TTCL fiber ingebinafsishwa ingeipiku ZUKU fiber kwa wateja

Tomaa Mireni

JF-Expert Member
Sep 8, 2015
2,330
2,283
Kama ilivyo kwa taasisi za serikali kwa uzembe TTCL nao wamo. Nilienda 7SABA maonyesho nikakutana na maafisa nikakaribishwa vizuri na kutanfaziwa faiba mlangoni, nikaipenda. Nikaulizia taratibu nikaambiwa unajaza fomu anakuja savea na kuangalia eneo kisha unaletewa huduma. Nikauliza inaweza kuchukua muda gani mpaka kufungiwa? Akajibu ndani ya wiki moja tu.

Akachukua taarifa zangu, nikafika nyumbani nikajaza ombi online. Nikasubiri wiki ya kwanza hola, ya pili hola, nikaenda makao yao posta nikajibiwa ombi limepokelewa kanda yako. Nikaelekezwa niende huko.

Nikakaa tena wk 2 nyingine ndio nikaenda mpaka Nyerere rd karibu na kiwanda cha sigara nikauliza kuhusu ombi langu. Nikaambiwa kweli ila "NITAFIKIWA TU" foleni kubwa kidogo afu pia kuna changamoto ya vifaa kwa hiyo niwe mvumilivu.

Toka mwezi wa saba muda muda huu naandika hata simu sijawahi kupigiwa miezi minne, kweli wako serious na kazi kweli?

Nikakimbilia voda supakasi siku 4 tu mzigo ninao mkononi. Kuna jamaa nae alituma maombi amehangaika mwishowe kakimbilia airtel.

Kwa sasa zuku fiber ndio habari ya mjini kwa waoishi ushuani na maeneo yenye watu wengi, kama Ttcl ingekuwa makini na malengo ingekuwa kwa haraka sana sababu Ttcl kwa mwezi ni 55000 tu unafungiwa wakati zuku ni 75000.
 
Scars aje kukupa somo hivi ulisema TTCL mpk waje ni lazima sura yako ifanane na kigogo mmoja wa serikalini
Namshangaa kasubiria wiki mbili tu anakata tamaa

Wenzake tulianza hadi kuzoeleka na wafanyakazi wa pale ofisini.

Yani ilifika muda ukiingia tu ofisini wanaanza "aaah Scars naona leo umetokea kwani Eliya hakukucheki kukupa feedback"

Kwa wale wateja waliokuwa wanaanza kuja kujaza fomu walikuwa wakinikuta wanajua na mimi ni mfanyakazi wa TTCL.

Sasa mwamba kaanza zoezi season ya Nyerere day kafuatilia wiki mbili tayari katupa taulo.

Watu tumetumia kila aina ya mbinu ambayo tuliona inaweza kusaidia, tumefikia hatua ya kutuma email za malalamiko hadi kwa wakurugenzi huko wenye vitengo vya juu lakini chafu... wajinga wamezidi kukaza.
 
Kama ilivyo kwa taasisi za serikali kwa uzembe TTCL nao wamo. Nilienda 7SABA maonyesho nikakutana na maafisa nikakaribishwa vizuri na kutanfaziwa faiba mlangoni, nikaipenda. Nikaulizia taratibu nikaambiwa unajaza fomu anakuja savea na kuangalia eneo kisha unaletewa huduma. Nikauliza inaweza kuchukua muda gani mpaka kufungiwa? Akajibu ndani ya wiki moja tu.

Akachukua taarifa zangu, nikafika nyumbani nikajaza ombi online. Nikasubiri wiki ya kwanza hola, ya pili hola, nikaenda makao yao posta nikajibiwa ombi limepokelewa kanda yako. Nikaelekezwa niende huko.

Nikakaa tena wk 2 nyingine ndio nikaenda mpaka Nyerere rd karibu na kiwanda cha sigara nikauliza kuhusu ombi langu. Nikaambiwa kweli ila "NITAFIKIWA TU" foleni kubwa kidogo afu pia kuna changamoto ya vifaa kwa hiyo niwe mvumilivu.

Toka mwezi wa saba muda muda huu naandika hata simu sijawahi kupigiwa miezi minne, kweli wako serious na kazi kweli?

Nikakimbilia voda supakasi siku 4 tu mzigo ninao mkononi. Kuna jamaa nae alituma maombi amehangaika mwishowe kakimbilia airtel.

Kwa sasa zuku fiber ndio habari ya mjini kwa waoishi ushuani na maeneo yenye watu wengi, kama Ttcl ingekuwa makini na malengo ingekuwa kwa haraka sana sababu Ttcl kwa mwezi ni 55000 tu unafungiwa wakati zuku ni 75000.
Samia atakuambia ''tumeshindwa, hatuwezi bila wawekezaji''. Nakuapia ni uongozi mbovu wa CCM umeshindwa na siyo watanzania wote. Unawaweka watu kama kina Mwingulu na Makonda kwenye uongozi halafu utegemee ufanisi? Mini hili la kubinafsisha kila kitu huwa nalipinga kabisa. Kuna nchi nyingi tu nazijua serikali zina mashirika yanayofanya vizuri sana. Hivi kama Internet ilivyo bidhaa hot sasa hivi utakosa wateja? Halafu hawa wenye makampuni ya watu binafsi huwa wanahonga ili vitu vya serikali vife na vya kwao viendelee.
 
Samia atakuambia ''tumeshindwa, hatuwezi bila wawekezaji''. Nakuapia ni uongozi mbovu wa CCM umeshindwa na siyo watanzania wote. Unawaweka watu kama kina Mwingulu na Makonda kwenye uongozi halafu utegemee ufanisi? Mini hili la kubinafsisha kila kitu huwa nalipinga kabisa. Kuna nchi nyingi tu nazijua serikali zina mashirika yanayofanya vizuri sana. Hivi kama Internet ilivyo bidhaa hot sasa hivi utakosa wateja? Halafu hawa wenye makampuni ya watu binafsi huwa wanahonga ili vitu vya serikali vife na vya kwao viendelee.
Hata mm ndio nachojua, taasisi za serikali zikifanya vizuri za kibinafsi zinaweza kuanguka sababu ya gharama. Uzembe mwingine uko pale Posta, nina parcel ina miezi miwili sasa sijapigiwa simu, lakini kampuni ya speedaf siku 10 tu mzigo mkononi, hi unafikiri utachagua wapi?
 
Nilijaza fomu ttcl mwanzo wa mwaka huu mpaka leo sijawahi kuwaona

Kila nikienda naambiwa atakuja saveya
Hili shirika hakuna kazi wanafanya zaidi ya kututia hasara.
 
Back
Top Bottom