Eric Cartman
JF-Expert Member
- May 21, 2009
- 11,960
- 11,221
Ungelikuwa wewe ndio mkurugenzi faida yako ni sh 8 billion una market share ya 1%-3% na strategy yako ni kukuwa kwa kuongeza idadi ya wateja.Sijasema ni gawio ni kodi nilichosema ni kuwa mashirika ya umma yanatakiwa kutoa gawio kisheria kama vile tunavyotakiwa kulipa kodi kisheria.
Hiyo sh billoni 2 unadhani ina manufaa kuitumia kwenye promotional and marketing campaigns za kuvutia wateja wale ambao unaweza wafikia kwa sasa au kumpa serikari ambae nayeye anataka kuona unakuwa?
Ni hivi biashara sio politics mwisho wa siku kama wewe ndio serikari unataka kuona wanakuwa na kurudisha faida iliyonona kuwatetea hao watu ni kuwadumaza kiakili ata sehemu kubwa ya hotuba ya mkurugenzi imejaa wimbo wa mapambio kwa raisi kushinda malengo ya kibiashara.
Nyota njema uonekana asubuhi kama tu walichonacho hakuna jitihada zozote za kukitumia to the maximum kwa malengo ya kupata wateja walio kwenye range kwanini udhani wakiongezewa mtaji watabadilika.
Ni hivi kwa management ile kupeleka pesa za walipa kodi in reality ni kuwanyima watanzania wengine huduma muhimu ambazo serikari ina jukumu la kuziboresha pia.
Hawa wanatakiwa wapewe targets kwanza wanazoweza kufikia kutokana na resource capability walizo nazo kuona kama kuna weledi wa biashara kabla ya kuanza kuwafikiria mbeleni. Ingelikuwa mimi ndio serikari ningewata wafikie hata wateja milllion moja kwanza surely wanaweza wapata hao kupitia mijini ukijumlisha mikoa yote.
Ndiyo haya ya ATCL miaka nenda miaka rudi tuwe na ndege zetu, sijui tunaletewa ndege mbovu kila siku zinaharibika ndio maana sio reliable etc. Matokeo yake wameletewa ndege mpya tena model za kileo za kumwaga zimeishia kupaki kumbe tatizo alikuwa kukosekana kwa ndege tu bali na uwezo pia wa kufanya hiyo biashara.