NILIONDOKA HOME, nikaenda kufanya kazi mkoa fulani hapa tz, nimekaa huko kwa muda mrefu. waifu anafanya kazi hapa dsm. ....nimeoa nina watoto. tatizo lilinitokea, nikiwa huko nilikutana na mwanamke mmoja, ni mrefu, mwembamba kidogo ila hips kubwa, ni mzuri ajabu, mamake ni mtutsi babake mchaga wa marangu, mara ya kwanza ilikuwa kama utani, tukaanza urafiki, tukaenda kupima, tukawa negative, tukaanza kutumia ndomu, nilikuwa nakaa lodge hivyo wiki mbili za mwanzo alikuwa anahudhuria kwenye lodge kila siku.
alihamia kabisa, na akaacha kazi, tukawa tunaishi wote kwenye lodge. sikujua ni kitu gani aliona kwangu, sijui nilimfanya vizuri sana ila toka siku ya kwanz anilimwambia mimi nimeoa mke wangu yuko dsm na ni mIkali sana na ana wivu, tukawa tunafanya tu.
kati ya miezi karibia sita au saba, tulikaa lodge tofautitofauti, ila tulikuwa tunakaa pamoja. kazi yangu ilikuwa ni ya kufanyia tu ndani ya lodge na kama kwenda ofisini ni kwenda naye pamoja na kuweka doc kwa bos na tunarudi wote, yeye hakutaka kuniacha hata mara moja akiogopa nitamtoroka, ati nitabadilisha lodge na kumkimbia. alinipenda akawa analia usiku machozi ati anatamani kama angekutana na mke wangu akubaliane naye amruhusu awe mke wa pili, atamheshimu sana mke wangu, akawa anajilaumu kwamba ni kwanini mimi niliwahi kuoa kabla sijakutana na yeye?
tukiwa sita kwa sita mara nyingi namuona anatoa mikelele kuwa kwanini nimewahi kabla sijakutana naye, manake angekuwa mke wangu. aling'angá nia kuniita mume na mimi nikawa nakata jina hilo. nilikuwa nashangaa, kwanini mwanamke mzuri hivi analia machozi na yuko serious, hatanii, kwamba anatamani angekuwa mke wangu hata wa pili haingekuwa shida kwake?....mimi ni mwanaume sina sura nzuri najijua, ni nunda mweusi....yeye ana weupe wa kichaga na umbo na sura ya kinyarwanda (mamake alikimbia ile genocide)....babake ni tajiri tu ana bar kibao mwanza pale.
SIKU MOJA TUKIWA TUMEKAA, akaniambia anatamani kama angebeba damu yangu, kwasababu anajua mimi sitamuoa kwani nampenda sana mke wangu kuliko yeye. nilimtisha kuwa mke wangu atakutoa roho ukijifanya kuning'ang'ania...mzuriiii,....nilikuwa makini kuhesabu tarehe siku za mimba na bleed yake,....nimejikuta nimetwika mimba tayari,...ana mimba ya miezi minne sasaivi,...ninahudumia mimba na yeye nampenda ile sitamuoa na nilishamwambia mkataba wetu ni mtoto tu, si yeye...amefurahi sana kubeba damu yangu tumboni mwake...sasaivi amehamia arusha anafanya kazi kule......napigiana naye simu kila siku kabla ya kufika home, ana akili sana, ni mwaminifu sana kati ya mademu niliowaikuwa nao.
najua niliteleza, nilimtenda waifu kosa kubwa...juzi waifu anasali kwa mwingira, aliniamsha saa kumi za usiku akasema ameonyeshwa na Mungu kwenye ndoto kuwa mimi nina mke mwingine, akaniambia yote niliyoyafanya...niliogopa, lakini wkasababu mimi ni mbabe kidogo nilimfokea kwanini ananivurugia usingizi na kwanini ananiambia hivyo, nikapotezea...lakini niliumia moyoni kwanini nilifanya vile...kumtelekeza mwanamke yule na mimba naona sio fresh, pamoja na kwamba anaweza kulea yeye mwenyewe, .......nitaanzaje kumwambia waifu kuwa nina mtoto nje?...waifu ananipenda sana na mimi nampenda kuliko wanawake wote duniani najua tutasameheana lakini pa kuanzia sijui....yule wa arusha na mimba yangu, nashukuru Mungu hatakinukisha.....