TRA ‘watibua nyongo’ za Wanzanzibari

Wowwww

Kama interpretation yako ya kipengele hicho unaiweka ZNZ sawa na nchi ya kigeni huo ni uamuzi wako wewe haimaanishi TRA wanafanya hivyo na inaonyesha umepoteza wakati wako mwingi sana kuitafuta hiyo na ukaona ndiyo punching line.lakini kosa ni kutokuijua katiba yako inasemeje na ikakupelekea kusherehesha kipengele hicho kutoka na ufahamu wako mdogo au just umeeamuwa hivyo ili kufikia lengo lako ulilokusudia.Lakini nenda TRA kaulize ni ukitoa mzigo zanzibar kuuleta bongo unatozwa 18% kwani hata hao wanaolalamika bandarini wanahangaishwa na maofisa wa TRA basi hiyo pesa wanayoichukua basi ni asilimia ndogo sana na hata risiti unakuwa hupewi.sijui kama uko TZ au Nje lakini kwanza nenda bandarini jaribu kuuliza utapata ukweli halisi au nenda Ofisi za TRA kaulizie.
PS: Pengine kwenye ndoto yako tu zanzibar itakuwa mkoa lakini in real world kitu hicho hakitotokea

Kama uelewa wako ndio huu basi sina cha kukusaidia. Hapa nimekuwekea pdf kutoka kwenye website ya TRA lakini wewe unaniambia niende bandarini au ofisi za TRA nikaulizie. Hii pdf imetayarishwa na hao hao TRA kutuondelea wewe na mimi usumbufu wa kuwafuata kuwauliza kuhusu masuala kama haya. Katika kifungu cha VAT, TRA wameeleza bayana kuwa bidhaa yeyote itakayoingia kutoka nje ya Tanzania BARA itatozwa kiasi hicho cha kodi. Kama bidhaa kutoka Zanzibar zisingehusika wangesema bidhaa yeyote itakayoingia katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itatozwa kiasi hicho cha VAT. Kwa kukazania kuwa mizigo kutoka Zanzibar isamehewa chini ya sheria hii ni sawa na kusema kuwa Zanzibar iko ndani ya Tanzania BARA. Kama afisa wa TRA anamhangaisha mtu na anakataa kutoa risiti kwa pesa anayopewa huyo ni wa kumpeleka kwa Pilato akashikishwe adabu. Lakini kama umemkatia kitu kidogo ili asikutoze hiyo asilimia, sidhani kama utakuwa na ubavu wa kudai risiti ya rushwa au kumpeleka kwa Pilato.

Mimi binafsi wala sina haja ya Zanzibar kugeuzwa mkoa wa Tanzania Bara. Ninachosema ni kuwa kwa vile imejitangaza nchi kamili nje ya Tanzania BARA basi haya ni baadhi ya majukumu yake. Katiba inaingiaje hapa wakati ni Zanzibar wenyewe wanaodai kuwa katiba yao inasema kuwa wao ni nchi kamili yenye mipaka yake na sehemu ya mipaka hiyo ni kati yake na Tanzania Bara. Kwa mtaji huo, basi Zanzibar ni nchi ya kigeni kama Kenya na wengine. Kama ilivyo kwenye masuala ya mafuta, ndivyo ilivyo kwenye VAT.

Amandla.......
 
No consensus on status of Z`bar tourism sector


The guardian reporter
Zanzibar President Amani Abeid KarumeZanzibar President Amani Abeid Karume has said tourism is not a Union matter and the Zanzibar Business Council should stop faulting Tanzania's diplomatic missions over their perceived failure to promote tourist attractions found in the Isles.
ZBC members aired their misgivings to Karume, who also serves as the council's chairman, saying the missions have persistently ignored Zanzibar when executing drives aimed at "selling" the country's tourist attractions to the world.
In remarks at a ceremony here on Tuesday to bid him farewell, the outgoing Zanzibar President said: "Under the constitution, tourism is not a Union matter. Each side of the United Republic of Tanzania must therefore promote its respective tourist attractions independently in collaboration with diplomatic missions of its choice."
He added that Tanzanian embassies or high commissions that had taken the trouble of promoting Zanzibar's tourist attractions "have been doing us a favour".
"What is of greater importance and relevance is for our own institutions engaged in activities linked to the tourism industry to prepare and issue quality promotional documents for the diplomatic mission to use in selling the Isles as a tourist destination of merit," said Karume.
He also urged businesspeople from Zanzibar participating in international trade fairs to carry with them brochures and other documents meant to promote the Isles' tourism sector.
Mohammed Juma Abdallah of Safina Tours had earlier told the ZBC chairman, that Zanzibar tourism had stagnated, leading to a fall in foreign exchange earnings, "mainly because Tanzanian ambassadors abroad have not been promoting it".
He said Tanzania's Embassy in France has been doing a commendable job promoting Tanzania Mainland's tourist attractions, including the Ngorongoro and Serengeti national parks, supported by the Tanzania National Parks (TANAPA).
"I once attended a trade fair in France in which the Tanzanian diplomatic mission took part, but I did not see any Zanzibar tourist attractions advertised. This is a problem which calls for an urgent and lasting solution," noted Abdallah.
However, Foreign Affairs and International Cooperation deputy minister Seif Ali Iddi told this paper yesterday that it was the responsibility of every Tanzanian diplomatic mission to promote tourism for both the Mainland and Zanzibar.
He said Foreign Affairs and International Cooperation was a Union matter "and the ministry has the role and duty of serving the whole of the United Republic of Tanzania".
"Zanzibar has as much right as the Mainland of using our embassies, high commissions and consulates to promote its tourist attractions. This applies even if it is such that tourism is not a Union matter," said the deputy minister.
According to Zanzibar Tourism, Trade and Investment minister Samia Suluhu Hassan, it is illegal for foreigners to operate as tour guides in the Isles.
He said the Isles government would descend on foreigners using locals to set up companies offering tour guide services on their behalf.
 
..sasa kwenye suala la mafuta wanadai Zenj ni nchi.

..yakija masuala ya kulipa kodi, wanadai Zenj siyo nchi.

..wana lao jambo hawa.

..kuepuka usumbufu huu ni bora muungano ukavunjwa na badala yake tushirikiane kupitia EAC.
 
Wakuu heshima mbele!

Let me come in here,TRA kwa mujibu wa sheria za nchi hii (JMT) wana wajibu wa kukusanya ushuru wa Forodha Znz na kodi ya mapato(income tax),ZRB kimeundwa hapa znz kwa madhumuni ya kusimamia kodi za ndani hapa znz(sales tax,VAT)

Utata wa kulipa kodi mara 2 kwa wazanzibari unapatikana sana kwenye ushuru wa forodha pale bidhaa zilizoingizwa nchini kutoka nje zinapolipiwa ushuru wa forodha hapa zanzibar baada ya kujikadiria kodi na kukubaliwa na TRA hapa zanzibar na hatimaye bidhaa hizo kuvuka kuja Tanzania bara.

Ni suala la kiutaalamu tu ndilo linalotatiza hapa,uthaminishaji wa mizigo,magari nk kwa upande wa TRA zanzibar ndio tatizo!!thamani wanayoikubali ni ya chini kuliko TRA bara!

Ni tatizo la ndani ya TRA kwa ujumla!tatizo liko ndani ya TRA msahafu unaotumika kuthaminisha bidhaa bara utumike kuthaminisha bidhaa hapa znz,ni mamlaka moja kwa nn wanatoza ushuru wa forodha mara 2?????????wazanzibari ndio hoja yao,na ni ya msingi kwa maoni yangu.wazanzibari hawajataa kulipa kodi kama bara na ndio maana wamekua wakilipa hiyo tofauti kila mara wanapoleta mizigo yao huko kwa machogo!Tuliambiwa kuwa na hata bunge lilishaambiwa kuwa tatizo hili litakwisha pale mtandao wa Asycuda utakapofungwa znz,mtandao upo tayari hapa znz lakini tatizo liko palepale!
 
..sasa kwenye suala la mafuta wanadai Zenj ni nchi.

..yakija masuala ya kulipa kodi, wanadai Zenj siyo nchi.

..wana lao jambo hawa.

..kuepuka usumbufu huu ni bora muungano ukavunjwa na badala yake tushirikiane kupitia EAC.
Joka kuu
Pole sana dada/kaka hebu jaribu kuangalia na kuijua article of Union inasemaje kuhusu suala la mafuta na kodi ya forodha.utaona orodha gani ni mambo ya muungano na yepi si ya muungano.
Na nimegundua kitu kimoja baseless complain zinatokana na watu kutokujua mambo gani yanayotufanya sisi kuwa ni muungano na yepi kila sehemu inajitegemea na hayo malalamiko yaliyotolewa na wadau wa Utalii zanzibar yote ni kutokujua vitu gani ni vya muungano na vp sivyo vya muungano. kwa hivyo bondi ya utaalii T.bara siyo jukumu lake kuitangaza zanzibar. lakini bodi ya utalii zanzibar ndiyo jukumu lake kwa kushirikia na balozi za tanzania za nje. kwa mambo ya nje ni masuala ya muungano. kama uzembe umetokea basi nina uhakika bodi ya utalii znz ndiyo ya kulaumiwa Unless kama wakisema walikosa ushirikiano na kutoka ubalozini na kitu chengine balozi za tanzania hazi fanyi favour kwa ZNZ kama muheshimiwa raisi alivyosema.kwani zile balozi ziko pale kwa ajili ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.
Ahsante sana KiparaDar kwa ufafanuzi wako.na kitu chengine kinachosababisha magari ZNZ kuwa rahisi ni kuwa Wafanya biashara wakubwa wanaponunua magari kama japaan au hongkong wanakuwa wana ya dissemble yale magani na mengi cheinses hukatwa na yanaingizwa zanzibar as a scraper(second hand materials) na ushuru wake huwa mdogo sana ukilinganisha na gari na kuna watu huwa wanaleta zaidi ya magari 60 kwa namna hiyo na ikifika zanzibar wana ya assemble tena.lakini jee wamekimbia ushuri No.. kwa sababu wameingiza vile vitu kwa njia ya halali na kama inavyotakiwa na TRA.
Wacha tuache kubishana na tujiulize chombo kile kile kinachochukua ushuru wa forodha Zanzibar kwa nini kichukue mara mbili?lakini siyo sababu iliyokwisha kuelezwa na Fundi mchundo hapo mwanzo kwani TRA iko responsible sehemu zote za muungano.
 
Kizibao said:
Pole sana dada/kaka hebu jaribu kuangalia na kuijua article of Union inasemaje kuhusu suala la mafuta na kodi ya forodha.utaona orodha gani ni mambo ya muungano na yepi si ya muungano.
Na nimegundua kitu kimoja baseless complain zinatokana na watu kutokujua mambo gani yanayotufanya sisi kuwa ni muungano na yepi kila sehemu inajitegemea na hayo malalamiko yaliyotolewa na wadau wa Utalii zanzibar yote ni kutokujua vitu gani ni vya muungano na vp sivyo vya muungano. kwa hivyo bondi ya utaalii T.bara siyo jukumu lake kuitangaza zanzibar. lakini bodi ya utalii zanzibar ndiyo jukumu lake kwa kushirikia na balozi za tanzania za nje. kwa mambo ya nje ni masuala ya muungano. kama uzembe umetokea basi nina uhakika bodi ya utalii znz ndiyo ya kulaumiwa Unless kama wakisema walikosa ushirikiano na kutoka ubalozini na kitu chengine balozi za tanzania hazi fanyi favour kwa ZNZ kama muheshimiwa raisi alivyosema.kwani zile balozi ziko pale kwa ajili ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.
Ahsante sana KiparaDar kwa ufafanuzi wako.na kitu chengine kinachosababisha magari ZNZ kuwa rahisi ni kuwa Wafanya biashara wakubwa wanaponunua magari kama japaan au hongkong wanakuwa wana ya dissemble yale magani na mengi cheinses hukatwa na yanaingizwa zanzibar as a scraper(second hand materials) na ushuru wake huwa mdogo sana ukilinganisha na gari na kuna watu huwa wanaleta zaidi ya magari 60 kwa namna hiyo na ikifika zanzibar wana ya assemble tena.lakini jee wamekimbia ushuri No.. kwa sababu wameingiza vile vitu kwa njia ya halali na kama inavyotakiwa na TRA.
Wacha tuache kubishana na tujiulize chombo kile kile kinachochukua ushuru wa forodha Zanzibar kwa nini kichukue mara mbili?lakini siyo sababu iliyokwisha kuelezwa na Fundi mchundo hapo mwanzo kwani TRA iko responsible sehemu zote za muungano.

Kizibao,

..hoja yangu bado iko pale pale.

..nini kinawazuia wa-Zenj kuondoa suala la ushuru na forodha toka ktk mambo ya muungano? mumefanya hivyo kwa mafuta, mbona ktk TRA mnakuwa wazito?

..Zenj pia inalalamika kwamba Tanganyika inawadhulumu ktk masuala ya misaada, fedha, na benki kuu. kitu cha ajabu majuzi Maalimu kaulizwa kama ataanzisha benki kuu ya Zenj akapatwa na kigugumizi.

..inaelekea haya masuala ya kila siku kulia kero kero ni mtaji wa kisiasa wa wanasiasa wa Zenj. masuala hayo yakiondolewa ktk muungano kutakuwa hakuna wa kumlaumu.

NB:

..kwa kifupi haya malalamiko ya TRA ni juhudi za kuigeuza Zenj kuwa pango la wakwepa kodi.

..binafsi sielewi kwanini mfanyabiashara anunue bidhaa China/Dubai, aziteremshe Zenj, halafu apakie tena mwenye jahazi na kuzileta Tanganyika.

..kama mfanyabiashara huyo atatengeneza faida basi ni kwa ujanja-ujanja wa kukwepa kodi. ujanja huu hata wa-Tanganyika wanahusika.
 
Kizibao,

..hoja yangu bado iko pale pale.

..nini kinawazuia wa-Zenj kuondoa suala la ushuru na forodha toka ktk mambo ya muungano? mumefanya hivyo kwa mafuta, mbona ktk TRA mnakuwa wazito?

..Zenj pia inalalamika kwamba Tanganyika inawadhulumu ktk masuala ya misaada, fedha, na benki kuu. kitu cha ajabu majuzi Maalimu kaulizwa kama ataanzisha benki kuu ya Zenj akapatwa na kigugumizi.

..inaelekea haya masuala ya kila siku kulia kero kero ni mtaji wa kisiasa wa wanasiasa wa Zenj. masuala hayo yakiondolewa ktk muungano kutakuwa hakuna wa kumlaumu.

NB:

..kwa kifupi haya malalamiko ya TRA ni juhudi za kuigeuza Zenj kuwa pango la wakwepa kodi.

..binafsi sielewi kwanini mfanyabiashara anunue bidhaa China/Dubai, aziteremshe Zenj, halafu apakie tena mwenye jahazi na kuzileta Tanganyika.

..kama mfanyabiashara huyo atatengeneza faida basi ni kwa ujanja-ujanja wa kukwepa kodi. ujanja huu hata wa-Tanganyika wanahusika.

Joka kuu,,,
So lame kasome article of union utajua kwa kwa nini TRA hailalamikiwi kuwa suala la muungano na mafuta wanalalamika inaoyesha huna hata idea just unasikia watu wanaongea tu na hujui wanamaanisha nini?Maalim Seif hakukutwa na kigugumizi na jibu lake lilikuwa clear kwani zanzibar ilishiriki katika kuchagia mtaji wa benk kuu baada ya kufa kwa EAC ya mwanzo lakini ilikuwa haipati gawiyo la faida ya bank kuu kwa miaka yote hiyo.Na kitu chengine yaani yule mtu anaeshusha mzigo Mombasa na akauingiza TZ yeye its okay na ni lakini kuushusha mzigo ZNZ ni kosa na anakuwa anakwepa kulipa kodi. kwani Zanzibar anakusanya kozi nani? si TRA? your poits is no naive....

P:S Kasome article ya muungano na uifahamu vizuri ndiyo utoe maoni kwani inaonyesha huna hata idea ya kitu unachokiongea
 
Kizibao,

..tatizo ni kwamba hamtaki kulipa kodi.

..wanaoteremsha mzigo Mombasa hawalalamika kwamba wanalipishwa kodi wakifika Horohoro.

..kwamba ushuru na forodha iko kwenye makubaliano ya mwanzo ya Muungano haimaanishi kwamba masuala hayo hayawezi kuondolewa ikiwa ni kikwazo kwa Zenj.

..Benki Kuu ya Tanzania ilianzishwa kabla EAC haijavunjika. Zenj inaweza kuanzisha benki yake kuu na kudai kilicho chao toka benki ya Tanzania ya sasa hivi. kwanini hamfanyi hivyo wakati mnadai kwamba mnadhulumiwa?

..ndiyo maana wengine tunasema, ikifika masuala ya kutaka kukwepa kodi na ku-take advantage of Tanganyikans, mnajidai ndugu zetu na sehemu ya Tanzania, likija suala kama mafuta mnadai Zenj ni nchi huru.
 
Swala la tofauti ya ushuru wa forodha kati ya Tanganyika na Zanzibar linaeleweka. Zanzibar na Tanganyika kama nchi zina haki ya kuweka viwango vya ushuru ili kukidhi matakwa na maendeleo ya watu wao. Bahati nzuri au mbaya tumeungana na kuwa Tanzania katika mambo fulani tu kila moja ina eneo lake la kiuchumi. Kila nchi inaendesha uchumi wake wa ndani. Sasa ukiingiza mali Zanzibar, endapo kiwango cha kodi ni kidogo kuliko Tanganyika itumie huko huko. Ukiivusha itabidi ulipie tofauti ya kiwango. Hii iliathiri sana uchumi wa Zanzibar na Tanganyika kwa Zanzibar kupokea mali nyingi kuliko mahitaji ya ndani na Tanganyika kukosa mapato ya kodi ya ushuru wa forodha. Wananchi wa Zanzibar hamuonewi kwa hili. Hata mimi nikipeleka zawadi ya gari Zanzibar nitatakiwa nirejeshewe na TRA kodiziada niliyolipia Tanganyika endapo gari hilo halijatumika Tanganyika kwa muda unaoruhusiwa.
Ni kweli Zanzibar inaweza kuwa Dubai ya Afrika Mashariki lakini uingizaji wa mali hizo kwenye eneo la uchumi mwingine utabidi ufuate taratibu za kule inakoingizwa na si itokako.
Dawa ya Tatizo hili ni kuwa na viwango sawa vya ushuru.
 
Msavila said:
Swala la tofauti ya ushuru wa forodha kati ya Tanganyika na Zanzibar linaeleweka. Zanzibar na Tanganyika kama nchi zina haki ya kuweka viwango vya ushuru ili kukidhi matakwa na maendeleo ya watu wao. Bahati nzuri au mbaya tumeungana na kuwa Tanzania katika mambo fulani tu kila moja ina eneo lake la kiuchumi. Kila nchi inaendesha uchumi wake wa ndani. Sasa ukiingiza mali Zanzibar, endapo kiwango cha kodi ni kidogo kuliko Tanganyika itumie huko huko. Ukiivusha itabidi ulipie tofauti ya kiwango. Hii iliathiri sana uchumi wa Zanzibar na Tanganyika kwa Zanzibar kupokea mali nyingi kuliko mahitaji ya ndani na Tanganyika kukosa mapato ya kodi ya ushuru wa forodha. Wananchi wa Zanzibar hamuonewi kwa hili. Hata mimi nikipeleka zawadi ya gari Zanzibar nitatakiwa nirejeshewe na TRA kodiziada niliyolipia Tanganyika endapo gari hilo halijatumika Tanganyika kwa muda unaoruhusiwa.
Ni kweli Zanzibar inaweza kuwa Dubai ya Afrika Mashariki lakini uingizaji wa mali hizo kwenye eneo la uchumi mwingine utabidi ufuate taratibu za kule inakoingizwa na si itokako.
Dawa ya Tatizo hili ni kuwa na viwango sawa vya ushuru.

Msavila,

..you have made very good points.

..tatizo ni kwamba ikipendekezwa viwango sawa vya kodi, Zenj wanadai kwamba wao ni nchi huru, na kipato cha wananchi wake ni kidogo, hivyo wanataka wapange wenyewe kiwango kidogo.

..sasa baada ya kujipangia kiwango kidogo cha ushuru, wafanyabiashara wa huko waagiza bidhaa nyingi kuzidi mahitaji ya Zenj, halafu wanajaribu kuzifusha zije Tanganyika. wakifika huku Tanganyika wakidaiwa tofauti ya kodi wanadai wao si nchi huru, bali eneo la Tanzania.

..kinachokera zaidi bidhaa zenyewe wala hazizalishwi hapo Zenj. kwa msingi huo haziwafaidishi wananchi walio wengi.

..I am telling you, there is no way we can come to an agreement with Zanzibaris. Suluhisho ni kuuvunja muungano uliokuwepo sasa hivi, na kuendeleza mashirikiano yetu kupitia Jumuiya ya Afrika Mashariki.
 
Back
Top Bottom