TTCL yaomba Sh 1.7 trilioni kuboresha huduma zake

TTCL yaomba Sh 1.7 trilioni kuboresha huduma zake

Akili yetu Watz ni Mungu tu anayeijua!
Wakati washindani wao akina Voda, Tigo nk wanaitafuta hiyo pesa usiku na mchana kutoka kwa wateja wao TTCL wanaomba kwa serikali ambapo hizo pesa ni kodi za washindani wao. Lakini kwenye gawio hawaiombi serikali "kuwapa pesa ya kutoa gawio kwa serikali"!

Inafurahisha sana...
 
Sasa kama kulikuwa na viongozi wa serikali waliofanya juu chini kuiua TTCL ili makampuni ya nje waliyoyaleta yafanikiwe, unategemea itashindana vipi?
Vizuri, hao viongozi ni akina nani na unaamini hivi tunavyoongea hawapo tena kwenye mfumo wa maamuzi!?
Pia siamini kama uchumi wa soko unaipa nafasi kampuni inayobebwa kupenya kirahisi maana washindani nao wanajua jinsi ya kwenda na mazingira. Hoja hapa ni kwa njia gani tunazozitumia ili kampuni yetu iweze kuhimili vishindo mkuu lakini kwa hizi ruzuku daima zinaishia mifukoni mwa mafisi.
 
Huyu Omary Nundu bado yupoga tu, ma CCM bwana hawawezi maisha tofauti na kujipachika kwenye taasisi za serikali na kuiba iba.

TZS 1.7 Trillion kwa ajiri ya kuboresha huduma za simu za mezani. Nani anatumia simu za mezani siku hizi? Yaani tutumie 1.7 Trillion kwenye obsolete life style? ndio ma strategists wa TTCL hawa?

Mi nilidhani wanaomba hela kwa ajiri ya 5G Technology?

= ajili

Mbona unaipenda sana "ajiri" au unataka kuajiri? Au unatafuta ajira?
 
TTCL Bwana sijajua kama kuna wahasibu wenye CPA

Tunahitaji buniness oriented mind na sio 'makada' kwenye hizi ofisi kuweza kushindana na TiGO, Voda ama Airtel, bahati mbaya kwenye karne hii ya kasi ya mawasiliano bado taasisi ambayo ingeweza kuwa monopoly kwenye hii sekta inasubiri huruma ya serikali.

Nahisi tunatatizo pahala na sio kwa sababu ya kuwa au kutokuwa na CPA.
 
Hoja hapa ni kwa njia gani tunazozitumia ili kampuni yetu iweze kuhimili vishindo mkuu lakini kwa hizi ruzuku daima zinaishia mifukoni mwa mafisi.
Huoni kuwa uongozi mpya chini ya Omary Nundu TTCL inafanya vizuri na ikiweza kuweka minara nchi nzima itaweza kuhimili vishindo vya akina vodacom?
 
TTCL yaomba Sh1.7 trilioni kuboresha huduma zake


pic+ttcl.jpg


Dar es Salaam. Mwenyekiti wa bodi ya Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Omary Nundu amesema shirika hilo linahitaji Sh1.77trilioni kuboresha huduma zake za simu za mkononi na mezani.

Nundu ametoa kauli hiyo leo Jumanne Mei 21, 2019 katika hafla ya shirika hilo kutoa gawio la shilingi 2.1bilioni kwa Serikali iliyokwenda sambamba na uzinduzi wa awamu ya pili ya huduma ya video conference.

Source: Mwananchi

Ukitaka vichekesho zaidi bonyeza *nyumbanikumenoga# then piga.

Tunasubiri gawio la ATCL ili tucheke zaidi.
Kwani hawa ttcl wanataka trillioni 1.7 wanataka kulunch satelite yao huko angani au maana sijaelewa bado..

Kama ni kwa ajili ya satelite swa serikali iwatafutie hiyo hela ila kama ni tofauti watafute wenyewe..
 
TTCL yaomba Sh1.7 trilioni kuboresha huduma zake


pic+ttcl.jpg


Dar es Salaam. Mwenyekiti wa bodi ya Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Omary Nundu amesema shirika hilo linahitaji Sh1.77trilioni kuboresha huduma zake za simu za mkononi na mezani.

Nundu ametoa kauli hiyo leo Jumanne Mei 21, 2019 katika hafla ya shirika hilo kutoa gawio la shilingi 2.1bilioni kwa Serikali iliyokwenda sambamba na uzinduzi wa awamu ya pili ya huduma ya video conference.

Source: Mwananchi

Ukitaka vichekesho zaidi bonyeza *nyumbanikumenoga# then piga.

Tunasubiri gawio la ATCL ili tucheke zaidi.
Tusipoteze pesa zetu kwa hilo shirika linaloendeshwa kisiasa,tunataka tuumie mara ngapi?
Pesa inayoombwa ni ya walipa kodi,bila kodi zetu hakuna shirika hilo.Kama tuna nia njema tuliuze kwa wananchi wawe na hisa za kutosha.Lakini mambo ya kuamuka unatengua unateu bila kuangalia athali ya uchumi wa shirika.Hatujajitawala leo,tunazo akili za kutosha.
 
wanahitaji hicho kiasi cha pesa kutoka kwa nani tena wakati huu ni mwaka wa pili mfululizo wao kuigawia serekali yetu pendwa?
Hapo kuna tatizo unaomba
Sh 1.7 trilioni halafu unatowa gawio la shilingi 2.1bilioni
 
Back
Top Bottom