Tsvangirai hoi kwa Mugabe

Tsvangirai hoi kwa Mugabe

CURRENT ISSUE

JF-Expert Member
Joined
Jun 20, 2013
Posts
256
Reaction score
57
Dalili zote zinaonyesha kuwa waziri mkuu wa Zimbabwe yatamkuta yaliyomkuta Raila wa Kenya.Maeneo mengi aliyokuwa na wabunge sasa yamechukuliwa na chama tawala cha rais Mugabe.Wananchi walijitokeza kwa wingi sana kuchagua kiongozi wampendaye,na kwa matokeo ya ubunge yanavyoonyesha,kwa upande wa rais watampa Mugabe na ndio maana Tsvangirai ameanza kutoa shutuma mbalimbali.Hivyo kwa matokeo haya Watanzania tunapaswa kujifunza kwa wenzetu.Tusikurupuke kuchagua tu,tufanye tathmini ya nani anafaa kuwa kiongozi wa taifa letu.Uchaguzi wa 2014 utusaidie kufanya hilo,tusiruhusu kujifunza kwa njia ngumu kama waliyotumia Zimbabwe.Wamejifunza hivi walivyofanya baada ya umwagaji wa damu mwaka 2008,hivyo hivyo na Kenya.Chonde chonde watz tusiingie kwenye hali hiyo,tufanye maandalizi mapema ili kuepusha vurugu,tuwape walio shikilia mpini tayari.
 
Jione ulivyo na ujinga..Tofauti na Tanzania Mugabe ni mtetezi wa wananchi wake dhidi ya dhuluma za mabeberu na pia anapinga ufisadi..Wewe unashauri nini?? peleka hizi hoja zako kwenye familia yenu na usituletee upuuzi hapa..Mugabe ni mtetezi wa rasilimali za watu na sio muabudu mabwana wa MAGHARIBI kama walivyo CCM..

Eti "tuwape walioshikilia mpini tayari" shame on you!!.
 
Jione ulivyo na ujinga..Tofauti na Tanzania Mugabe ni mtetezi wa wananchi wake dhidi ya dhuluma za mabeberu na pia anapinga ufisadi..Wewe unashauri nini?? peleka hizi hoja zako kwenye familia yenu na usituletee upuuzi hapa..Mugabe ni mtetezi wa rasilimali za watu na sio muabudu mabwana wa MAGHARIBI kama walivyo CCM..

Eti "tuwape walioshikilia mpini tayari" shame on you!!.
Kwa Zimbabwe jifunzeni,na wala sio Zimbabwe tu hata hapa Kenya kwa majirani zetu.Fikiria kidogo aje mwanao wa kumzaa aanze kungangania kuingia chumbani kwa baba,utamkubalia???Kama huwezi kubali basi jua na wengine ndio hivyo hawawezi kukubali kiulaini hivyo.Cha kufanya kuepusha shari mpishe.
 
Jione ulivyo na
ujinga..Tofauti na Tanzania Mugabe ni mtetezi wa wananchi wake dhidi ya
dhuluma za mabeberu na pia anapinga ufisadi..Wewe unashauri nini??
peleka hizi hoja zako kwenye familia yenu na usituletee upuuzi
hapa..Mugabe ni mtetezi wa rasilimali za watu na sio muabudu mabwana wa
MAGHARIBI kama walivyo CCM..

Eti "tuwape walioshikilia mpini tayari" shame on you!!.

acha unafiki wewe. tangia lini chadema wakamsupport mugabe? huko ni kutapatapa baada ya kushindwa. juzi mlimsifia sana Tsvangirai na kumwona ni mpambanaji mzuri. leo kaangushwa na babu tena vibaya sana mnamwona babu ndo shujaa. hayo mlifanya pia kwa odinga. kabla ya uchaguzi mlimpamba sana. aliposhindwa mkamkana. kweli dhambi ya usaliti inawatafuna chadema kama Mwampamba alivyobainisha
 
Watanzania tutaenda katika vituo vya kupigia kura tukiweka matatizo yetu mbele,Mambo ya Kenya na Zimbabwe sisi hayatuhusu.Kenya na Zimbabwe zina matatizo yanayofanana ya Ukabila na hata kura zao hupigwa kwa kuangalia ukabila zaidi kuliko kitu kingine.Kenya kuna Wakikuyu/Wakalenjin kwa upande mmoja dhidi ya Waluo kwa upande mwingine.Zimbabwe kuna Shona vs Ndebele.Tsvangirai na Mugabe wanatoka miongoni mwa haya makabila hasimu.Lakini hapa Tanzania hali ni tofauti hatumchugui Rais kwa ukabila wake bali kwa sifa zinginezo.Tanzania hatuna Kabila ambalo linaamini lina hakimiliki ya kutawala Nchi kwamba Nchi ikiongozwa na Rais toka Kabila lingine eti Kabila lililoko madarakani litapoteza kila kitu,Hapana sisi hatupo hivyo kabisa.
 
Kwa Zimbabwe
jifunzeni,na wala sio Zimbabwe tu hata hapa Kenya kwa majirani
zetu.Fikiria kidogo aje mwanao wa kumzaa aanze kungangania kuingia
chumbani kwa baba,utamkubalia???Kama huwezi kubali basi jua na wengine
ndio hivyo hawawezi kukubali kiulaini hivyo.Cha kufanya kuepusha shari
mpishe.

mkuu, vyama vingi vya upinzani barani afrika havikubaliki na wananchi kutokana na jinsi vinavyojipambanua na unafiki wa viongozi wake. pia kitendo cha baadhi ya watu kutoruhusu ushindani ndani ya vyama hivyo ni tatizo. chukulia hapa kwetu. kuna watu wazuri ndani ya chadema zaidi ya mbowe na slaa ila hawapewi nafasi. haiingii akilini uchaguzi wa ndani wa chama unafutwa simply kuna mtu anahofu kuwa atashindwa kwenye uchaguzi.

pia viongozi wa vyama vya upinzani wengi wao si waadilifu. mathalan, mtu anajinasibisha kuwa anapambana na ufisadi ilhali yeye mwenyewe ni fisadi
 
Et tuwape walioshikilia mpini tayari!
Peleka huko shat lako la yllw na grn.
ucdhan bado watz 2mell.
 
Mtabadili sana ID mwaka huu, eti mtoa mada nae ni mtu mzima aliyekaa chini na kuwaza nn cha kuandika,
 
Kwa Zimbabwe jifunzeni,na wala sio Zimbabwe tu hata hapa Kenya kwa majirani zetu.Fikiria kidogo aje mwanao wa kumzaa aanze kungangania kuingia chumbani kwa baba,utamkubalia???Kama huwezi kubali basi jua na wengine ndio hivyo hawawezi kukubali kiulaini hivyo.Cha kufanya kuepusha shari mpishe.

Kwa akili yako fupi unajifanya unawasilisha mawazo ya wazimbabwe! Unadhani hiyo zimbabwe ni ile ya Mulongo?
 
Dalili zote zinaonyesha kuwa waziri mkuu wa Zimbabwe yatamkuta yaliyomkuta Raila wa Kenya.Maeneo mengi aliyokuwa na wabunge sasa yamechukuliwa na chama tawala cha rais Mugabe.Wananchi walijitokeza kwa wingi sana kuchagua kiongozi wampendaye,na kwa matokeo ya ubunge yanavyoonyesha,kwa upande wa rais watampa Mugabe na ndio maana Tsvangirai ameanza kutoa shutuma mbalimbali.Hivyo kwa matokeo haya Watanzania tunapaswa kujifunza kwa wenzetu.Tusikurupuke kuchagua tu,tufanye tathmini ya nani anafaa kuwa kiongozi wa taifa letu.Uchaguzi wa 2014 utusaidie kufanya hilo,tusiruhusu kujifunza kwa njia ngumu kama waliyotumia Zimbabwe.Wamejifunza hivi walivyofanya baada ya umwagaji wa damu mwaka 2008,hivyo hivyo na Kenya.Chonde chonde watz tusiingie kwenye hali hiyo,tufanye maandalizi mapema ili kuepusha vurugu,tuwape walio shikilia mpini tayari.

Inaonekana hata uwezo wako wa kufuatilia mambo ya siasa ni mdogo kama unashindwa kujua uchaguzi wetu ni 2015 iweje ulete topic hapa ambayo aina mashiko na ambayo aina mtizamo? Kajipange tena na ccm yako.
 
Tsangarai alipopewa uwaziri mkuu alienda UK akawaambia wazimbabwe a.k.a wazimwi walioahamia UK kuwa they must come back home kwa sababu sasa mambo ni mazuri. Jamaa walimzomea live mpaka mkutano ukavunjika. Yaani Tsangarai yeye kupata uwaziri mkuu ndio anaona kwamba maisha sasa yamekuwa mazuri!

Hawa ndio wanasiasa wetu. Hivi sasa anaanza kulalamikia uchaguzi ili apewe kinafasi kingine cha uongozi serikalini kimvutevute kimaisha.

Hata Tanzania wapo wagombea ambao wanajifanya hawamtambui Rais ili wabembelezwe kwa kupewa power sharing deal. Lakini bahati nzuri hawakufanikiwa. Hata hivyo tujiandae kuwa huko mbele watarudia tena tabia yao ya kukataa maamuzi ya wapiga kura.

Msikilize hapa anavyozomewa kwa kauli yake ya kibinafsi Tsvangirai in london cathedral 20 june 2009 - YouTube

Hata Dr. Slaa baada ya kufahamika kuwa ni fisadi na mbinafsi mwenye uroho watu wengi wameacha kumuamini. Tsangarai watu walimuamini sana wakamuona ndio tumaini la Zimbabwe, lakini alivyoonja shavu tu kawaangusha. Matokeo yake ndio kama uchaguzi unavyoonyesha...
 
Jione ulivyo na ujinga..Tofauti na Tanzania Mugabe ni mtetezi wa wananchi wake dhidi ya dhuluma za mabeberu na pia anapinga ufisadi..Wewe unashauri nini?? peleka hizi hoja zako kwenye familia yenu na usituletee upuuzi hapa..Mugabe ni mtetezi wa rasilimali za watu na sio muabudu mabwana wa MAGHARIBI kama walivyo CCM..

Eti "tuwape walioshikilia mpini tayari" shame on you!!.

Hivi baso wananchi wake wanakwenda na laki tano kununua nyanya na mboga sokoni?
 
Wapiga kura zaidi ya milioni maeneo ya mjini hawakuruhusiwa kupiga kura,.unategemea nini. Mke wa Mugabe alitangulia kusema kuwa wamepanga ikulu milele na hakuna wa kuwaondoa. Kupanga ikulu milele maana yake ninii? Ni kwamba hata kwa wizi au mtutu ni lazima washinde. Sasa fair play iko wapi? Huyu Mugabe hadi afie ofisini kwa kuogopa kushtakiwa. Lakini ni funzo kwa upinzani. Kila mtu anataka madaraka. Hapakuwa na sababu ya chama cha Waziri Mkuu kugawanyika. Watu wakumbuke umoja ni nguvu na upinzani unavyozidi kugawanyika ndiyo furaha ya chama tawala.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
By WISE BOY
Mtabadili sana ID mwaka huu, eti mtoa mada nae ni mtu mzima aliyekaa chini na kuwaza nn cha kuandika,
Ila si hali halisi,acha kujidai hujui yanayoendelea Zimbabwe.

Mugabe ni mtetezi wa wanyonge;Alinyang'anya ardhi wazungu na kuwapa maskini LKN CCM hii inakumbatia matajiri na wauza madawa ya kulevya!

Itikadi ya Jongwe zinaendana sambamba na za CHADEMA
 
Jione ulivyo na ujinga..Tofauti na Tanzania Mugabe ni mtetezi wa wananchi wake dhidi ya dhuluma za mabeberu na pia anapinga ufisadi..Wewe unashauri nini?? peleka hizi hoja zako kwenye familia yenu na usituletee upuuzi hapa..Mugabe ni mtetezi wa rasilimali za watu na sio muabudu mabwana wa MAGHARIBI kama walivyo CCM..

Eti "tuwape walioshikilia mpini tayari" shame on you!!.

Umesema Mugabe anachukia ufisadi?

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Zimbabwe kwa afrika kwa elimu ndio inaongoza!!!
Mugabe degree alizo nazo amna raisi wa Afrika anaye mkuta so ni number nyingine na kwa umri pia yni ni company ya kina nyerere ndio maana wazimbabwe wana mheshim!!
Hana mambo ya magamba ata kidogo!!
 
Jione ulivyo na ujinga..Tofauti na Tanzania Mugabe ni mtetezi wa wananchi wake dhidi ya dhuluma za mabeberu na pia anapinga ufisadi..Wewe unashauri nini?? peleka hizi hoja zako kwenye familia yenu na usituletee upuuzi hapa..Mugabe ni mtetezi wa rasilimali za watu na sio muabudu mabwana wa MAGHARIBI kama walivyo CCM..

Eti "tuwape walioshikilia mpini tayari" shame on you!!.

unajitukana bila hata kujua hujui kuwa slaa ni kibaraka wa wajerumani na denmark au unakurupuka tu.
 
Back
Top Bottom