Treni Yagonga Gari Makusudi

Treni Yagonga Gari Makusudi

Goodrich

JF-Expert Member
Joined
Jan 29, 2012
Posts
2,091
Reaction score
1,179
Ni kituo cha mwananchi tabata.
Treni ameligonga kwa makusudi gari lilikuwa limekwama kutokana na traffic jam inayosababishwa na marori maeneo hayo ya relini.
Mara baada ya kuligonga gari ikiwa mwendo
mdogo kabisa lilirudi nyuma kuchukua abiria na kuendelea na safari.
Gari hiyo aina ya defender iliachwa nyanganyanga

NB
Tunasema treni imegonga gari kwa kuwa kila aliyekuwepo aliamini kwamba treni ingesimama au ilipaswa kusimama kwanza kuchukua abiria badala ya kuwapita abiria kwenda kugonga gari.

Aidha kila aliyeshuhudia aliona wazi kuwa kitendo hicho ni cha makusudi hasa ukizingatia treni ilikuwa mwendo mdogo na barabara inaonekana tokea mbali.
 
dereva wa difenda ni mjinga. yeye ndio kagonga treni. foleni aliiona kwanini alisimamisha gari juu ya reli.
 
Kisheria hakupaswa kukaa katikati ya reli, sababu ya kwamba kulikua na traffic jam haina mashiko. Kwa ufupi imekula kwake
 
Kwa sheria za nchi hii hapo sio treni imegonga gari bali ni gari limegonga treni,labda ungesema yule (hivi muongoza treni anaitwa nani?) angepunguza mwendo na kumsubiri mwenye gari atoe hilo gari lake.Ila kisheria hapo treni iko sawa
 
gari imegonga treni makusudi kwa nini akae kwenye barabara ye train
 
yaani huyo atafidia mafuta ya treni Dar Mwanza
 
Kama treni ingetoka kwenye reli ikaigonga hiyo defender basi title ya thread ipo sahihi, otherwise vice-versa is true.
 
Huyu dereva wa hiyo treni ni mataakoo sana.....
Hata kama uko sawa kisheria, haimaanishi ugonge wakati unaweza kuepuka!!!
Busara zikitumika ipasavyo kuna mambo mengine wala hayahitaji sheria...

Kisheria hakupaswa kukaa katikati ya reli, sababu ya kwamba kulikua na traffic jam haina mashiko. Kwa ufupi imekula kwake
 
Kama treni ingetoka kwenye reli ikaigonga hiyo defender basi title ya thread ipo sahihi, otherwise vice-versa is true.

Hata mimi nimefungua haraka treni ilitoka kwenye reli. Uderva wa mazoea ni hatari. Je trafiki wamepima? Huyo dereva wa defenda anayo kesi ya kujibu. Makosa yake ni 1. Kendesha bila ya kuchukua tahadhari i.e alama za barabarani; 2. Kusimama kwenye njia ya reli kwa minajili ya kuizuia; 3. Kusababisha ajali; 4. Kusababisha usumbufu kwa watumiaji wengine wa barabara; kama alikimbia - 5. Kukimbia baada ya kusababisha ajali (ikiwa kama hakukuwa na ulazima kadiri ya mazingira ya ajali i.e kuokoa maisha yake); 6. ......
Kwa bahati mbaya kwa sasa sitoweza kuweka bayana vifungu vya sheria. Pole yake: bima itamkana, na anaweza kunyea ndoo. Sijui mtasema shetani ndiye aliyesababisha!
 
Hata mimi nimefungua haraka treni ilitoka kwenye reli. Uderva wa mazoea ni hatari. Je trafiki wamepima? Huyo dereva wa defenda anayo kesi ya kujibu. Makosa yake ni 1. Kendesha bila ya kuchukua tahadhari; 2. Kusimama kwenye njia ya reli kwa minajili ya kuizuia; 3. Kusababisha ajali; 4. Kusababisha usumbufu kwa watumiaji wengine wa barabara.
Kwa bahati mbaya kwa sasa sitoweza kuweka bayana vifungu vya sheria. Pole yake: bima itamkana, na anaweza kunyea ndoo. Sijui mtasema shetani ndiye aliyesababisha!

Duh kumbe iko hivi
 
tuwe tunafwata taratibu na sheria zilizowekwa, na akili na busara pia.
watanzania tumekuwa na tatizo sugu la kutofwata sheria na taratibu za nchi. huo ulikuwa uzembe uliotokana na kutotaka kufwata sheria ya kutokaa katika reli.
sasa hv waenda kwa miguu wengi wamekuwa wakigongwa na magari kwa kutovuka katika sehemu maalumu za kuvukia waenda kwa miguu unakuta kila mtu kwa wakati wake sehemu yoyote ya barabara anachomoka na kuvuka barabara. hii inawaletea shida sana waendesha vyombo vya moto.
bodaboda wamekuwa wapita ovyoovyo tu akiona upenyo kakatiza na kusababisha ajali nyingi ambazo zingeepukika.

tujenge utamaduni wa kufwata sheria na taratibu za nchi. ndio maana tukienda nchi za wenzetu tunapata shida kwa sababu wenzetu wako vizuri katika kufwata sheria.
 
Huyo dereva wa treni anapaswa kupigwa kipapai.
Ingekua ni msafara wa wakuu au Obama angegonga?
 
Huyo driver MPUUZI! Hao ndio waendesha magari wasiozingatia sheria au kutozijua kabisaaaa! Umaona foleni haiendi, bado unasogeza gari relini!!! Nadhani alifikiri anakatiza "Machinga Complex".
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom