Phillipo Bukililo
JF-Expert Member
- Dec 29, 2015
- 18,473
- 13,624
Sitetei mshahara wake, natetea creativity yake. Ni yeye ambaye alikuja na wazo la nyumba zote za NHC kupakwa rangi ya pinki. Alipokwenda kwenye mabenki ikawa rahisi kupewa mikopo, ikawa rahisi kuaminiwa kwanini haikuwa taabu kwa wamiliki wa mabenki kuzitambua nyumba zote zilizokuwa chini ya NHC. Aliyepita mbona hakuweza kuwa na ubunifu wa aina hiyo?. Hivi sasa shirika linajenga nyumba nyingi kila kona ya Tanzania, inawezekana leo hii nyumba hizo hazina wapangaji/wanunuzi, lakini tukumbuke kuwa lengo ni Tanzania ya watu wa kipato cha kati. Maana yake ni kwamba wateja wengi wa nyumba hizi watapatikana siku za mbeleni, kadri ambavyo uzalishaji wa viwanda utakavyoleta tija, kadri ambavyo uwezo wa mtanzania wa kawaida wa kuyamudu maisha yake utakavyoongezeka.
Siwezi kuuongelea mshahara wa Nehemia Mchechu, at least ninajiona kama ninao wajibu wa kuheshimu ubunifu wake mpaka akaweza kuyavuta mabenki yakaipatia NHC fedha nyingi za ujenzi wa nyumba, ambazo nyingi kati ya hizo zitakuja kuwafaa watanzania katika siku zijazo.
Siwezi kuuongelea mshahara wa Nehemia Mchechu, at least ninajiona kama ninao wajibu wa kuheshimu ubunifu wake mpaka akaweza kuyavuta mabenki yakaipatia NHC fedha nyingi za ujenzi wa nyumba, ambazo nyingi kati ya hizo zitakuja kuwafaa watanzania katika siku zijazo.