TTCL imesababisha nifukuzwe Kazi

TTCL imesababisha nifukuzwe Kazi

hp4510

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2012
Posts
8,916
Reaction score
9,727
Mimi Nilikuwa ni system adm wa kampun moja ya wazungu hapo Masaki, sasa jana bosi wangu alikuwa na mkutano wa online na mkurugenzi mkuu ambae yupo Marekani.

Kutokana na umuhimu wa hayo maongezi yao ikabidi bosi wangu aniombe ushauri kuhusu ni mtandao gani ambao una strong internet connection.

Kutokana na matangazo ya TTCL ya siku hizi, nikaona hawa jamaa watakuwa wamebadilika sana, kumbe Dah Nilikuwa naingia choo cha kike, nikamshauri bosi wangu kwa mbwembwe nyingi kuwa TTCL ni best kampany.. mmh nikapewa pesa za kwenda kununua line ya TTCL, nikaenda moja kwa moja makao makuu pale Samora, kufika pale nikanunua line kwa sh 2000 na muda wa maongezi....

Huwezi kuamini ishu ya kusajili line tu ilinichukua masaa 3 mpaka bosi akawa ananipigia simu kwamba vipi tena mbona unachelewa?

Ikabidi niondoke kurudi ofisini na yule mhudumu akaniambia niweke line kwenye simu na itafunguka tu yenyewe, nikafika ofisini nikampatia bosi wangu ile line na nikampa maelezo kuwa aweke kwenye simu na itafunguka tu yenyewe....

Dah mpaka saa 12 jioni hakuna kitu, bahati nzuri nilichukua namba ya yule dada alienihudumia nikampigia simu, jibu lake ndio niliishiwa pozi zote...

Akasema kesho asubuhi niende na hiyo line oh my god bosi akaanza kubadilika rangi akaanza kupiga simu kwa wazungu wenzake na kila mzungu akawa anatoa lawama kwangu kuwa why nilichagua TTCL ikiwa wenyewe tu wafanyakazi wa TTCL hawatumii huo mtandao....

So kwa hasira bosi kanifukuza kazi coz nimempa ushauri wa kampuni ambayo Nilikuwa najua fika kuwa huduma zake ni mbovu.

Ushauri wangu kwa TTCL ni kwamba fungeni hiyo kampuni yenu mpaka hapo ambapo mtakuwa tayari kuingia kwenye soko la ushindani.

=======
MAJIBU TOKA TTCL:
Ndugu hp4510

Kampuni ya Simu Tanzania(TTCL) inaomba radhi kwa matatizo na usumbufu uliotokea.

Maoni yako ni muhimu kwetu na yametupa changamoto ya kuendelea kuboresha zaidi huduma zetu na kuchukua hatua stahiki kwa wafanyakazi wetu.

Tafadhali kwa mawasiliano zaidi, wasiliana nasi kupitia customercare@ttcl.co.tz au unaweza kupiga namba 100 (Kwa kutumia laini ya TTCL) au 0222 100 100 (kwa kutumia mitandao mingine) ili tuweze kushauriana zaidi.

Pia unaweza kutembelea Kituo chetu cha huduma kwa wateja kilichopo Posta, Mtaa wa Samora ili uweze kuonana na Meneja wa TTCL mkoa wa DSM kati, Ndugu Diwani Mwamengo kwa kushauriana zaidi, Ndugu Diwani anapatikana kwa simu namba 0732 100 008.

Imetolewa na Ofisi ya Uhusiano
18/08/2016
 
Duh pole sana, nenda TTCL na barua yako ya kufukuzwa kazi wambie
1. Wakulipe fidia ya kukupa taarifa za uongo ambazo umeziamini na matokeo yake kusababishwa kufukuzwa kazi?
2. Rudi kwa Mwajiri wako mwambie sababu za kufukuzwa kwako kazi hazina uhusiano wa moja kwa moja bali umesha wachukulia hatua/wachonganishi ambao ni TTCL.
3. Washauri TTCL wabadili hata rangi za Logo na Tshirts zenye rangi nyeusi vijana wa Promo wanaonekana wamechoka sana pia haina mvuto kivile.
4. Tumia changamoto ya kufukuzwa kwako kazi kwa kuanzisha Kampuni ya kuandaa Mikutano/Kusimamia maandalizi na kuwezesha mikutano online Bongo
 
Kampuni yoyote ya maana huwa ina stable internet provider sio kununua line kama mtu anayetaka kuweka kwenye laptop home.Mkuu hukutumia vizuri uwezo wako katika kushauri na kusaidia kampuni kwenye mambo muhimu kama internet connection & proper subscriber.Pole sana
 
pole mkuu ila ni kwel umefukuzwa kaz aisee?
 
Bossi wako amefanya sahihi kukufukuza. Kama kweli wewe ni system admin na mshauri wa teknolojia siku zote unamshauri mtu based on what has worked better on your experience. Ulitakiwa uwe ushatumia huo mtandao kabla ya kurecommend. Research research research and always be on top of issues .
Take it positive itakusaidia kuwa makini siku za usoni.
 
Back
Top Bottom