kilambasahani
Member
- Jan 23, 2014
- 28
- 3
Picha tafadhari!
Leo ni ajali ya pili hiyo maana asubuhi sana rav 4 imegonga garimoshi hilo kwenye makutano ya barabara ya kuelekea shekilango na ubungo maziwa.
Uzembe wa madereva ni upande mmoja.....
Kisheria treni haigongi....ila kuna taratibu wanapaswa kuzifuata ili kulinda watu na magari yanayovuka treni. Kama eneo lina magari mengi wanapaswa kuweka geti na taa za kizuia magari pindi treni inapokaribia.
hebu ficha up......vu wako! sitaki kuamini kuwa wewe ni kilaza kiasi hicho!Hekima ya namna gani ulitaka itumike?Angeepukaje kuigonga gari hiyo?kwa kutoka kwenye rail na kupita pembeni?au kwa kufunga breki za ghafla?unayajua madhara ya breki za ghafla kwa treni?Unajua ni muda gani na kwa umbali gani treni inaweza kusimamishwa na ikakubali kusimama?kabla hujaandika jaribu kukifahamu unachotaka kukiandika.
We dereva unaona kabisa kuna foleni alafu reli imekatisha na wewe unaenda kusimama kati kati ya reli utakuwa dereva makini kweli? Huu ndo uzembe huwezi simama kati kati ya reli na unaiona kabisa lazima uache gap
hebu ficha up......vu wako! sitaki kuamini kuwa wewe ni kilaza kiasi hicho!Hekima ya namna gani ulitaka itumike?Angeepukaje kuigonga gari hiyo?kwa kutoka kwenye rail na kupita pembeni?au kwa kufunga breki za ghafla?unayajua madhara ya breki za ghafla kwa treni?Unajua ni muda gani na kwa umbali gani treni inaweza kusimamishwa na ikakubali kusimama?kabla hujaandika jaribu kukifahamu unachotaka kukiandika.
Ni kituo cha mwananchi tabata.
Treni ameligonga kwa makusudi gari lilikuwa limekwama kutokana na traffic jam inayosababishwa na marori maeneo hayo ya relini.
Mara baada ya kuligonga gari ikiwa mwendo
mdogo kabisa lilirudi nyuma kuchukua abiria na kuendelea na safari.
Gari hiyo aina ya defender iliachwa nyanganyanga
NB
Tunasema treni imegonga gari kwa kuwa kila aliyekuwepo aliamini kwamba treni ingesimama au ilipaswa kusimama kwanza kuchukua abiria badala ya kuwapita abiria kwenda kugonga gari.
Aidha kila aliyeshuhudia aliona wazi kuwa kitendo hicho ni cha makusudi hasa ukizingatia treni ilikuwa mwendo mdogo na barabara inaonekana tokea mbali.
tuwe tunafwata taratibu na sheria zilizowekwa, na akili na busara pia.
watanzania tumekuwa na tatizo sugu la kutofwata sheria na taratibu za nchi. huo ulikuwa uzembe uliotokana na kutotaka kufwata sheria ya kutokaa katika reli.
sasa hv waenda kwa miguu wengi wamekuwa wakigongwa na magari kwa kutovuka katika sehemu maalumu za kuvukia waenda kwa miguu unakuta kila mtu kwa wakati wake sehemu yoyote ya barabara anachomoka na kuvuka barabara. hii inawaletea shida sana waendesha vyombo vya moto.
bodaboda wamekuwa wapita ovyoovyo tu akiona upenyo kakatiza na kusababisha ajali nyingi ambazo zingeepukika.
tujenge utamaduni wa kufwata sheria na taratibu za nchi. ndio maana tukienda nchi za wenzetu tunapata shida kwa sababu wenzetu wako vizuri katika kufwata sheria.
Ni kituo cha mwananchi tabata.
Treni ameligonga kwa makusudi gari lilikuwa limekwama kutokana na traffic jam inayosababishwa na marori maeneo hayo ya relini.
Mara baada ya kuligonga gari ikiwa mwendo
mdogo kabisa lilirudi nyuma kuchukua abiria na kuendelea na safari.
Gari hiyo aina ya defender iliachwa nyanganyanga
NB
Tunasema treni imegonga gari kwa kuwa kila aliyekuwepo aliamini kwamba treni ingesimama au ilipaswa kusimama kwanza kuchukua abiria badala ya kuwapita abiria kwenda kugonga gari.
Aidha kila aliyeshuhudia aliona wazi kuwa kitendo hicho ni cha makusudi hasa ukizingatia treni ilikuwa mwendo mdogo na barabara inaonekana tokea mbali.
Na hasa Kama aliona ubahili kulipiacomprehensive
insurance
Haswaaa...hili wengi hawalijui..na hasa wakujifunzia uchochoroniUdereva wa kujihami ni udereva wa kutumia akili kaka
Mkuu mwendesha treni si tu alikua anamkomoa mwenye defender...alikua analitoa kwenye njia yake kisha ndo apakie abiria aendelee na safari...kwani mkuu mara ngapi tunasimama na magari yetu kutoa kizuizi(mwiba au jiwe) ili tupite vizuri?Eleweni hoja ya jamaa. Treni haina na urefu wa kufika barabarani inaposimama kuchukua abiria kituoni. Mwendesha treni amefanya makusudi, akakipita kituo ili akaligonge gari, baada ya kuligonga ina maana ameshapitiliza kituo chake, akalazimika kurudi nyuma ili awe usawa wa kituo chake achukue abiria, na hii inaonyesha alipitiliza makusudi. Kwa ufupi tusiishie kujadili sheria tu, tuangalie na nia ya muendesha treni