubunifu na uthubutu (mf. Mchechu). Magufuli akiamua kuwatmua wafuasi wote wa Lowassa, ataishia kutengeneza kikosi cha NDIO MZEE na ktk outcome ataumbulia kauli za TUNAHUJUMIWA MZEE,,,amuombe Mungu amjalie moyo kama wa Mandela,otherwise ataishia kuwa kichekesho
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom